Saturday, January 11, 2020

RIDHIWANI AWATAKA WAZAZI KUPELEKA WATOTO WALIOFIKIA UMRI WA KWENDA SHULE.

Na Shushu Joel

MBUNGE wa jimbo la Chalinze Mh Ridhiwani Kikwete amewataka wazazi wote katika jimbo lake kuwapeleka watoto wote waliotimiza umri wa kwenda shule ili waanze masomo haraka iwezekanavyo.


Wito huo ameutoa alipokuwa akizungumza na baadhi ya wazazi katika moja ya vikao vyake dhidi ya wananchi wake.


Alisema kuwa elimu ni ufunguo wa maisha hivyo kila mzazi ni lazima ahakikishe mwanae anaenda kuanza shule.


Aliongeza kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli imetusaidia kwa kiasi kikubwa wananchi wa chalinze kwa kutupatia misaada mbalimbali ya kielimu hivyo jukumu tulilonalo wazazi ni kujitokeza kwa wingi ili kuwaandikisha watoto wetu wenye umri wa kuanza masomo ya msingi katika shule mbalimbali zilizopo jimboni.


Aidha Kikwete aliongeza kuwa chalinze imejipanga kisawasawa kwa kushirikiana na wananchi wake kuhakikisha wanakuwa kinara wa miundombinu ya utoaji wa elimu kwa watoto ili kuongeza ufanisi wa elimu kwenye jimbo hilo.


"Elimu bure imesaidia kuwapunguzia changamoto wananchi wengi hapa nchini hivyo pongezi za pekee ziende kwa Rais Magufuli kwani awali jambo hili lilikuwa kero kwa wananchi lakini sasa hivi lipo shwari "Alisema Kikwete.


Naye Mohammed Mzimba mmoja wa wazazi amempongeza mbunge huyo kwa jinsi anavyojitoa kutoa hamasa ili kuandikisha watoto mashuleni.


Hivyo nae amewataka wazazi wenzake kuchangamka kuwapeleka watoto shule ili waweze kupata elimu yao itakayowasaidia siku za baadae.


Aidha aliongeza kuwa elimu ya msingi ndio chanzo cha kupata elimu ya juu na kuwataka wazazi wasitegemee kuwasimamia watoto wao kwenye elimu za juu huku wakiwa wamepuuza elimu ya msingi.


"Watoto wetu wakipata elimu  bora tokea msingi wakifika elimu za juu itakuwa rahisi kwao kuwa na utambuzi wa hali ya juu"Alisema Mzimba.


Aidha amempongeza Rais Magufuli kwa usimamizi wa fedha za elimu bure kwenye shule mbalimbali .
Sara Juma amesifu jinsi mbunge Kikwete anavyojitoa kwa wananchi kwa lengo la kuhamasisha wazazi kuandikisha watoto wao kuanza shule mapema.

WAKAZI WA ZINGA BAGAMOYO WALILIA AGIZO LA RAIS MAGUFULI

 Mke wa Rais Mstaafu wa serikali ya awamu ya nne ambae ni Mbunge wa kuteuliwa, Mama Salma Kikwete akizungumza na wana-Jumuia ya UWT wa Kata ya Zinga akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja.
 Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo mkoani Pwani Dkt. Shukuru Kawambwa akizungumza na wana-Jumuia ya UWT wa Kata ya Zinga akoambatana na Mke wa Rais Mstaafu wa serikali ya awamu ya nne Mama Salma Kikwete, ambae pia ni Mbunge wa kuteuliwa. Picha na Omary Mngindo


.........................................


Na Omary Mngindo, Bagamoyo.

WAKAZI wa Vijiji vinavyounda Kata ya Zinga wilayani ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wamesikitishwa kwa kitendo cha kupuuzwa agizo la Rais John Magufuli, la kuwataka wananchi wasiolipwa fidia katika mradi wa EPZ wapewe maeneo yao.


Kilio hicho kimetolewa na Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi katani hapo Mukhisin Mintanga, mbele ya Mke wa Rais Mstaafu wa Serikali ya awamu ya nne Mama Salma Kikwete, akiwa katika ziara ya kuimarisha Jumuia ya Wanawake (UWT) wilayani humo.


