Tuesday, June 4, 2024

MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI UGANDA-TANZANIA WAFIKIA ASILIMIA 29.

 

Na Alodia Babara, Bukoba

Mradi wa bomba la mafuta ghafi unaotekelezwa kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani  Tanga nchini Tanzania umefikia asilimia 29.


Mradi huo ambao utagharimu zaidi ya  sh.trilioni 8 ulisainiwa mkataba wake mwaka 2021 kati ya Rais wa Uganda Yowel Kaguta Museven pamoja na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, mradi unaendelea kutekelezwa na umefikia asilimia 29.


Afisa katika kitengo cha mawasiliano bomba la mafuta EACOP Abass Abraham akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Kagera June 03, mwaka huu juu ya mwongozo kuhusu mradi wa bomba hilo amesema kuwa, hadi sasa mabomba yaliyopokelewa ni ya kusambaza umbali wa kilomita 500 na kituo cha kupokea mabomba na kuyaboresha kiko mkoa wa Tabora.


"Asilimia 80 ya bomba la mafuta ziko nchini Tanzania na asilimia 20 ziko upande wa Uganda, kwa Uganda ni kilomita 296 na upande wa Tanzania ni kilomita 1,147 bomba litapita katika wilaya nane"amesema Abraham


Abraham ameeleza kuwa, bomba litafukiwa ardhini ili kukwepa athari za kimazingira, vitajengwa vituo sita vya kusukuma mafuta ili mafuta yaweze kufika kwa wakati Tanga na mafuta kuweza kuingia kwenye matenki ambapo vituo viwili vitakuwa nchini Uganda na vinne vitakuwa hapa nchini Tanzania.


Akizungumzia upande wa fidia amesema hadi kufikia Januari,2024 asilimia 99 ya waguswa wa mradi walikuwa wameshapata fidia kwa Tanzania na idadi ya waguswa ni zaidi ya watu 8,363 miongoni mwao waliojengewa nyumba ni waguswa wapatao 339 na kufikia Machi,2024 walikuwa wamekabidhiwa nyumba hizo.


Kwa Kagera waguswa hao toka mwaka jana wanasaidiwa kutayarisha mashamba kupata pembejeo hadi hatua ya kuvuna na wanasaidiwa ufugaji mdogo mdogo mfano, mbuzi na ngombe, kabla ya program hiyo waguswa walikuwa wanapewa chakula.


Aidha, baada ya mradi huo kuanza itatumika nguvu ya aina tatu ya umeme ili mradi usiweze kukwama katika kusukuma mafuta ghafi ikiwemo, umeme wa Tanesco, generator pamoja na umeme wa nguvu ya jua (solar).


Gharama za kukamilisha ujenzi wa mradi wa bomba zinatarajiwa kufikia takribani shilingi trilioni 8 za Kitanzania, bomba hilo litajengwa na kuendeshwa na kampuni za TOTAL ya Ufaransa, CNOOC ya China na TULLOW ya Uingereza, kwa ubia na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)


KESI YA WANANDOA KUJERUHI JIRANI YAPIGWA KALENDA

 


Na Mwandishi Wetu

SHAHIDI wa upande wa mashitaka, Kiran Lalit Ratilal, ameshindwa kutoa ushahidi katika kesi  ya kujeruhi inayowakabili wanandoa Bharat Nathwan (57) na Sangita Bharat (54), kwa sababu wakili wa utetezi katika kesi hiyo yupo Mahakama ya Rufani kwenye shauri lingine.


Wanandoa hao ambao ni raia wa Tanzania wenye asili ya kihindi wanaoishi Mtaa wa Mrima - Kisutu, jengo la Lohana Dar es Salaam wanaotuhumiwa kwa mashitaka manne likiwemo la kujeruhi waliyoyatenda Julai 21,2023 kinyume cha sheria.


Kesi hiyo ililetwa jumatatu tarehe 3 Juni mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa kwa mashahidi wa upande wa mashtaka, mashahidi watatu wameshatoa ushahidi wao.


