Sunday, February 25, 2018

NMB YASAIDIA VIFAATIBA VYA MIL. 5, HOSPITALI YA BAGAMOYO.


Meneja wa NMB kanda ya Mashariki, Aikasia Muro (wa nne kulia) akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga (mwenye suti) moja ya vifaatiba walivyotoa msaada kwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo, wanaoshuhudia wa pili kushoto ni mwenyekiti wa halmashauri ya bagamoyo, Ally Ally Issa na wa tatu kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Afya Hospitali ya Wilaya Bagamoyo, Mwajuma Saidi Masaiganah.
...............................................
Benki ya NMB imesaidia vifaa tiba katika Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo vyenye thamani ya shilingi milioni tano.

Akizungumza katika kukabidhi vifa hivyo, Meneja wa NMB kanda ya Mashariki, Aikasia Muro alisema Benki hiyo imefikia hatua hiyo ikiwa ni katika mipango yake ya kurudisha faida inayopata kwenye jamii.

Alisema NMB katika mipango yake imekuwa ikishiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile kusaidia katika sekta ya Elimu, kusaidia vifaa vya ujenzi, sekta ya Afya na kusaidia watu katika kipindi cha majanga kama ya mafuriko na ajali mbalimbali.

Alisema Hospitali ni sehemu ambayo kila mwana jamii anafika kupata huduma za matibabu na hivyo kupeleka msada katika hospitali ni sawa na kusaidia jamii nzima.

Aliongeza kwa kusema kuwa, Benki ya NMB ni Benki pekee yenye matawi mengi nchini na hivyo kuwa na wateja wengi hali inayopelekea kufikiria kuridisha fadhila kwa jamii ikiwa ni pamoja na kutoa misaada mbalimbali.

Akipokea msaada huo, mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid mwanga ameishukuru Benki hiyo kwa msaada huo na kusema kuwa ni kuonyesha mahusiano mema baina ya Benki hiyo na Serikali.

Alisema vifa hivyo vitasaidia kwa Hospitali ya Bagamoyo kwakuwa Hospitali hiyo inahudumia watu kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya wilaya ya Bagamoyo.

Wakati huohuo, Mkuu  huyo wa wilaya huyo amewataka madiwani katika halmashauri ya Bagamoyo kuandaa maeneo kwenye kata zao ya kujenga zahanati ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya wilaya.

Alisema kuwepo kwa Zahanati kwenye kata kutasaidia wagonjwa kutibiwa kwenye kata zao na kwamba watakaokwenda Hospitali ya wilaya ni wale ambao wameshindikana kutibiwa kwenye zahanati.

Nae Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya Dkt. Salvio Wikesi alisema anatoa shukrani kwa Benki ya NMB kwa kuwapatia vifaa hivyo ambavyo vitasaidi katika kuwahudumia wagonjwa wanaofika katika Hospitali hiyo.

Alisema katika vifaa vilivyotolewa ni pamoja Delivery kit moja ambapo alisema kwenye muongozo wa wizara ya afya Hospitali ya Bagamoyo inatakiwa kuwa na Delivery kit 10 na kwamba hospitali hiyo sasa ina Delivery kit tano baada ya kupokea moja kutoka NMB.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni tano vilivyotolewa na benki ya NMB ni pamoja na Mashuka 35,  Vitanda 6 pamoa na magodoro yake, Kitanda cha kuifungulia 1, Seti 1 ya vifaa vya kujifungulia (Delivery kit) na Mashine ya kupimia BP 1.
 Meneja wa NMB kanda ya Mashariki, Aikasia Muro (wa tano kulia) akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga (wa tatu kushoto) moja ya vifaatiba walivyotoa msaada kwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo.
 Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga, (wa pili kushoto) Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally (wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Afya Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo, Mwajuma Saidi Masiganah ( wa tatu kushoto, kwa pamoja wakimkabidhi kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Dkt. Salvio Wikesi (katikati) wa tatu kulia ni Meneja wa NMB kanda ya Mashariki, Aikasia Muro, Meneja wa NMB tawi la Bagamoyo wakishuhudia baada ya wao kukabidhi kwa Mkuu wa wilaya.
 Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga, akitoa neno la shukrani kwa NMB mara baada ya kupokea msaada wa vifaatiba.
 Meneja wa NMB kanda ya Mashariki, Aikasia Muro, akizungumza wakati wa kukabidhi vifaatiba hivyo katika ukumbi wa Halmashauri Bagamoyo.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya Dkt. Salvio Wikesi, akitoa neno la shukrani kwa Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo kwa kutafuta wafadhili pamoja NMB kukubali kusaidia vifaatiba katika Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo.

