Saturday, August 8, 2026

VERONICA MREMA WA TANZANIA AINGIA SITA BORA TUZO ZA ISU ELIHLE 2026 AFRIKA

 

Na Mwandishi Wetu


Mtanzania Veronica Mrema , mwanachama wa Mtandao wa Mabloga Tanzania , TBN, anayeendesha jukwaa la kidijiti la  M24 TANZANIA MEDIA ni miongoni mwa waandishi wa  habari sita  waliochaguliwa kuendelea na mchakato wa tuzo za ISU Elihle kwa mwaka 2026 Barani Afrika.




Veronica ametajwa katika orodha hiyo baada ya wazo lake la habari kuhusu watoto wanaoishi na ugonjwa wa Siko Seli kupitiwa, na kuonekana ni bora.




Jopo la majaji wa tuzo hizo limesema kulikuwa na mawazo 155 ambayo walipokea kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

Hatua ya Veronica kutajwa kwenye tuzo hiyo inaongeza rekodi nzuri katika uandishi wa habari za afya na maendeleo na kuiweka Tanzania katika nafasi ya kuendelea kutoa waandishi wa habari wanaotumia kalamu zao kuibua changamoto za watoto na kuchochea mabadiliko yenye manufaa kwa jamii.




Kupitia wazo lake lililochaguliwa Veronica atafanya uchunguzi na kuibua simulizi kuhusu mzigo unaoongezeka wa ugonjwa wa Siko Seli miongoni mwa watoto nchini Tanzania, akiangazia kwa kina namna ugonjwa huo unavyoathiri maisha ya watoto, kuanzia afya zao, lishe, elimu, ukuaji wa kimwili, pamoja na ustawi wao wa kihisia na kisaikolojia.




Kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya, idadi ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa wa Siko Seli nchini imeongezeka kutoka takribani watoto 8,000 hadi 14,000 kila mwaka, hali inayoifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye mzigo mkubwa wa ugonjwa huo Afrika na duniani. 




Tanzania inatajwa kuwa miongoni mwa nchi tatu zenye idadi kubwa ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo Barani Afrika kila mwaka huku ikishika nafasi ya nne duniani.




Pamoja na ukubwa wa tatizo hilo, bado kuna watoto  hukumbana na changamoto za kuchelewa kugundulika, ukosefu wa huduma maalum za matibabu na uelewa mdogo wa jamii kuhusu ugonjwa huo.




Veronica atakusanya simulizi za watoto wanaoishi na Siko Seli, wazazi na walezi wao, wataalamu wa afya, wataalamu wa lishe pamoja na watunga sera, kwa lengo la kuonesha hali halisi ya maisha yao na kuibua suluhisho zinazoweza kuboresha afya na ustawi wa watoto hao.




Akizungumza baada ya kutangazwa kuwa mmoja wa washindi, Veronica amesema amepokea kwa heshima kubwa kutajwa katika orodha hiyo ya ISU Elihle.




"Ni fursa ya kuendelea kutumia uandishi wa habari kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

"Kuchaguliwa miongoni mwa waandishi sita kutoka kazi 155 zilizowasilishwa ni heshima kubwa kwangu na kwa Tanzania. 




Lakini zaidi ya yote, ni nafasi ya kuhakikisha sauti za watoto wanaoishi na Siko Seli zinasikika.




"Ninaamini simulizi hizi zitasaidia kuongeza uelewa wa jamii na kuhimiza uwekezaji zaidi katika uchunguzi wa mapema, huduma za afya na lishe kwa watoto hawa," amesema.




Ameongeza atatumia uandishi wa habari unaozingatia ushahidi, takwimu na simulizi za wahusika ili kuonesha changamoto halisi zinazowakabili watoto wenye Siko Seli na kuibua mijadala itakayochochea maboresho ya sera na huduma za afya.




ISU Elihle Award inalenga kuhamasisha uandishi wa habari unaoweka watoto katikati ya simulizi na unaochochea mijadala yenye kuleta mabadiliko ya sera, uwajibikaji na hatua za kuboresha ustawi wa watoto barani Afrika.




Pamoja na Veronica Mrema wa Tanzania, washindi wengine wa ISU Elihle Award 2026 ni David Arome wa The Development Report [Nigeria] na Hind Fawzi wa Medina FM [Morocco], Rakiya Mohamed wa Blueprint [Nigeria], Wezzie Joy Gausi wa Times Group [Malawi] na Kelvin Tambo wa Capital Radio [Malawi].




Kupitia tuzo hiyo, washindi watapata fursa ya kutekeleza miradi yao ya uandishi kwa msaada wa wahariri na wataalamu wa uandishi wa habari, pamoja na ushauri wa kitaalamu [mentorship] ili kuhakikisha simulizi hizo zinafikia viwango vya juu vya ubora na kuleta athari chanya kwa jamii.




Katika hatua hii, pia watapewa kiasi cha R.10,000 ili kwenda kutekeleza miradi ya uandishi wa makala kulingana na mawazo yao ya habari ambayo waliyawasilisha katika mchakato huo wa kwanza.




Baadae kazi zao zitapitia mchakato wa awamu ya pili ambapo zitashindanishwa ili kupata washindi watatu bora, miongoni mwao.


KIKWETE ATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI YA MJI BAGAMOYO NANENANE

 

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ametembelea Banda la Halmashauri ya Mji Bagamoyo katika maonesho ya Nanenane kanda ya mashariki Mkoani Morogoro.


