Monday, June 3, 2024

JELA MIAKA 50, KWA UBAKAJI, WIZI NA UHUJUMU UCHUMI.

 

Na Mwandishi wetu, Lindi

Mahakama ya hakimu mkazi Lindi chini ya hakimu mkazi mfawidhi consolata singano imewahukumu kazili kafanya  mwenye umri wa miaka 47 mkazi wa dare es salaam na jonh mondo  maarufu kama kikwete kwa jina  la utapeli mwenye umri wa miaka 55 mkazi wa msavu mororgoro kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kubaka na kwenda jela miaka 20 kwa kosa linguine la utakatishaji fedha.


Hili ni shauri  la uhujumu uchumi namba tatu la mwaka 2022 ambapo kulikua na  jumla ya mashahidi 32 kutoka mikoa ya lindi, mtwara, Ruvuma, dar es salaam, Dodoma na morogoro  na vielelezo 35.


Kesi hii ilikua chini ya hakimu mkazi mfawidhi  consolata singano ambapo upande wa jamuhuri ukiongozwa na wakili wa serikali godfrey mramba  ambapo ameiambia mahakama yakwamba watuhumiwa walifanya vitendo vya uzalilishaji wa kingono kwa kuwaingilia wanawake wawilia  bila ridhaa yao na kuwasababishia hasara kiuchumi kwa kuwaibia kiasi hicho cha fedha huku upande wa watuhumiwa wakiongozwa na wakili hagai mwambingu wakikana makossa yote 16.


Hukumu hii imesomwa ndani ya saa nne na dakika 40 ambapo baada ya kusikiliza pande zote mili ndipo hakimu akatoa hukumu kwenda jela kila mmoja miaka 30  kwa kosa la kubaka.


Makossa manne yaan   la 3,4,5,6,7  la wizi kila kosa kutumikia kifungo cha miaka mitano kila mmoja.


Kuhusu kosa la nane la mtuhumiwa  jonh mkondo  kughushi nyaraka za benki yeye amehukumiwa kwenda jela miaka saba  na kosa la tisa la kufoji nyaraka kwa wote waili nalo wataenda jela miaka saba kila mmoja.


Aidha kosa la kumi la kutoa nyaraka za uongo wote wawili watatumikia kifungo cha miaka saba  kila mmoja  na kosa la 12,13 na 14  kwa  mshatakiwa wa kwanza kazili kaftani  kusajili laini za simu kwa kutumia majina ya watu na kuzitumia bila ridhaa yao kinyume na sharia ya mawasliano na posta atatumikia kifungo cha miezi 36 jela au kulipa faini ya shilingi milioni 15.


Kosa la 15 la utakatishaji fedha kwa mtuhumiwa wa kwanza ataenda jela miaka 20 na huku kosa la 16 pia la utakatishaji fedha wote wawili watatumikia pia kifungo cha miaka 20 jela.


 Bada ya kuwahukumu kisha hakimu singano akasema mtuhumiwa wa kwanza kazili atatakiwa kumlipa fidia muhanga wa ubakaji shilingi milioni 5 na kosa la tatu kwa mshatkiwa wa pili nae atalipa fidia kwa muhanga wa kubakwa shilingi milioni 5.


No comments:

Post a Comment