Monday, February 19, 2024

MILIONI 800 KUWASAIDIA WAHANGA WA MAFURIKO MULEBA.

 


Na Alodia Babara

 Bukoba,

Walengwa wapatao 482 walioathirika na mafuriko pamoja na upepo mkali  katika wilaya za Muleba na Manispaa ya Bukoba mwaka jana wanatarajia kupata msaada wa kibinadamu wenye malengo mbalimbali utakaoghalimu zaidi ya sh. milioni 800 kutoka taasisi zisizo za kiserikali.

Msaada  huo ambao unatolewa na Kanisa la Kiinjili la Kirutheli Tanzania KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi kwa ufadhili wa taasisis inayojihusisha na shughuli za kibinadamu kwa watu wenye majanga nchini Tanzania (TCRS) na taasisi ya Actalliance Tanzania Forum utakuwa wa mwaka mmoja utawezesha kutimiza malengo sita ambayo ni msaada wa chakula, uboreshaji wa makazi, msaada wa kisaikrojia, huduma za maji, elimu na Afya na usafi wa mazingira.

Akizindua mradi huo Februari 19, mwaka huu mkuu wa mkoa wa Kagera Fatuma Mwassa alisisitiza mambo matatu ikiwemo  matumizi ya fedha za walengwa, usimamizi mzuri pamoja na  elimu ya maafa kwa walengwa.

 Mwassa alieleza kuwa, anazo taarifa kuwa mradi huo utahusisha maswala ya fedha, akaelekeza maafisa wanaohusika na maafa upande wa Serikali kama maafisa maendeleo ya jamii, watendaji wa kata, madiwani na viongozi hadi ngazi ya wilaya kushirikiana na uongozi wa kanisa la Kiinjili la Kirutheli Tanzania dayosisi ya Kaskazini Mgharibi katika uhakiki wa walengwa ambao ni harisia ili mradi usije kunufaisha ambao siyo walengwa.

“Viongozi kuanzia ngazi ya kitongoji hadi wilaya ni lazima kushiriki kikamilifu wakati wa uhakiki na kutoa huduma kwa walengwa wanaostahili na ndiyo maana nyinyi viongozi mmehudhuria uzinduzi huu” amesema Mwassa.

Amesisitiza hilo baada ya kukumbana na changamoto wakati wa kugawa chakula kwa waathirika hao kilicholetwa na kamati ya maafa kutoka ofisi ya Waziri mkuu kwani ziliingizwa siasa na likaibuka vuguvugu wakitaka watu wote wapewe msaada huo na watu waliokuwa kwenye kata zilizokumbwa na maafa wakajitokeza wakidai wote wana shida.

Amesema tathimini ilishafanyika wenye uhitaji walishatambuliwa na kuwa viongozi wasiende kuzua la kuzua kwa kulazimisha wengine kuingia kwenye hiyo risti, kaya ambazo zitahusika baada ya uchunguzi ni 482 inajullikana na ndiyo bajeti iliyopo.

“Nitumie nafasi hii kusisitiza kuwa fedha zitakazotolewa zitumike kwa matumizi yaliyokusudiwa zisiwe chanzo cha ndoa kuvunjika na kusababisha ukatili wa kijinsia katika familia za walengwa” amesema Mwassa

Aidha aliongeza kuwa, mradi ujikite sana kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kujifunza namna ya kukabiliana na maafa, mfano wananchi waelimishwe kutojenga sehemu hatarishi zinazoweza kuhatarisha maisha yao na familia zao serikali inaposema maeneo haya hayafai kujengwa makazi basi watu wote wakubaliane na waache maeneo hayo.

Kwa  upande wake Mkurugenzi wa taasisi inayojihusisha na shughuli za kibinadamu kwa watu wenye majanga nchini Tanzania TCRS Samwel Mlay amesema kuwa, mradi utakuwa wa mwaka mmoja ulianza kutekelezwa Desemba mwaka jana na utakamilika Desemba mwaka huuu, utawezesha kutimiza malengo sita ambayo ni msaada wa chakula, uboreshaji wa makazi, msaada wa kisaikrojia, huduma za maji, elimu na afya na usafi wa mazingira.

