Thursday, January 4, 2018

DC BAGAMOYO AZINDUA CHANJO YA VITAMIN "'A'' HALMASHAURI YA CHALINZE


 Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo Alhaj, Majid Mwanga, akimpatia mtoto dawa ya vitamin A ikiwa ni ishara ya kuzindua chanjo ya vitamin A na dawa za minyoo katika kituo cha Afya Chalinze.
Mkuu wa  wilaya ya Bagamoyo Alhaj, Majid Mwanga amezindua chanjo ya vitamin A na dawa za minyoo katika Halmashauri ya Chalinze.

Ktika uzinduzi huo mkuu huyo wa wilaya amewapongeza watumishi wa Afya katika Halmashauri ya Chalinze ambao wanafanya kazi kwa kujituma huku akiwataka kuongeza juhudi katika kuwahudumia wananchi.

Aidha, amewataka wale wenye tabia ya kutoa lugha kali kwa wagonjwa kuacha mara moja na badala yake wazingatie kanuni na taratibu za kazi yao katika kutekeleza majukumu yao ya kitaalamu.

Majid aliongeza kwa kuwataka wazazi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo ya vitamin A na na dawa za minyoo ili kuwaepusha na magonjwa ambayo yanaweza kuzuilika.

wakati huohuo aliwataka kinamama kufika mapema katika vituo vya Afya na Zahanati kwaajili ya vipimo ili kubaini endapo kuna tatizo kwa mtoto aliyopo tumboni liweze kushughulikiwa mapema.

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Mratibu wa Afya Halmashauri ya Chalinze, Dkt. Miriamu Malekela alisema zoezi linaloendelea katika vituo vya kutolea huduma za Afya na kwamba linatarajia kukamilika Januari 17, 2018

Baadhi ya wazazi waliofika kituo cha Afya Chalinze kuwapatia watoto wao chanjo ya vitamin A na dawa za minyoo.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, Majid Mwanga akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kituo cha Afya Chalinze.

No comments:

Post a Comment