Friday, July 26, 2019

KAMPUNI ZA BIMA ZATAKIWA KUPANUA WIGO WA HUDUMA.

Kamishna wa Sera kutoka wizara ya fedha na mipango, Mgonya Benedicto, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango katika ufunguzi wa mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo.

Serikali imezitaka kampuni za bima nchini kuongezaa idadi ya wananchi wanaotumia bima hasa wakulima na wafugaji ili kufikia lengo la serikali la kufikisha asilimia 50 ya watu wazima wanaopata huduma ya bima ifikapo mwaka 2029.


Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philipo Mpango wakati wa ufunguzi wa mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo.


Katika hutuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kamishna wa Sera kutoka wizara ya fedha na mipango, Mgonya Benedicto, Dkt. Mpango amesema ushirikiano kati ya serikali na Kampuni za bima utaleta tija ili kuimarisha sekta ya bima hapa nchini.


Alisema watanzania wengi uchumi wao unategemea kilimo, hivyo ni vyema sasa kampuni za bima zikafikiria kupanua wigo wa huduma ya bima ili iweze kuwafukia wakulima na wafugaji ili nao wafaidike na bima za mazao na mifugo.


Aliongeza kwa kusema kuwa, sekta ya bima hapa nchini imekuwa na mchango mdogo kwenye pato la taifa na kwamba ili kuongeza mchango wa sekta hiyo mipango imara na madhubuti inahitajika ikiwa ni pamoja na mageuzi katika mazingira ya udhibiti na usimamizi wa sekta, ushirikiano wa kimkakati na taasisi zingine na utashi wa kufanya mabadiliko.


Aidha, alisema serikali inapenda kuona mamlaka ya bima na kampuni za bima zinajiandaa kutoa mchango katika uchumi wa viwanda ili kwenda sambamba na juhudi za serikali za kufikia kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.


Dkt. Mpango aliwahakikishia washauri na madalali wa bima kuwa, serikali ya awamu ya tano imeweka kipaumbele katika sekta ya fedha hasa bima.


Alitumia nafasi hiyo kuitaka Mamlaka ya Usimamizi wa bima Tanzania (TIRA) kutekeleza sheria ya bima ya mwaka 2019 na marekebisho yake ili kuhakikisha taifa linanufaika na uwepo wa sekta ya bima hapa nchini.


Aliongeza kuwa, Mamlaka ya Usimamizi wa bima Tanzania (TIRA) na wadau wengine wanapaswa kuweka mazingira wezeshi ili kuhakikisha kwamba upatikanaji wa bidhaa na huduma za bima na kuimarishwa ili kuwafikia watanzania wengi zaidi.


Dkt. Mpango alimalizia kwa kuwataka Mamlaka ya Usimamizi wa bima Tanzania (TIRA) na wadau wote wa bima waweke juhudi katika katika kutoa elimu kwa umma ili kujenga uelewa kwa wananchi.


Kwa upande wake Kamishna wa bima Tanzania, Dkt. Musa Juma amesema miongoni mwa mikakati ya kukuza uelewa kwa jamii kuhusu umuhimu wa huduma ya bima ni kutumia vyombo vya habari ili wananch wengi waweze kuhamasika na kujiunga na bima.


Alisema watu wengi hawaelewi umuhimu wa bima hali inayopelekea kuona haiwahusu jambo ambalo linapaswa kurekebshwa kwa kutoa elimu.


Dkt. Juma alisema Mamlaka ya bima inajipanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa bima ili kufanikisha malengo ya kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa huduma ya bima.


Nae Rais wa Chama cha Washauri na Madalali wa Bima (TIBA), Amir Kiwanda, amesema kuna changamoto kubwa ya kuwafikia wananchi wa vijijini hasa wakulima na wafugaji kwakuwa wengi wao hawapatikani sehemu moja na kwamba hawana vyama vya kuwaunganisha.


Alisema mkutano huo unatoa fursa kwa washiriki kuwasilisha changamoto mbalimbali zinazikaabili sekta ya bima ili kuwe na azimio la pamoja kutokana na mapendekezo ya wadau.


Kauli mbiu ya mwaka huu ni "Bima jumuishi kwa ukuaji wa Uchumi na kupunguza Umasikini"
  Kamishna wa bima Tanzania, Dkt. Musa Juma, akizungumza katika mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo.
 
Rais wa Chama cha Washauri na Madalali wa Bima (TIBA), Amir Kiwanda, akizungumza katika mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo.
 
