Sunday, June 2, 2019

MADIWANI CHALINZE WAPEWA ELIMU

Diwani wa kata ya Mkange, Hussein Juma Hading'oka akichangia mada katika mafunzo hayo.
Afisa Mipango wa Halmashauri ya Chalinze, Shaabani Millao, akitwasilisha mada mbele ya madiwani wa Halmashauri hiyo.
.............................................


Na Omary Mngindo, Lugoba


MADIWANI wa Halmashauri ya Chalinze wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wamepatiwa mafunzo maalumu ya namna ya kusimamia miradi ya maendeleo katika maeneo yao.


Mafunzo hayo ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI, kuhusu usimamiaji wa miradi, kupitia sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2016 kuingiza utaratibu huo kwa kifungu 64 (5) cha sheria hiyo ya mwaka 2016.


Madiwani wakiongozwa na Mwenyekiti Said Zikatimu, Makamu Juma Mpwimbwi na Mkurugenzi Amina Kiwanuka, wakufunzi wa mafunzo Shaabani Millao ofisa mipango wa halmashauri na Dkt. Daud Paschal kutoka Chuo Kikuu Mzumbe idara ya Uhasibu na fedha wametoa mada mbalimbali.


Akisoma mada katika kikao hicho, Millao amewaambia madiwani hao kwamba, ofisi hiyo kupitia sekretariet za mikoa na Mamlaka za mitaa imetekeleza kwa ufanisi mkubwa miradi ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya na shule za msingi na sekondari.


"Kifungu 64 (6) cha sheria hiyo kinatoa maana ya matumizi ya manunuzi ya umma ambayo ni utaratibu wa ushirikiano wa taasisi za umma kufanya ujenzi kwa kutumia wafanyajazi wake na mitambo yake yenyewe au kwa kushirikiana na taasisi za umma au nyingine binafsi," ilieleza sehemu ya taarifa ya Millao.


Imeongeza kwamba utaratibu huo umefafanuliwa katika sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2011, kanuni ya 167 ya ununuzi ya mwaka 2013 na sheria ya (marekebisho) ya 2016 kanuni ya 64 za ununuzi wa umma ya mwaka huo.


Taarifa ya Dkt. Paschal imegusia masuala ya fedha ambayo imewataka wanaosimamia miradi katika maeneo ya wananchi kuwajulisha wananchi fedha zinazoingia katika miradi yao, hatua itayowaongezea hamasa ya kujitoa kwenye utekelezaji wake.


"Fedha lazima zipokelewe kwa kukiri mapokezi ha kiadi kilichopokelewa, jamii husika ijulishwe kupitia mikutano kiasi kilichopokelewa, pia kuhimizwa wahusika kuchangia nguvu ili wajisikie kuwa wao ni wamiliki wa miradi," ilieleza taarifa ya Dkt. Paschal.


Kwa upande wao madiwani Ramadhani Mwinyikondo na Malota Kwaga wametaka mwongozo wa namna zinavyopatikana kamati za kusimamia miradi, na kujulishwa tofauti ya Mkandarasi na utaratibu mpya.


Rehema Mwene amegusia changamoto ya kuchelewa malipo ambapo mara kadhaa wamekuwa wakiambiwa kikwazo ni epika, hivyo wameomba washirikishwe kikamilifu ili wajionee sababu zinazochangia hali hiyo ya ucheleweshwaji wa malipo mbalimbali.


Kwa upande wake Zikatimu alisema kuwa utaratibu wa sasa wa manunuzi umekuwa mkombozi katika utekelezaji wa miradi ukilinganidha na hapo awali, ambapo miradi mingi ilikuwa inasuasua kutokana na mlolongo wa kumpata mkandarasi.

WAKAZI PWANI WATAKIWA KUONGEZA UPENDO

Na Omary Mngindo, Kibaha.


WAKAZI Mkoa wa Pwani wametakiwa kuendeleza umoja, upendo na mshikamano, ambao hauna ubaguzi wa dini ya aina yeyote.


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa huo Mhandisi Evarist Ndikilo, katika futari iliyoandaliwa na mmiliki wa shule ya KIPS iliyoko Kibaha Mailimoja mkoani hapa Alhaj Yusufu Mginanga ambae pia ni mmiliki wa hoteli Njuweni.


Alisema kwamba dini imeendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya haraka nchini, kutolana na viongozi wake kuwahimiza waumini wake katika kuzingatia upendo, umoja na mshikamano na kuondoa utofauti ambao zinaambatana na udini.