Mlay amesema, mradi utaghalimu zaidi ya shl milioni 800 walengwa wapatao 482 walioathirika na mafuriko pamoja na upepo mkali  katika wilaya za Muleba na Manispaa ya Bukoba mwaka jana watanufaika na mradi huo ambapo katika wilaya ya Muleba ni kata mbili za Kashalunga na Kalambi na Manispaa ya Bukoba ni kata nne za Rwamishenyi, Hamugembe, Bilele na Kashai  zinatarajia kupata msaada wa kibinadamu katika nyanja mbalimbali kutoka katika  taasisi zisizo za kiserikali

Diwani wa kata ya Kashai Ramadhan Kambuga amesema kuwa, kutolewa kwa misaada hiyo kutasaidia kupunguza maumivu kwa wananchi waliokumbwa na mafuriko na upepo mkali.

 

Amesema wananchi waliokumbwa na athari za mafuriko na upepo walishatambuliwa hivyo hawatakwenda kinyume na wale waliotambuliwa kikubwa viongozi wa Serikali walishawatembelea na kuwabaini na mahitaji ya kila mmoja, hawataongeza wala kupunguza mlengwa kila mmoja alishawekwa kwenye utaratibu hivyo uadilifu, busara na hekima vitaendelea kutumika.

Hata hivyo mafuriko hayo kwa wilaya ya Muleba yalitokea Octoba 15, mwaka jana na kwa manispaa ya Bukoba yalitokea Oktoba 18, mwaka jana.


DIVISHENI YA ELIMU SEKONDARI YAFANYA KIKAO KAZI CHALINZE.

 

Divisheni ya Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo, imefanya kikao kazi kufanya tathmini ya utendaji kazi ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya matokeo ya kidato cha pili na cha nne kwa mwaka 2023 ili kuweka mikakati mbalimbali katika kuboresha utendaji kazi ili kufikia Malengo ya utendaji kazi (Key Performance Indicators).

Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 19 Februali 2024 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete uliopo katika Halmashauri hiyo na kuhusisha Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali na binafsi na walimu wa Taaluma katika Shule zote za Sekondari katika Halmashauri ya Chalinze.

Akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi Afisa Elimu wilaya ya Chalinze, Bi Salama Ndyetabura alieleza mafanikio na Changamoto mbalimbali zinazoikabili Divisheni ya Elimu Sekondari, huku akiishukuru Halmashauri ya Chalinze kwa kuweza kujenga maabara kwa baadhi ya Shule za Sekondari katika Halmashauri hiyo

Afisa Elimu Sekondari, ametoa pongezi kwa wakuu wa Shule kwa usimamizi bora wa miradi kwa kumpongeza Mkuu wa Shule Changalikwa Mwl Benasian Ituja kwa Kusimamia ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Mbwewe kwa kuisimamia kwa weledi na maarifa hata kutotengeneza hoja yoyote ya ukaguzi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Bwana Ramadhani Possi ametoa pongezi za dhati kwa walimu wote wa Sekondari, Maafisa Elimu na Maafisa kata kwa jinsi wanavyofanya kazi kwa weledi na uadilifu katika kutoa maarifa kwa watoto wa Taifa hili.

Possi aliwapongeza kwa kukuza taaluma na kupata matokeo mazuri ya kidato cha nne na cha pili kwa mwaka 2023.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri amewasisitiza watendaji wa kata kushirikiana na walimu ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wote waliofaulu kuingia kidato cha kwanza kuripoti kwa wakati na kuweza kuendelea na masomo.





Saturday, February 10, 2024

MIZIGO YAONGEZEKA BANDARI YA MTWARA


 Na Albert Kawogo, Mtwara

BANDARI ya Mtwara imeongeza kiasi cha mizigo inayohudumiwa hapo kutoka kiasi cha tani laki nne hadi tani milioni 1.6 katika kipindi cha mwaka 2022/2023.

Chachu ya ongezeko hilo linatokana na hatua kubwa ya kimkakati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA kufanya maboresho yenya thamani ya shilingi bilioni 157.8 kwenye eneo la gati ya bandari hiyo sambamba na ununuzi wa mtambo wa kupakia na kushusha mizigo.

Ferdinand Nyathi meneja wa Bandari ya Mtwara amewaeleza wahariri wa habari  kutoka Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) waliotembelea bandari hiyo kuwa,  jitihada kubwa zinazofanywa na TPA kwenye uwekezaji wa miundombinu ya bandari ndio zinaongeza ufanisi katika utendaji.