Wakili wa Serikali Mwandamizi, Grace Mwanga alidai kuwa wana shahidi mmoja na wapo tayari kuendelea na ushahidi, baada ya kudai hayo, upande wa utetezi ulidai kuwa ni kweli kesi ipo kwenye hatua ya ushahidi, lakini kwa bahati mbaya siku ya ijumaa walipata barua kutoka Mahakama ya Rufaa.


"Ni kweli kesi imekuja kwa kusikilizwa, lakini kwa bahati mbaya siku ya ijumaa tulipokea barua kutoka Mahakama ya Rufaa, kwa hiyo wakili ameenda huko,"alidai Wakili Mwanaisha Mshobozi


Baada ya Mshobozi kudai hayo, Wakili Mwanga alidai kutokana na maombi hayo hawana pingamizi, wanaomba wapangiwe tarehe nyingine ya usikilizwaji ambayo alipendekeza iwe Julai, mwaka huu ambapo hakimu alisema ni mbali sana.


Hakimu Lyamuya aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 25, 2024 kwa ajili ya usikilizwaji, ambapo shahidi Kiran Lalit alionywa na mahakama kufika tarehe hiyo kwa ajili ya kutoa ushahidi.


"Shahidi kwa bahati mbaya Wakili wa washtakiwa hayupo, tumeelezwa hapa yupo Mahakama ya Rufani, unatakiwa tarehe tutakayopanga uwepo mahakamani,"alisema Hakimu


Awali, Fundi Seremala, Dominic Mpakani (43) aliileza mahakama jinsi mshitakiwa Bharat Nathwan allivyomshambulia jirani wake, Lalit Ratilal kwa kumpiga kichwa kifuani kisha akadondoka chini na nakupoteza fahamu kwa muda.


Aidha, alidai kuwa kulikuwa na ugomvi kati ya mke wa Bharat (Sangita Bharat) na mke wa Lalit, (Kiran) ambao walikuwa wakirushiana maneno kwa ukali kwa lugha ya kihindi huku, baada ya muda kidogo waume zao walifika kwa pamoja na kuingilia ugomvi huo.


Alidai kuwa Julai 21,2023 alikuwa nyumbani kwa Lalit Ratilal maeneo ya mtaa wa Mrima katika jingo la Lohana, alimuita kwa ajili ya kuifanyia kazi zinazohusiana na mbao na kazi zingine ndogo ndogo.


Alidai kuwa alifika katika jengo hilo saa tatu asubuhi ambapo bosi wake huyo anakaa floor ya tatu, wakati anaendelea na kazi alidai kuwa Sangita alikuwa amesimama kwenye mlango lake na Kiran alikuwa amesimama kwenye mlango wake, ambapo Sangita Bharat alianza kuzungumza kwa ukali na kwa jaziba akitumia lugha ya kihindi.


"Lakini nilimsikia mke wa Bharat, Sangita akimwambia mke wa Lalit kwamba uchafu wake apeleke huko ambapo vitu vyote vilikuwa vimewekwa katika eneo la Lalit na hakuna kitu chochote kilichokuwa katika eneo la Sangita. Baada ya dakika kadhaa sijui walipiga simu au vipi waume zao walikuja kwa wakati mmoja na malumbano ya maneno yakaendelea kwa wote wanne," alidai Fundi Mpakani.


Shahidi huyo alidai kuwa, wakati malumbano ya maneno hayo yanaendelea wote walikuwa wamesimama kwenye mlango wa Lalit, baada ya muda Bharat akampiga kichwa Lalit na Lalit akadondoka chini na kupoteza fahamu.


Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, washitakiwa hao ambao ni raia wa Tanzania jinsia ya kihindi wanaoishi Mtaa wa Mrima - Kisutu, jingo la Lohana Dar es Salaam wanaotuhumiwa kwa mashitaka manne waliyoyatenda Julai 21,2023.


