Saturday, January 25, 2020

NAIBU WAZIRI MGALU ASEMA MRADI WA PERI -URBAN KUWAKOMBOA WANANCHI WAPATAO ELFU 38


Naibu Waziri wa Nishati wa kati kati Subira Mgalu akizungumza na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya umeme kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Kisarawe pamoja na baadhi ya viongozi wengine wa Tanesco, pamoja na REA, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri wa nishati Subira Mgalu.

Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu kulia akiwa ameshikilia cheti maalumu alichopatiwa na ,Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo ikiwa ni ishara ya kuonyesha jitihada zake alizozifanya katika kuchangia kampeni ya tokomeza siro ambayo ilianzishwa kwa ajili ya wanafunzi kufanya vizuri katoka masomo yao.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Hamisi Dikupatile akizungumza jambo kuhusiana na serikali ya awamu ya tano jinsi ilivyosaidia kuwaletea mradi wa umeme kwa wananchi wake pamioja na namna utakavyoleta mabadiliko ya kimaendeleo.

Baadhi ya wananchi wakiwa wametulia kwa ajili ya kumsikiliza Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kutembelea na kukagua miradi mbali mbali katika sekta ya nishati ya umeme (PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU).
.....................................................


VICTOR  MASANGU, KISARAWE .

WANANCHI zaidi ya elfu 38 kutoka maeneo ya Wilaya ya  Kigamboni, Ukonga, Bagamoyo, Kibaha pamoja na  Wilaya ya Kisarawe kutoka zaidi ya mitaa na vitongoji zaidi ya 62  ambao walikuwa wanateseka kwa kipindi cha muda mrefu kukaa gizani katika makazi yao bila ya kuwa na nishati ya umeme wanatarajia kuondokana na hali hiyo baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa kusambaza umeme Peri- Urban ambao una lengo zaidi  katika maeneo yaliyopo  pembezoni mwa miji.

Hayo yalibainishwa  na Naibu waziri wa nishati Subira Mgalu wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wilaya ya Kisarawe  yenye lengo la kukagua na kutembelea miradi  mbali mbali ya umeme ambapo amemuagiza mkandarasi wa kampuni ya Namis kuhakikisha anakamilisha  mradi huo ifikapo mwezi Mei Mwaka huu lengo ikiwa ni kuwafikishia umeme wananchi ili waweze kuutumia katika shughuli mbali mbali za kujiletea maendeleo  ikiwemo kuanzisha ujenzi wa viwanda vidogo vidogo.

Mgalu alisema kwamba lengo kubwa la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inaboresha miundombinu ya nishati ya umeme sambamba na kusambaza umeme hasa katika maeneo ya vijijini kwa lengo la kuweza kuwaletea mabadiliko chanya ya kimaendeleo kupitia nishati ya umeme kupitia miradi mbali mbali ya ujazilishi pamoja na mingine inayosimamiwa na Tanesco pamoja na REA.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwani kutawaondolea kero na usumbufu mkubwa wananchi hususan kwa wale wa maeneo ya vijijini ambao walikuwa wanateseka  kwa kipindi kirefu  kukaa gizani na kutoa pongezi kwa Rais wa awamu ya tano Dk. Dk John Pombe Magufuli kwa kuweza kuboresha sekta ya nishati ya umeme katika maeneo mbali mbali.


“Kukamilika kwa mradi huu sisi kwa upande wetu kama Wilaya ya Kisarawe kutaweza kupunguza changamoto mbali mbali za wananchi ambao walikuwa wanasumbuka kwa kipindi kirefu kutokana na kukosa huduma ya nishati ya umeme kwa hiyo tunapenda kumshuru sana Rais wetu wa awamu ya tano Dr. John Pombe Magufuli kwa kuweza kutenga fedha ambazo zitaweza kutuletea mabadiliko chanya katika sekya ya umeme, alisema Jokate.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Kisarawe akizungumza kwa niaba ya madiwani wenzake Hamisi Dikupatile alibainisha kwamba licha ya kuwepo kwa changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika suala zima la upatikanaji wa umeme lakini kwa sasa serikali ya awamu ya tano kupitia mpango wake wa kusambaza umeme  katika maeneo ya vijijini umeweza kuwanufaisha  wananchi wengi na kuwaondolea adha ya kuishi wakiwa gizani.


