Viongozi wa
Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) kutoka nchini Zambia wamewasili nchini kwa
ajili ya ziara ya kujifunza na kubadilishana ujuzi na Wakala wa Nishati
Vijijini (REA).
REA Zambia
ambao wameongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Zambia anayeshughulikia
Umeme, Mhandisi Arnold Simwaba wamewasili Tanzania Juni 21, 2026 katika Uwanja
wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu
Wizara ya Nishati Tanzania, Wilson Nyamanga pamoja na Mkurugenzi wa Umeme
Vijijini kutoka REA Tanzania, Mhandisi Jones Olotu, Mkurugenzi wa Rasilimali
Watu na Utawala wa REA Tanzania, Renatus Msangira.
Uongozi wa
REA Zambia utakuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya Siku 7 ambapo pamoja na vikao
vya kubadilishana ujuzi, wajumbe hao wanatarajiwa kutembelea miradi mbalimbali
ya umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini.




No comments:
Post a Comment