Tuesday, July 16, 2024

WAZIRI MKUU AZINDUA MITAMBO YA KISASA YA KURUSHIA MATANGAZO.

 





Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Julai 15, 2024 amekagua na kuzindua mitambo na vifaa vipya vya kurushia matangazo vya kampuni ya Azam Media Limited.


Vifaa hivyo ni pamoja na Magari ya kisasa ya kurushia matangazo (OB Van), kamera za kisasa pamoja na mfumo wa kusaidia maamuzi viwanjani (VAR).


Vifaa hivyo vilivyogharimu shilingi bilioni tano vitatumika katika kurushia matangazo ya mpira wa miguu wa ligi Kuu Tanzania bara na Zanzibar pamoja na michezo mingine.


Akizungumza na wafanyakazi wa Azam Media pamoja na wadau wa michezo Mheshimiwa majaliwa amesema manunuzi ya vifaa hivyo ni mapinduzi makubwa katika tasnia ya habari kwani kunaifanya Tanzania kuwa nchi ya kipekee kuwa na vifaa vya kisasa vya aina yake katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Mheshimiwa Majaliwa pia ameshuhudia uzinduzi wa chaneli mpya ya Azam 4 HD ambayo itatumika kurusha ligi kuu ya Ufaransa (Legue 1) na ligi kuu ya Ujerumani (Bundesliga)

MCHINJITA AWAVUNA VIGOGO CHADEMA LINDI KUHAMIA ACT

 




NA HADIJA OMARY 



JUMLA ya wanachama 45 wa chama cha Demockasia na Maendeleo CHADEMA na viongozi wao Mkoani Lindi wamekihama chama chao na kujiunga na chama cha ACT wazalendo



Wanachama hao wamejiunga na chama cha Act kwa kurejesha Kadi zao za uanachama  na kupewa Kadi mpya za ACT, zoezi lililoongozwa na makamu Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo bara Bwana Isihaka Mchinjita 



Viongozi waliojiunga ACT ni pamoja na  aliekuwa Mwenyekiti Mkoa wa Lindi, Zainab Lipalapi; Mwenyekiti BAVICHA Mkoa wa Lindi, Said Mzee; Katibu wa Jimbo, Musa Rwegoshora; Mwenyekiti wa Wazee Jimbo, Bakari Likaku; Mweka Hazina wa Jimbo, Mohamed Mandoyo; na Mwenyekiti BAVICHA Jimbo, Doa Omari.



Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi Kadi zao mpya za ACT wazalendo  Mchinjita amewapongeza wanachama kwa uamuzi wao wa kujiunga  na chama hicho  na kwamba wamechagua  jukwaa sahihi


Nae  Bwana Mussa Rwegoshora  ambae alikuwa katibu wa chama cha Demockasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya Lindi amesema,  wameamua kujiunga na ACT kwa ajili ya kuunganisha nguvu ya pamoja ili kutetea maslah na Maendeleo ya Wana Lindi hivyo ni wajibu wao kuwa na jukwaa la pamoja la upinzani



" Sisi wote tumeamua kujiunga na ACT kwa ajili ya ukombozi wa Jimbo la Lindi na wala haya hayakuja kwa ghafla  ni mpango wa mwenyezimungu, wakati tunaendelea kudhoofika na madalali wa siasa mungu akasema hili haliwezekani ngoja wenya haki wakae huku na wenye dhulma waendelee kudhulumu wenzao"


TFCG YAWEZESHA UPATIKANAJI WA HATI MILIKI ZA KIMILA 738 HALIMASHARI YA MTAMA 

 



Na Hadija Omary 


Katika kuiwezesha jamii kwenye usimamizi shirikishi wa misitu ya asili na kuondoa migogoro ya umiliki wa Aridhi shirika la kuhifadhi misitu Tanzania (TFCG) limewezesha upatikanaji wa hati miliki za kimila 738 kwa  wananchi wa vijiji 10 vya halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi 





Kijiji cha mihima ni miongoni mwa vijiji 10 vya halmashauri ya Mtama vilivyopo kwenye mradi wa  kuongeza usimamizi shirikishi wa misitu chini ya  shirika la kuhifadhi misitu Tanzania (TFCG)  baadhi ya wananchi walinufaika na hati miliki za kimila wanaeleza  faida na manufaa ya hati hizo




