Friday, January 12, 2018

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATOA SIKU 18 BAGAMOYO KUPIGA CHAPA NG'OMBE..

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallaah Ulega ametoa siku 18 kwa Halmashauri ya Bagamoyo kukamilisha zoezi la upigaji chapa mifugo ili kuondoa usumbufu baina ya wafugaji na jamii ya wananchi wengine.

Kauli hiyo ameitoa mjini Bagamoyo alipokuwa akizungumza katika kikao kilichowajumuisha wakuu wa idara, viongozi wa uvuvi na wananchi wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

Ulega alisema zoezi la upgaji chapa ni agizo la serikali na kwamba mtumishi yeyote atakaeshindwa kutimiza wajibu wake katika kutekeleza majukumu yake atachukuliwa hatua za kinidhamu.

Aidha, aliwaonya maafisa mifugo wanaoshindwa kutekeleza agizo hilo wakidhani ni swala la kisiasa hatua kali zitachukuliwa dhidi yao kwa kuaidi amri halali ya serikali ya kutaka Ng'ombe wote kupigwa chapa.

Alisema zoezi hilo likikamilika litasaidia kuondoa uvamizi holela wa wafagaji katika maeneo mbalimbali kwakuwa Ng'ombe wote watafahamika asili ya eneo lao la makazi na hivyo kuondoa kabisa migogoro ya wafugaji na wakulima inayosababishwa na wafugaji kuhama hama bila ya utaratibu maalum.

Kufuatia agizo hilo Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga ametoa siku mbili  kwa maafisa mifugo wa Halmashauri ya Bagamoyo kuwasilisha mpango wa utekelezaji wa agizo la kupiga chapa mifugo.

Majid amemuhakikishia naibu waziri kutekeleza agizo hilo kupitia wataalamu wa idara ya mifugo ndani ya Halmashauri ya Bagamoyo.

Awali akisoma taarifa kwa Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Fatuma Latu amesema Halmashauri ya Bagamoyo ina jumla ya Ng'ombe elfu ishirini na nane mia tano thelasini na nne 28,534,  kati yao Ng'ombe 9,914  tu ndio waliopigwa chapa ambapo sawa na asilimia 34 tu ya ng'ombe wote waliopo ndani ya Halmashauri hiyo.


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga akizungumza na katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo mbele ya Naibu waziri wa mifugo. 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Fatuma Omari Latu akizungumza katika uukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo mbele ya naibu waziri wa Mifugo na Uvuv, Abdallah Hamisi Ulega.

 

No comments:

Post a Comment