Posts

JKCI YAENDELEA KUWA LULU UTALII TIBA AFRIKA

Image
  Madaktari wake waitwa Zambia kufanya upasuaji wa moyo Na Mwandishi Wetu   Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya afya umeendelea kuipaisha Tanzania ambapo sasa madakati bingwa wanne wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete JKCI wako nchini Zambia wakiendelea  kufanya upasuaji wa moyo. Timu hiyo ya madakari hao itashirikiana na wenzao wa Hospitali ya Taifa ya Moyo ya Zambia na watafanyakazi upasuaji wa moyo kwa muda wa wiki moja . Mkuu wa ujumbe huo, Dk Viviane Mlawi wa (JKCI),  ambaye ni daktari bingwa wa moyo kwa watoto, alisema  ujumbe huo pia umeambatana na mtaalam mbobezi wa chumba cha upasuaji na mtaalamu wa usingizi katika upasuaji Moyo. Alisema wameambatana pia na mbobezi katika  kuhudumia wagonjwa wa nje wanaokuja kupata matibabu Tanzania,  Dk. Maiyer Msengi na wauguzi wawili ambao ni wabobezi wa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU). Dk Mlawi alisema malengo makubwa ya safari hiyo  ni matano ambayo ni kufanya u...

MAJID MWANGA AZINDUA SAMIA BODABODA DAY, MLELE.

Image
  Tarehe 23 September 2024 imekuwa ni siku ya neema na kukumbukwa kwa maafisa usafirishaji wa wilaya ya Mlele maarufu Kama bodaboda hii ni baada ya Ofisi ya mkuu wa wilaya ya mlele chini ya mkuu wa wilaya Mh Alhaj Majid mwanga kuandaa siku maalumu ya SAMIA BODABODA DAY iliyo fanyika halmashauri ya mlele shule ya msingi inyonga na kupambwa na kauli mbiu ya MIMI NI KIJANA WA SAMIA "nitashiriki uchaguzi wa serikali za mitaa November 27/ 2024 Siku hiyo maalumu ya boda boda Samia day imeyakutanisha makundi yote ya BODABODA kutoka pande zote za halmashauri ya mlele na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali Kama Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya mlele BI SIGILINDA MDEMU, Pia Wakuu mbalimbali wa taasisi, akiwemo mkuu wa kitengo cha usalama barabarani ambae alipata wasaa wa kutoa nasaha kwa madereva hawa wa bodaboda na kuwaasa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali mbazo zimekuwa zkijitokeza mara kwa mara kutokana na uzembe. Akizungumza katika si...

SERIKALI YAIPONGEZA GREEN ACRES KWA KUENDELEA NA KUFANYA VIZURI KITAALUMA.

Image
  Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeipongeza shule ya msingi na sekondari, Green Acres ya jijini Dar es Salaam kwa namna ambavyo imekuwa ikifanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa kuanzia ngazi ya Wilaya hadi taifa. Pongezi hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu wa Wizara ya Elimu,  Sayansi na Teknolojia, Victor George, wakati wa mahafali ya 24 ya  shule hiyo  yaliyohusisha wanafunzi wa awali, msingi na sekondari. “Nawapongeza sana kwa kuendelea kufanya vizuri kitaaluma na nawashauri muendelee kuwekeza kwa wanafunzi hawa maana bila hivyo hatuwezi kuwa na taifa bora la kesho na mmeweka miundombonu mizuri ambayo inawawezesha kusoma kwa utulivu,” alisema. Alisema serikali ya awamu ya sita imeweka kipaumbele kwenye kuwekeza kwenye ngazi zote za  elimu kuanzia awali, msingi sekondari, vyuo vikuu vikuu vya kati ili watoto wanaopata fursa ya kwenda huko kupata elimu bora. “Vijana huu ni mwanzo tu wa safari ndefu ya maisha, msione mmefi...

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MTYANGIMBOLE KWA NIABA YA MIRADI 30 YA MAJI MKOA WA RUVUMA.

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan leo September 24,2023 ameweka Jiwe la Msingi la Mradi wa Maji Mtyangimbole Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma kwa niaba ya Miradi 30 ya Maji inayotekelezwa Mkoani humo. Mradi wa tank la Maji Mtyangimbole una uwezo wa kupokea Lita milioni 1.9 na utahudumia Wananchi takribani 14,000.

NAIBU QADHI MKUU AMPONGEZA SHIRAZI KWA KUJENGA MSIKITI DAR ES SALAAM.

Image
  Na Mwandishi Wetu Naibu Qadhi Mkuu, Ali Khamis Ali amempongeza mfanyabiashara Shiraz Rashid kwa kujitolea kujenga Msikiti wa Imam Ali Bin Abu Talib eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam. Alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki wakati wa hafla ya uzinduzi wa Msikiti huo hafla ambayo ilihudhuriwa na wageni mbalimbali mbali wakiwemo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao. Alisema lengo la kujenga Msikiti huo ni kuhudumia waumini kwenye ibada ya swala tano na aliwashauri watanzania wengine kuiga mfano huo kwani hiyo ni kazi ya MwenyeziMungu. “Tunatoa wito watu wengine waige mfano wa Shiraz ili tujenge nyumba za ibada kwani nyumba hizi zinasaidia kurejesha utulivu na amani kwa watu kufanya ibada, huu ni moyo wa upendo wa ndugu yetu aliouonyesha kwa hiyo natoa wito kwa wengine waige,” alisema Naye Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh, Walid Kawambwa, alisema ujenzi wa Msikiti huo ni jambo jema na kuwataka watu wengine kuanzisha ujenzi kama huo kwani hiyo ni kazi ya MwenyeziMungu. “Mtume al...