Timu ya wasimamizi wa Afya Halmashauri ya Bagamoyo (CHMT) wakifuatilia kwa karibu makabidhiano ya vifaatiba kutoka kwa Benki ya NMB yayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo.
Meneja wa NMB tawi la Bagamoyo (kulia) akifuatilia makabidhiano ya vifaatiba vyenye thamani ya shilingi milioni 5, vilivyotolewa na Benki hiyo kwa hospitali ya wilaya ya Bagamoyo.

Timu ya kutoka NMB tawi la Bagamoyo wakiongozwa na Meneja wa kanda ya Mashariki, Aikasia Muro, (wa pili kulia) wakipiga picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, (wa pili kushoto) wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Afya, Mwajuma Saidi Masaigana, na wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally.
 Timu ya wasimamizi wa Afya Halmashauri ya Bagamoyo (CHMT) wakipiga picha ya pamoja na meza kuu.

Saturday, February 24, 2018

DC BAGAMOYO ATOA SIKU 3 WINDE (RAZABA)

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga,kihutubia wakuu wa idara katika Ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo Tarehe 23 February 2018.

Na Athumani Shomari 
.....................................
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga, ametoa siku tatu kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kufuatilia taarifa za watu wanaogawana viwanja katika shamba linalomilikiwa na Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) lililopo kijiji cha Winde kata ya Makulunge.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa agizo hilo Tarehe 22 Februry 2018 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kufuatia taarifa za kuwepo watu wanaogawana viwanja ndani ya shamba hilo bila ya kujali mipaka na umiliki halali walionao RAZABA.

Alimtaka mkurugenzi kumpa taarifa za kitaalamu kuhusu mipaka ya RAZABA ili kubaini ukubwa wa eneo lililovamiwa na kuangalia hatua za kuchukua ili kunusuru eneo hilo ambalo lipo chini ya umiliki wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar .

Alisema hatua za haraka zichukuliwe ili kusitisha zoezi linaloendelea katika eneo la RAZABA na kuwaepusha watu wasie kutapeliwa kwa kuuziwa au kugaiwa eneo linalomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Aidha, Mkuu  huyo wa wilaaya aliwataka wataalamu wa Ardhi Halmashauri ya Bagamoyo kufanya kazi zao kwa weledi ikiwa ni pamoja na kuzingatia maadili ya kazi zao.

Kufuatia hali hiyo, Mkuu huyo wa wilaya alitoa wito kwa wananchi wanaotaka Viwanja wilayani Bagamoyo kufika ofisi za Ardhi ili kupewa maelekezo yaliyokuwa sahihi juu ya wapi hakuna mgogoro wa kiumiliki ili kuondoa usumbufu unaoweza kujitokeza kwa kupewa eneo ambalo tayari lina umiliki wa mtu mwingine.

Mkuu huyo wa wilaya alisema wananchi wa kijiji cha Winde waliwasilisha malalamiko yao mbele ya Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo ya Makazi Wiliam Lukuvi ambapo walitaka mipaka ya RAZABA iwekwe wazi ili kutenganisha kati ya eneo la wananchi na RAZABA jambo ambalo tayari limeshafanyika.

KAULI YA CCM WILAYA YA BAGAMOYO NOVEMBA 18, 2017

Tarehe 18 Novemba 2017, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bagamoyo Abduli Rashidi Sharifu alisema Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Bagamoyo kinatambua uwepo wa kjiji cha Winde na kwamba hakijawahi kuvunjwa wala kuondolewa kwenye ramani ya Bagamoyo.

akizungumza katika Mkutano ulioitishwa katika kijiji cha Winde kata ya Makurunge wilayani Bagamoyo, Sharifu alisema Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) ina mipaka yake na wananchi wa winde wana mipaka yao hivyo kila mmoja anapaswa kuheshimu mipaka yake.

