KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAKUTANA NA WATENDAJI WA WIZARA YA MADINI.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Subira Mgalu (Mb), wamekutana na Watendaji wa Wizara ya Madini wakiongozwa na Waziri wake. Mhe. Anthony Mavunde (Mb) Agosti 11, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Bunge.
Katika kikao hicho, Kamati imepokea na kujadili taarifa ya Wizara ya Madini kuhusu hali ya sekta ya madini nchini, ikijumuisha uzalishaji, biashara, masoko, uwekezaji, mauzo ya nje na makusanyo ya maduhuli ya Serikali.
Baada ya kupokea na kujadili taarifa hiyo, Wajumbe wa Kamati walitoa maoni yao ya kuboresha sekta ya madini nchini kuanzia kwenye uchimbaji, uuzwaji na masuala ya kodi yanayohusika katika biashara ya madini.





Comments
Post a Comment