Posts

MRADI WA BOMBA LA MAFUTA KUANZA JANUARI 2027

Image
  Na Alodia Dominick,  Bukoba, Mradi wa bomba la mafuta ambao utekelezaji wake wa jumla umefikia asilimia 87.7 unatarajia kukamilika na kuanza rasmi Januari 15,2027. Mradi huo ambao mkataba wake ulisainiwa mwaka 2021 unatarajiwa kuanza rasmi ifikapo Januari 15, 2027 na kutokana na mkataba mradi utadumu takribani miaka 25. Mratibu wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kusafirisha mafuta ghafi Afrika Mashariki (EACOP) Jumanne Saidi akitoa mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari mkoani Kagera juu ya mradi wa bomba la mafuta na maendeleo yake ameeleza kuwa, mradi huo utaanza rasmi Januari 15,2027. Amesema sh.bilioni 35.6 zimetumika kulipa fidia kwa wananchi wapatao 10,144 maeneo yote yanayopitiwa na bomba la mafuta na nyumba zilizoguswa ni 340, kwa Kagera ni nyumba 119 ambapo waguswa kwa Kagera wako 118.  "Mikoa inayopitiwa na bomba la mafuta ni nane ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Manyara, Dodoma na Tanga na katika mkoa wa Kagera unapita katika wilay...

MIL 360 ZA BAKAA KUTEKELEZA MIRADI VIPORO MANISPAA TABORA

Image
  MIL 360 ZA BAKAA KUTEKELEZA MIRADI VIPORO MANISPAA TABORA Na Allan Kitwe, Tabora MADIWANI wa halmashauri ya manispaa ya Tabora wameazimia fedha zote zilizotengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ulioishia Juni 2026 na hazikutumika (bakaa) zisirudishwe TAMISEMI bali zitumike kukamilisha miradi viporo. Hayo yamebainishwa na Katibu wa Madiwani wa CCM Bahati Adam Ntiruhungwa (diwani wa Kata ya Ng’ambo) alipokuwa akitoa maazimio yao kwenye kikao cha robo ya nne ya baraza kilichoketi leo Mjini hapa. Ameeleza kuwa madiwani ndio wawakilishi wa wananchi katika Kata zao, hivyo wana dhamana ya kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa katika maeneo yao inakamilika kwa wakati kwa manufaa ya wananchi. ‘Madiwani wa CCM tumeazimia miradi viporo yote ikamilishwe, na fedha za bakaa, zaidi ya shilingi milioni 364 ziombewe kibali ili zitumike kumalizia miradi iliyoanza kutekelezwa katika msimu uliopita’, amebainisha. Ntiruhungwa ameitaka Ofisi ya Mkurugenzi kuhakikisha wakazi wa kata zote wananufaika n...

SUBIRA MGALU AULIZA HATUA YA FIDIA KWA WANANCHI WA BARABARA YA MAKOFIA–MLANDIZI

Image
  SUBIRA MGALU AULIZA HATUA YA FIDIA KWA WANANCHI WA BARABARA YA MAKOFIA–MLANDIZI Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. CPA Subira Khamis Mgalu, ameuliza Serikali kuhusu hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya kuwalipa fidia wananchi wanaopitiwa na mradi wa Barabara ya Makofia–Mlandizi katika Kata ya Yombo. Akitoa swali la nyongeza, Mhe. Subira amesema barabara hiyo imefungamanishwa na mpango wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na eneo la viwanda la Kwara, hivyo umuhimu wake unaendelea kuongezeka. Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema kuwa Wizara tayari imekamilisha tathmini ya fidia na imewasilisha mahitaji hayo katika Wizara ya Fedha. Amesema Serikali inaendelea na taratibu za kupata fedha, na mara fedha zitakapopatikana, wananchi waliostahili watalipwa fidia ili hatua za ujenzi wa barabara hiyo ziweze kuendelea.

