Monday, March 19, 2018

ULEGA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA KWA MKAKATI MZURI WA KUINUA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI


Katika picha katikati kushoto Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Uvinza Bw. Haroon Chande akimueleza Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega Anayeangalia Chaga kuhusu chaga hizo za kuanikia dagaa zilizojengwa na mradi wa kuhifadhi mazingira wa ziwa Victoria LIVEMP chaga ambazo ameeleza zimekuwa na msaada mkubwa kwa wavuvi wa dagaa wanaotumia mwalo wa Muyobozi uliyobo Wilayani uvinza katika kijiji cha Mwakizega.
Chaga za kisasaa za kukaushia dagaa katika mwalo wa Muyobozi, uliyopo katika kijiji cha Mwakizega Wilayani Uvinza, Mwalo ambao ulijengwa na Mradi wa kuhifadhi mazingira ya ziwa Victoria LIVEMP , chaga hizo zinatumika na wavuvi kukaushia dagaa.
Wavuvi wakiteketeza wao wenyewe nyavu haramu zilizokamatwa katika oparesheni ya kupambana na uvuvi haramu katika ziwa Tanganyika Mbele ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega alipofanya ziara katika Mwalo wa Muyobozi Wilayani Uvinza.
............................

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Uvinza kwa kuwa na mikakati thabiti ya kupambana na uvuvi haramu na kutatua kwa kiasi kikubwa migogoro ya wakulima na wafugaji kwa kuwekeza kwenye Ranchi za mifugo.

Ulega ameyasema hayo alipokuwa katika ziara ya kugagua Mwalo wa Muyobosi uliyopo Wilayani uvinza ambapo alisema jitihada hizo za wilaya zitachangia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo na serikali kwa ujumla, kwani ina mkakati wa kutenga maeneo ya Ranchi kwa ajili ya wafugaji.

“Nataka niwahakikishie mimi na wizara yangu tutakuwa tayari kuhamia hapa kulisimamia jambo hili mtakapo tenga hayo maeneo ya kufugia, ili kuwaweka tayari wafugaji katika maeneo hayo na huo ndiyo muharobaini wa kwenda kuondoa  matatizo ya wakulima na wafugaji katika nchi yetu kwa mipango ya namna hii inawezekana kabisa, hicho ni kipaumbele chetu mimi na waziri wangu Mhe. Luhaga Mpina katika uongozi wetu tutahakikisha kama siyo kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji basi tutaindoa kabisa, kwa kushirikiana vyema na Halmashauri zetu” Alisema Ulega.

 Ulega alisisitiza suala la mapambano dhidi ya uvuvi haramu na ulinzi wa Rasilimali za uvuvi na suala zima la ufugaji wa samaki, nakuwaasa kuachana kabisa na utamaduni wa kuagiza samaki kutoka nje ya nchi.

Naibu Waziri Ulega  alisema kuwa fedha nyingi zimewekwa katika mwalo huo wa Muyobozi na kuwataka wavuvi katika eneo hilo kuutumia vizuri mwalo huo wenye hadhi ya kimataifa ambapo ameleza kwa mwaka wa fedha uliopita mwalo huo peke yake umechangia kiashi cha shilingi milioni 28 “ Ninaamini kama mtapasimamia vyema mahala hapa patachangia pato la taifa mara nne zaidi ya mwaka jana. Ninyi ndo muwe walinzi wa kwanza wa rasilimali hizi ili nchi yetu iweze kuinuka” Alisisitiza

Awali, akiongea katika ziara hiyo mwenyekiti wa kijji cha Mwakizega ambapo mwalo wa Muhyobozi umejengwa Bw. Jaffari Abdalah, alisema mwalo huo unakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwa nipamoja na gati la mwalo huo kuwa na urefu wa mia 20 ambazo ni chache kwa boti kuegesha kupakua na kupakia kabla na baadha ya shuguli za uvuvi , hivyo ameiomba serikali kuongeza urefu wa gati hiyo ili mitumbwi mikubwa na midogo iweze kufanya shughuli za uvuvi vizuri.