Katika shitaka la kwanza la kujeruhi linalomkabili Nathwani peke yake, ambapo anatuhumiwa Julai 21,2023 akiwa eneo la mtaa wa Mrima-Kisutu, jingo la Lohana, ndani ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam kinyume cha sheria alimsababishia madhara makubwa Kiran Lalit kwa kuzamisha kichwa chake kwenye ndoo la saruji iliyochanganywa.

Pia, katika shitaka la pili la shambulio la mwili linalomkabili Nathwani peke yake, ambapo tarehe hiyo na eneo hilo alimsababishia madhara Lalit Ratilal katika mwili wake kwa kumpiga kichwa, ngumi na mateke kichwani.

Ilidaiwa kuwa katika shitaka la tatu na la nne linalomkabili Sangita peke yake, ambapo anatuhumiwa kutoa matusi makubwa dhidi ya Lalit na Kiran kitendo ambacho kilileta fujo kwa namna ambayo inaweza kuleta uvunjifu wa amani.


Monday, June 3, 2024

WADAU WA USHIRIKA WATOA MSAADA HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA 

 





Na Mwandishi wetu, Lindi.

Kuelekea siku ya jukwaa la ushirika linalotarajiwa kufanyika hapo kesho juni 04, 2024 wadau wa ushirika Mkoa wa Lindi wamekabidhi misaada mbalimbali ya kibinaadamu kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Wilaya ya Ruangwa pamoja na kupanda miti hospitalini hapo



Misaada hiyo iliyokabidhiwa ni pamoja na sabuni za unga pamoja na sukari ambavyo vimegawiwa kwa akina Mama waliojifungua katika hospitali hiyo


Akizungumza na Waandishi wa Habari, Bi. Cesilia Socitenes amesema kuwa huduma zilizofanyika katika Hospitali ni moja ya utekelezaji wa misingi Saba ya ushirika ambapo msingi wa saba unaelekeza kuijali jamii.


Ameongeza kuwa katika utekelezaji wa msingi huo wa Saba, wanachama wa Vyama vya Ushirika watachangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa wengi ambao matibabu yao yanauhitaji wa damu.


Kwa upande wake, Ndg. Richard Zengo, Mrajisi Msaidizi anayesimamia Sehemu ya Vyama Visivyo vya Kifedha kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika amesema kuwa moja ya malengo makuu ya Jukwaa la Ushirika ni kuhimiza utekelezaji wa msingi wa saba wa Ushirika ambao ni kujali jamii.


Zengo amesisitiza kuwa shughuli zote zinazofanyika ni kuonesha kwa vitendo namna Ushirika unavyoungana na Serikàli ya Awamu ya Sita katika kutekeleza masuala ya kusaidia jamii inayotuzunguka.

JELA MIAKA 50, KWA UBAKAJI, WIZI NA UHUJUMU UCHUMI.

 

Na Mwandishi wetu, Lindi

Mahakama ya hakimu mkazi Lindi chini ya hakimu mkazi mfawidhi consolata singano imewahukumu kazili kafanya  mwenye umri wa miaka 47 mkazi wa dare es salaam na jonh mondo  maarufu kama kikwete kwa jina  la utapeli mwenye umri wa miaka 55 mkazi wa msavu mororgoro kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kubaka na kwenda jela miaka 20 kwa kosa linguine la utakatishaji fedha.


Hili ni shauri  la uhujumu uchumi namba tatu la mwaka 2022 ambapo kulikua na  jumla ya mashahidi 32 kutoka mikoa ya lindi, mtwara, Ruvuma, dar es salaam, Dodoma na morogoro  na vielelezo 35.