TARURA YATENGA BIL. 1 KUKABILIANA NA EL NINO TABORA

Image
  TARURA YATENGA BIL. 1 KUKABILIANA NA EL NINO TABORA  Na Allan Kitwe, Tabora WAKALA wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoani Tabora wametenga zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo mbalimbali ili kukabiliana na wingi wa mvua za el nino. Hayo yamebainishwa jana na Afisa wa Wakala huo, Mhandisi Nehemia Chacha kwa niaba ya Meneja wa TARURA Mkoa wa Tabora alipokuwa akitoa taarifa ya hali ya barabara kwenye kikao cha madiwani wa halmashauri ya manispaa. Ameeleza kuwa ili kuhakikisha miundombinu ya barabara katika manispaa hiyo inapitika wakati wote wamekamilisha ujenzi wa madaraja makubwa 2 ya kimkakati katika kata za Ndevelwa, Misha na Kabila. Mhandisi amefafanua kuwa daraja la Ndevelwa ambalo lilikuwa kero kubwa sana kwa wananchi limegharimu zaidi ya shilingi milioni 460 na limekamilika kwa asilimia 100 na sasawananchi wameanza kulitumia, kero imeisha Daraja la pili ni lile linalounganisha Kata za Misha na Kabila ambalo lil...

TAASISI ZA UMMA ZAAGIZWA KUJENGA VICHOMEA TAKA

Image
  TAASISI ZA UMMA ZAAGIZWA KUJENGA VICHOMEA TAKA   Na Allan Kitwe, Tabora TAASISI za umma na binafsi Mkoani Tabora zimetakiwa kutumia vichomea taka katika maeneo yao ili kuteketeza taka za kibaiolojia na kikemea na nyinginezo ili kulinda afya ya binadamu na mazingira yanayowazunguka. Wito huo umetolewa juzi na Meneja wa Wakala wa Maabara ya Mifugo Tanzania (TVLA) Kanda ya Magharibi, Dkt. Qwari Bura, kwenye uzinduzi wa mtambo wa kisasa wa kuchomea taka uliojengwa kwenye Ofisi za Maabara ya Mifugo. Alisema kuwa mtambo huo ni maalumu kwa ajili ya kuchomea taka hatarishi hivyo taasisi zote zinapaswa kuiga mfano huo, badala ya kuteketeza taka kwa njia za kawaida ambazo ni hatarishi kwa afya ya jamii na mazingira. Dkt. Qwari alibainisha kuwa mtambo huo una uwezo wa kuchoma hadi kilo 30 za taka ngumu na hatarishi kwa wakati mmoja. Dkt Bura alidokeza kuwa TVLA itatoa huduma hiyo bure kwa wananchi wote wanaohitaji kuchoma taka za kibaiolojia, ila taasisi za Serikali zitatakiwa kuc...

CCM YAPONGEZA MAFANIKIO MANISPAA TABORA

Image
CCM YAPONGEZA MAFANIKIO MANISPAA TABORA Na Allan Kitwe, Tabora HALMASHAURI ya Manispaa Tabora imepongezwa kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana hadi sasa ambayo yamekuwa kichocheo kikubwa cha kuboreshwa huduma za kijamii katika kata zote 29. Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Mjini Komredi Mohamed Katete alipokuwa akitoa salamu za chama kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichoketi leo katika ukumbi mpya wa manispaa hiyo. Katete ameeleza bayana kuwa manispaa hiyo imepiga hatua kubwa kimaendeleo kutokana na kazi nzuri iliyofanyika kwenye miradi ya maendeleo, hali ambayo imepelekea kutatuliwa changamoto za wananchi. ‘Nakupongeza sana Mstahiki Meya, ndugu yangu Gullam-Hussein Dewj, Mkurugenzi wa Manispaa Dkt John Pima, Mkuu wa Wilaya Upendo Wella, Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu wote, kwa kazi yenu njema’, amesema. Amebainisha wazi kuwa sasa hivi wananchi wanapata huduma bora za kijamii katika kata zote tofauti na hali ilivyokuwa huko nyuma, malalamiko yaliku...

BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI

Image
  BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei za bidhaa za mafuta kwa mwezi Septemba 2026.  Bei ya petroli imeshuka kwa Shilingi 102 kwa lita, huku bei ya dizeli ikishuka kwa Shilingi 101 kwa lita. Bei hizo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 2 Septemba 2026, saa 6:01 usiku. EWURA inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia, ambapo mabadiliko ya bei yanaendelea kuathiriwa pamoja na mambo mengine na hali ya kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati. Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015, bei za mafuta zinaendelea kupangwa kwa kuzingatia mfumo wa soko. Wafanyabiashara wote wa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zisizozidi bei elekezi, na wananchi wanashauriwa kutoa taarifa EWURA kwa kituo chochote cha mafuta kitakachouza zaidi ya bei elekezi.