Monday, June 17, 2024

RC LINDI AZIAGIZA HALMASHAURI KUANZISHA NA KUHUWISHA MADAWATI YA ULINZI MASHULENI

 

NA HADIJA OMARY, LINDI.



Mkuu wa Mkoa wa Lindi ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa huo kuhakikisha zinafufua au kuunda madawati ya ulinzi ya watoto  sambamba na kuunda klabu za watoto mashuleni zitakazowasaidia kuelezea na kutatua changamoto zao


Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa huko katika kijiji cha chienjele halmashauri ya Ruangwa Jana Juny 16/2024 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi , Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Patrick Sawale  amesema vyombo hivyo ni  muhimu  kwa ajili ya kutetea maslahi yao pindi watoto wanapokuwa wamefanyiwa ukatili. 



Amesema ili Taifa liweze kuendelea kupiga hatua ni muhimu kutilia maanani mahitaji  ya watoto  ikiwa pamoja na watoto  masikini , walemavu na walio na mazingira magumu zaidi kutengewa mafungu toka katika bajeti kuu ya serikali na zile za Halmashauri.



hata hivyo ameendelea  kuikumbusha Jamii kuwa inawajibu wa  kutoa taarifa na ushahidi kuhusu mtoto ambae haki zake zinakiukwa na wazazi na walezi au ndugu yoyote kwenye  serikali za mitaa na kwenye vyombo vya dola kwa vitendo vya ulawiti, ubakaji na ukatili  wanaofanyiwa  watoto  ili serikali ichukue hatua na adhabu zitolewe.



Akitoa salamu za Wilaya ya Ruangwa Mkuu wa Wilaya hiyo Hassan Ngoma amesema siku hiyo ya Mtoto wa Afrika ni muhimu kwa Nchi za Afrika kutathimini na kueleza Dunia mabadiliko Makubwa yaliyofanywa na Nchi hizo Katika kuwapambania watoto hao Katika kuondoa changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ubaguzi wa rangi unyanyapaa Elimu na kadhalika


 


Awali afisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Lindi ndugu Charles Kigahe alieleza changamoto kadhaa zinazowakabili watoto wa Mkoa huo wa Lindi 


Miongoni changamoto hizo ni pamoja na Watoto kutotimiziwa haki ya kupata elimu, hii imetokana na wazazi kutoona umuhimu wa kuwafuatilia watoto pindi wakiwa shuleni ambapo imesababisha watoto kuacha shule.



Watoto kukosa malezi ya wazazi, hii imetokana na wazazi kutengana ambapo mtoto anaendelea kulelewa na mzazi mmoja au bibi. Watoto kukosa mahitaji ya msingi kwa sababu ya kutoelewana kwa wazazi,

Watoto kufanyiwa ukatili wa kingono.



Changamoto nyingine ni Migogoro ya ndoa kwa wazazi,  ambapo wazazi wanaachana inapelekea mtoto kuendelea kuhangaika na hatimaye kuacha shule.

Wazazi na walezi hawatimizi wajibu wao wa kuwalea watoto ambapo inasababisha kuongezeka kwa watoto wa mtaani.


Kauli mbiu ya siku ya Mtoto wa Afrika 2024 ni Elimu jumuishi kwa watoto izingatie maadili, maarifa na stadi za kazi










No comments:

Post a Comment