Bw. Jaffar pia alisema wavuvi wa Muyobozi wanakabiliana na changamoto ya kukosa elimu kupitia mafunzo yanayoendana na wakati huu wa kisasa katika sekta ya uvuvi.

MAGARI 50 YA WAGONJWA YAGAIWA KWA HALMASHAURI.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo (Mb) akimkabidhi moja ya gari la wagonjwa aina ya Suzuki Maruti, Ashura Nkya ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Babati katika bandari ya Dar es Salaam jana.
Baadhi ya magari aina ya Suzuki Maruti ambayo Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliamuru yagawiwe katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuhudumia Sekta ya Afya nchini.
.......................................

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Selemani Jafo, ameendesha zoezi la kugawa magari 50 ya wagonjwa aina ya Suzuki Maruti (Ambulances) kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini Jijini Dar es Salaam.

Magari hayo ambayo awali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliagiza yafanyiwe utaratibu wa kisheria wa kiforodha na yagawanywe kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa ili yatumike kwa kuwahudumia wananchi katika vituo mbalimbali vya afya nchini.

“Hii ni agenda ya Mhe. Rais ya kutaka kuhakikisha watanzania wanapata huduma bora, ambulance hizi ulaji wake wa mafuta ni mdogo sana na zitatusaidia katika halmashauri nyingi,”amesema Jafo.

Aidha, Mhe. Jafo amemshukuru sana Rais wa John Magufuli kwa kuonyesha mapenzi makubwa lakini pia amependezwa na Watumishi wa Wizara, Mikoa na Halmashauri zote kuweza kuhudhuria hafla hiyo muhimu iliyofanyika bandarini Jijini Dar es Salaam.
 
Naye Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Zainabu Chaula amemshukuru Waziri wa Nchi TAMISEMI na Waheshimiwa Wabunge wote kwa utendaji wao na kuwataka wabunge kuwa na lugha ya ufahamu mmoja ili kuboresha utendaji Serikalini.

“Kwa niaba ya watendaji nawashukuru sana waheshimiwa Wabunge, nilitamani tutembee pamoja kwa maana ya kuwa na uelewa wa pamoja na ndio maana Mhe.Waziri amewakabidhi wabunge magari nao watukabidhi sisi,”Amesema.

Charles Kichere Kamishna Mkuu wa Mapato Tanzania, amesema awali magari hayo aliyaona Mhe. Rais alipofanya ziara bandarini na kwamba magari hayo yalikuwa yameteleekezwa na mmiliki wake kutofahamika na ndipo rai, aliagiza kufuata utaratibu wa forodha na kuyataifisha magari hayo na kasha yagawiwe kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.

Kwa upande wake Mhe. Prof Norman Sigalla King, Mbunge wa Makete, amemshukuru Mhe. Rais kwa kutoa ambulance hizo kwa ajili ya kuimarisha huduma za mama wajawazito.

“kwanza nitoe shukrani za pekee kabisa kwa kupewa ambulance kwa ajili ya wilaya yangu ya Makete nakumbuka niliomba kwa ajili ya tarafa za Ukutama, Matamba, Magomba, Tulongwa na Niwaho”amsema.

Amebainisha umbali wa kata ya Ukutama hadi Makete mjini ni kilomita 70 na hivyo itawanusuru wakina mama dhidi ya vifo vya uzazi visivyotarajiwa.

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya Kigoma, Hakimu Ndatama amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwapatia ambulance ambayo itaokoa vifo vya akina mama na watoto kwa kiasi kikubwa.

MAGAZETI YA LEO TAREHE 19 MARCH 2018.

Sunday, March 18, 2018

MOTO WATEKETEZA NYUMBA BAGAMOYO.


Nyumba moja imeteketea kwa moto baada ya mota huo kutokea ndani ya nyumba hiyo majira ya saa sita mchana kitongoji cha Bong'wa kata ya Magomeni wilaya ya Bagamoyo.