KAULI YA HALMASHAURI YA BAGAMOYO JUNI 22, 2016.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo Aliy Aliy alipiga marufuku utoaji wa hati za ardhi ikiwemo hati za kimila, katika maeneo yanayopakana na ardhi iliyohifadhiwa kama vile Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) inayomilikiwa na wizara kilimo na maliasili Zanziba, na Ranchi ya ruvu iliyopo wilayani Bagamoyo ambayo iko chini ya umiliki wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO).

Mwenyekiti huyo wa Halmashauri alitoa kauli hiyo Juni 22, 2016. katika Mkutano Mkuu Maalum wa kijiji cha Kidomole kata ya Fukayosi Halmashauri ya Bagamoyo na kuongeza kuwa Afisa aridhi atakaebainika kutoa hati ndani ya maeneo hayo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwemo kusimamishwa kazi.

Kauli hiyo ya Mwenyekiti huyo ilikuja kufuatia taarifa za kuuzwa kwa baadhi ya maeneo ndani ya Ranchi hizo jambo ambalo ni kinyume na sheria kwakuwa kampuni zinazomiliki maeneo hayo bado hazijavuliwa umiliki wake.

MSIMAMO WA WANANCHI WA WINDE.
  Wananchi wa kitongoji cha RAZABA Kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo wilaya ya Bagamoyo,wakionyesha mabango yao kudai Ardhi yao ambayo kwa sasa inamilikiwa na Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) kwenye mkutano uliofanyika Tarehe 18 Novemba 2017, kitongoji cha RAZABA. ambapo mgeni rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bagamoyo, Abdul Rashid Sharifu.

HISTORIA YA MGOGORO KWA UFUPI
Mgogoro  wa watu wa kijiji cha Winde na Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) umedumu kwa zaidi ya miaka 40 sasa huku RAZABA ikidai kuchukua eneo hilo kwa kuwalipa fidia wananchi hao toka mwaka 1977 na wananchi wa kijiji cha Winde wakidai hawajawahi kulipwa fidia.

MSIMAMO WA RAZABA.
Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) inasema RAZABA imeanzishwa rasmi mwaka 1977 mwezi wa kumi na kwa makubaliano kati ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo jumla ya  heka 77,663 zilikabidhiwa kwa serikali ya mapinduzi Zanzibar chini ya wizara ya kilimo na maliasili kwa lengo la ufugaji wa Ng'ombe na kwamba wananchi wote walilipwa fidia toka wakati huo. 
Bango linaloonyesha kwamba eneo hilo linamilikiwa na Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) chini ya wizara ya kilimo na maliasili ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.
Ramani ya eneo la Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA).

DAWASA KUONDOA TATIZO LA MAJI BAGAMOYO.


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, (katikati) akiongoza Mkutano wa kujadili upatikanaji wa maji Bagamoyo pamoja na kuanzisha mfumo wa kusafirisha maji taka.
........................................................... 
Wadau wa maji wilayani Bagamoyo wamekutana kujadili namna ya kuboresha miundombinu ya maji safi pamoja na kuandaa mpango mkakati wa kuanzisha namna kusafirisha maji taka ili mji wa Bagamoyo ubaki safi na salama.

Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga alisema kufuatia kukua kwa mji wa Bagamoyo ipo haja ya kujadili namna bora ya kusafirisha maji taka badala ya kuwa na maeneo yasiyo rasmi kwa utupaji wa taka.

Alisema lengo la mkutano huo ni kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu mradi wa maji taka ambao DAWASA tayari wameshafanyia upembezi yakinifu juu ya utekelezaji wa mradi huo.

Akizungumza katika Mkutano huo, Mhandisi wa Miradi Chrisitian Gava alisema katika kipindi cha mwaka 2014 mpaka 2016 Mamlaka ya maji safi na maji taka Dar es Salaam (DAWASA) imeongeza uzalishaji kutoka mita za ujazo milioni 262 mpaka mita za ujazo milioni 466 kwa siku  ambazo zinazalishwa katika mitambo ya Ruvu juu na Ruvu chini iliyoko Bagamoyo.

