Na Oscar
Mbuza, MNRT
BODI ya
Mfuko wa Kuhifadhi Wanyawapori (TWPF) imetembelea kiwanja kinachomilikiwa na
Mfuko huo eneo la Njedengwa katika
Manispaa ya Dodoma ambacho kitapangiwa matumizi yake hivi karibuni.
Msafara wa
Bodi hiyo umeongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya TWPF Profesa Jafari Kideghesho
akiambatana na Mkurugenzi wa Idara ya
Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Alexander Lobora na baadhi ya
wajumbe wa Bodi.
Wajumbe
wengine ambao wameshiriki ziara hiyo ni
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) Dkt.
Eblate Mjingo na Kamishna wa Uhifadhi
kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Mlage Kabange.
Aidha ujumbe
huo pia ulimjumuisha Kamishna Msaidizi
Mwandamizi wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCCA),
Victoria Shayo aliyemwakilisha Kamisha wa Uhifadhi wa NCCA.
Akizungumza
baada ya kukagua eneo hilo lililopo Kitalu Namba 16, lenye ukubwa wa mita za
mraba 39,700, Profesa Kideghesho amesema ameridhishwa na usimamizi na uhifadhi
wa kiwanja hicho ambacho kitapangiwa matumizi yake hususani kwenye maendeleo ya
uhifadhi wa wanyamapori hivi karibuni.
Naye
Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii,
Dkt. Lobora amesema wizara italitumia eneo hilo kama eneo la mkakati la
uendeshaji wa shughuli za uhifadhi wa wanyamapori nchini.
Mfuko wa
Hifadhi ya Wanyamapori Tanzania ni wa kudumu maalum kwa ajili ya kusaidia
kutatua baadhi ya changamoto zinazohitaji fedha kwenye uhifadhi.
Madhumuni ya
Mfuko ni kurahisisha na kusaidia uhifadhi wa wanyamapori, ndani na nje ya
maeneo yaliyohifadhiwa. Bodi ya TWPF ina wajumbe tisa.

No comments:
Post a Comment