Thursday, January 18, 2018

MARUFUKU KUWACHANGISHA MICHANGO WANAFUNZI- RC PWANI.


Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo amesema mwalimu Mkuu yeyote atakayechangisha michango kwa wanafunzi na kupelekea uzito wa kwa wazazi na walezi kuwapeleka watoto shule atachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kazi.
Hayo aliyasema jana Tarehe 17 Januari 2018, wilayani Bagamoyo alipofanya ziara katika Halmashauri ya Chalinze ambapo alitembelea shule ya Sekondari Mboga ili kuoana idadi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza amba wmeripoti shuleni hapo.
Alisema Rais Dkt. John Magufuli ametangaza elimu bure kwa wananchi wote hivyo haipaswi kwa mtu yeyote kukwamisha dhamira ya Rais magufuli ya kutoa elimu bure.
Alisema wapo baadhi ya walimu wakuu wamekuwa kikwazo cha watoto kwendda shule kwa kuwapa orodha kubwa ya mahitaji hali inayopelekea kuondoa dhana nzima ya elimu bure kwa wananchi.
Alisema ni marufuku kwa walimu wakuu wote mkoani Pwani kuweka masharti kwa mwanafunzi kuripoti shule kwa nama yeyote ile.
Aidha, Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani alitoa siku saba kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa wanaripoti shule na kwamba kata ambayo itashindwa kutekeleza hilo Mratibu elimu kata atasimamishwa kazi.
Wakitoa taarifa ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2018 mbele ya Mkuu wa Mkoa maafisa elimu wa Halmashauri ya Bagamoyo na Chalinze wamesema mpaka sasa wanafunzi walioripoti shuleni kwa Halmashuri ya Chalinze ni asilimia 50. 63 na Halmashauri ya Bagamoyo ni asilimia 43.48 tu.

No comments:

Post a Comment