Thursday, October 3, 2024

NACHINGWEA KUFANYA BONANZA LA KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA

 

Na Mwandishi wetu, Lindi.


Kuelekea Uchaguzi wa Serikali za mitaa, vijiji na vitongoji unaotarajiwa kufanyika November 27 mwaka huu Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi inatarajia kufanya bonanza la kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kikamilifu Katika uchaguzi huo



Akizungumza na mwandishi wetu, kaimu mkurugenzi  halmashauri hiyo Joshua Mnyang'ali alisema kuwa bonanza hilo litafanya siku ya jumamosi 5/10/2024 katika uwanja wa majengo ambao michezo mingi itafanyika huku kukiwa na  wasanii mbalimbali wakipamba jukwaa la burudani kwa wakazi wa wilaya ya Nachingwea.


Amesema bonanza hilo linalenga kutoa elimu ya kushiriki kikamilifu uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji katika wilaya ya Nachingwea, kuhamasisha maswala ya Amani pamoja na kuelezea shughuli mbalimbali za Maendeleo zilizofanywa na serikali


Mwenyekiti wa halmashauri ya Nachingwea Adinani mpyagila ametoa wito kwa wananchi wa Nachingwea pamoja na wa Maeneo jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki bonanza Hilo kubwa 



No comments:

Post a Comment