Kesi hii ilikua chini ya hakimu mkazi mfawidhi  consolata singano ambapo upande wa jamuhuri ukiongozwa na wakili wa serikali godfrey mramba  ambapo ameiambia mahakama yakwamba watuhumiwa walifanya vitendo vya uzalilishaji wa kingono kwa kuwaingilia wanawake wawilia  bila ridhaa yao na kuwasababishia hasara kiuchumi kwa kuwaibia kiasi hicho cha fedha huku upande wa watuhumiwa wakiongozwa na wakili hagai mwambingu wakikana makossa yote 16.


Hukumu hii imesomwa ndani ya saa nne na dakika 40 ambapo baada ya kusikiliza pande zote mili ndipo hakimu akatoa hukumu kwenda jela kila mmoja miaka 30  kwa kosa la kubaka.


Makossa manne yaan   la 3,4,5,6,7  la wizi kila kosa kutumikia kifungo cha miaka mitano kila mmoja.


Kuhusu kosa la nane la mtuhumiwa  jonh mkondo  kughushi nyaraka za benki yeye amehukumiwa kwenda jela miaka saba  na kosa la tisa la kufoji nyaraka kwa wote waili nalo wataenda jela miaka saba kila mmoja.


Aidha kosa la kumi la kutoa nyaraka za uongo wote wawili watatumikia kifungo cha miaka saba  kila mmoja  na kosa la 12,13 na 14  kwa  mshatakiwa wa kwanza kazili kaftani  kusajili laini za simu kwa kutumia majina ya watu na kuzitumia bila ridhaa yao kinyume na sharia ya mawasliano na posta atatumikia kifungo cha miezi 36 jela au kulipa faini ya shilingi milioni 15.


Kosa la 15 la utakatishaji fedha kwa mtuhumiwa wa kwanza ataenda jela miaka 20 na huku kosa la 16 pia la utakatishaji fedha wote wawili watatumikia pia kifungo cha miaka 20 jela.


 Bada ya kuwahukumu kisha hakimu singano akasema mtuhumiwa wa kwanza kazili atatakiwa kumlipa fidia muhanga wa ubakaji shilingi milioni 5 na kosa la tatu kwa mshatkiwa wa pili nae atalipa fidia kwa muhanga wa kubakwa shilingi milioni 5.


WIZI WA MTOTO MWENYE UALBINO MULEBA, WATATU WAKAMATWA.

 

Alodia Babara, Muleba,

Noela Asimwe Novath mtoto mwenye umri wa miaka miwili na nusu mwenye ualibino  ameibwa katika mikono ya mama yake baada ya mtu mmoja  asiyejulikana kupiga hodi nyumbani kwao na kuomba msaada wa chunvi akidai amenga’twa na nyoka katika kijiji cha Bulamula kata ya Kamachumu  wilaya ya Muleba mkoani Kagera.


Mama mzazi wa mtoto huyo Judith Richard amesema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 30, mwaka huu saa 7:30 jioni wakati mama huyo akiwa amekaa ndani na mtoto wake ndipo mtu huyo alipokuja na kupiga hodi bila kutaja jina lake na kusema kuwa, amenga’twa na nyoka hivyo  anaomba msaada wa chunvi.


Judith amefungua mlango na kumuona mtu ambaye alikuwa akitembea kwa kuchechemea bila kujua kumbe alikuwepo mtu mwingine amejibanza  ukutani ambapo aliyekuwa amejibanza ukutani alimkaba koo na aliyekuwa anachechemea  aliingia ndani na kutokomea na mtoto kusikojulikana.


 “Kuna mtu alipiga hodi akaniita mama Asimwe naomba unisaidie chunvi  nikamuuliza wewe nani akajibu mie Kelvin, nikamuuliza  wa wapi? akajibu wa humu humu kitongojini Mbare awali roho ikasita baadaye nikawaza siwezi kujua atakayenisaidia nikafungua mlango nikiwa nimewasha tochi ya simu yangu nilimuona mtu amaejibanza ukutani muda huo huo alikuja haraka akanikaba shingo  dakika kama nne amenikaba na aliyekuwa anajifanya anachechemea aliingia ndani na kutokomea na mtoto wangu” amesema Richard.