Alisema uzalishaji huo umekuwa hadi kufikia kiwango hicho baada ya kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli Mwezi Juni 2017.

Aliongeza kwa kusema kuwa,  kufuatia hali hiyo uzalishai wa maji kwa ujumla katika maeneo yanayohudumiwa na DAWASA ikiwemo wilaya ya Bagamoyo umeongezeka kutoka mita za ujazo milioni 300 mpaka mita za ujazo milioni 544,000 kwa siku.

Aidha,  alisema uzalishaji wa maji kutoka Ruvu juu, Ruvu chini, mtoni, na Visima vidogo umeongezeka kutoka lita milioni 300 mpaka lita milioni 502 kwa siku.

Alifafanua kuwa, katika kuhakikisha adha ya maji inaondoka katika wilaya ya  Bagamoyo DAWASA inaendelea na mradi wa ujenzi wa tenki la kuhifadhia na kusambaza maji katika maeneo ya mji wa Bagamoyo lenye ukubwa wa mita za ujazo 6000, ambalo lina uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni sita.

Alisema Tenki hilo litakapokamilika litahudumia wananchi wa maeneo ya Mpii, Zinga, Kiromo, Kitopeni, Ukuni, Kerege, Buma, Mataya, Bagamoyo mjini na ukanda maalum wa ewekezaji EPZA.

Akizungumzia Mradi wa usanifu wa mpango wa muda mrefu na muda mfupi wa kujenga mfumo wa kutibu majitaka, Mhandisi Christian Gava alisema tayari muandaaji wa mpango mkakati ambae ni Mhandisi mshauri (Consultant) ameshaanza kazi  kwaajili ya kupembua na kuandaa mpango mkakati wa muda mrefu pamoja na kupendekeza  mfumo nafuu wa kutibu majitaka katika wilaya za Kibaha, Bagamoyo na eneo  maalum la uwekezaji wilayani Bagamoyo  (BSEZ).

Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Kawambwa amesema mji wa Bagamoyo unakuwa kwa kasi hivyo ni vyema mikakati ya kukabiliana na majitaka iwepo ili kwenda sambamba na ukuaji wa mji.

Alisema katika kkufanya mji kuwa wa kisasa usiokuwa na taka kila mahali, ni vyema maandalizi ya kitaalamu yakafanyika mapema ili kila mwananchi ajue namna ya kusafirisha majitaka badala ya kuacha kila mtu atupe taka kwa namna anayoitaka yeye.

Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Mwenyekiti wa mkutano huo ambae  ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga alisema anamshukuru Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya maji safi na maji taka (DAWASA) kwa kushirikiana na serikali ya wilaya ya Bagamoyo katika kuboresha miundombinu ya maji safi na maji taka ndani ya Wilaya ya Bagamoyo. 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Fatuma Latu akiwatambulisha washiriki wa mkutano huo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo ambae ndiye Mwenyekiti wa Mkutano huo. 
Mhandisi wa Miradi kutoka mamlaka ya maji safi na maji taka (DAWASA) Christian Gava akiwasilisha Taarifa ya Miradi ya kusambaza maji safi pamoja na kutibu maji taka katika wilaya ya Bagamoyo.
Wahandisi kutoka DAWASA wakisikiliza kwa makini mapendekezo kutoka kwa washiriki wa mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Halmashari ya Bagamoyo.
Madiwani wa Halmashauri ya Bagamoyo pamoa na watalamu wa Halmashauri hiyo wakisikiliza Taarifa ya wataalamu wa DAWASA. 
Mwenyekiti wa mkutano huo ambae ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga (katikati) kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Kawambwa, Kushoto ni Makamo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo,  Saidi Ngatipula.

Thursday, February 22, 2018

NAIBU WAZIRI WA NISHATI AWASHA KITUO CHA UMEME MBAGALA.



Naibu waziri wa nishati awasha umeme kituo cha Mbagala baada ya mradi huo kukamilika.

