Tuesday, September 24, 2024

NAIBU QADHI MKUU AMPONGEZA SHIRAZI KWA KUJENGA MSIKITI DAR ES SALAAM.

 

Na Mwandishi Wetu


Naibu Qadhi Mkuu, Ali Khamis Ali amempongeza mfanyabiashara Shiraz Rashid kwa kujitolea kujenga Msikiti wa Imam Ali Bin Abu Talib eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam.


Alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki wakati wa hafla ya uzinduzi wa Msikiti huo hafla ambayo ilihudhuriwa na wageni mbalimbali mbali wakiwemo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao.


Alisema lengo la kujenga Msikiti huo ni kuhudumia waumini kwenye ibada ya swala tano na aliwashauri watanzania wengine kuiga mfano huo kwani hiyo ni kazi ya MwenyeziMungu.


“Tunatoa wito watu wengine waige mfano wa Shiraz ili tujenge nyumba za ibada kwani nyumba hizi zinasaidia kurejesha utulivu na amani kwa watu kufanya ibada, huu ni moyo wa upendo wa ndugu yetu aliouonyesha kwa hiyo natoa wito kwa wengine waige,” alisema


Naye Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh, Walid Kawambwa, alisema ujenzi wa Msikiti huo ni jambo jema na kuwataka watu wengine kuanzisha ujenzi kama huo kwani hiyo ni kazi ya MwenyeziMungu.


“Mtume alipoingia Madina alijenga Msikiti kwanza kwa maana kwamba ile ni sehemu ya Waislamu kukutana na kujadiliana na washirikiane kufanya mambo yao pale kwa hiyo namshukuru Shiraz kwa kunialika kuja kwenye ufunguzi huu,” alisema Sheikh Walid







Picha mbalimbali za ufunguzi wa Msikiti wa Imam Ali Bin Abu Talib eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam, 

No comments:

Post a Comment