Wednesday, August 2, 2023

DIWANI AWAKUMBUSHIA WALIMU UTUMISHI BORA


 NA. ELISANTE KINDULU, CHALINZE


DIWANI wa kata ya Bwilingu ,katika halmashauri ya Chalinze mkoa wa Pwani, Mh. Nassar Karama amesisitiza walimu kufanya kazi kwa bidii na kufuata kanuni za Utumishi wa umma ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Mh. Nassar ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na walimu wa shule ya msingi Kibiki katika kata ya Bwilingu, alipowatembelea leo shuleni hapo.

Mh. Nassar amesema Jambo pekee linalomjengea mwalimu heshima ni pamoja uadilifu na ufanisi katika kazi yake ya ualimu vitakavyomfanya kuepuka migogoro na mwajiri wake.

Aidha Mh.Nassar amesema Kuwa kata yake bado inauhitaji mkubwa wa shule shikizi kutokana na wanafunzi wengi kusafiri umbali mrefu kufuata shule kongwe Mahali zilipo.

" Mfano Maeneo ya Kibiki Maziwa na Kitoho Kuna wimbi kubwa la wanafunzi kutembea umbali mrefu kuja kusoma hapa. Lazima tuone namna ya kuanzisha miradi ya Ujenzi wa shule kwenye maeneo yenye changamoto", alisema Diwani huyo.

 Mh. Diwani aliuelekeza uongozi wa shule hiyo kuitisha vikao vya wazazi na wadau wa maendeleo ya elimu kwa ajili ya uhamasishaji wa kuwapatia watoto chakula shuleni, kuhimiza maadili pamoja na masuala ya kitaaluma.

Katika ziara hiyo walimu walitoa changamoto mbalimbali za kikazi zinazowakabili ikiwamo uhaba wa nyumba za walimu, uzio na kuwepo barabara inayopita pembezoni mwa eneo la shule ambayo jamii itakuwa ikiitumia badala ya barabara ya Sasa ambayo inapita katikati ya viwanja vya shule hiyo 










MGOGORO WAMALIZIKA MKANGE; WANANCHI WARIDHIA UJENZI WA BARABARA UENDELEE

Mkange, Chalinze


Mgogoro uliosababisha kusimama kwa utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Afrika ya Mashariki katika kata ya Mkange , umemalizika leo baada ya wananchi wa kata hiyo kukubali kupokea fidia na kupisha ujenzi wa barabara hiyo baada ya kukutana na Mbunge wa jimbo hilo la Chalinze Ndg . Ridhiwani Kikwete.


Mbunge huyo Ndg. Kikwete, ameeleza kufurahishwa kwake na kauli hiyo ya wananchi na amekielezea kitendo hicho kuwa cha kiungwana sana . Akieleza kwenye mkutano huo , Mbunge ameeleza kuwa maamuzi yaliyofikiwa ni wazi yanafungua sio tu milango ya maendeleo katika ukanda huu lakini pia ni ufunguzi mkubwa wa fursa za kukuza kiuchumi kwa wananchi hao.


Wakiongea katika nyakati tofauti, wananchi wa kata hiyo wamemshukuru Mbunge wao kwa kuingilia kati ili kulipatia ufumbuzi jambo Hilo lililodumu kwa muda mrefu. Pia wananchi hao walimshukuru Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia malipo hayo ya fidia.





 

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA BARABARA YA INYALA MKOANI MBEYA


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akikagua Barabara ya mchepuko katika mlima Inyala mkoani Mbeya
....................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameupongeza uongozi wa Wakala ya Barabara nchini (TANROAD) pamoja na Mkoa wa Mbeya kwa usimamizi mzuri na kukamilisha ujenzi wa barabara ya mchepuko katika eneo la mlima wa Inyala mkoani Mbeya.
 
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akikagua barabara ya mchepuko katika Mlima Inyala iliogharimu shilingi bilioni 6.9 leo tarehe 01 Agosti 2023. Amesema eneo hilo lilikuwa likikabiliwa na ajali nyingi zilizogharimu Maisha ya watu hivyo kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo utasaidia katika kukabiliana na adha hiyo.
 
Makamu wa Rais ametoa rai kwa madereva na watumiaji wa vyombo vya moto nchini kuwa waangalifu na kufuata sheria za usalama barabarani ili kunusuru Maisha ya watumiaji wa barabara. Ametoa wito kwa madereva kujenga utaratibu wa kukagua magari mara kwa mara ili kuepusha ajali zinazoweza kujitokeza kutokana na ubovu wa vyombo vya moto.
 
Aidha Makamu wa Rais amewataka askari wa usalama barabarani kufanya kazi kwa uadilifu kwa kusimamia sheria za usalama barabarani ili kulinda Maisha ya wananchi wanaotumia barabara hizo.
 