Tukio hilo la ilimesababisha taharuki kwa wakazi wa mitaa ya jirani baada ya mitungi ya gesi iliykuwemo ndani ya nyumba hiyo kulipuka kwa sauti nzito na kuruka umbali kutoka ndani nyumba hiyo.

kufuatia hali hiyo wananchi wameweza kutoa ushirikiano ili kuudhibiti moto huo usiingie nyumba nyingine ambazo zimejengwa kwa karibiana.

Aidha Jeshi la zimamoto na uokoaji Bagamoyo limeweza kufika eneo la tukio na kuwahi kuudhibiti moto usende nyumba nyingine nyumba iliyoshika moto ikiwa tayari imeshika mota kwa kasi kutokana na mitungi ya gesi iliyokwemo ndani ya nymba hiyo.

Afisa wa zamu wa zima moto, ambae ni  Mkaguzi Msaidizi wa Zimamoto, A/INSP. Samweli Ponela alisema toka kupata taarifa hiyo imewachukua dakika tano kufika eneo la tukio na kuanza kupambana na moto huo.

Aidha, Ponela alitoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za majanga ya moto kupitia namba 114 na sio namba za watu binafsi ambao huwenda hawapo kazini.

Alisema taarifa ya tukio hilo wameipata kupitia askari wa zimamoto ambae hakuwa zamu jambo ambalo husababisha pia kuchelewa kupata taarifa za moto.

Chanzo cha moto huo hakijafahamika ingawa inaaminika ni kulipuka kwa mtungi wa gesi ambapo jumla mitungi ya gesi kumi na sita 16 imekutwa ndani huku mitungi sita ikiwa imeripuka yenyewe kabla ya kulipuliwa na jeshi la zimamoto.

Miongoni mwa watu waliokimbilia tukio hilo mama mmoja ambae hakufahamika jina lake alijeruhiwa na mtungi wa gesi baada ya mtungi wa gesi kulipuka na kuruka umbali wa mita mita 15 ambapo mama huyo ulimjeruhi kwenye miguu.

MBEGU YA MAHINDI YA W. 21 09 YAZINDULIWA BAGAMOYO.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga ( wa pili kushoto mwenye miwani) akizindua rasmi Mbegu ya mahindi ya W. 21 09 katika msimu wa kilimo 2018. pamoja nae kulia ni Mkurugenzi wa fedha na utawala, Shabani Hussein kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na wapili kulia ni
mtafiti wa mbegu hiyo ya mahindi ya  W. 21 09 kutoka kituo cha utafiti Ilonga wilayani Kilosa, Mikidadi Hamidu.

Na Athumani Shomari
......................................

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga amezindua Mbegu bora ya Mahindi ya W. 21 09 katika msimu wa kilimo 2018 itakayotumika na wakulima wa mahindi kwaajili ya kuzalisha mahindi mengi na yenye ubora.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu huyo wa wilaya alisema mbegu hiyo itawapa fursa wananchi wa Bagamoyo kuvuna mazao mengi na yenye ubora hali itakayowasaidia kukabiliana na soko la ajira wilayani humo.

Alisema wilaya ya Bagamoyo ipo katika ujenzi wa viwanda hivyo ili mwananchi aingie kwenye ushindani wa ajira anahitaji kuwa na chakula kitakachomuwezesha kuwa na utulivu wa akili na mwili.

Akizungumzia utafiti mkurugenzi wa fedha na utawala, Shabani Hussein kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) alisema tume hiyo inafadhili tafiti mbalimbali ikiwemo mbegu za mahindi na muhogo ili wakulima wapate matokeo mazuri ya kile wanachopanda.

Afisa mipango wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Bestina Daniel alisema mbegu hiyo ambayo imefanyiwa utafiti katika kituo cha Ilonga kilichopo Kilosa imetia michakato yote ya kuthibitishwa na kuidhinishwa kwaajili ya kuingia sokoni kwa matumizi.