Amesema baada ya mtu huyo kumwachia alianza kupiga kelele za kuomba msaada ndipo mke wa shemeji yake alitoka  na yeye kuanza kumsaidia kupiga kelele za kuomba msaada wanakijiji walikusanyika.


Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt Abel Nyamahanga  amesema kuwa, jeshi la polisi limeshaweka mtego kila sehemu kwa ajili ya kuwakamata watu waliofanya kitendo cha wizi wa mtoto huyo.


Dkt Nyamahanga ameitaka jamii ya wakazi wa Muleba kuendelea kuonyesha mshikamano katika kumtafuta mtoto huyo kama ambavyo walifanya toka tukio lilivyotokea.


“Sisi kama serikali kwa kushirikiana na jeshi la polisi tunaendelea kupambana na mitego yote tuliyoitega tulitoa taarifa kila kona ili kuwanasa wahalifu, maelekezo yetu kama serikali ukiona matukio haya yameanza, wameanza kutikisa kiberti kijiji chochote ndani ya wilaya ya Muleba wenye binadamu mwenye ualibino kupitia kwa maafisa ustawi wa jamii waripoti kila siku juu ya usalama wa watu hawa”


“Na nyie wanawake msiwaache watoto wenu bila mtu yeyote mkaenda kuchota maji umbali wa mita kadhaa tuwalinde kwa kila namna na kwa gharama yoyote kwa sababu ni binadamu wenzetu” amesema Dkt Nyamuhanga.


Aidha, kaimu kamanda mkuu wa jeshi la polisi mkoa Kagera Yusuph Daniel amesema wanaendelea na msako wa kutafuta wahalifu waliohusika kupora mtoto huyo na wamefanikiwa kuwakamata watu watatu washukiwa wa tukio hilo akiwemo baba mzazi wa mtoto huyo.


Kamanda Daniel amesema katika uchuguzi wanaoendelea nao bado ni mapema kusema tukio hilo la kupora mtoto mwenye Ualbino limehusisha  imani za kishirikina na bado hakuna mwananchi yeyote ambaye amethibitisha hilo.


Jeshi la polisi mkoa Kagera linatoa wito kwa wananchi  kushirikiana na polisi kata kufanya msako  kwa ajili ya kumpata mtoto huyo na kutoa taarifa za uhalifu unaotokea kwenye maeneo yao.


Saturday, June 1, 2024

NMB YATOA MSAADA VIFAA TIBA VYA MILIONI 10 HOSPITALI YA BAGAMOYO

 

Benki ya NMB yatoa msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo ikiwa ni kutekeleza majukumu yao ya kusaidia wananchi katika kuimarisha afya zao.


Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Meneja wa kanda ya Dar es salaam, Ferdinand Mpona, amesema NMB imetekeleza msaada huo ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali chini ya uongozi wake Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda, amesema wanaishukuru Benki ya NMB kwa kutoa vifaa hivyo kwani vitasaidia katika matibabu ya afya za wananchi.


Amesema serikali imetenga fedha za kujenga na kukarabati majengo mbalimbali ya Hospitali ya Bagamoyo hivyo inapokea taasisi binafsi zikajitolea kusaidia vifaatiba inasaidia kuongeza ufanisi katika kuwahudumia wananchi.


Vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na Vitanda vitano vya kujifungulia kinamama wajawazito, pamoja na magodoro yake, na viti vya magurudumu (wheelchairs) ishirini kwaajili ya kubebea wagonjwa ambavyo vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 10.







Friday, May 31, 2024

DED BAGAMOYO AFUNGUA MAFUNZO KUHUSU MABORESHO YA MITAALA YA ELIMU YA AWALI, MSINGI, SEKONDARI NA UALIMU KATIKA SHULE YA SEKONDARI BAGAMOYO MKOANI PWANI.

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw Shauri Selenda tarehe 30 Mei 2024 amefungua mafunzo kuhusu maboresho ya mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari katika Shule ya Sekondari ya Bagamoyo Mkoani Pwani.