Ziara ya Mama Salma iliyoanzia Jimbo la Chalinze na kumalizia Bagamoyo, akiwa Zinga amepokea changamoto kadhaa ikiwemo ya fidia, ambapo Mintanga alisema kuwa pamoja na Rais Magufuli kutoa kauli hiyo, lakini hakuna utekelezaji wake.


"Rais Magufuli alipokuja alitoa agizo kwamba, wananchi ambao hawajalipwa fidia kupisha mradi wa EPZ waruhusiwe kuendeleza maeneo yao, lakini wanapokwenda halmashaauri au ofisi za EPZ wanambiwa maeneo yamewekewa GN, mpaka itenguliwe na Waziri mwenye dhamana," alsema Mintanga.


Akizungumzia hilo, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa alimwambia Mama Salma kwamba, suala hilo alishaanza kulifanyikazi, lakini kwa bahati mbaya Waziri aliyekuwepo amebadilishwa Wizara.


"Mheshimiwa Mama Salma suala hili awali lilinichanganya, nikahoji hivi ni nani aliye juu ya Rais, sababu Rais Magufuli ameshaagiza kuwa waliokosa fidia wapewe maeneo yao lakini hakuna utekelezaji, ndipo nikaelezwa kuwa kuna hatua za kufuatiliwa wizarani kuhusiana na GN," alisema Dkt. Kawambwa.


Akizungumza na wanachi hao, Mama Salma alisema kwamba amelichukua hilo, na kuwa ataungana na Mbunge Kawambwa katika kulifanyia kazi, ili agizo lililotolewa na Rais liweze kutekelezwa mapema iwezekanavyo.


Aidha Mama Salma amewataka wakazi wilayani hapa kushiriki zoezi la uboreshwaji wa daftari la makazi, linalotaraji kuanza tarehe moja mwezi wa pili, litakalodumu kwa siku saba ili wasipoteze haki zao za msingi za kuchagua viongozi katika maeneo yao.


"Zoezi la uboreshaji wa daftari la makazi litaanza tarehe moja mwezi wa pili mwaka huu, niwaombe tuzitumie siku saba za zoezi hilo, kuboreshe taarifa zetu, mfano mtu ulikiwa unaishi Lindi sasa upo Bagamoyo unalazimika kufanya hivyo," alisema Mama Salma.

Thursday, January 2, 2020

HOSPITALI MKURANGA YAPATIA X-RAY NA ULTRA SOUND

Pichani Waziri Suleiman Jafo mwenye suti akiwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalla Ulega (Shati jeupe) Zaynab Matitu Vulu, Mkuu wa wilaya Philbeto Sanga na Mganga Mkuu wa wilaya wakishuhudia uzinduzi wa mashine ya X-ray kwenye hospitali ya Mkuranga. Picha na Omary Mngindo.
.........................................


Na Omary Mngindo, Mkuranga.

SERIKALI kupitia Wizara ya afya imeipatia hospitali ya wilaya ya Mkuranga mashine za X-ray na Ultra Sound, ikiwa ni uboreshaji wa huduma hiyo hospitalini hapo.

Hayo yamebainika kwenye uzinduzi wa vifaa hivyo, uliofanywa na Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jafo, ambapo amemshukuru Rais Dkt. John Magufuli kupitia Waziri wa afya Ummy Mwalimu, kwa msaada huo.

Mbunge wa jimbo la mkuranga Abdallah Ulega ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi ametoa shukrani mbele ya Waziri wa TAMISEMI Alhaj Suleiman Jafo, na mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani Zaynab Vulu, kwenye hafla ya uzinduzi wa mashine hizo hospitalini hapo.

Ulega alisema kuwa hispitali hiyo inayobeba wagonjwa wengi kutoka wilaya mbalimbali na Mkoa wa Dar es Salaam, imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya vifaa tiba ikiwemo mashine ya X-ray na Ultra Sound ambapo alimuomba Rais Magufuli juu ya hilo.