Nae mtafiti wa mbegu hiyo ya mahindi ya  W. 21 09 kutoka kituo cha utafiti Ilonga wilayani Kilosa, Mikidadi Hamidu alisema Mbegu hiyo ya mahindi ina uwezo wa kutoa gunia 35 kwa ekari moja endapo mkulima atazingztia kanuni za kilimo cha mahindi.

Kwa upande wake, Afisa kilimo wa Mkoa wa Pwani George Kapilima alisema wilaya ya Bagamoyo inaongoza kwa kilimo cha mahindi Mkoani wa Pwani, huku zao la mahindi likishika nafasi ya pili baada ya zao la muhogo mkoani humo.

Alisema katika msimu wa kilimo wa mwaka 2016/2017 Mkoa wa Pwani ulizalisha tani laki moja na kumi 110,000 ambapo Halmashauri ya Chalinze iliyopo ndani ya wilaya ya Bagamoyo ilizalisha tani elfu sitini na tano 65,000 za mahindi.

Alisema mazao yanayoongoza mkoani Pwani ni Muhogo, Mahindi na Mpunga ambapo alisema mbegu hiyo ya W. 21 09 itasaidia kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi wilaya ya Bagamoyo na Mkoa wa Pwani kwa ujumla.

 Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga, akipanda mahindi ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi mbegu ya W. 21 09 katika kitongoji cha Kilemela kata ya Kerege wilayani Bagamoyo.

Afisa kilimo wa Mkoa wa Pwani George Kapilima kushoto
akipanda mahindi ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi mbegu ya W. 21 09 katika kitongoji cha Kilemela kata ya Kerege wilayani Bagamoyo.
 mkurugenzi wa fedha na utawala, Shabani Hussein kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) akizungumza katika uzinduzi wa mbegu mpya ya mahindi ya W. 21 09.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga ( wa pili kushoto mwenye miwani) akizindua rasmi Mbegu ya mahindi ya W. 21 09 katika msimu wa kilimo 2018. pamoja nae kulia ni Mkurugenzi wa fedha na utawala, Shabani Hussein kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na wapili kulia ni

mtafiti wa mbegu hiyo ya mahindi ya  W. 21 09 kutoka kituo cha utafiti Ilonga wilayani Kilosa, Mikidadi Hamidu, anaekabidhiwa ni Anna Macha kutoka kikundi cha Tupendane kijiji cha Kongo.

MWALIMU JOHN MPONDA WA TaSUBa AFARIKI.


Mwalimu wa sanaa Bagamoyo, kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) JOHN MPONDA, amefariki dunia leo Tarehe 18 Mach 2018, TaSUBa zamani ilijulikana kama Chuo Cha Sanaa Bagamoyo

Mwalimu Mponda ambaye ni Mtaalam wa Dance Theory na Dance Choreography Chuoni hapo ndiye pia alikuwa Mwenyekiti wa Tamasha la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo amefariki mapema hii leo katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Aidha, amekuwa akiigiza katika matangazo ya TV ya Taasisi mbalimbali kuhusu ujumbe wa kujikinga na Malaria na pia HAKI ELIMU.


Mwalimu John Mponda atakumbukwa kwa ucheshi wake akiwa kazini hata nje ya kazi kwa watu wa rika zote.

Taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwake Blok P Bagamoyo na baadae kutolewa maamuzi ya lini atazikwa na wapi.
 Mwalimu John Mponda kushoto enzi za uhai wake akiwa katika majukumu yake ya kikazi.

Friday, March 16, 2018

YANGA YAAPA KUPINDUA MATOKEO BOTSWANA HAPO KESHO LIGI YA MABINGWA AFRIKA



Yanga inaendelea na maandalizi yake ikiwa ugenini kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano wa klabu bingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana utakaochezwa siku ya Jumamosi machi 17, 2018.

Mjumbe wa kamati ya utendaji na Katibu wa Kamati ya Mashindano Yanga Samuel Lukumay amesema kambi inaendelea vizuri kila kitu kipo sawa na wachezaji wote waliosafiri na timu wako salama kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi.

