Tuesday, September 17, 2024

MADAKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA WAWEKA KAMBI MKOANI LINDI

 

Na Hadija Omary, LINDI.


Wananchi Mkoani Lindi wametakiwa kutumia siku sita za ujio wa madaktari bingwa na ubingwa bobezi wa Rais Samia kupata huduma za kibingwa kwa karibu katika hospitali za Wilaya  za Mkoa huo


 

Rai hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi Dkt Kheri Kagya Jana  septemba 16, 2024 wakati wa kuwapokea madaktari hao bingwa na bingwa bobezi wa Rais Samia katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa lindi kisha kuwakabidhi kwa waganga wakuu wa halmashauri sita za mkoa huo



Madaktari hao watakuwepo kwa muda wa siku 6 kuanzia Jana Septemba 16 hadi 21 wakitoa huduma za kibingwa kwenye hospitalli zote za halmashauri Mkoani Lindi lengo likiwa  kusogeza huduma za kibingwa na ubingwa bobezi karibu zaidi na wananchi pamoja na kuwajengea uwezo wataalam wa afya kwa ngazi ya halmashauri kutoa huduma hizo za kibingwa.



Dkt. Kagya ametaja madaktari waliopokelewa ni pamoja na madaktari bingwa wa huduma za magonjwa ya kike na uzazi, upasuaji, mfumo wa mkojo, magonjwa ya ndani, huduma za mifupa, watoto, ganzi na usingizi.



Amesema huduma hizo zitatumia bima na kwa wagonjwa wasio na bima watamuona daktari na Kuchangia Kiasi kidogo kwa utaratibu wa kawaida kama atahitajika kupata huduma nyingine ikiwemo vipimo, upasuaji na dawa.



Awali, akizungumza Mwakilishi kutoka Wizara ya afya ambaye pia na mratibu wa madaktari hao waliotoka hospitali mbalimbali hapa Nchini  Faraja Mgeni amewakumbusha Madaktari kwenda kufanya kazi kwa kujituma zaidi na kuzingatia maadili ili kutimiza lengo la Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Wizara ya Afya kwa wananchi huku akiomba waganga wakuu kwenye halmashauri kuwapa ushirikiano wa kutosha ili waweze kutimiza majukumu yao.





No comments:

Post a Comment