Tuesday, July 16, 2024

MCHINJITA AWAVUNA VIGOGO CHADEMA LINDI KUHAMIA ACT

 




NA HADIJA OMARY 



JUMLA ya wanachama 45 wa chama cha Demockasia na Maendeleo CHADEMA na viongozi wao Mkoani Lindi wamekihama chama chao na kujiunga na chama cha ACT wazalendo



Wanachama hao wamejiunga na chama cha Act kwa kurejesha Kadi zao za uanachama  na kupewa Kadi mpya za ACT, zoezi lililoongozwa na makamu Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo bara Bwana Isihaka Mchinjita 



Viongozi waliojiunga ACT ni pamoja na  aliekuwa Mwenyekiti Mkoa wa Lindi, Zainab Lipalapi; Mwenyekiti BAVICHA Mkoa wa Lindi, Said Mzee; Katibu wa Jimbo, Musa Rwegoshora; Mwenyekiti wa Wazee Jimbo, Bakari Likaku; Mweka Hazina wa Jimbo, Mohamed Mandoyo; na Mwenyekiti BAVICHA Jimbo, Doa Omari.



Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi Kadi zao mpya za ACT wazalendo  Mchinjita amewapongeza wanachama kwa uamuzi wao wa kujiunga  na chama hicho  na kwamba wamechagua  jukwaa sahihi


Nae  Bwana Mussa Rwegoshora  ambae alikuwa katibu wa chama cha Demockasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya Lindi amesema,  wameamua kujiunga na ACT kwa ajili ya kuunganisha nguvu ya pamoja ili kutetea maslah na Maendeleo ya Wana Lindi hivyo ni wajibu wao kuwa na jukwaa la pamoja la upinzani



" Sisi wote tumeamua kujiunga na ACT kwa ajili ya ukombozi wa Jimbo la Lindi na wala haya hayakuja kwa ghafla  ni mpango wa mwenyezimungu, wakati tunaendelea kudhoofika na madalali wa siasa mungu akasema hili haliwezekani ngoja wenya haki wakae huku na wenye dhulma waendelee kudhulumu wenzao"


No comments:

Post a Comment