"Nawapongeza viongozi wa dini mkoani Pwani, baadhi yenu hivi karibuni tumesafiri kwenda kujionea mradi mkubwa wa umeme wa maji Mto Rufiji, unaotekelezwa na serikali chini ya Rais Dkt. John Magufuli, nawapongeza kwa kazi zenu za kuhimiza amani, umoja, upendo na mshikamano," alisema Mhandisi Ndikilo.


Aliongeza kwamba mradi huo unaotaraji kuinufaisha nchi yetu katika kuhakikisha kunakuwepo na umeme wa uhakika, amewaomba viongozi wa dini wamuombee Rais aendelee kuwa na afya njema, pia kwa kazi kubwa ya kuuanzisha mradi huo ulioasisiwa na watangulizi wake.


"Wakoloni hawakuupenda mradi huu, sababu kubwa ni kwamba wamejua ungeleta maendeleo makubwa katika nchi yetu ya Tanzania, hivyo hatua ya Rais Magufuli kuuendeleza ni kitendo cha ujasili wa hali ya juu, tuanapaswa kuunga mkono kwa kazi hiyo," alisema Mhandisi huyo.


Kwa upande wake mkurugenzi wa Kampuni hiyo Alhaj Mfinanga amewataka wakazi mkoani hapa, pasipo kujali itikadi zao za dini, rangi wala siasa katika kuhakikisha kila mmoja anamsaidia Rais Magufuli katika utekelezaji wa ujenzi wa nchi, huku akisisitiza elimu.


Akizungumzia shule ya KIPS, Mfinaga alisema kwamba ilianzishwa mwaka 2002 ikiwa ni shule ya awali na msingi, ambapo tangu kipindi hicho inaendelea na utoaji wa elimu na kwamba wanafunzi wanafanya vizuri katika mithihani yao ya kuingia kidato cha kwanza.


Baadhi ya waumini wa dini waliohudhulia futari wamemshukuru mmiliki wa shule hiyo, huku wakimhaidi Mkuu wa Mkoa kwamba wataendelea na utoaji wa elimu katika nyanja mbalimbali ikiwemo kudumisha amani, umoja, upendo na mshikamano.

JUMAA ASAIDIA PWANI POLISI VIFAA VYA UJENZI

MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani Humoud Jumaa, akimkabidhi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP. Wankyo Nyigesa, risiti iliyonunuliwa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi milioni 2.8.
.................................................... 

Na Omary Mmgindo, Kibaha.

MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani Humoud Jumaa, amekabidhi Jipsam 100 na ndoo tano za rangi vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 2.8.


Katika hafla fupi iliyofanyika eneo linalojengwa nyumba 20 za jeshi hilo mkoani Kibaha mjini hapa, Jumaa amemkabidhi Kamanda wa jeshi hilo Wankyo Nyigesa Jipsam hizo, kwa ajili ya ujenzi huo unaolenga kuwaweka pamoja askari hao.


"Nilikuja nikakutana na Kamanda Nyigesa kanielezea mikakati ya ujenzi wa nyumba 20 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali chini ya Dkt. John Magufuli inayotazama sekta zote, ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani, leo nimekabidhi jipsam na ndoo za rangi za sh. Mil. 2.8,


"alisema Jumaa. Alisema kuwa anapongeza jeshi hilo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wilayani hapa na Mkoa kwa ujumla wanaishi kwa amani, upendo na mshikamano mkubwa ambao unachangiwa na uwepo wa askari Polisi.


"Nimpongeze Rais Dkt. John Magufuli kwa uongozi wake unaojali maendeleo ya watu wake, tunashuhudia inavyoboresha sekta zote zikiwemo elimu, afya, miundombinu, umeme na ulinzi na usalama tunatakiwa kumuunga mkono kwa vitendo," alisema Mbunge huyo.


Kwa upande wake Kamanda Nyigesa alisema kwamba kwa sasa ili kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwezi wa sita, wanahitaji kiasi cha zaidi ya sh. Mil. 20 ili kukamilisha zoezi hilo, huku akiwaomba wadau zaidi wajitokeze katika kukamilisha mchakato huo.


"Niwaombe wabunge wengine na wadau mbalimbali wajitokeze katika kuunga mkono serikali yetu katika kuboresha masuala ya kimaendeleo kwenye nyanja zote," alisema Nyigesa. "


Tunapokea misaada kutoka kwa watu mbalimbali paaipokujali itikadi za kisiasa, polisi wananchi wote weti pasipokujali itikadi zao za kisiasa," alimalizia Kamanda Nyigesa.