Yahaya mtonda ni meneja mradi wa kuongeza usimamizi shirikishi wa misitu kutoka TFCG amesema malengo ya utoaji wa hati hizo  ni kuiwezesha  jamii  kuzingatia misitu ya hifadhi ya vijiji kutoingiliwa na matumizi mengine





Victor shao ni mkuu wa kitengo cha maliasili na  uhifadhi wa mazingira halmashauri ya Mtama amesema tangu mwaka 2020 tfcg ilipoanzisha mradi wa kuongeza usimamizi shirikishi wa misitu katika halmashauri hiyo  vijiji hivyo vimeweza  kuanzisha sheria ndogo ndogo ili kuhakikisha wananchi hawavamii misitu hiyo

Thursday, July 11, 2024

KITUO CHA UTAFITI RUANGWA KAMPASI YA UDSM KUKAMILIKA NDANI YA MIEZI 18

 






NA HADIJA OMARY 





Naibu makamu mkuu wa chuo kikuu cha Dar es salaam ambae ni mratibu wa Mradi wa elimu ya juu kwa mageuzi ya uchumi (HEET) Profesa Benadeta Kiliani amesema watahakikisha  ujenzi wa kituo cha utafiti wa sayansi ya Kilimo  na chakula  cha chuo kikuu cha Dar es salaam unaofanyika katika kijiji cha Likunja  wilayani Ruangwa unakamilika ndani ya miezi 18




Profesa kiliani Ameyasema hayo katika kikao kazi cha uzinduzi wa kamati ya "kasema" ambayo ni sehemu ya ulinzi na usalama wa mradi huo na  yenye jukumu la kuweka kumbukumbu za kile kinachoendelea katika mradi



Profesa kilian ametoa wito kwa kamati na  wananchi wa Ruangwa kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa mradi huo



Kamati hiyo ya " kasema " Ina wajumbe watano na inalengo la kukusanya na kushughulikia maoni au malalamiko ya wananchi katika eneo la mradi  husika 



Jukumu lingine la kamati hiyo ni kuweka kumbukumbu za kile kinachoendelea na kufanyika katika mradi huku ikiwa sehemu ya ulinzi na usalama katika utekelezaji wa mradi




Kwa upande wake Naibu mratibu wa Mradi  huo wa Elimu ya juu kwa mageuzi ya uchumi ( HEET)  Liberato Haule amesema mradi huo  unaotekelezwa  na chuo kikuu cha Dar es salaam umedhaminiwa na serikali kupitia fedha ya mkopo kutoka benk ya dunia ukilenga kuboresha huduma za Elimu ya juu nchini ili iweze kuchangia maendeleo ya uchumi.



Amesema mradi huo unatekelezwa katika maeneo mapya 14 ambapo mpaka sasa maeneo mapya matatu tayari yameshafikiwa ambayo ni pamoja na Ngongo (Manispaa ya Lindi), Likunja Wilayani Ruangwa pamoja na Halmashauri ya Bukoba mkoani  Kagera 





Mwenyekiti wa Halmashari hiyo Andrew  Chikongwe anatumia fursa hiyo kuitaka kamati hiyo kutimiza wajibu wao kwa maslah ya halmashauri hiyo





Baadhi ya viongozi na watendaji walioshiriki katika uzinduzi wa kamati hiyo wamepokea kwa shauku na matumaini makubwa na kwamba kituo hicho kitakuwa msaada  kwa wakulima na kuongeza fursa za kiuchumi



Wednesday, July 10, 2024

WAFUNGWA/MAHABUSU ZAIDI YA 7,000 WANUFAIKA NA KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID.

 

Na Mwandishi Wetu


 


KAMPENI ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Legal Aid imeanza kuzunguka kwenye magereza mbalimbali hapa nchini kuwapa msaada wa kisheria wafungwa na mahabusu na mpaka sasa imeshawahudumia zaidi ya  7,000.


 


Hayo yamesemwa julai 09, na Kaimu Mkrugenzi wa Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Ester Msambazi wakati akizungumza kwenye banda la Mama Samia Legal Aid Campain katika maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaama (DITF) yanayoendelea barabara ya Kilwa wilayani Temeke.


