Tuesday, July 16, 2024

TFCG YAWEZESHA UPATIKANAJI WA HATI MILIKI ZA KIMILA 738 HALIMASHARI YA MTAMA 

 



Na Hadija Omary 


Katika kuiwezesha jamii kwenye usimamizi shirikishi wa misitu ya asili na kuondoa migogoro ya umiliki wa Aridhi shirika la kuhifadhi misitu Tanzania (TFCG) limewezesha upatikanaji wa hati miliki za kimila 738 kwa  wananchi wa vijiji 10 vya halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi 





Kijiji cha mihima ni miongoni mwa vijiji 10 vya halmashauri ya Mtama vilivyopo kwenye mradi wa  kuongeza usimamizi shirikishi wa misitu chini ya  shirika la kuhifadhi misitu Tanzania (TFCG)  baadhi ya wananchi walinufaika na hati miliki za kimila wanaeleza  faida na manufaa ya hati hizo




Yahaya mtonda ni meneja mradi wa kuongeza usimamizi shirikishi wa misitu kutoka TFCG amesema malengo ya utoaji wa hati hizo  ni kuiwezesha  jamii  kuzingatia misitu ya hifadhi ya vijiji kutoingiliwa na matumizi mengine





Victor shao ni mkuu wa kitengo cha maliasili na  uhifadhi wa mazingira halmashauri ya Mtama amesema tangu mwaka 2020 tfcg ilipoanzisha mradi wa kuongeza usimamizi shirikishi wa misitu katika halmashauri hiyo  vijiji hivyo vimeweza  kuanzisha sheria ndogo ndogo ili kuhakikisha wananchi hawavamii misitu hiyo

No comments:

Post a Comment