Thursday, July 11, 2024

KITUO CHA UTAFITI RUANGWA KAMPASI YA UDSM KUKAMILIKA NDANI YA MIEZI 18

 






NA HADIJA OMARY 





Naibu makamu mkuu wa chuo kikuu cha Dar es salaam ambae ni mratibu wa Mradi wa elimu ya juu kwa mageuzi ya uchumi (HEET) Profesa Benadeta Kiliani amesema watahakikisha  ujenzi wa kituo cha utafiti wa sayansi ya Kilimo  na chakula  cha chuo kikuu cha Dar es salaam unaofanyika katika kijiji cha Likunja  wilayani Ruangwa unakamilika ndani ya miezi 18




Profesa kiliani Ameyasema hayo katika kikao kazi cha uzinduzi wa kamati ya "kasema" ambayo ni sehemu ya ulinzi na usalama wa mradi huo na  yenye jukumu la kuweka kumbukumbu za kile kinachoendelea katika mradi



Profesa kilian ametoa wito kwa kamati na  wananchi wa Ruangwa kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa mradi huo



Kamati hiyo ya " kasema " Ina wajumbe watano na inalengo la kukusanya na kushughulikia maoni au malalamiko ya wananchi katika eneo la mradi  husika 



Jukumu lingine la kamati hiyo ni kuweka kumbukumbu za kile kinachoendelea na kufanyika katika mradi huku ikiwa sehemu ya ulinzi na usalama katika utekelezaji wa mradi




Kwa upande wake Naibu mratibu wa Mradi  huo wa Elimu ya juu kwa mageuzi ya uchumi ( HEET)  Liberato Haule amesema mradi huo  unaotekelezwa  na chuo kikuu cha Dar es salaam umedhaminiwa na serikali kupitia fedha ya mkopo kutoka benk ya dunia ukilenga kuboresha huduma za Elimu ya juu nchini ili iweze kuchangia maendeleo ya uchumi.



Amesema mradi huo unatekelezwa katika maeneo mapya 14 ambapo mpaka sasa maeneo mapya matatu tayari yameshafikiwa ambayo ni pamoja na Ngongo (Manispaa ya Lindi), Likunja Wilayani Ruangwa pamoja na Halmashauri ya Bukoba mkoani  Kagera 





Mwenyekiti wa Halmashari hiyo Andrew  Chikongwe anatumia fursa hiyo kuitaka kamati hiyo kutimiza wajibu wao kwa maslah ya halmashauri hiyo





Baadhi ya viongozi na watendaji walioshiriki katika uzinduzi wa kamati hiyo wamepokea kwa shauku na matumaini makubwa na kwamba kituo hicho kitakuwa msaada  kwa wakulima na kuongeza fursa za kiuchumi



No comments:

Post a Comment