KILWA WATENGA MILIONI 16 KUINUA UBORA WA ELIMU.
Mwalimu Mshamu Ndandavale Ofisa Elimu vifaa na Takwimu wa Wilaya ya Kilwa akizungumza na BAGAMOYO KWANZA BLOG, ofisini kwake. Mwalimu Ayub Mwakatika, Mratibu Elimu Kata ya Tingi Halmashauri ya Wilaya ya kilwa Mkoani Lindi Miongoni mwa waratibu Elimu waliopatiwa Pikipiki na Mradi wa Kuinua ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP T) ............................................ Na Hadija Omary, LINDI. Serikali Wilayani kilwa Mkoani Lindi imetenga kiasi cha Tsh. Milioni 16 kwa ajili ya kuendeleza shuguli mbali mbali zilizokuwa zikifanywa na Mradi wa kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP T) ambao umekwisha muda wake ili usimamizi huo wa Ubora wa Elimu uweze kuwa Endelevu. Hayo yameelezwa na Mwalimu Mshamu Ndandavale Ofisa Elimu vifaa na Takwimu wa Wilaya hiyo kwa niaba ya Ofisa Elimu Msingi jana Ofisini kwake alipokuwa akizungumza na Bagamoyo kwanza Blog. Mradi huo wa kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP T) ulianza mwaka 2015 Ukiwa na malengo ya K...