"Uwekezaji  umeimarishaji  mifumo ya bandari na matunda ya kazi hii ni kwamba msimu wa korosho ambao sasa uko mwishoni tumeweza kuhudumia meli kubwa 28" Alisema Nyathi

Nyathi aliendelea kufafanua kuwa Bandari hiyo imekuwa ikisafirisha makaa ya mawe, saruji ya kiwanda Cha Dangote Cement ambapo saruji hiyo husafirishwa kupelekwa Zanzibar na Comoro.

Naye Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania Dk George Fasha alisema Bandari ya Mtwara ni Bandari ya kimkakati kwa ushoroba wa kusini.

Dk Fasha alisema mpango wa sasa ni kuanza usafirishaji wa madini ya graphite kutoka Wilaya Ruangwa Lindi,huku akisisitiza kuwa ili kuimarisha ushoroba huo TPA inaendelea kuboresha Bandari za MbambaBay ili iweze kusaidia bandari ya Mtwara kuhudumia mizigo ya Malawi na Msumbiji.

Thursday, February 8, 2024

RAIS SAMIA ASIKITISHWA NA MAUAJI YA PALESTINA.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania inasikitishwa na vita vinavyoendelea Palestina vinavyosababisha mauaji ya watoto na raia wasio na hatia.

Rais Samia ameyasema hayo Tarehe 07 february 2024 katika sherehe za mwaka mpya 2024 (Diplomatic Sherry Party) kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wawakilishi wa Mashirika ya kimataifa zilizofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.

Aidha, amesema Tanzania inaunga mkono usuluhishi kati ya Palestina na Israeli kwa kutoa wito wa kusitisha mapigano na kupatiwa misaada ya kibinadamu.

Wakati huohuo Rais Samia amesema Haki, Demokrasia, Sheria na Utawala bora vitadumishwa kwa watu wote wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Amesema ili kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki, kikosi kazi huru cha kupitia na kushauri mageuzi muhimu katika mfumo wa siasa kiliundwa ambapo kiliwasilisha ripoti yake mwaka 2023

Rais Samia pia amesema mapendekezo mengi ya kikosi kazi yaliyopokelewa na serikali na wadau wote yalihusu kuongeza uwazi katika michakato ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na uteuzi wa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi.


UWT NA KIPAUMBELE CHA MAZINGIRA WEZESHI KUINUA WANAWAKE KIUCHUMI

 


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt Doto Biteko akimkabidhi Nakala ya Makubaliano kati ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC)  Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda (MCC) jijini Dodoma Tarehe 07 February 2024.

.......................

DODOMA 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt Doto Biteko  amemkabidhi Nakala ya Makubaliano kati ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC)  kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda (MCC) katika Hafla ya Utiaji Saini wa Makubaliano hayo.

Aidha, Mwenyekiti Chatanda alishiriki hafla hii kwa lengo la kuhakikisha UWT inakuwa mstari wa mbele katika kuchangia uwepo wa mazingira wezeshi ya kuwainua Wanawake Kiuchumi kuanzia katika utoaji elimu na hamasa kwa jamii.

UWT IMARA JESHI LA MAMA SAMIA KAZI IENDELEE.


Tuesday, February 6, 2024

ALIYEMKATA KIGANJA KATIBU WA BAKWATA BUKOBA AUWAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA.

 

Na Alodia  Babara

Bukoba,

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Abdulmalick Yahya (42) mkazi wa wilaya ya Muleba ambaye alikuwa mtunza ghala katika mradi wa ujenzi wa BAKWATA Bukoba (BAKWATA COMPLEX) amefariki baada ya kushambiliwa na wananchi wenye hasira kufuatia tukio alilofanya la kumshambulia katibu wa BAKWATA wilaya ya Bukoba na kumkata kiganja cha mkono.

Katibu wa Bakwata wilaya ya Bukoba Hamza Zakaria (43) akiwa anaendelea na matibabu katika hospital ya rufaa ya mkoa, Bukoba amesimulia alivyoshambuliwa na aliyekuwa mtunza ghala la ujenzi wa BAKWATA Complex na kuanza kumkata kwa panga kisha kutenganisha kiganja na kiwiko cha mkono wa kushoto.