Alisema kwamba serikali ya awamu ya tano imeweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Kisarawe kwa kuwawekea  miundombinu ya nishati ya umeme ambayo itaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa kuwainua katika kuendesha shughuli zao mbali mbali za kiuchumi na kuwaondolea wimbi la umasikini na kuwaleta maendeleo.


“Kwa kweli sisi watu wa kisarawe tunashukuru sana kwa Rais wa awamu ya tano Dk.Pombe Magufuli kwa kuweza kutuleta mradi huu wa umeme ambao kwa kweli utakuwa ni mkombozi  mkubwa kw wananchi kwni walikuwa wanapata usumbufu mkubwa kutokana na ukosefu wa nishati ya umeme hivyo kwa upande wetu ni jambo kubwa sana,”alisema Dikupatile.

                                     

VULU AHIMIZA DAFTARI LA WAPIGA KURA

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani Zaynabu Matitu Vulu akionesha moja ya vieilelezo vyenye taarifa mbalimbali alizochangia bungeni zinazohusu chabgamoto za wana-Pwani, alipokuwa akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuia zake kwenye Kijiji cha Kisangile Kata ya Marui Kisarawe Pwani. Picha na Omary Mngindo.
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wanawake wa (UWT) Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa Pwani Sophia Gunia akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuia zake wa Kata ya Marui, wakiwa katika ziara ya kuhamasisha uboreshaji wa daftari la wapigakura. Picha na Omary Mngindo.


...................................................

Na Omary Mngindo, Kisarawe.

MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani Zaynabu Matitu Vulu, amewataka viongozi wa kisiasa na wa Serikali kuwahimiza wananchi kujitokeza katika zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura.

Zoezi hilo linalolenga kuwapatia fursa wananchi kuhakikisha majina yao kwenye daftari hilo, lengo kubwa ni kwa wananchi hao kuweza kusubiriki zoezi la kupigia kura katika chaguzi zinazotarajiwa kufanyika mwaka huu wa 2020, kuanzia udiwani, ubunge na Rais.

Vulu ametoa rai hiyo katika Kijiji cha Kisangile Kata ya Marui wilaya ya Kisarawe mkoani hapa, akiwa kwenye ziara iliyoratibiwa na Jumuia ya Wanawake ya Chama cha Mapinduzi (UWT) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Sophia Gunia.

Alisema kuwa zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura linalotarajiwa kuanza Feb 2 litakalodumu kwa siku saba, limeandaliwa na serikali kwa lengo la kuwapatia nafasi wa-Tanzania kuhakiki majina yao kwenye daftari hilo.

"Serikali imeandaa daftari hilo kwa lengo la kuwapatia fursa wananchi kuhakiki majina yao, hatua itakayomwezesha mlengwa kupata nafasi ya kushiriki zoezi la kupiga kura kwa kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi," alisema Vulu.

Aidha alitolea ufafanuzi wa tofauti wa kadi ya kupigia kura na kitambulisho cha taifa, baada ya mkazi aliyejitambulisha kwa jina la Khalfan Mussa kuhoji utofauti wa kadi hiyo ya kupigiakura na kitambulisho cha taifa.

Kwa upande wake Sophia ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuia hiyo alisema kwamba, zoezi hilo litakalodumu kwa wiki moja halitakuwa na muda wa nyongeza, hivyo amewaasa wana-Kisarawe kuchangamkia fursa hiyo ili waweze kuwa na haki ya kuchagua na kuchaguliwa.

"Tusijiingize katika kadhia ambayo hivi sasa wananchi wengi imetukuta inayohusiana na kitambulisho cha Taifa, tulitangaziwa kipindi kirefu kuhusiana na zoezi hilo, lakini tulipuuza hatimae hivi sasa tunahangaika na kuitupia lawama Serikali," alisema Mwenyekiti huyo.

Diwani wa Kata hiyo Salehe Mfaume alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha zoezi hilo likifika linafanyika kwa mafanikio makubwa, huku akiwaasa viongozi wa ngazi zote kushirikiana kwa lengo la kulifanikisha.