Tuesday, September 24, 2024

MAJID MWANGA AZINDUA SAMIA BODABODA DAY, MLELE.

 

Tarehe 23 September 2024 imekuwa ni siku ya neema na kukumbukwa kwa maafisa usafirishaji wa wilaya ya Mlele maarufu Kama bodaboda hii ni baada ya Ofisi ya mkuu wa wilaya ya mlele chini ya mkuu wa wilaya Mh Alhaj Majid mwanga kuandaa siku maalumu ya SAMIA BODABODA DAY iliyo fanyika halmashauri ya mlele shule ya msingi inyonga na kupambwa na kauli mbiu ya MIMI NI KIJANA WA SAMIA "nitashiriki uchaguzi wa serikali za mitaa November 27/ 2024



Siku hiyo maalumu ya boda boda Samia day imeyakutanisha makundi yote ya BODABODA kutoka pande zote za halmashauri ya mlele na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali Kama Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya mlele BI SIGILINDA MDEMU, Pia Wakuu mbalimbali wa taasisi, akiwemo mkuu wa kitengo cha usalama barabarani ambae alipata wasaa wa kutoa nasaha kwa madereva hawa wa bodaboda na kuwaasa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali mbazo zimekuwa zkijitokeza mara kwa mara kutokana na uzembe.


Akizungumza katika siku hiyo maalum ya SAMIA BODABODA DAY, Mkuu wa wilaya ya Mlele Alhaj Majid Mwanga amewataka vijana wilayani humo kuweka kumbukumbu ya tarehe ya uchaguzi wa serikali za mitaa ili kila mmoja aweze kushiriki.



Alisema usoefu unaonyesha vijana wengi hawajitokezi kupiga kura jambo ambalo wanajinyima haki yao kikatiba ya kuwachagua viongozi wanaowataka ili wawaletee maendeleo.


Aliongeza kwa kusema kuwa vijana wa wilaya ya Mlele wanapaswa kutambua kuwa wana mambo matatu ya kufanya katika uchaguzi wa serikali za mitaa unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba.


Majid Mwanga, ameyataja mambo matatu hayo kuwa ni viajna waombe nafasi za kugombea nafasi za uongozi, wajiandikishe na kisha wakapige kura siku ya uchaguzi.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele Bi Sigilinda Mdemu, amesema ni matumaini yake kuwa vijana watajitokeza kupiga kura ili kuchagua viongozi wao 


Kwa upande wao vijana hao wa bodaboda wamesema wamefurahishwa sana na kitendo cha kuwakusanya pamoja na kufanya siku maalum kwao jambo lilioongeza upendo na mshikamano baina yao na serikali pia.


Aidha, wameomba ushirikiano huo uendelee kila siku na kujenga mahusiano mema baina ya waendesha bodaboda na mkuu wa usalama barabarani wilaya (DTO) ili vijana waweze kupata elimu ya usalama barabarani mara kwa mara.













No comments:

Post a Comment