"Ilikuwa ni majira ya saa 10:00 asuhuhi siku ya Tarehe 2 februali 2024 wakati nikiwa kazini kwangu nilitoka kwenda duka la jirani kuangalia viatu kwa mtu mmoja anaitwa Khalid ndipo alitokea Abdulmalick Yahya akiwa ameshika panga na kuanza kunishambulia" amesema Hamza

Ameendelea kusimulia kuwa, alipomkata panga la kwanza alikinga mkono alipotaka kumkata tena walishikana mikono na badae akajitoa kwenye mikono yake na kutaka kukimbia kutokana na kwamba  alikuwa amevaa kanzu ambayo ilimtega miguu akashindwa  kukimbia na badala yake alianguka chini.

"Kwa kuwa alikuwa anaendelea kunifukuza alinikuta hapo hapo chini akaanza kunikata mapanga huku  nikiendelea kukinga mkono wa kushoto ndipo baadaye nilijifanya nimefariki dunia alipokata mara ya mwisho akaona sijitingishi akaondoka" ameongeza Hamza.

Amesema ndani ya dakika kama tano hivi alimuona mtu anayemfahamu akamuita wakampa msaada wa kumbeba na vijana wengine na kumpeleka hospital ya rufaa ya mkoa wa Kagera, Bukoba ambapo anaendelea kupatiwa matibabu na anaendelea vizuri.

Amesema huyo aliyemkata mapanga hakuwa na visa naye labda kama vilitokana na ujenzi uliokuwa unaendelea msikitini, siku zilizopita alikuwa ni mtunza ghala na alikuwa ni miongoni mwa watu waliokamatwa wanaiba nondo na saruji akawa amesimamishwa kuendelea kusimamia ghala hilo, sasa alihisi kuwa alichongewa na Hamza na alikuwa ni mtu wa muda mrefu pale msikitini.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera, Blasius Chatanda, amethibitisha kutokea kwa matukio hayo mawili na kusema kuwa, Abdulmalick Yahya (42) mkazi wa wilaya ya Muleba ambaye alikuwa mtunza ghala katika mradi wa ujenzi wa BAKWATA Bukoba (BAKWATA COMPLEX) kabla hajakumbwa na umauti Februari 02,2024 majira ya saa 11:30 asubuhi katika barabara ya Kawawa karibu na ofisi za Bakwata mkoa alifika na kuanza kumkata mapanga Hamza Zakaria (43) katibu wa BAKWATA wilaya ya Bukoba.

Amesema wakati akitenda tukio hilo watu waliokuwepo walimzuia asiendelee kumshambulia bila mafanikio na walipoona anataka kuwashambulia na  wao walianza kumshambulia na alibahatika kuokolewa na jeshi la polisi na kumkimbiza hospital ya rufaa ya mkoa, Bukoba ambapo wakati akiendelea kupata matibabu alifariki dunia.

Kamanda Chatanda alieleza kwamba, chanzo cha tukio hilo ni kusimamishwa kazi ya kusimamia ghala la kutunza vifaa vya ujenzi wa BAKWATA complex  kwa Abdulmalick na kamati ya ujenzi Februari mosi ,2024 ambapo Abdulmalick alimtuhumu katibu wa BAKWATA, Bukoba kwamba ndiyo chanzo cha hayo yote na akaahidi kulipiza kisasi.

Amesema kuwa, alimkata mkono wa kushoto ambao kiganja chake alikitenganisha kabisa na kiwiko na alikatwa mapanga mengine mawili kichwani japo ni kwa bahati nzuri hayakuweza kupasua fuvu.

Ametoa rai kwa wananchi wa mkoa huo kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake kufuata sheria na taratibu za nchi.




HATUTAWAFUMBIA MACHO WANAOJIITA BOKO HARAMU NDANI YA MKOA WA PWANI - Mramba

 

Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Pwani ndg David Mramba amesema hawako tayari kuwafumbia macho wanaojiita boko haramu kwani kujiita hivyo ni kuhatarisha maisha ya Watanzania.

Mramba ameyasema hayo leo tarehe 06/02/2024 katika Ofisi za CCM Mkoa wa Pwani kuwa CCM ina macho mengi hata mtu akiwa kwenye shimo ataonekana na akibainika hataachwa salama kimaadili.

