Wednesday, July 12, 2017

TaSUBa YAPATA BODI MPYA.

index
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison G. Mwakyembe anapenda kuufahamisha umma kuwa wajumbe wa bodi ya ushauri wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) wamepatikana kulingana na taratibu za uteuzi wa bodi hiyo kumalizika.

Bodi inaundwa na watu kumi akiwemo Mwenyekiti, wajumbe watano wa kuteuliwa kwa umahiri wao na wajumbe wanne wanaotumikia bodi hii kutokana na nafasi zao kwa sasa.

1.   George Daniel Yambesi – Mwenyekiti wa Bodi
2.   Lilian Godfrey Kihiyo (Brave Law Associates) – Mjumbe
3.   Benson Sethiel Lyimo (TIB) – Mjumbe
4.   Marco Mkomwa Aidano (NBAA) – Mjumbe
5.   Arbogast Wenceslaus Kimasa (Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali) – Mjumbe
6.   Gasper Mapunda (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam) – Mjumbe
7.   Herbert F. Makoye (Mtendaji Mkuu TaSUBa) – Mjumbe
8.   Leah Kihimbi (Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Sanaa) – Mjumbe
9.   Haji Mbaruku Kejo (Mwenyekiti Chama cha Wafanyakazi TaSUBa) – Mjumbe
10.  Isdory S. Moshi (Rais wa Serikali ya Wanafunzi  TaSUBa) – Mjumbe
Ili kulijenga taifa lenye kuendeleza na kuzingatia tamaduni zetu Mhe. Mwakyembe anawatakia wajumbe wote kila la kheri katika kutekeleza majukumu yao ndani ya bodi ya TaSUBa.

Uteuzi wa bodi ya ushauri wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ulianza tarehe 19 Juni, 2017. 
Imetolewa na:

Zawadi Msalla
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
12/07/2017

No comments:

Post a Comment