Kamishna wa Sera kutoka wizara ya fedha na mipango, Mgonya Benedicto, akifurahia jambo na Kamishna wa bima Tanzania, Dkt. Musa Juma, katika mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo.
 
Washiriki wa mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo wakisikiliza mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika mkutano huo.


 Washiriki wa mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo wakisikiliza mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika mkutano huo.
 
Kamishna wa Sera kutoka wizara ya fedha na mipango, Mgonya Benedicto, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wajumbe wa Chama cha Washauri na Madalali wa Bima (TIBA), katika mkutano wa nne wa mwaka wa washauri na madalali wa bima nchini uliofanyika leo tarehe 26 julai 2019, mjini Bagamoyo.

Thursday, July 25, 2019

Kampuni ya Puma kuendelea kutoa elimu ya mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi



Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Dominic Dhanah
Mwandishi Wetu
Kampuni ya Puma Energy Tanzania imesema itaendelea kutoa elimu ya mafunzo ya usalama barabarani kwa shule za msingi mbalimbali ikiwa ni mkakati wake wa kupunguza ajali nchini.
Pia kampuni hiyo imetoa mafunzo ya usalama barabarani kwa zaidi ya wanafunzi 4500 katika shule tano za msingi Jijini Dodoma huku ikiahidi kuendelea kutoa elimu hiyo na kufanya kazi kwa karibu na Serikali ili kuhakikisha inawafikia wanafunzi wengi zaidi ambao watakuwa mabalozi kwa wengine.
Akizungumza leo Julai 25 jijini Dodoma mbele ya mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Vijana,  Athony Mavunde, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Dominic Dhanah, amesema programu hiyo ya mwezi mmoja kwa jiji hilo ilihusisha mafunzo ya usalama barabarani kwa walimu 15 na wanafunzi 4500, katika shule tano
“Puma Energy Tanzania imeamua kuja jijini Dodoma kwa sababu ya ukuaji wa haraka wa jiji hili ambapo shughuli za kijamii na ongezeko la watu na magari ambayo yanahatarisha usalama wa watoto wanapokwenda shuleni na kurudi nyumbani,” amesema.
Dhahana amebainisha lengo ni kuwafanya watoto kuwa na uelewa wa matumizi ya barabara ili kuongeza uelewa kuhusu dhima nzima ya usalama barabarani kwa Watanzania.
“Lengo letu kama kampuni ni kuongeza wigo ili kufikia shule nyingi zaidi nchi nzima. Puma Energy Tanzania itaendelea kuwekeza katika kampeni ya usalama barabarani ikishirikiana na serikali kupitia jeshi la Polisi ili kuokoa maisha ya watanzania,” amesema.
Kwa upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi ,Ajira na Vijana Anthony Mavunde amesema Puma Energy Tanzania ni kampuni iliyoamua kutoa elimu ya usalama barabara nchini huku akitoa ombi kwa kampuni hiyo kufundisha walimu ili wakifundisha masomo ya kawaida wawe pia wanataka na elimu ya usalama.
“Nimesikia ombi la walimu na wanafunzi la kuhitaji alama za barabarani, hivyo Serikali itaendelea kuweka alama hizo pia nimezungumza na wenzetu wa Puma wamekubali kupaka rangi za usalama barabarani na wataanza na shule tano ambazo zimepatiwa elimu hii ya usalama  barabarani,”amesema Mavunde.

Wahamiaji waliokuwa wanaelekea ulaya warudishwa




Walinzi wa pwani nchini Libya wamesema jana wamewakamata wahamiaji karibu 40 ambao walikuwa wanaelekea Ulaya nje ya pwani ya bahari ya Mediterania na kuwapeleka katika vituo vya kuwashikilia ambavyo vilishambuliwa mapema mwezi huu.

Msemaji wa kikosi hicho cha walinzi wa pwani Ayoub Gassim amesema boti ya mpira iliyokuwa imewachukua wahamiaji 38, wengi wao wamisri, ilizuiwa siku ya Jumanne nje ya pwani hiyo kiasi ya kilometa 65, mashariki mwa mji mkuu, Tripoli.