Mafunzo hayo, yamelenga kuwapitisha washiriki katika muundo wa Elimu, Maboresho Elimu Msingi na Sekondari pamoja na Ualimu.


" Ndugu zangu nyinyi mliopo hapa ni asilimia ndogo sana ya washiriki wanaohitajika kupata mafunzo haya, hivyo nawaomba muwe makini kutumia muda Ili muweze kupata Yale yaliyotarajiwa kutoka kwa wawezeshaji wetu ". Alisema Bw Selenda.


Mafunzo haya ya siku mbili yanajumuisha Walimu Wakuu 78 toka Shule za Msingi za Serikali na binafsi Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo. Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Ofisi ya Raisi- TAMISEMI






Thursday, May 30, 2024

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO 2024

SOMA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI KWA MWAKA 2024.

UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2024



CHAGUA MKOA ULIKOSOMA


MKOA WA KAGERA KUANZISHA MASHAMBA YA KAHAWA ZAIDI YA HEKTA 4,000

 

Na Alodia Dominick,

Bukoba.

Mkoa wa Kagera unatarajia kuanzisha mashamba ya pamoja ya kahawa zaidi ya hekta 4,000 lengo likiwa ni kuondoa umaskini kwa wananchi wa mkoa huo.


Hayo yamebainika katika mkutano wa wadau wa kahawa uliofanyika Mei 29, mwaka huu katika ukumbi wa mkuu wa mkoa huo.


Akifungua mkutano huo mkuu wa mkoa wa Kagera Fatma Mwassa, amesema kuwa, kuanzishwa kwa mashamba ya pamoja ya  kahawa ni agizo la Wizara ya kilimo ililolitoa hivi karibuni kwa bodi ya kahawa Tanzania (TCB) kuhakikisha inatoa matrekta na Wizara itatoa miche ya mibuni zaidi ya milioni 5.


"Dhamira ya serikali ni kupanua kilimo cha kahawa, sote tunayo kumbukumbu kahawa ilivyokosa bei wakulima wengi walikata miche ya kahawa hivyo mashamba mengi yana miche michache ya kahawa na tunao uwezo wa kuzalisha mara mbili ya kahawa  tuliyo nayo katika mkoa wetu wa Kagera"


"Tukifanya hivyo hata ile ya kutajwa tajwa eti sisi ni wa pili kutoka mwisho kwa umaskini itaisha tutakuwa tunashikilia namba 10 bora za uchumi Tanzania, sisi kama mkoa tukishirikiana na wizara ya kilimo tumeamua kufungua mashamba ya pamoja ya kahawa kwa mwaka huu tunaenda kuanzisha hekta 4,000 wilaya za Karagwe na Muleba ili kufikia mwaka 2030 mkoa wa Kagera umaskini usiwepo tena" amesema Mwassa.


Aidha amesema kuwa, baada ya kuanzishwa kwa mashamba hayo watakuwa wanakata hekali mbili wanagawia wakulima na wale watakaohitaji hekali zaidi watapatiwa.


Katibu Tawala mkoa wa Kagera (RAS) Steven Ndaki amesema kuwa, mkoa wa Kagera ndiyo mkoa wa kwanza Tanzania kwa uzalishaji wa zao la kahawa kwa mwaka huzalisha tani 60,000 hadi tani 80,000 ingawa uzalishaji huo unakumbwa na changamoto mbalimbali.


Changamoto hizo ni pamoja na utoroshaji wa kahawa ambapo baadhi ya wananchi wanalazimika kuivuna kahawa kabla ya wakati na kusababisha ubora wa kahawa kushuka.


Ametaja  lengo la kikao hicho kuwa ni kujadili fursa, mafanikio na changamoto na mwisho watoke na mkakati utakaowezesha kudhibiti ubora, kuongeza tija na kuimarisha mfumo wa masoko wa zao hilo.