Friday, May 31, 2019

WAISLAMU WATAKIWA KUWASAIDIA MASIKINI.

 Mwenyekiti wa Taasisi ya  Adullah Aid Tanzania, Arif Yusuf
 ..........................................

Na Shushu Joel,chalinze.

TAASISI ya Miraj Islamic Centre yenye makao yake mkuu jijini Dar es Salaam imetoa wito kwa watu wote walio na nafasi ya kipato kuweza kuwasaidia wasio na kipato kama ilivyoagizwa katika vitabu vya Mungu. 


Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa taasisi hiyo Sheikh Arif Yusuf Abdulrehman maarufu Arif Tanzania alipokuwa akizungumza na baadhi ya waislamu wakati wa zoezi la kugawa futari kwa wakazi wa vikindu wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.


Arif, alisema kuwa Taasisi yake imekuwa miongoni mwa taasisi za kuigwa ndani na nje ya Tanzania kwa jinsi inavyojitolea kuwasaidia watanzania wote bila ya kujali dini zao wala kabila huku lengo likiwa ni kuwaonyesha wale wasio na uwezo kuona ni sawa na wenye uwezo.


"Unaposaidia wenzako Mwenyezi Mungu anakuongezea kutokana na jinsi wale unaowasaidia wanavyokuombea uweze kupata ili uendelee kuwasaidia zaidi"Alisema Arif Tanzania. 


Aliongeza kuwa kwa kipindi hiki cha mwezi huu wa Ramadhani taasisi ya Miraj Islamic imewezesha sehemu mbalimbali kwa ajili wananchi vyakula na tende kwa baadhi ya mikoa kama vile Arusha, Pwani, Mwanza, Kigoma, Zanzibar na Mikoa mingine kwa kusudi la kuwasaidia wasio na uwezo wala kipato ila wanafunga Ramadhani.


Aidha alisema kuwa Taasisi yake imekuwa msaada mkubwa kwa serikali kutokana na jinsi inavyojitoa katika masuala ya kusaidia watu mbalimbali ili waweze kujikwamua katika maisha yao, watu hao ni pamoja na kuwasaidia usafiri walemavu, vijana kuwapatia mashine za kukamulia juice na wengine kuwapatia pikipiki kwa ajili ya kufanya shughuli za boda boda, kinamama kuwawezesha kwa Vyerehani ya ushonaji. 


Hivyo kama kila mwenye nafasi ya kipato akijitolea kwa moyo mmoja basi watakuwa wamewafikia watanzania wengi na kuwawezesha ili nao waondokane na umasikini walionao. 


Pia Arif Tanzania ameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt John Magufuli kwa jinsi inavyofanya kazi zake na Viongozi wa Dini zote na kuwakomboa watanzania wa hali za chini. 


Kwa upande wake Ashura Juma (81) mkazi wa vikindu katika wilaya ya mkuranga mkoani Pwani ameipongeza taasisi ya Miraj Islamic Centre kwa jinsi inavyojitolea katika kutoa misaada mbalimbali kwa wanyonge.


 Aliongeza kuwa kwa kipindi hiki cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kupitia taasisi hiyo familia yake imekuwa moja ya wanufaikaji wakubwa kwa kupata misaada mingi ikiwemo Chakula kwa ajili ya futari, fedha na mahitaji mengine mengi ya kibinadamu. 


Aidha Mama huyo amemtaka Mwenyekiti wa taasisi hiyo Arif Tanzania kuendelea na tabia hiyo ya kujitolea kwani wanufaika wako wengi na wataendelea kumuombea ili aweze kupata. 


Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa halmashauri ya chalinze katika wilaya ya bagamoyo, Mbunge wa jimbo hilo Ridhiwani Kikwete amesema kuwa misaada hiyo inayotolewa na taasisi hiyo imekuwa na tija kubwa kwa waumini wa dini ya kiislamu kutokana na uhitaji wa futari kwenye kipindi hiki. 


Mbali na hilo Kikwete alisema kuwa pongezi hizo si kwa wananchi bali hata serikali imekuwa ikinufaika na Arif Tanzania kupitia taasisi zake zinazojitolea kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya wanyonge. 


"Kutokana na jinsi taasisi hii inavyojitolea katika ufanikishaji wa wa misaada ni lazima sie kama wawakilishi tuisemee vizuri ili wengine wajitokezw "alisema