“Maandalizi yanaendelea vizuri hatukupata shida yoyote tangu tunakuja hadi tumefika, tulitembelewa na balozi wa Tanzania nchini Afrika kusini ambaye ndio anasimamia pia Botswana akapata muda wa kuzungumza na vijana na kuwatia hamasa na kuwaambia katika mpira kilakitu kinawezekana kwa hiyo tunaweza kugeuza matokeo.”

“Hakuna majeruhi yoyote kiujumla kambi inaendelea vizuri bila tatizo lolote”
Mchezo wa awali uliozikutanisha yanga na Township Rollers kwenye uwanja wa Taifa, yanga ilipoteza kwa kufungwa 2-1 hivyo inahitaji kushinda kuanzia 2-0 ili kukata tiketi ya moja kwa moja kufuzu hatua ya makundi ya vilabu bingwa Afrika.

TAIFA STARS YASHIKA MKIA AFRIKA MASHARIKI KATIKA VIWANGO VYA UBORA WA SOKA DUNIANI



Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), limetoa orodha ya Viwango Vya Ubora wa Soka ambapo Tanzania imeshika nafasi ya mwisho ukanda wa Afrika Mashariki.

Uganda inaongoza kwa Afrika Mashariki ikiwa nafasi ya 78 huku Kenya ikiwa nafasi ya pili kwa kushika namba 105, Rwanda ya tatu ikiwa nafasi ya 112 na Tanzania ikiwa mkiani katika nafasi ya 146.

Kwa upande wa Afrika, Tunisia inaongoza kwa kushika nafasi ya 23 huku Germany wakisalia nafasi ya kwanza Duniani na Brazili ikiwa nafasi ya pili.
Kumi bora ya FIFA ipo namna hii

1: GERMANY
2: BRAZIL
3: PORTUGAL
4: ARGENTINA
5: BELGIUM
6 :POLAND
7: SPAIN
8: SWITZERLAND
9: FRANCE
10: CHILE

WANAVYUO WAFUNDISHE KUJIAJIRI- KASSIM MAJALIWA.



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa William Anangisye, ofisini kwa Waziri Mkuu Mjini Dodoma, Machi 16, 2018.
...........................................


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ni umuhimu mfumo wa ufundishwaji wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini ukaboreshwa ili wanapomaliza waweze kujiajiri.

“Kumekuwa na tatizo kubwa la wasomi wetu kuwa na mtazamo kwamba wanapomaliza masomo yao lazima waajiriwe. Upo umuhimu wa kubadili mtazamo huo kwa kuwapa mbinu zitakazowawezesha kujiajiri.”

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Machi 16, 2018) alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. William Anangisye, ofisini kwake mjini Dodoma.

Amesema wanafunzi hao wanapomaliza wanatarajiwa wawe na uwezo wa kubuni mbinu mbalimbali za kujiajiri na kuondokana na mtazao wa kusubiri ajira za kuajiriwa maofisini.

Waziri Mkuu amesema wasomi hao wanaweza kuchukua kauli mbiu ya Rais Dkt. John Magufuli ya uchumi wa viwanda kwa kuanzisha kilimo cha mazao mbalimbali yatakayotoa malighafi za viwandani.

Pia Waziri Mkuu amesema wasomi hao wanaweza kujikita katika shughuli za uchimbaji wa madini au usindikaji wa mazao mbalimbali, hivyo tayari watakuwa wamejiajiri kwa sababu ajira si za ofisini pekee.

Aidha, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam aliyestaafu Profesa Rwekaza Mukandara kwa kazi nzuri aliyoifanya kipindi cha uongozi wake.

Kwa upande wake, Profesa Anangisye amesema mzigo aliopewa wa kuiongoza taasisi hiyo si mwepesi, hivyo ameahidi kufanya kazi kwa bidii na hatokwenda kinyume na matarajio ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Kiongozi huyo amesema katika kuhakikisha wanaboresha masomo chuo hapo wameanzisha skuli ya kilimo na uvuvi, hivyo wanatarajia kuanzisha mashamba ya mfano kwa ajili ya mazao mbalimbali.