Amesema wako watu wanataka kuwatishia Wanaccm kwa kujiita wao ni boko haramu jambo ambalo si jema ndani ya CCM.

" Unapojiita boko haramu tafsiri yake wewe ni mtekaji na mbakaji hivyo lazima tuwashughulikie watu wa aina hiyo  amesema Mramba

Ameendelea kusema kuwa hakuna kikundi ndani ya CCM kitakachokuwa na uwezo wa kubadili mawazo ya Wanaccm kwa kuwatishia.

Amesema wako wanaowatishia Viongozi walioko madarakani wakidai kuanza kutengeneza safu zao huku wakijipachika majina ya aina hiyo.

Hatutawavumilia wanaokiuka taratibu za Chama na tuko tayari kuwaadhibu ili Chama na wanachama wabaki salama  amesema Mramba

Acheni vihelehele vya kuwasumbua Viongozi walioko madaraka waacheni watekeleze Ilani ya CCM kwa mioyo safi* - asema Mramba

Mramba amezungumzia usemi usemao kuwa acha haki iamue haki usitafute haki pasipo haki akimaanisha unaweza ukawa na haki ya kugombea nafasi yoyote lakini ukaipoteza haki hiyo kwa sababu ya rafu za mapema.

Amehitimisha kwa kuwataka Wanaccm kulinda heshima ya Chama na kujilinda wao ili wakati wa uchaguzi wasiwe kikwazo kwenye vikao vya mchujo.

Taarifa hii imeandaliwa na

Idara ya Siasa, Uenezi na Mafunzo CCM
Mkoa wa Pwani.


WAFANYABIASHARA WA MAFUTA ZINGATIENI MAISHA YA WANANCHI - DKT. BITEKO

 

Na Mwandishi wetu, Dodoma

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Chama cha Waagizaji na Wasambazaji wa Mafuta nchini (TAOMAC) ambapo amewataka wafanyabiashara hao pamoja na faida wanayoipata wazingatie maslahi wananchi wa hali ya chini.

Ameyasema hayo tarehe 06 Februari, 2024 jijini Dodoma katika kikao ambacho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo changamoto mbalimbali ambazo wanafanyabiashara hao wanazikabili.

Amesema Serikali siku zote iko tayari kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara na kuwekea mazingira wezeshi ya biashara zao ili waweze kuwajibika kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za usimamizi katika sekta husika.

“Tunapofanya biashara hii ya mafuta lazima tuangalie mtanzania maskini ambaye anategemea sekta hii kujikwamua kimaisha, isifike mahala kila mwisho wa mwezi watu wote wanashika vichwa wakihofia kupanda kwa bei ya mafuta… Serikali inafanya kila jitihada kupunguza makali ya bei ya mafuta hivyo nanyi mlizingatie suala hili.”amesema Dkt. Biteko

Dkt. Biteko ameishukuru TAOMAC kwa ushirikiano wao kwa Serikali katika kuhakikisha kuwa nchi inakuwa na mafuta ya kutosha na kueleza kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wao katika ukuaji wa Uchumi wa nchi.

Amesema uhusinao uliopo kati ya Serikali na TAOMAC unahitaji kuwa endelevu na pale zinapotokea changamoto zitafutwe njia za kukabiliana nazo kwa mstakabali wa Taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAOMAC, Kalpesh Mehta ameishukuru Serikali kwa mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara wa mafuta na utayari wa Serikali kushughulikia changamoto kadhaa zinazojitokeza katika sekta hiyo.

Akizungumzia mazingira hayo, Mkurugenzi Mtendaji, Raphael Mgaya amesema ushirikiano wa TAOMAC kwa serikali hauepukiki ili kuhakikisha nchi inapata mafuta ya kutosha hivyo wapo tayari kushirikiana na Serikali.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Watendaji kutoka  Taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Benki Kuu  ya Tanzania (BoT) Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba.







TAKUKURU KAGERA YABAINI MAPUNGUFU KATIKA MIRADI 16.

 

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kagera Pilly Mwakasege akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu  Octoba hadi Desemba 2023

..................................

Na Alodia Babara

Bukoba

TAASISI ya kuzuia na kupamba na Rushwa mkoa wa Kagera kwa kipindi cha Oktoba-Desemba 2023, imefuatilia miradi 19 yenye thamani  zaidi ya shilingi bilioni 6.1 ambapo kati ya hiyo miradi 16 yenye thamani zaidi ya shilingi bil.4.2 imebainika kuwa na mapungufu yaliyohitaji marekebisho.