Amesema wahamiaji walihamishiwa katika kituo cha kuwashikilia cha Tajoura. Umoja wa Mataifa umeeleza wasi wasi wake mkubwa jana kuwa wahamiaji hao wapya wamepelekwa Tajoura, ambako shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa linakadiria kuwa wakimbizi 200 na wahamiaji wanashikiliwa hap

RC MAKONDA AENDELEA KUTIMIZA AHADI YA UFADHILI WA MATIBABU YA UPASUAJI WA MOYO KWA WATOTO 60 KUTOKA FAMILIA DUNI


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo Juni 25 amepokea zaidi ya Shilingi Milioni 23 kutoka kwa wadau ambao wameguswa na kampeni aliyoanzisha ya ufadhili wa matibabu ya upasuaji moyo kwa watoto 60 kutoka familia zenye hali duni.
Miongoni mwa Wadau waliomuunga Mkono RC Makonda ni Mbunge wa Kibaha Mjini Mhe. Sylvester Koka ambae amekabidhi hundi ya Shilingi milioni 10 kwaajili ya matibabu ya watoto 5 huku Mkurugenzi wa Dorka Catering Bi. Dorothy Kansolele akichangia milioni 6 na mkurugenzi wa kampuni ya Abe Professional Sound Bw. Abraham Ngomko akichangia Milioni 6 kwaajili ya matibabu ya watoto 3.
Akipokea fedha hizo RC Makonda amezikabidhi kwa uongozi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete na kueleza kuwa zitasaidia kugharamia zaidi ya Watoto10 kwenye upasuaji wa awamu ya pili.
Aidha RC Makonda amewashukuru wadau wote wanaondelea kumuunga mkono kwenye kampeni hiyo inayolenga kuokoa maisha ya watoto ambao wangeweza kupoteza maisha kutokana na wazazi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu.
Kwa upande wao wadau waliokabidhi fedha hizo wameeleza kuwa wataendelea kuunga mkono zoezi hilo kwa kuongeza fedha nyingine kwakuwa wanaamini kampeni aliyoanzisha RC Makonda ni njema na linapaswa kuungwa mkono na wadau mbalimbali ili kuokoa maisha ya watoto.
Itakumbukwa kuwa RC Makonda alitoa ahadi ya kufadhili matibabu ya upasuaji wa moyo kwa watoto 60 kwa muda wa miezi sita ambapo kila mwezi watatibiwa watoto10 na hadi sasa tayari amefanikisha matibabu ya watoto 30 kati ya 60 alioahidi.


Makamu Wa Rais Kufungua Maonesho Ya Nanenane Kitaifa 2019 Mkoani Simiyu

Na Stella Kalinga, Simiyu

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019, yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi Mjini Bariadi kuanzia tarehe 29/07/2019 hadi 08/08/2019.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati akizungumza na waandishi wa habari  katika mkutano maalum wa kutoa taarifa kwa Umma uliofanyika  Mjini Bariadi, Julai 24, 2019.

Mtaka amesema Mhe Makamu wa Rais atafungua rasmi maonesho hayo Agosti Mosi, 2019 na waoneshaji mbalimbali zikiwemo Taasisi, Mashirika mbalimbali na wajasiriamali wataanza kuonesha teknolojia, huduma na bidhaa zao Julai 29, 2019 ikiwa ni maandalizi ya ufunguzi rasmi utakaofanywa na Mhe. Makamu wa Rais.

“Shughuli ya ufunguzi itafanywa tarehe 01/08/2019 na Mhe. Makamu wa Rai, haya ni maonesho ambayo yatakaribisha viongozi wa Kitaifa, Agosti 03, 2019 tutakuwa na Mhe. Waziri Mkuu, Agosti 06, 2019 tutakuwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda na Kilele tunatarajia kuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli” alisema.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba amesema ameridhishwa na maandalizi ya Maonesho ya nanenane yanayoendelea mkoani Simiyu na kutoa wito kwa wakulima na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maonesho haya ili kuja kujionea teknolojia mbalimbali zitakazojibu changamoto za wakulima, wafugaji na wavuvi.

Aidha, Mhe. Mgumba ametoa wito kwa waoneshaji kuwa wabunifu katika teknolojia, huduma na bidhaa watakazoonesha ili maonesho haya yawe  chachu ya kuwasaidia wakulima, wavuvi na wafugaji  kuongeza tija katika uzalishaji

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amesema matarajio ya mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ni kuwa na maonesho ya tofauti na mwaka jana, lengo likiwa ni kuifanya kanda hiyo kuwa ni mahali pa kudumu pa wakulima, wafugaji na wavuvi kuwa na maonesho ya kilimo biashara.

Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanafanyika kwa mara ya pili sasa mkoani Simiyu tangu Kanda ya Ziwa ilipogawanywa katika kanda mbili yaani, Kanda ya Ziwa Mashariki(Simiyu, Mara na Shinyanga) na Kanda ya Ziwa Magharibi(Mwanza, Geita na Kagera) ambapo mwaka huu yanaadhimishwa chini ya kauli Mbiu:-“KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI”