Sunday, December 31, 2017

SUBIRA MGALU ATOA AGIZO KWA TANESCO.



 Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wilayani Bagamoyo kwa nyakati tofauti katika ziara yake ya siku mbili aliyoianza jana Tarehe 30 Desemba 2017 na leo Tarehe 31 Desemba 2017.
...........................
Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewataka mameneja wa Tanesco mikoa na wilaya kote nchini kuwaunganishia umeme wananchi wakaokuwa wameomba na kukamilisha malipo yao ndani ya siku saba tu.

Agzo hilo amelitoa wilayani Bagamoyo alipokuwa katika ziara ya kukagua mradi wa kusambaza umeme vijijini REA awamu ya tatu unaotekelezwa nchi nzima.

Alisema kila meneja wa TANESCO anatakiwa kuhakikisha kuwa, wateja wote waliojaza fomu na kukamilisha malipo yao wanatakiwa kuunganishwa umeme ndani ya siku saba tu ili kuondoa usumbufu kwa wananchi wa kusubiri kuunganishiwa umeme kwa muda mrefu.

Aidha, alisema kufuatia agizo hilo atafanya ziara kwenye ofisi za TANESCO nchi nzima ili kuona idadi ya wananchi walioomba na kulipia huduma ya umeme na idadi ya waliounganishwa na kwamba meneja atakaeshindwa kutekeleza hilo anapaswa kutoa maelezo juu ya kwanini mteja hakuunganishiwa umeme ndani ya siku saba toka kulipia kwakwe.

Naibu waziri huyo wa Nishati amewataka Wananchi waliopo kwenye vijiji vinavyopitiwa na mradi wa kusambaza umeme vijijini REA wametakiwa kutumia fursa ya mradi huo kuchukua fomu na kulipia gharama ya shilingi elfu ishirini na saba tu ili waunganishiwe umeme kupitia REA awamu ya tatu.

Alisema Serikali imewathamini wananchi wake kwa kuwepelekea mradi wa kusambaza umeme vijijini REA ili kila mwananchi apate huduma hivyo ni matarajio ya serikali kuona fursa hiyo inatumika vizuri.

 Kwa upande wao wabunge wa jimbo la Bagamoyo na Chalinze wamempongeza Naibu waziri huyo wa kwanza mwanamke katika wizara ya nishati kwa kujali wananchi na kuwatembelea vijijini.

Dkt. Shukuru Kawambwa Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo amesema kufika kwa naibu waziri huyo vijijini kutampunguzia maswali anayoulizwa na wananchi kuhusu vijiji ambavyo havijafikiwa na umeme.

Nae mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amesema wananchi wanajenga imani na serikali yao ya awamu ya tano hasa pale wanpoona kiongozi kama Naibu waziri anawatembelea na kusikiliza vilio vya wananchi
Alisema mfumo huo unawafanya wananchi kuimanini serikali yao hasa pale ilani ya chama Cha mapinduzi inatekelezwa kwa vitendo.

Wakati huo huo Naibu waziri wa Nishati huyo amewahakikishaia wananchi wa Kijiji cha Kongo kata ya Yombo wilayani Bagamoyo, kuwa watapata umeme katikati ya januari 2018 ili kuwaondolea kero ya kukosa umeme katika kijiji hicho kwa zaidi ya miaka 40 sasa.

Katika hatua nyingine Naibu waziri wa nishati ambae ni Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani amechangia shilingi laki mbili kwaajili ujenzi wa ofisi ya CCM katika kijiji cha Kongo kata ya Yombo wilayani Bagamoyo.

Mradi wa kusambaza umeme vijijini REA awamu ya tatu mzunguuko wa kwanza unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni 2019 kwa kufikisha umeme katika vijiji 3559 ambapo REA awamu ya tatu mzunguuko wa pili unatarajiwa kuanza kutekelezwa 2019-2021 ili kutekeleza lengo la serikali la kuvipatia umeme vijiji vyote 7873 vilivyobaki ifkapo mwaka 2021.


 Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wilayani Bagamoyo kwa nyakati tofauti katika ziara yake ya siku mbili aliyoianza jana Tarehe 30 Desemba 2017 na leo Tarehe 31 Desemba 2017.
Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akitoa maelekezo kuhusu nguzo za umeme zilizokaa kwa muda mrefu katika kijiji cha Kongo kata ya Yombo wilayani Bagamoyo.
Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akipokea na kusoma mabango yaliyowasilishwa kwake na wananchi wa kijiji cha Kongo kata ya Yombo Halmashauri ya Bagamoyo wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani wakilalamikia kukosa umeme kwa zaidi ya miaka 40 sasa licha ya kuwa kijiji hicho ndicho chenye mtambo maji wa Ruvu chini.

Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akisikiliza maelezo ya kitaalamu kutoka kwa Msimamizi wa Miradi ya umeme vijijini REA Mkoa wa Pwani Mhandisi Mohamed Sauko (Kushoto) kushoto mwa Naibu waziri ni Meneja wa TANESCO wilaya ya Bagamoyo Daniel Michael Kyando, na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa.

No comments:

Post a Comment