WATOTO 1,500 WENYE MATATIZO YA MOYO WASUBIRI MSAADA.

Image
  Kikwete kuongoza harambee matibabu yao mwezi ujao Na Mwandishi Wetu RAIS mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, anatarajiwa kuongoza harambee ya kuchangia matibabu ya watoto 1,500 wanaougua magonjwa mbalimbali ya moyo ili wapate matibabu kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na Naibu Spika wa Bunge, Musa Azzan Zungu, wakati akizungumzia harambee hiyo inayotarajiwa kufanyika tarehe 2, Novemba mwaka huu kwenye hoteli ya Rotana jijini Dar es Salaam. Alisema takwimu za Wizara ya Afya zinaonyesha kuwa kati ya watoto 100 wanaozaliwa, wawili wanakuwa na matatizo ya moyo na kwamba hadi sasa watoto 1,500 wameandikishwa kwaajili ya kupata matibabu hayo lakini hawana uwezo. Naibu Spika ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Heart Team Africa Foundation, alisema watoto hao wasipopata matibabu hayo kwa wakati wanaweza kupoteza maisha hivyo aliwaomba watanzania kujitokeza wakati wa harambee hiyo kuwachangia matibabu. “Nawaomba wat...

MACHIFU WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUENZI UTAMADUNI.

Image
  Wasema atasaidia kurejesha maadili yanayoendelea kuporomoka Na Mwandishi Wetu VIONGOZI wa Kimila kutoka mikoa mbalimbali nchini, wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha Tamasha la Utamaduni la Kitaifa pamoja na kuongeza thamani ya viongozi wa mila iliyoonekana kushuka kwa miaka mingi. Wamesema hatua hiyo ya kuthamini, kufufua misingi na kuenzi tamaduni zilizokuwa zimeanza kuwekwa kando itasaidia kwa kiwango kikubwa kulinda maadili na tamaduni za Kitanzania. Wakizungumza kwa nyakati tofauti mkoani Ruvuma linakofanyika kongamano hilo la tatu la utamaduni la kitaifa, viongozi hao wa kimila wamesema kwa miaka mingi mila na tamaduni za Kitanzania zilionekana kutokuthaminiwa lakini Rais Samia ametambua umuhimu wake na kufufua. “Tunamshukuru Chifu Hangaya (Rais Samia), yeye kama kiongozi namba moja wa Machifu wote Tanzania, ameona umuhimu wa kuenzi mila na tamaduni zetu ambazo zilikuwa zimeachwa kupewa kipaumbele sana, kwa kifupi ni kwamba amezifufua na kuupa thamani kubwa u...

TASSIM YAANDAA MAONYESHO YA VIWANDA VIDOGO DODOMA.

Image
  Na  Mwandishi Wetu SERIKALI imewaalika wananchi na wadau mbalimbali kuhudhuria mkutano wa kukusanya maoni kuhusu Sera mpya ya biashara ndogo ndogo (SMEs) utakaofanyika mkoani Dodoma . Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. John  Simbachawene, wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa siku ya viwanda vidogo vidogo (TAMISID). Siku ya viwanda vidogo vidogo inayotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu mkoani Dodoma inaratibiwa na Chama cha Wenye Viwanda Vidogo Tanzania Association of Small Scale Industries and Manufacturers (TASSIM). Alisema serikali ilikusanya maoni ya watu mbalimbali kwenye awamu ya kwanza hivyo imeamua kuandaa mkutano wa awamu ya pili kuchukua maoni kwa wale ambao walikosa nafasi kwenye awamu ya kwanza. Alisema mkutano huo utafanyika wiki hii mkoani Dodoma na kuwataka wananchi,  wajasiriamali, wafanyabiashara kushiriki kwenye mkutano huo ili watoe maoni ya kuchangia kuboresha sera hiyo. “Wizara inaendelea...

RAIS SAMIA AKUTANA NA MKUU WA JESHI LA POLISI IGP WAMBURA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura pamoja na Makamishna wa Jeshi hilo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 20 Septemba, 2024 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura pamoja na Makamishna wa Jeshi hilo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 20 Septemba, 2024

TAMASHA LA UTAMADUNI KITAIFA LAFUNGULIWA SONGEA.

Image
Na Mwandishi Wetu, RUVUMA WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro amewaasa watanzania kuzingatia miiko, mila na desturi za kitanzania na kuwarithisha watoto na vijana ili kujiepusha na tamaduni za kigeni zisizofaa kwa jamii. Aidha, ameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuwachukulia hatua kali wale wanaoua mila na desturi za watanzania kwenye mitandao ya kijamii. Akizindua Tamasha la tatu la Utamaduni Kitaifa kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea, alisema kusipokuwa na utamaduni hakutakuwa na utu na wasipouenzi hawatauendeleza. “Ili Taifa liwe hai lazima tuenzi na kuendeleza utamaduni wetu, na lazima turithishe utamaduni wetu kwa vijana na watoto na lazima tuwafundishe watoto wetu mila na desturi za kitanzania, Kiswahili tuwafundishe miiko mbalimbali na historia yetu kwa kuwa hawa watoto ni taifa la kesho,”alisema. Alisema katika maadhimisho ya tamasha hilo ilitolewa semina ya maadili na utamaduni iliyofundisha jinsi ya kuenzi utamaduni na namna ya kukabilia...