Septemba 11 mwaka 2022 Makamu wa Rais alitembelea eneo la Inyala na kuagiza mambo mbalimbali ili kukabiliana na ajali zilizokuwa zinajitokeza katika eneo hilo ikiwemo kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya mchepuko katika mlima Inyala, kupanua ukubwa wa barabara kutoka mita 6.7 hadi mita 10.5 pamoja na kuweka taa za barabarani katika eneo la kukagulia magari.
 
Halikadhalika Makamu wa Rais amekagua ujenzi wa Zahanati ya Shamwengo iliopo eneo la Inyala ambayo mwaka 2022 aliagiza ikamilishwe ili kusaidia majeruhi waliokuwa wanapata ajali katika mlima Inyala.

Amesema ameridhishwa kwa kukamilika kwa zahanati hiyo na kuwapongeza wananchi wa eneo hilo kwa kujitoa kusaidia watu waliokuwa wakipata ajali katika eneo la mlima Inyala. Ameongeza kwamba serikali itapeleka shilingi milioni 110 kwaajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa katika zahanati hiyo.
 












Tuesday, July 18, 2023

DKT. KIDA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA BIASHARA NA UWEKEZAJI WA EAC

 No description available.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida ameongoza ujumbe wa Serikali ya Tanzania kushiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Biashara na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi ya Marekani.

Mkutano huo umefanyika Julai 18, 2023 nchini Kenya ambapo Dkt. Kida amemwakilisha Waziri wa Ofisi hiyo Prof. Kitila Mkumbo ambapo Marekani na Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zimejadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara na kuvutia uwekezaji.

Aidha, wamejadiliana kutumia kikamilifu fursa za soko la mpango wa AGOA nchini Marekani, Mkataba wa eneo huru la biashara Afrika (AfCFTA) na mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wengine waliohudhuria mkutano huo ni Mwakilishi wa Biashara wa Serikali ya Marekani Mhe. Balozi Katherine Tai, Mawaziri wa Biashara na Uwekezaji wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na sekta binafsi ya Tanzania imewakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Raphael Maganga.

No description available.

Monday, February 20, 2023

SERIKALI KUJENGA VETA KILA WILAYA.

 No description available.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda, akizungumza wakati alipotembelea Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo mjini Bagamoyo.

........................................................................

Na Athumani Shomari.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan itajenga vyuo vya VETA katika kila wilaya nchini.

Waziri, Prof. Mkenda aliyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizungumza katika ziara aliyoifanya Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo mjini Bagamoyo, ambapo alisema Rais Samia tayari ameilekeza Wizara ya Elimu kuwa, kila wilaya iwe na chuo cha VETA.

Alisema tayari wizara ya elimu imejipanga kutekeleza maelekezo ya Rais samia ya kujenga chuo cha VETA kila wilaya ambapo wilaya zote 64 zitajengwa kwa mkupuo pamoja na kimoja kitakachojengwa mkoani Sngwe.

Prof Adolf Mkenda, aliyasema hayo kufuatia ombi la Mbunge wa Bagamoyo, Muharam Mkenge aliyemuomba Waziri huyo wa Elimu kujenga chuo cha VETA katika jimbo la Bagamoyo ili vijana wa Bagamoyo waweze kujifunza fani mbalimbali katika chuo hicho.

Mkenge alisema kwa sasa Bagamoyo inakuwa kwa kasi katika uwekezaji wa viwanda na kutoa fursa mbalimbali kwa vijana wazawa wenye ujuzi wa fani mbalimbali na kuongeza kuwa fursa hizo hazitakuwa na faida kwa vijana wa Bagamoyo ikiwa hawatakuwa na ujuzi wa fani yoyote.

Aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa kuna ushindani mkubwa katika soko la ajira hivyo uwepo wa chuo cha VETA chenye kutoa ujuzi wa aina mbalimbali kutasaidia kwaa vijana wa Bagamoyo kukabiliana na ushindani katika soko la ajira na kufaidika na uwekezaji unaofanyika katika jimbo hilo.

Alisema tayari mchakato wa kupata eneo la kujenga chuo hicho kwa Bagamoyo umeshakamilika na kupata eneo lenye ukubwa ekari 38 ambzo zitatumika kujenga chuo cha VETA.

Aidha, Mbunge Muharam Mkenge alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuelekeza fedha za elimu katika jimbo la Bagamoyo hali iliyopelekea kuanzishwa kwa shule mpya za sekondari ambazo zimesaidia kuwapungzia watoto kwenda umbali mrefu kufika shuleni.

No description available.

Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, akizungumza mbele ya Waziri wa Elimu, katika Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo mjini Bagamoyo.

No description available.No description available.

 Katikati ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda, wakwanza kulia ni Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na Utawala wa ADEM, Dkt. Emanuel Molel, wa pili kulia ni Mwakilishi wa Kamishna wa Elimu, Bw. Manori Venance, na watatu kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya ushauri ADEM, Dkt. Naomi Katunzi, kutoka kushoto wa kwanza ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, wapili kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Halima Habib Okash, na watatu kushoto ni Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Siston Masanja.

 No description available.

No description available.