"Nilimweleza Waziri Ummy Mwalimu kuhusiana na azma ya kununua vifaa hivyo, kwamba tumetenga pesa kupitia halmashauri kwa ajili ya kununua vifaa hivyo, lakini Dada yangu Ummy akaniambia nizipeleke katika ujenzi wa madarasa, yeye atanipatia," alisema Ulega.

"Leo nina furaha kwa ndugu yangu Jafo kufika kwa tendo la uzinduzi wa mashine hizi ambazo tayari zimeshaanza kutoa huduma, tumeambiwa na Mganga Mkuu kuwa mgonjwa mmoja tu alipelekwa Muhimbili kwa ajili ya kipimo kikubwa zaidi," alisema Ulega.

Aliongeza kuwa mashine ya X-ray iliyofungwa ni sawa na ya Muhimbili, ambapo ukipiga picha hata ukienda miaka mingapi utaikuta, huku akimshukuru Rais Magufuli kwa upendo mkubwa alionao kwa wana-Mkuranga.

Akizungumza kabla ya Waziri Jafo, Mbunge wa Viti Maalumu mkoani hapa Zaynab Vulu aliishukuru serikali kwa juhudi za kuboresha upatikanaji wa huduma kwenye hospitali hiyo kongwe wilayani hapo.

"Hospitali yetu ya Mkuranga ni kongwe inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo vifaa hivi vilivyoletwa kutoka kwa Rais wetu Magufuli kupitia Waziri mwenye dhamana ya afya Ummy Mwalimu," alisema Vulu.

Akizungumza na mamia ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo, Waziri Jafo alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kupambana na changamoto sugu zilizokuwa zinazowakabilia wananchi.

"Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais John Magufuli miradi mingi ya kimaendeleo inaendelea kufanyika, upande wa sekta ya afya zahanari zinajengwa na kuboreshwa sanjali na vituo vya afya na hospitali," alisema Jafo.

CCM YAAHIDI SIASA SAFI MWAKA 2020.

Na Silvia Mchuruza, Kagera.
 
Katibu wa chama cha mapinduzi taifa Dkt.Bashiru Ally amesema kuwa chama cha mapinduzi kinaahidi siasa safi kwa watanzania kutokana  na kutekeleza miradi mingi ya maendeleo ambapo amesema hizo ni salamu za mwaka huu 2020.


Ameyasema hayo wakati akizungumza na wajumbe pamoja na madiwani Wa Kata zote za wilaya Bukoba mkoani Kagera amewataka viongozi hao kuwa na moyo wa kufanya siasa safi ambapo amesema chama kitatetea zaidi haki za akina mama na hawatobaguliwa kutokana na nguvu yao katika jamii kuwa kubwa zaidi kwa kuwa wanawake nao wana haki kama wanaume.


Hata hivyo ameongeza kuwa hamasa kubwa ya uchaguzi imeisha kutokana na watu wenye pesa kununua uchaguzi ambapo amesema kwa mwaka huu uchaguzi utakuwa ni wa sheria na haki sawa kwa watu wote na uchaguzi unaofuata sheria za kikatiba.


” Wapo watu wanataka tume huru iwasaidie sasa niwaambie tume huru aipigi kura bali inasimamia uchaguzi na ccm ilianza kuwatafuta wapiga kura toka mwaka 1954 na ndiyo maana tunaamini tutashinda tena bila kutumia pesa au kutoa rushwa” alisema Dkt.Bashiru.


Sambamba na hayo amesema chama kimewatafuta wapiga kura kwa nguvu halali kwa kutumia siasa safi kwa kutengeneza miundombinu kama maji, umeme, Barbara, na uimalishaji wa ulinzi kwa raia wake.


“Lakini pia wapiga kura tumewatafuta kwa kuwasomesha watoto wao elimu bure,kutoka mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya huu lakini ccm aijawatafuta wapiga kura kwa kuwapa starehe kama watu wengine wanavyosema tunatakiwa kuwapa moyo ya kufanya kazi kiahalali hiyo ndiyo Ccm”


Aidha amemalizia kwa kusema chama cha mapinduzi kitaeshimu maamuzi ya umma kutokana na chama kutaka siasa safi ikiwa umma ulikiamini chama kwa mwaka ya kwanza na hats mala ya pili chama kitaaminiwa kishinde kwa kishindo.