Alisema wameamua kwenda magerezani kwani wanaamini kwamba kuna watu wanaweza kujikuta kwenye mazingira hayo kwa kukosa tu wakili au watu wa kuwaongoza kwenye mashauri yanayowakabili.


“Kuna watu wako mahabusu kwasababu tu wamekosa mwongozo wa kisheria na wakipata mwongozo wanaweza kutoka kwa dhamana au suala linalomkabili likazungumzwa na pande zote mbili na likafikia mwisho,” alisema


Kuhusu wafungwa, alisema kuna watu wanaweza kuwa wamefungwa kifungo cha ndani lakini kupitia kampeni hiyo wanaweza kumsaidia akapata kifungo cha nje kwa kufanyakazi za kijamii au kukata rufaa mahakama za juu.


“Kwa hiyo huduma ya msaada wa kisheria kwa watu walioko kizuizini ni muhimu sana na huwa tunaenda kwenye vituo vya polisi na kwenye magereza na tunapokwenda magerezani tunatoa elimu ya haki jinai kwa watu walioko gerezani,” alisema


Alisema wamekuwa wakitoa elimu kuhusu ukamataji upelelezi uendeshaji wa mashauri, haki na wajibu wa mahabusu na wafungwa wanapokutwa na hatia kwenye kesi mbalimbali za jinai na kupewa kifungo cha ndani.


Alisema wamekuwa wakitoa elimu kuhusu namna ya kupata dhamana na kukata rufaa kwa wale ambao wamehukumiwa lakini hawajaridhishwa na hukumu walizopewa kwenye Mahakama mbalimbali nchini.


“Kupitia kampeni hii tunatoa ushauri kwa mfungwa au mahabusu mmoja mmoja tunakwenda na wanasheria wanaitwa mmoja moja wanashauriwa wanachotakiwa kufanya na wanaandaliwa nyaraka kwasababu wengine wamekaa mahabusu muda mrefu inabidi waandaliwe kila kitu,” alisema


Alisema timu ya wanasheria imekuwa ikiambatana na watu kutoka Ofisi ya Raifa ya Mashtaka, Wizara ya Katiba na Sheria, Jeshi la Polisi Makao Mkuu, Jeshi la Magereza Makao Makuu, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.


“Kwa mfano tukikuta mtu amekaa ndani muda mrefu shauri lake linapigwa dana dana, ushahidi haukamiliki kwa wakati anayehusika hapo atakuwa anayetoka ofisi ya mashitaka kwa hiyo atawajibika kufuatilia kujua kesi imekwamia wapi na kisha ataikwamua na itaanza kusikilizwa na kwenda haraka ili mtu apate haki,” alisema.


Alisema timu hiyo pia imekuwa ikimshirikisha Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Mkoa na vyombo vingine vya utoaji wa haki ngazi ya mkoa wakati wa kusikiliza mashauri hayo ya wafungwa na mahabusu.


“Kuna wafungwa na mahabusu wanapewa msaada wa kisheria na  wanatoka kabisa mahabusu au jela na kuna wengine tunawapa elimu tu ya namna ya kudai haki zao wanapoona zinakiukwa  kwa hiyo wengi wameshanufaika na kampeni hii ambayo imefika mikoa saba,” alisema



Alisema Mama Samia Legal Aid Campaign pia imekuwa  ikiwapa msaada wa kisheria wahamiaji haramu ambao kesi zao zimeshasikilizwa na kutolewa maamuzi warejeshwe nchini kwao lakini wanakosa namna ya kuondoka.


Alisema wamekuwa wakiwasaidia kuhakikisha wanakwenda nchini mwao kwani baadhi ya wahamiaji hao wamekuwa wakishindwa kurudi kwao kutokana na kukosa fedha za kuwafikisha kwenye nchi zao.






Thursday, June 27, 2024

ETDCO YAENDELEA KUJENGA MIUNDO MBINU YA KUSAFIRISHA UMEME MRADI WA TABORA - KATAVI 132kV

 

Kaimu Meneja Mkuu Kampuni ya ETDCO CPA Sadock Mugendi, Amesema Wanaendelea kujenga miundo mbinu ya Umeme Nchini ikiwemo Njia ya kusafirisha umeme kutoka  Tabora  hadi Katavi ambao ni mradi wa kusafirisha  Umeme na tayari  Mradi Umefkia Asilimia 67.