Kufuatia kuwashwa kwa kituo hicho, Wananchi wa Mbagala ,Kigamboni ,Tandika na Mkuranga na Wenye Viwanda watapata Umeme wenye Nguvu na wenye uhakika ambao hautokatika.

Naibu waziri wa Nishati, amewapongeza wananchi wakazi wa maeneo hayo Kwa kuwa na subira huku akiwapa pole kwa kero ya umeme ya muda Mrefu.

Aidha, alisema amewashukuru Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo ya Kigamboni Dk Ndungulile na Mhe Mangungu na Wakuu wa Wilaya Kwa kufuatilia Jitahada za kuondosha Kero hiyo ya Upatikanaji wa Nishati ya Uhakika katika Maeneo hayo.

Alisema Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli imefanya juhudi kubwa kutekeleza mradi huo ili wananchi waondokane na kero hiyo.

Alisema kufuatia ushirikiano alionao yeye pamoja na Waziri wa nishati Dk Medard Kalemani wameweza kufanikisha Miradi mbalimbali ya Nishati ya umeme hapa nchini hali inayopelekea wananchi kujenga imani na serikali yao ya awamu ya tano katika utekelezaji wa miradi.

Aliongeza kwa kusema kuwa, kufuatia ushirikiano na Waziri wa nishati, imepelekea kuwa karibu na Wataalam wote wa TANESCO pamoja na Wakandarasi na hatimae kufanikisha mradi huo na miradi mingine iliyo chini ya wizara hiyo.

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MAHAFALI YA 34 YA CHUO KIKUU HURIA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki matembezi ya mahafali ya 34 ya Chuko Kikuu Huria pamoja na Mkuu wa chuo hicho Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda (kulia) kuelekea kwenye uwanja wa Halmashauri ya  Bariadi kwenye sherehe za mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania.
..............................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewakumbusha wahitimu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuwa Vyeti walivyotunukiwa  ni tuzo halali kwa juhudi na jitihada walizoonesha darasani.

Makamu wa Rais aliyasema hayo wakati wa sherehe za mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria yaliyofanyika kwenye uwanja wa Halmashauri Bariadi mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais alisema “ Jamii inategemea mtaipatia tuzo ya utendaji bora na ufanisi katika fani zenu utakao akisi viwango vilivyoainishwa kwenye vyeti vyenu”.

Makamu wa Rais aliupongeza uongozi wa chuo kwa jitihada zake katika kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais hasa katika sula la Uchumi wa Viwanda ambapo chuo hicho kimefanya Kongamano kubwa la Elimu ya Juu na Uchumi wa Viwanda mjini Bariadi lakini pia chuo hicho kipo kwenye mchakato wa Kigoda cha kiprofesa cha Viwanda na Maendeleo.

Makamu wa Rais aliwakumbusha uongozi wa chuo katika jitihada zake za kutekeleza majukumu ya chuo , uendelee kujikita kwenye kauli mbiu yake Elimu Bora na Nafuu kwa Wote .

Katika Mahafali hayo ambayo zaidi ya wanafunzi 941 wamehitimu kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na nchi za jirani ambapo wanafunzi saba (7) walihitimu Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa ya Chuo Kikuu Huria.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Huria Tanzania Profesa Rwekaza Mukandala wakati wa mahafali ya 34 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye uwanja wa Halmashauri ya Bariadi mkoani Simiyu.



Sehemu ya Wanafunzi waliohitimu katika Chuo Kikuu Huria wakiwa kwenye sherehe za mahafali ya 34 ya chuo hicho.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

Wednesday, February 21, 2018

NAIBU WAZIRI WA NISAHATI AKAGUA MITAMBO YA UMEME ITAKAYOFUNGWA MTWARQ



Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amekagua mitambo miwili ya umeme yenye uwezo wa kuzalisha megawati 2 kila mmoja itakayofungwa katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia cha Mtwara.

Amekagua mitambo hiyo tarehe 21 Februari, 2018 katika eneo la Mkandarasi, jijini Dar es Salaam ambapo kampuni ya Mantrac ndiyo iliyopewa kazi ya kufunga mitambo hiyo.