Kamanda wa taasisi hiyo mkoani humo Pilly Mwakasege amesema kuwa kiasi hicho ni sawa na asilimia 68.50 ya fedha za miradi ambapo kumekuwa na ongezeko la asilimia 18.77 ya miradi hiyo, ukilinganisha na kipindi cha Julai-Septemba mwaka jana.

Mwakasege ameeleza hayo leo Februari 06,2024 wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao kwa kipindi cha robo tatu ya mwisho wa mwaka 2023 ambapo,miradi iliyohusika ni ya ujenzi wa miundombinu ya shule mpya za msingi na sekondari, maji, zahanati pamoja na ujenzi wa madarasa ya msingi na sekondari ili kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kuendana na thamani ya fedha iliyotumika.

Mwakasege amesema kuwa kwa kipindi hicho walipokea malalamiko 92 kati ya hayo 58 hayahusu rushwa ambapo 34 yanahusu rushwa na majalada yamefunguliwa ambapo 20 uchunguzi wake umekamilika na hatua stahiki zinatarajiwa kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria.

“Idara zilizolalamikiwa ni Halmashauri ambapo idara ya fedha kesi moja, Elimu 10, Afya saba, Utawala 12, Biashara moja, Kilimo nane, Ardhi saba, Mazingira tatu na mengine yalihusu sekta binafsi ambayo ni 12, ikiwemo  Maji tatu, Ujenzi tisa, Maliasili saba, Nishati moja, Uhamiaji mbili, Polisi nne, Mahakama tatu, Uchukuzi moja na mamlaka ya mapato Tanzania moja" ameeleza Mwakasege.

 Amesema katika progaramu ya Takukuru rafiki ambayo inatekelezwa kwa kushirikisha wadau katika ngazi ya kata ambapo wananchi hupata fursa ya kuibua kero zinazowakabili katika maeneo yao ambapo kwa kipindi cha Oktoba-Desemba walitembelea kata 11 na kupokea kero kuhusu sekta za Elimu, Afya, Maji, Fedha na Nishati ambapo ufuatiliaji wake unaendelea.

Aidha amevitaja vipaumbele vya Takukuru kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi mwaka huu ambavyo ni kuelimisha Umma kupitia njia mbalimbali ili kuongeza ushirikishwaji wa wananchi katika kuzuia vitendo vya rushwa, kutatua kero mbalimbali katika jamii kupitia programu ya Takukuru Rafiki na kuendelea kufuatilia rasilimali za Umma kupitia ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo ili kuzuia ufujaji wa fedha za Umma.

 Nyingine ni kufanya chambuzi za mifumo kwa lengo la kuzuia rushwa zinazosababishwa na mapungufu yaliyopo kwenye mifumo ya utendaji wa sekta ya Umma na sekta binafsi ambapo amewahimiza wasimamizi wa miradi ya maendeleo kuwa waadilifu na kuhakikisha fedha zote za miradi zinatumika vizuri.


Monday, February 5, 2024

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA MSD

 



Na. WAF, Dodoma

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI imeitaka Bohari ya Dawa (MSD) kuongeza ufanisi, ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha dawa zinanunuliwa, zinahifadhiwa sehemu sahihi, kusambaza dawa hizo kwa wakati katika sehemu zenye uhitaji na kukusanya madeni ili kuweza kuwa imara na taasisi endelevu.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI, Mhe. Stansilaus Nyongo baada ya kupokea taarifa ya hali ya utendaji na majukumu ya Bohari ya Dawa (MSD).

Mhe. Nyongo amesema kuwa wao kama wawakilishi wa wananchi wataendelea kuishinikiza serikali kuiwezesha MSD kupata mtaji ili kujiendesha kiufanisi katika kusambaza dawa kwa wakati.

“Bohari kuu ina majukumu ya kununua, kutengeneza, kuhifadhi dawa pamoja na kusambaza dawa katika vituo vya  vyote nchini”. Ameeleza  Mhe. Nyongo.

Mhe. Nyongo amesema kwa ujumla kamati imeridhishwa na hali ya utendaji wa Bohari ya Dawa na mipango yake ya utek