NAIBU WAZIRI MGALU ASEMA MRADI WA PERI -URBAN KUWAKOMBOA WANANCHI WAPATAO ELFU 38
Naibu Waziri wa Nishati wa kati kati Subira Mgalu akizungumza na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya umeme kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo. Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Kisarawe pamoja na baadhi ya viongozi wengine wa Tanesco, pamoja na REA, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri wa nishati Subira Mgalu. Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu kulia akiwa ameshikilia cheti maalumu alichopatiwa na ,Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo ikiwa ni ishara ya kuonyesha jitihada zake alizozifanya katika kuchangia kampeni ya tokomeza siro ambayo ilianzishwa kwa ajili ya wanafunzi kufanya vizuri katoka masomo yao. Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Hamisi Dikupatile akizungumza jambo kuhusiana na serikali ya awamu ya tano jinsi ilivyosaidia kuwaletea mradi wa umeme kwa wananchi wake ...