Baada ya kukagua mitambo hiyo, Naibu Waziri alisisitiza kuwa, Serikali inafuatilia kwa karibu utekelezaji wa  kazi  hiyo lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa  mitambo hiyo inafikishwa na kusimikwa mkoani Mtwara mapema iwezekanavyo ili kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika mkoa wa Mtwara pamoja na Lindi.

Kabla ya kukagua mitambo hiyo, Naibu Waziri Mgalu alifanya kikao na watendaji wa kampuni hiyo ya Mantrac pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lengo likiwa ni kufahamu maendeleo ya kazi hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Mantrac, Ahmed Saleh alimweleza Naibu Waziri kuwa mpaka sasa mitambo hiyo tayari imewasili jijini Dar es Salaam na kinachosubiriwa kwa sasa ni kuwasili kwa kontena maalum zitakazotumika kuwekea mitambo hiyo kabla ya kusafirishwa kuelekea mkoani Mtwara.

Aliongeza kuwa, kazi ya usafirishaji wa mitambo hiyo kwenda mkoani Mtwara itafanyika mwanzoni mwa mwezi Aprili mwaka huu na kwamba kazi ya kufunga mitambo hiyo, majaribio na makabidhiano itafanyika tarehe 9 hadi 30 mwezi Aprili mwaka huu.

Kituo cha kuzalisha umeme kwa Gesi asilia mkoani Mtwara kina mitambo Tisa yenye uwezo wa kuzalisha megawati 2 kila mmoja. Kituo kwa sasa kinazalisha umeme wa kiasi cha megawati 16 kufuatia mtambo namba Tisa kuwa nje kwa matengenezo.

Kuongezeka kwa mashine hizo mbili mpya (4 MW) kutafanya uwezo wa kituo hicho kuongezeka na  kufikia megawati 22 na hivyo kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara.



Sunday, February 18, 2018

NAIBU WAZIRI NISHATI ATOA WIKI MOJA KWA WAKANDARASI WA REA.


Naibu waziri wa Nishati Subira Mgalu ametoa wiki moja kuanzia leo Tarehe 18 February 2018,  kwa  wakandarasi wote nchini wanaofanya kazi ya kusambaza umeme kupitia Mradi wa Umeme vijijini (REA) kuhakikisha wanapima (survey)  kwenye taasisi za uma zikiwemo Vituo vya Afya, Zahanati, na Shule .

Alisema lengo la Mradi huo ni kuhakikisha wananchi wa vijiini wanapata umeme huku sehemu zao za kupata huduma, Vituo vya Afya, Zahanati na shule  zikipewa kipaumbele katika kufikisha umeme.

Naibu waziri huyo wa Nishati ametoa kauli hiyo Wilayani Bagamoyo alipokuwa akizindua mradi wa umeme vijijini (REA) awamu ya tatu kitongoji cha Migude kata ya Kiromo. 

Aliwataka wakandrasi hao kuhakikisha maeneo yote ya Zahanati, Vituo vya Afya, Shule na Miradi ya maji yanapimwa (yanafanyiwa  survey) kwakuwa agizo la serikali maeneo hayo yafikiwe na huduma ya Nishati katika utekelezaji wa REA awamu ya tatu. 

Alisema maeneo hayo yanapaswa kufanyiwa matayarisho ya miundombinu ikiwa ni pamoja na upimai (survey) ili yafikiwe na Umeme.

Aliongeza kwa kusema kuwa,  Mkandarasi atakaeshindwa kufuata maelekezo ya serikali atakuwa ameshindwa kazi na mkataba wake utasitishwa ili apatikane mkandarasi atakaeweza kufanya kazi kwa mujibu wa maelekezo ya serikali.

Kauli hiyo imekuja kufuatia Diwani wa kata ya Kiromo Wilayani Bagamoyo, Hasan Usinga (Wembe) kutoa taaraifa ya hali ya umeme katika kata yake ambapo alisema umeme huo haujafikishwa kwenye Zahanati.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa amepongeza utendaji kazi wa wizara ya Nishati chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa namna inavyoweza kufikisha umeme vijiini.

