Wednesday, June 22, 2016

MARUFUKU KUTOA HATI YA ARDHI KATIKA MAENEO YA RANCHI BAGAMOYO.


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Kushoto, Majid Hemedi Mwanga, akiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aliy Aliy katika mkutano uliofanyika kijiji cha Kidomole kata ya Fukayosi wilayani humo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo Aliy Aliy amepiga marufuku utoaji wa hati za ardhi ikiwemo hati za kimila, katika maeneo yanayopakana na ardhi iliyohifadhiwa kama vile Ranchi ya Zanzibar Bagamoyo (RAZABA) inayomilikiwa na wizara kilimo Zanziba, na Ranchi ya ruvu iliyopo wilayani Bagamoyo ambayo iko chini ya umiliki wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO).

Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ametoa kauli hiyo katika mkuu maalum wa kijiji cha Kidomole kata ya Fukayosi wilayani hapa na kuongeza kuwa afisa aridhi atakaebainika kutoa hati katika kipindi hiki ndani ya maeneo hayo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwemo kusimamishwa kazi.
Kauli hiyo ya Mwenyekiti huyo imekuja kufuatia taarifa za kuuzwa kwa baadhi ya maeneo ndani ya Ranchi hizo jambo ambalo ni kinyume na sheria kwakuwa kampuni zinazomiliki maeneo hayo bado hazijavuliwa umiliki wake.

Aidha, amemuomba mkuu wa wilaya ya Bagamoyo kuanda mpango wa uhakiki mipaka katika maeneo hayo ili kuondoa utata uliopo baina ya Ranchi hizo na wananchi hasa katika vijiji vinavyopakana na Ranchi hizo.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majidi Hemedi Mwanga, amewataka kuacha kuvamia maeneo yalihifadhiwa ili kuepusha usumbufu wa kuondolewa kwa nguvu na serikali.
Majidi alitolea mfano wa maeneo yalihifadhiwa ikiwa ni pamoja na Hifadhi za misitu, Ranchi za taifa na maeneo tengefu kwaajili ya shughuli maalumu kama vile Barabara.

Aidha, alisema serilkali ya wilaya haitavumilia kuona mwananchi yeyote anavamia maeneo hayo ili kujenga nidhamu ya utawala bora, haki na utii wa sheria bila ya shuruti.
Akitoa kauli hiyo katika mikutano ya kutatua migogoro ya aridhi wilayani hapa, mkuu huyo wa wilaya amewataka wananchi wenye mahitaji ya ardhi katika vijiji kushirikiana na viongozi wa vjiji kuainisha mahitaji yao ya aridhi ili kuona kama kuna haja ya kuomba kuongezewa ardhi kwaajili ya matumizi ya makazi na kilimo.

Hata hivyo aliwataka viongozi wa vijiji kuelezea aridhi waliyonayo katika vijiji vyao na wanaitumia kwa kazi ipi huku akiwataka kutoa ufafanuzi kuhusu watu waliopewa aridhi na vijiji ili kuona kama sheria zinamefuatwa.

Alisema si vyema kuona wananchi wanatafuta aridhi na kuvamia maeneo yaliyohifadhiwa wakati serikali ya kijiji inatoa aridhi kwa wawekezaji bila ya kufuata taratibu za ugawaji wa ardhi.

Imeandikwa na Athumani Shomari.

No comments:

Post a Comment