Baada ya wadau wa kahawa kujadili kwa undani wametoka na maazimio ambayo ni kila halmashauri kuweka mikakati ya kuzuia biashara ya magendo ya kahawa bila kutumia nguvu ili kulinda mapato ya wakulima pamoja na serikali, halmashauri za Karagwe na Muleba zitenge maeneo kwa ajili ya kilimo cha kahawa.


Maazimio mengine ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya uvunaji wa kahawa mbichi na utoroshaji wa kahawa, msimu wa ununuzi wa kahawa ufunguliwe mapema mwezi Aprili ili kuwezesha ununuzi wa kahawa aina ya arabica na kuzuia magendo, kuongeza tija na ubora wa kahawa.


Amcos ziwezeshwe kuweka mikakati ya kuwakopesha wakulima mapema kabla ya kuvuna ili kudhibiti biashara ya kahawa changa ikiwa bado shambani (obutura), mikutano ya wadau wa kahawa ngazi ya mkoa ihuishwe na wajumbe wote kutoka maeneo ya uzalishaji washirikishwe.


Serikali iwekeze kikamilifu kwenye mialo,  beria na mikapani kwa kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama katika kudhibiti utoroshaji wa kahawa.


MWENGE WA UHURU WAZINDUA KLABU YA WAPINGA RUSHWA NA DAWA ZA KULEVYA  GREAT MINDS SCHOOL 

 

NA HADIJA OMARY, LINDI

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2024 Godfrey mnzava amezindua klabu ya Wapinga Rushwa na Dawa za kulevya ya shule ya Great minds primary school iliyopo Halmashauri ya manispaa ya Lindi Mkoani Lindi .


Uzinduzi huo ulioenda sambamba kwa Shule hiyo kukabidhiwa  cheti cha ufunguzi,  uzinduzi rasm wa klabu hiyo ulifanyika jana   katika viwanja vya shule ya msingi Mnazi Mmoja Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ambako mkesha wa mwenge huo wa uhuru ulifanyika.


Akizungumza na wanafunzi, walimu , viongozi alioambapatana nao pamoja na wananchi waliojitokeza katika viwanja hivyo Mnzava  aliwataka wanafunzi na wana klabu hiyo kuendelea kujifunza vizuri maswala hayo ya Rushwa na mapambano dhidi ya Dawa za kulevya ili wawe mabalozi wazuri kwa wazazi, walezi na jamii kwa ujumla.


Awali akisoma risala kwa kiongozi huyo, Anjela Lukanga mwanafunzi wa shule ya Great minds, amesema klabu hiyo ina jumla ya wananchama 33 ambapo kati yao wasichana 12 na wavulana 21na inalengo la kuwajenga kimaadili pamoja na kushirikishwa kwenye mapambano dhidi ya Rushwa na Dawa za kulevya.


" Tunashukuru kwa kutuwezesha kutambua nafasi na wajibu wetu kwa kushiriki kuzuia na kupambana  na Dawa za kulevya  hapa Nchini sambamba na kutujengea uwelewa juu ya madhara na kuchukia Rushwa na dawa za kulevya katika maisha yetu hali tungali bado mashuleni.


Kwa upande wake salome mbonile kutoka ofisi ya mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya amesema ili kuhakikisha Elimu ya kuendeleza mapambano dhidi ya Dawa za kulevya inawafikia watu wengi  mamlaka hiyo imeanza kushirikiana na taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU kwa kuziongezea majukumu klabu za kupinga Rushwa zijifunze na kuzungumzia maswala hayo ya Dawa za kulevya.


" katika Mkoa wa Lindi tayari kama mamlaka tumesha ziongezea majukumu hayo shule  zipatazo 22 za Sekondari , 86 za msingi na vyuo klabu mbili " alisema Bi.Salome.


Ujumbe wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2024 kuhusu Dawa za kulevya ni " Epuka matumizi ya Dawa za kulevya zingatia utu. Boresha huduma za kinga na tiba