Katika hatua
nyingine kubwa ya kuharakisha maendeleo ya miundombinu na kuimarisha ukuaji wa
uchumi wa Taifa, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) umetangaza fursa za
uwekezaji katika miradi sita mikubwa ya barabara yenye urefu wa kilomita 969
kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).
Tangazo hilo
la kimataifa la kutafuta wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kwa ajili ya
kubuni, kujenga, kugharamia, kuendesha, kutunza na hatimaye kukabidhi miradi
hiyo kwa Serikali kupitia mfumo wa Design, Build, Finance, Operate, Maintain
and Transfer (DBFOMT), linaendelea kudhihirisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya
Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutumia nguvu ya sekta binafsi
kuharakisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo.
Hatua hiyo
pia inaakisi mafanikio ya mageuzi makubwa yanayosimamiwa na Kituo cha Ubia kati
ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji David
Kafulila, ambaye amekuwa mstari wa mbele kuhamasisha ushiriki wa sekta binafsi
katika uwekezaji wa miundombinu na huduma za kijamii nchini.
Miradi
iliyowekwa mezani kwa wawekezaji ni pamoja na upanuzi wa Barabara ya
Morogoro–Dodoma yenye urefu wa kilomita 260 kuwa njia nne, Barabara ya
Handeni–Kiberashi–Chemba–Kwamtoro–Singida yenye kilomita 384, upanuzi wa
Barabara ya Chalinze–Segera–Tanga yenye kilomita 246 kuwa njia nne pamoja na
ujenzi wa Kitonga Escarpment Bypass yenye kilomita 27.
Miradi
mingine ni Dar es Salaam Port–Kibaha Expressway yenye kilomita 42 na Dar es
Salaam CBD–Julius Nyerere International Airport Expressway yenye kilomita 10.
Kwa mujibu
wa TANROADS, miradi hiyo inalenga kupunguza msongamano wa magari, kuboresha
usafirishaji wa watu na mizigo, kuongeza ushindani wa uchumi wa Tanzania na
kuimarisha nafasi ya nchi kama kitovu cha biashara na usafirishaji katika
ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Kwa ujumla,
miradi hiyo ina urefu wa kilomita 969. Kwa makadirio ya wastani ambapo kilomita
moja ya barabara inaweza kugharimu takribani Dola za Marekani milioni moja sawa
na karibu tsh trilioni tatu za Kitanzania kwa zote.
.jpeg)
No comments:
Post a Comment