Mugendi amesema ETDCO ni kampuni Tanzu ya Shirika la Umeme Tanzania na ni suluhisho la miundo mbinu ya umeme kwani ipo kwa ajili ya kujenga na kukarabati miundo mbinu ya kusafirisha na kusambaza umeme.


Kaimu Meneja Mkuu CPA Sadock Amesema Mradi wa Kutoka Tabora kwenda Katavi wenye Urefu wa kilometa 383 wa msongo wa 132kV ambao Unatarajiwa kumalizika Mwaka huu kupelekea    Mkoa wa Katavi kupata  Umeme wa Uhakika pia Kuipunguzia Gharama Tanesco za Kununua Mafuta ya Dizeli kwajili ya Jenereta ili kuzalisha Umeme kwenye Mkoa Wa Katavi.


CPA Sadock Ameipongeza Serikali kuendelea kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati ili Kuhudumia Wananchi wake vizuri, Amesema Hayo Wakati Akitembelea Mradi wa Kimkakati wa Tabora kwenda Katavi wenye msongo wa 132kV.



Wednesday, June 26, 2024

KIKWETE MWENYEKITI WA BARAZA LA WAZEE WA SADC YUKO LESOTHO

 


NA MWANDISHI WETU, LESOTHO


Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo tarehe 26 Juni, 2024, yuko katika Ufalme wa Lesotho kwa nafasi yake kama Mwenyekiti wa Jopo la Wazee wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).


Jopo hili la Wazee wa SADC ambalo Makamu Mwenyekiti wake Mheshimiwa Paramasivum Pillay B. Vyapoory, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Mauritius, limekutana na Serikali na wadau mbalimbali ndani ya Ufalme wa Lesotho, kama mwendelezo wa juhudi ya kusaidia upatikanaji wa utulivu wa kisiasa katika Ufalme huo. 


Jopo limekutana na Mhe. Ntsokoane Samuel Matekane, Waziri Mkuu wa Ufalme wa Lesotho; Mhe. Nthomeng Justina Majara, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge; Mhe. Mamonaheng Mokitimi, Mwenyekiti wa Seneti; Viongozi wa Vyama vya Upinzani; Mhe. Constance Seoposengwe, Balozi wa Afrika Kusini nchini Lesotho na wadau mbalimbali.






WAZIRI MKUU AZINDUA VITABU VYA HISTORIA YA BUNGE

 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua vitabu vya historia ya Bunge ambavyo vitasaidia kuhamasisha tafiti na kujua zaidi kuhusu mchango wa Bunge katika maendeleo ya jamii nchini.


Amesema kuwa vitabu hivyo pia vitakuwa kielelezo cha mafanikio na changamoto ilizopitia Bunge la Tanzania katika kudumisha demokrasia na utawala wa sheria. “Historia yetu ni sehemu ya mchango wetu kwa jumuiya ya kimataifa katika kukuza amani, utulivu na maendeleo.”


Amesema hayo leo (Jumatano, Juni 26, 2024) wakati wa uzinduzi wa vitabu viwili vya historia ya bunge katika ukumbi wa Pius Msekwa, Jijini Dodoma.Vitabu vilivyozinduliwa ni Kitabu cha Historia ya Bunge kutoka 1926-2024 na Wabunge wa Tanzania na nafasi zao kuanzia mwaka 1965-2023


“Kumbukumbu za historia ya Bunge zinaweza kuchochea utafiti wa kitaaluma na maendeleo ya nadharia za kisiasa na utawala. Watafiti wanaweza kutumia taarifa hizi kujenga ufahamu mpya na kupendekeza mifumo bora ya kisiasa.”


Kwa upande wake Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amepongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa sehemu ya maono ya bunge ikiwemo kuridhia kulikabidhi bunge maeneo yote yanayozunguka jengo la bunge.