 Naibu waziri wa Nishati Subira Mgalu (katikat) akikagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini (REA) awamu ya tatu katika Kitongoi cha Migude kata ya Kiromo Wilayani Bagamoyo, kulia ni Diwani wa kata ya Kiromo, Hassan Usinga (Wembe) na kushoto ni Mwenyekiti wa kitongoji cha Migude, Kitumboy Bushiri.
 Diwani wa kata ya Kiromo, Hassan Usinga (Wembe)wa kwanza kulia akifurahia ambo na Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Kawambwa.
Madiwani wa viti Maalum wa Halmashauri ya Bagamoyo wakifuatilia hutuba ya naibu waziri wa Nishati ( hayupo pichani) kutoka Kulia ni Hafsa Juma Kilingo, wa katikati ni Shumina Ismail Rashid na wa kwanza kushoto ni Togo Omari Hega.
Wananchi waliohudhuria kumsikiliza Naibu waziri wa Nishati kitongoji cha Migude 
 Naibu waziri wa Nishati Subira Mgalu, akipeana mkono na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Migude, Kitumboy Bushiri ikiwa ni ishara ya kuzindua Mradi wa REA awamu ya tatu katika kitongoi hicho.

Wananchi wa Kitongoji cha Migude wakifurahi umeme baada ya Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu kuwahakikishia umeme utapatikana katika eneo hilo na nchi nzima.

JAFO AAGIZA MKANDARASI KUFANYA KAZI KWA BIDII KUKAMILISHA DARAJA LA KIMALAMISALE



Waziri wa  Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo amemuagiza mkandarasi anayejenga daraja wa Kimalamisale wilayani Kisarawe kufanyakazi usiku na mchana ili daraja hilo liweze kukamilika kabla ya Mvua za masika hazijaanza.

Waziri Jafo ametoa agizo hilo alipotembelea kukagua mradi wa ujenzi wa daraja hilo ambao unagharimu kiasi cha Sh.Milioni 390.

Hatua hiyo ya Jafo imetokana na mradi huo kuchelewa hapo awali kutokana na Mvua kubwa za vuli zilizokuwa zinanyesha.

Amesema mradi huo unatarajiwa kuwa kiungo muafaka kwa barabara ya Kimalamisale ambapo kukamilika kwa daraja hilo kutakuwa ukombozi mkubwa kwa wananchi.

Amebainisha kuwa kwasasa mvua zinaponyesha magari yanashindwa kupita kutokana kujaa maji mengi katika mto Muyombo unaotenganisha wilaya ya Kibaha na Kisarawe mkoani Pwani. 

Katika ukaguzi huo, Mkandarasi wa mradi huo amemwambia Waziri Jafo kuwa ameshanunua jenerata kubwa ambalo watalitumia wakati wa usiku ili aweze kukamilisha ujenzi huo.

Ameahidi kwamba watajitahidi kufanyakazi kwa kasi kubwa ili kuwahi  Mvua za masika na wasipate hasara ya kuchelewesha mradi.

Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo.

SERIKALI KUFANYA UCHUNGUZI WA KIFO CHA MWANAFUNZI ALIYEPIGWA RISASI.



Waziri wa Elimu na Mafunzo Profesa Joyce Ndalichako na Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Injinia Hamad Yusuph Masauni wakimfariji mama mzazi wa marehemu Akwiline Baftaha Mwanafunzi wa Cho cha Usafirishaji NIT aliyefariki kwa majeraha  baada ya kujeruhiwa na  risasi juzi. 

Akiwa kwenye daladala. Kufuatia vurugu za maanamano ya wafuasi wa Chadema ,Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ametuma salami za rambirambi kwa familia kufuatia kifo hicho.
....................................

Serikali imewahakikishia Watanzania kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya uchunguzi kufuatia kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) Akwilina Baftaha Akwilini, aliyefariki kwa kupigwa risasi mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, leo jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamad Masauni amesema kuwa Serikali itahakikisha uchunguzi huo unafanyika kwa weledi na utaalamu ili haki iweze kupatikana na yeyote aliyehusika atachukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.

