Thursday, August 3, 2023
Wednesday, August 2, 2023
DIWANI AWAKUMBUSHIA WALIMU UTUMISHI BORA
MGOGORO WAMALIZIKA MKANGE; WANANCHI WARIDHIA UJENZI WA BARABARA UENDELEE
Mkange, Chalinze
Mgogoro uliosababisha kusimama kwa utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Afrika ya Mashariki katika kata ya Mkange , umemalizika leo baada ya wananchi wa kata hiyo kukubali kupokea fidia na kupisha ujenzi wa barabara hiyo baada ya kukutana na Mbunge wa jimbo hilo la Chalinze Ndg . Ridhiwani Kikwete.
Mbunge huyo Ndg. Kikwete, ameeleza kufurahishwa kwake na kauli hiyo ya wananchi na amekielezea kitendo hicho kuwa cha kiungwana sana . Akieleza kwenye mkutano huo , Mbunge ameeleza kuwa maamuzi yaliyofikiwa ni wazi yanafungua sio tu milango ya maendeleo katika ukanda huu lakini pia ni ufunguzi mkubwa wa fursa za kukuza kiuchumi kwa wananchi hao.
Wakiongea katika nyakati tofauti, wananchi wa kata hiyo wamemshukuru Mbunge wao kwa kuingilia kati ili kulipatia ufumbuzi jambo Hilo lililodumu kwa muda mrefu. Pia wananchi hao walimshukuru Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia malipo hayo ya fidia.
MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA BARABARA YA INYALA MKOANI MBEYA
Tuesday, July 18, 2023
DKT. KIDA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA BIASHARA NA UWEKEZAJI WA EAC
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida ameongoza ujumbe wa Serikali ya Tanzania kushiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Biashara na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi ya Marekani.
Mkutano huo umefanyika Julai 18, 2023 nchini Kenya ambapo Dkt. Kida amemwakilisha Waziri wa Ofisi hiyo Prof. Kitila Mkumbo ambapo Marekani na Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zimejadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara na kuvutia uwekezaji.
Aidha, wamejadiliana kutumia kikamilifu fursa za soko la mpango wa AGOA nchini Marekani, Mkataba wa eneo huru la biashara Afrika (AfCFTA) na mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Wengine waliohudhuria mkutano huo ni Mwakilishi wa Biashara wa Serikali ya Marekani Mhe. Balozi Katherine Tai, Mawaziri wa Biashara na Uwekezaji wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na sekta binafsi ya Tanzania imewakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Raphael Maganga.

Monday, February 20, 2023
SERIKALI KUJENGA VETA KILA WILAYA.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda, akizungumza wakati alipotembelea Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo mjini Bagamoyo.
........................................................................
Na Athumani Shomari.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan itajenga vyuo vya VETA katika kila wilaya nchini.
Waziri, Prof. Mkenda aliyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizungumza katika ziara aliyoifanya Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo mjini Bagamoyo, ambapo alisema Rais Samia tayari ameilekeza Wizara ya Elimu kuwa, kila wilaya iwe na chuo cha VETA.
Alisema tayari wizara ya elimu imejipanga kutekeleza maelekezo ya Rais samia ya kujenga chuo cha VETA kila wilaya ambapo wilaya zote 64 zitajengwa kwa mkupuo pamoja na kimoja kitakachojengwa mkoani Sngwe.
Prof Adolf Mkenda, aliyasema hayo kufuatia ombi la Mbunge wa Bagamoyo, Muharam Mkenge aliyemuomba Waziri huyo wa Elimu kujenga chuo cha VETA katika jimbo la Bagamoyo ili vijana wa Bagamoyo waweze kujifunza fani mbalimbali katika chuo hicho.
Mkenge alisema kwa sasa Bagamoyo inakuwa kwa kasi katika uwekezaji wa viwanda na kutoa fursa mbalimbali kwa vijana wazawa wenye ujuzi wa fani mbalimbali na kuongeza kuwa fursa hizo hazitakuwa na faida kwa vijana wa Bagamoyo ikiwa hawatakuwa na ujuzi wa fani yoyote.
Aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa kuna ushindani mkubwa katika soko la ajira hivyo uwepo wa chuo cha VETA chenye kutoa ujuzi wa aina mbalimbali kutasaidia kwaa vijana wa Bagamoyo kukabiliana na ushindani katika soko la ajira na kufaidika na uwekezaji unaofanyika katika jimbo hilo.
Alisema tayari mchakato wa kupata eneo la kujenga chuo hicho kwa Bagamoyo umeshakamilika na kupata eneo lenye ukubwa ekari 38 ambzo zitatumika kujenga chuo cha VETA.
Aidha, Mbunge Muharam Mkenge alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuelekeza fedha za elimu katika jimbo la Bagamoyo hali iliyopelekea kuanzishwa kwa shule mpya za sekondari ambazo zimesaidia kuwapungzia watoto kwenda umbali mrefu kufika shuleni.
Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, akizungumza mbele ya Waziri wa Elimu, katika Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo mjini Bagamoyo.


Katikati ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda, wakwanza kulia ni Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Utawala wa ADEM, Dkt. Emanuel Molel, wa pili kulia ni Mwakilishi wa Kamishna wa Elimu, Bw. Manori Venance, na watatu kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya ushauri ADEM, Dkt. Naomi Katunzi, kutoka kushoto wa kwanza ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, wapili kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Halima Habib Okash, na watatu kushoto ni Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Siston Masanja.