“Tunatarajia kujenga makumbusho ya bunge ambayo yatakuwa ni makubwa kwa nchi nzima ili mtu anapokuja bungeni apate historia ambayo tumeipitia kama nchi lakini pia historia ya bunge letu”




TANESCO, WAWEKEZAJI BINAFSI LUDEWA WAFIKIA MAKUBALIANO

 

TANESCO, WAWEKEZAJI BINAFSI LUDEWA WAFIKIA MAKUBALIANO


Ni kuhusu TANESCO kukabidhiwa  miundombinu ya kusambaza umeme*


Ludewa kujengwa kituo cha Kupokea na Kupoza umeme


Kapinga asema Vijiji 70  kati ya  76 Mbulu vimepatiwa umeme


Imeelezwa kuwa, Serikali na Wawekezaji wanaowauzia umeme wananchi katika baadhi ya kata za Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wamefikia makubaliano ya kisheria ili miundombinu ya usambazaji umeme katika Kata hizo ikabidhiwe kwa Shirika la Umeme Tanzania  (TANESCO).


Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga leo Juni 26, 2024 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu maswali mbalimbali ya Waheshimiwa Wabunge akiwemo Mbunge wa Ludewa, Mhe. Zacharius Kamonga aliyetaka kufahamu Serikali itamaliza lini changamoto za bei na mgao wa umeme katika Kata hizo.


Kapinga ameongeza kuwa, hatua zote za makabidhiano zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Mwezi Julai, 2024 na baada ya kukamilika, TANESCO watabadilisha mita za umeme ili ziendane na mifumo ya TANESCO na kuwawezesha wananchi wa Kata hizo kutumia umeme wa Gridi ya Taifa.


Alitaja Kata hizo kuwa ni Mawengi, Lubonde, Lugarawa, Lupanga, Mlangali, Madilu, Milo na Mawengi ambazo  zimekuwa zikipata umeme kutoka kwa Wawekezaji binafsi (JUWUMA na MADOPE HCL.


Kuhusu ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme kujengwa katika Wilaya ya Ludewa,  amesema Serikali inaangalia namna bora ya kutekeleza ujenzi huo ikiwa ni pamoja na kutumia Mpango wa Gridi Imara.


Amesisitiza kuwa, Wananchi wa Ludewa wanahitaji umeme mwingi na wa uhakika kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao vikiwemo viwanda vidogo na vikubwa. 


Vilevile amesema kuwa, Serikali kupitia Mkandarasi  Ok Electrical inatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme na tayari mkandarasi  ameshafanya upimaji na usanifu wa kina na mwanzoni mwa mwezi Julai 2024 anatarajiwa kuanza kusimika nguzo  ili kuziunganisha Kata hizo na Gridi ya Taifa.


Katika hatua nyingine, Serikali imemtaka  mkandarasi anayetekeleza mradi wa Usambazaji wa umeme katika  Vijiji vilivyopo  mwambao wa Ziwa Nyasa, kukamilisha utekelezaji wa mradi huo kwa wakati.


Naibu Waziri Kapinga amesema  kuwa iwapo mkandarasi huyo atashindwa kukamilisha mradi huo kwa muda uliopangwa, atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo wakandarasi wengine wazembe.


Pia, Kapinga amesema Serikali inaendelea 

 na usambazaji wa umeme vijijini katika Wilaya ya Mbulu   ambapo vijiji 70 kati ya 76 vimeshapatiwa umeme kupitia REA.


Aidha, kazi ya usambazaji umeme katika Vijiji  6 vilivyosalia inaendelea ambapo mkandarasi anafanya  kazi ya kuvuta waya na kuweka Mashineumba katika vijiji hivyo.


Pia Mradi wa Ujazilizi utapeleka umeme  katika Vitongoji vyote nchini kwa awamu tofauti.

Friday, June 21, 2024

CTI YALIA NA UTITIRI WA TOZO MIKOANI

 

Na Mwandishi Wetu


 


SHIRIKISHO la Wenye Viwanda (CTI), limeseme kuwepo kwa utitiri wa tozo katika kila mkoa na halmashauri kumekuwa kikwazo katika ustawi wa biashara na uwekezaji nchini.


 


Hayo yalisemwa  jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Shirikisho hilo, Leodegar Tenga katika warsha maalumu ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya viwanda vya chakula na vinywaji kupitia utafiti uliofanywa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utawala Bora na Maendeleo ya Wajasiriamali, Dk. Donath Olomi.