“Nawasihi watanzania kuwa na subira ili uchunguzi ufanyike na tutahakikisha uchunguzi huo unafanyika haraka iwezekanavyo na baada ya kukamilika wote waliohusika watachukuliwa hatua za kisheria”, alisisitiza Masauni.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako alisema kuwa Serikali imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha mwanafunzi huyo ambacho kilitokea wakati wa kudhibiti maandamano yaliyokuwa yakifanyika katika eneo la Mkwajuni, wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam.

“Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha mwanafunzi Akwilina na anaungana na wazazi, familia, ndugu, jamaa na watanzania wote kuwapa pole za dhati kutokana na msiba huo”, alisema Ndalichako.

Aidha Ndalichako alibainisha kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itagharamia shughuli zote za mazishi ya mwanafunzi huyo na amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo kusimamia shughuli zote za msiba huo.
Pia Ndalichako alitoa rai kwa watanzania kujiepusha na vitendo vyote ambavyo vinaweza kusababisha maafa kwa watu wasio na hatia.

Wednesday, February 14, 2018

WAZIRI KALEMANI ATOA WIKI MOA KWA MKANDARASI ANAYESAMBAZA UMEME VIJIJI


Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato,Dk Medard Kalemani akitoa maagizo ya utekelezaji wa usambazaji wa umeme kwenye maeneo ya vijiji na Kata za  Iparamasa pamoja  Kalembela wakati alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye mojo kati ya ziara zake za kukagua utekelezaji wa usambazaji wa umeme wa REA awamu ya tatu.
...............................................
Waziri wa Nishati,Dkt Medard Kalemani amemwagiza mkandarasi
shirika la White City  International ambaye anasambaza umeme wa rea
awamu ya tatu kwenye Vijini na kata za Iparamasa na Kalembela kuhakikisha anafanya kazi hiyo kwa haraka zaidi ili kuwasaidia wananchi ambao wamekuwa na kilio cha muda mrefu cha uhitaji wa nishati ya umeme.

Hayo aliyasema wakati alipokuwa kwenye ziara ya Kukagua na
kuangalia utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini  Wilayani Chato.

Ambapo Diwani wa kata ya Iparamasa Amos Jiji ,amemweleza Waziri wa
nishati ambaye pia ni mbunge wa Jimbo hilo matatizo ambayo yameendelea kujitokeza kutokana na kukosekana  kwa umeme kwenye  kata yake  na kwamba kwa sasa kuna nguzo ambazo zimekaa
kwa muda wa miezi mitatu bila ya kusambazwa kwa wananchi ambao wanashida na huduma hiyo.

 Mmoja kati ya wananchi wa kata hiyo ,Bw Peter Mabula ameelezea
kukosekana kwa umeme ni chanzo kikubwa ambacho kinakwamisha utendaji kazi hususani kwa upande wa biashara kutokana na wengi wao kutegemea nishati hiyo ili waweze  kuendesha  biashara zao.

Aidha kutokana na maombi hayo kutoka kwa Diwani pamoja na wananchi
Mbunge wa Jimbo la Chato na waziri wa nishati Dk Kalemani alitoa maagizo
kwa Mkandarasi kuhakikisha nguzo ambazo zimelala ndani ya miezi mitatu zisimame na kufikia siku ya alhamisi vijiji hivyo na kata hizo ziwe zimepata umeme.
“Nimesikia kuwa nguzo zimelala tu chini ndani ya miezi mitatu na kwamba mkandarasi alivyosikia nakuja ndio ameanza kazi sasa namwagiza kuwa ahakikishe alhamisi wiki ijayo awe amewasha umeme kwenye kata ya iparamasa na vijiji vyote na mimi siondoki hapa nitahakikisha namsimamia”Alisisitiza Kalemani.

Mradi wa usambazaji wa umeme vijijini  Mkoani
Geita,unatekelezwa na mkandarasi  wa Shirika la White City
International ambapo unatarajia kufanyika ndani ya miezi  16 kwenye
jumla  vijiji  220 vilivyopo  mkoani humo na jumla ya fedha ambazo
zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza mradi huo ni  Sh Bilioni 78.56.