Posts

TANZANIA KUPATA DOLA MILIONI 41 ZA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIANCHI

Image
  Tanzania kupata dola milioni 41 za uhifadhi wa bioanuwai, kuhimili mabadiliko ya tabianchi Tanzania inatarajiwa kunufaika na takribani Dola za Marekani milioni 41 kupitia madirisha mbalimbali ya ufadhili wa Global Environment Facility (GEF), kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi wa bioanuwai, urejeshwaji wa mifumo ikolojia na kujenga ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Hayo yamebainika katika mazungumzo kati ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi na Mratibu wa Bioanuwai wa GEF kwa Afrika, Bw. Jurgis Sapijanskas, yaliyofanyika Nairobi, Kenya, pembezoni mwa mikutano ya SBSTTA-28 na SBI-7 mwishoni mwa wiki. Katika mazungumzo hayo, imeelezwa kuwa takribani Dola za Marekani milioni 16 zimetengwa kupitia dirisha ya GEF – Trust Fund katika Mzunguko wa 9 (GEF-9), huku fursa nyingine zikijumuisha Dola milioni 20 kupitia Mfuko wa Least Developed Countries Fund (LDCF) kwa ajili ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, pamoja na Dola milioni...

NCHIMBI AMTEMBELEA KIKWETE NYUMBANI KWAKE

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, katika makazi yake, Kawe Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 10 Agosti 2026.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 10 AGOSTI 2026

Image
 

MRADI WA BOMBA LA MAFUTA MULEBA KUKAMILIKA SEPTEMBA-TPDC

Image
  Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Derick Moshi akizungumza na waandishi wa habari katika Kituo kilichopo Kijiji cha Kikagate, Kata ya Mubunda wilaya ya Muleba ................................ Na Alodia Dominick, Muleba Mradi wa bomba la mafuta uliotarajiwa kukamilika mwezi Julai mwaka huu  umekwama kukamilika kutokana na vipuli vinavyotoka nje ya nchi kutofika kwa wakati. Vipuli hivyo ambavyo havikutajwa vinatoka nchi gani vimekwamisha kuanza kusukumwa kwa mafuta ambayo yalitarajiwa kuanza kusukumwa mwezi Julai mwaka huu katika kituo cha Muleba   badala yake mradi huo utakamilika rasmi mwishoni mwa mwezi Agosti au mwanzoni mwa Septemba 2026. Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Derick Moshi, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, amesema kuwa, mradi wa bomba la mafuta ulitarajiwa kukamilika rasmi mwezi Julai mwaka huu lakini kutokana na vipuli ambavyo vinapaswa ...

SUBIRA MGALU KWENYE KILELE CHA NANENANE MOROGORO

Image
  Mbunge wa jimbo la Bagamoyo Mh. Subira Mgalu, ametembelea wajasiriamali, wakulima, wafugaji na wavuvi katika kilele cha maonesho ya wakulima nanenane 2026 kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro. Mgalu amewapongeza wote kwa juhudi zao za kukuza uchumi kupitia kilimo, ufugaji na uvuvi na kusema kuwa serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan inaunga mkono juhudi za wakulima ndiomana imetenga fungu maalum litakalogawanywa katika sekta za kilimo,uvuvi na wafugaji. Aidha, amewapongeza wajariamali kwa kuboresha bidhaa wanazozalisha na kuziweka kwenye muonekano wenye kuvutia ili kuingia kwenye ushindani wa kibiashara. Amesema ubora wa bidhaa unaanzia kwenye muonekano na kwamba,ubunifu wao kuboresha muonekano unawapa hadhi ya kufikia malengo waliyojiwekea katika kupeleka mbele bidhaa zao.

MAAGAZETI YA LEO TAREHE 09 AGOSTI 2026

Image