 


Utafiti huo ulioangazia namna tozo hizo zilivyo kikwazo kwa wafanyabiashara kwenye maeneo mbalimbali nchini.


 


Tenga alisema Dk Olomi ni mtafiti msomi na ameainisha vitu vingi ikiwemo mapendekezo ya kufuata kuondoa vikwazo hivyo, akisisitiza kuwa lengo ni kuwapa nafasi nzuri wafanyabiashara wakubwa wanaotamani kuja kuwekeza nchini.


 


Tenga alisema athari ya utofauti wa tozo unaathari kibiashara ikiwamo kuongezeka kwa bei za bidhaa, na hivyo kusababisha  mlaji kununua bidhaa ya bei ndogo kwa gharama kubwa.


 


“Kwa mfano mtu amevuna mazao yake Mbeya sasa ili aje kuuza Dar es Salaam kwenye soko kubwa atalazimika kusafirisha, sasa anatozwa huko  akifika Iringa anatozwa tena, njiani pia hivyohivyo anakutana na tozo nyingine akifika Dar es Salaam nako anakutana na tozo nyingine,” alisema.


 


“Tunataka huyu mfanyabiashara akishatozwa Mbeya asitozwe tena sehemu nyingine, tunapaswa tuwe na utaratibu ambao utatambua kama ameshatozwa, hatujafanikiwa kuondoa vikwazo. Tusipofanya hivyo tunawakwamisha hawa wafanyabiashara au watafanya ujanja wa kutoa rushwa njiani ili kupunguza hizo tozo,” alisema Tenga


 


Naye Dk. Olomi alisema kutokana na utafiti alioufanya alipendekeza kuwe na uwazi kuhusu  tozo hizo akifafanua kwamba katika halmashauri karibu zote tozo hizo hazijatangazwa mahali popote hivyo mwekezaji anayataka kuwekeza hawezi kujua viwango vya tozo na kama ziko kwa mujibu wa sheria au siyo.


 


Pia alipendekeza serikali iangalie namna ya kuondoa tozo zinazokinzana na kujirudia rudia kwenye mikoa na halmashauri nchini akitolea mfano kwamba mtu akiingiza lori mjini (kariakoo) kwaajili ya kupakia au kuondoa bidhaa atakutana na tozo ya maegesho.


 


Alisema pia lori hilo litatozwa malipo ya kuingia katikati ya Jiji na wakati mwingine haijulikani wapi ni mwisho wa kulipia kwa hiyo kuna maeneo kama hayo yanahitaji marekebisho.


 


Alisema mkanganyiko mwingine ni zile tozo zinazotozwa na halmashauri na nyingine serikali kuu. “kwa mfano tozo ya kupima afya kwenye viwanda unatozwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa kazi (OSHA) lakini pia serikali za mitaaa kiutaratibu zinatofautiana kama unapima  magonjwa yanayoambukizwa unapimwa na halmashauri na yale yasiyoambukiza unapimwa na OSHA na tozo wanayotoza kwa mtu mmoja ni sh 70,000 sasa ukiangalia hii haijakaa sawa,”


 


“Hizi tozo zisiwepo kama zinania ya kukomoa wenye viwanda bali zitumike kuweka mazingira mazuri kwahiyo kuna changamoto za aina hiyo,” alisema Dk Olomi


 


Mhandisi wa Viwanda Mkuu Kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Karoline Varelian alisema serikali itachukua  mapendekezo ya wadau hao, kuchambua na kuyafanyia kazi ili kuweka mazingira rafiki.


 


Alisema tayari Wizara imeshaanza kuzifanyia marekebisho baadhi ya sera na sheria ila kwa sasa watakwenda kuyafanyia kazi kwa haraka mapendekezo yaliyotolewa na wadau ili kuondoa mlalamiko ya wenye viwanda.


 


Alisema tozo zimekuwa nyingi  na kuahidi kuwa  watapitia ushauri uliotolewa kwenye utafiti uliofanywa na Dk Olomi ili kuwapunguzia mzigo wafanyabiashara hususani wenye viwanda vya chakula na vinywaji.