Thursday, September 12, 2024

MAGEUZI MAKUBWA WAKALA WA VIPIMO (WMA)

 

Na Albert Kawogo 


SERIKALI kupitia Wakala wa vipimo nchini (WMA)imefanya mageuzi makubwa yanayolenga kumlinda mlaji kwenye huduma na ubora wa vipimo vinavyotumika kwenye sekta za biashara, afya na mazingira.


 Mtendaji Mkuu wa WMA Alban Kiula amesema hayo jana wakati akiongea Jijini Dar es Salaam na Wahariri kutoka Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ukiwa ni mfululizo wa vikao vya Taasisi za Umma zilizoko chini ya msajili wa hazina. 


Kiula alisema WMA ina jukumu kubwa la kuilinda jamii kwenye athari zinazotokana na matokeo ya upimaji usio sahihi katika biashara na maeneo mengine mtambuka.


"Unaweza usiione hii hali lakini kuna madhara makubwa kijamii yatokanayo na upimaji usio sahihi hasa kiuchumi" Alisema Kiula


Mtendaji Mkuu alisema jukumu la WMA  haliishii tu kwenye kusimamia na kudhibiti vipimo bali pia taasisi hiyo inatoa ushauri wa kitaalam kuhusiana na vipimo Kwa serikali, mashirika ya umma na Taasisi binafsi.


Pia Kihula alisema moja ya mafanikio makubwa ya WMA ni kuongezeka kwa idadi ya vipimo vinavyohakikiwa na kuendelea na ununuzi wa vifaa vya kitaalam ambapo yote haya yameipa thamani taasisi hiyo


Akizungumza kwa niaba ya Wahariri Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania TEF Deodatus Balile alisema kazi kubwa ya kupongezwa imefanywa na WMA lakini bado changamoto ipo kwenye uchache wa watendaji kwakuwa jukumu lao kama WMA lina wigo mpana wa kiutendaji hasa kwenye yale maeneo yanayogusa walaji Kwa bidhaa za chakula na vifaa vya ujenzi.

No comments:

Post a Comment