Dkt Jakaya amewasalimu Wajasiliamali wote waliokuwa katika Banda na watumushi wote  pamoja na kuona bidhaa walizonazo katika maonesho hayo huku akipendezwa na ubunifu wao katika bidhaa zao.


Halmashauri ya Mji Bagamoyo imeendelea kuwa washiriki wazuri katika maonesho ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi Nanenane kwa kuendelea kuwa wabunifu wa utengenezaji wa Bidhaa mbalimbali kwa kila Mwaka.












Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ametembelea Banda la Halmashauri ya Mji Bagamoyo katika maonesho ya Nanenane kanda ya mashariki Mkoani Morogoro.


Dkt Jakaya amewasalimu Wajasiliamali wote waliokuwa katika Banda na watumushi wote  pamoja na kuona bidhaa walizonazo katika maonesho hayo huku akipendezwa na ubunifu wao katika bidhaa zao.


Halmashauri ya Mji Bagamoyo imeendelea kuwa washiriki wazuri katika maonesho ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi Nanenane kwa kuendelea kuwa wabunifu wa utengenezaji wa Bidhaa mbalimbali kwa kila Mwaka.



Thursday, August 6, 2026

SAMIA ANASIHI UTOAJI WA MIUNDOMBINU AFRIKA NZIMA.

 

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

amezitaka serikali za Afrika kuharakisha utoaji wa miundombinu na kubadilisha uwezo wa kiuchumi wa bara hilo kuwa faida zinazoonekana kwa watu wake.


Akifungua Jukwaa la Infra for Africa na Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50 leo jijini Dar es Salaam, Rais Samia alisema watu hupima maendeleo kupitia huduma na fursa zilizoboreshwa, badala ya sera na mipango ya maendeleo.


Alitaja umeme wa kuaminika, bandari zenye ufanisi, barabara na reli za kisasa, muunganisho wa kidijitali, na ajira nzuri kama viashiria vilivyo wazi vya maendeleo yenye maana.


Rais alisema miundombinu imara zaidi itaongeza ushindani wa Afrika, kuvutia uwekezaji, kupanua biashara ya ndani ya Afrika, na kuimarisha uchumi dhidi ya mshtuko wa kimataifa.


Rais Samia alisema Tanzania inatekeleza Dira yake ya Maendeleo ya Kitaifa ya 2050, ambayo inalenga kujenga uchumi jumuishi, wa viwanda unaoendeshwa na uvumbuzi, maendeleo ya ujuzi, na miundombinu ya kisasa.


Aliongeza kuwa Serikali inaboresha Bandari ya Dar es Salaam, Reli ya Standard Gauge, barabara, madaraja, na njia za kimkakati za usafiri ili kuimarisha nafasi ya Tanzania kama lango la biashara na usafirishaji kikanda.


Rais alibainisha kuwa uwekezaji huu pia unahudumia nchi jirani zinazohusishwa na ardhi, ikiwa ni pamoja na Burundi, Rwanda, Uganda, Zambia, Malawi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.


Rais Samia alisema uanachama wa Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) unaiweka nchi hiyo kama daraja la asili la biashara na uwekezaji wa kikanda.


Alizitaka zaidi nchi za Afrika kusindika zaidi maliasili zao ndani ya nchi, badala ya kuuza nje malighafi, ili kuunda ajira, kujenga ujuzi, na kupanua uwezo wa viwanda.


Rais pia aliangazia gesi asilia kama rasilimali ya kimkakati ya kuimarisha usalama wa nishati, kuendesha ukuaji wa viwanda, na kusaidia mabadiliko mapana ya kiuchumi nchini Tanzania na kote Afrika.


Akizungumza katika tukio hilo, Naibu Rais wa Kenya Profesa Kithure Kindiki alisema miradi mikubwa ya miundombinu inahitaji uongozi endelevu wa kisiasa, sera zinazotabirika, na mipango ya muda mrefu.


Alitoa wito wa kuimarisha uwezo wa kiufundi wa ndani, ufadhili bunifu, na ushiriki mkubwa zaidi wa jamii ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatoa faida pana na za kudumu.


Mwenyekiti wa Africa50 na Rais wa Kundi la Benki ya Maendeleo ya Afrika, Dkt. Sidi Ould Tah, alisema taasisi hiyo itaunga mkono serikali katika kubadilisha fursa za miundombinu kuwa miradi inayoweza kufadhiliwa na benki, iliyo tayari kwa uwekezaji.


Alisema muongo wa pili wa Africa50 unapaswa kuzingatia utekelezaji wa miradi wa haraka, uhamasishaji wa kina wa mitaji, na ushirikiano imara zaidi miongoni mwa serikali, taasisi za fedha za maendeleo, na wawekezaji binafsi.


Mawaziri kutoka Tanzania, Msumbiji, Nigeria, na Senegal pia walijadili nishati na ukuaji wa viwanda, wakisisitiza hasa gesi asilia, uongezaji wa thamani, na miundombinu ya mipakani.


Jukwaa lilisikia kwamba zaidi ya Waafrika milioni 600 bado hawana umeme.


Wakati huo huo, Tanzania imeongeza upatikanaji wa suluhisho safi za kupikia kutoka asilimia 6 mwaka 2021 hadi asilimia 28 mwaka 2026.


Wakati wa kongamano hilo, Tanzania pia ilisaini makubaliano yanayohusu huduma ya figo iliyopanuliwa, uwekezaji wa umma na binafsi katika usafirishaji wa umeme, na kuongezeka kwa matumizi ya gesi asilia viwandani.


Mikataba hiyo inahusisha Africa50, Wizara ya Afya ya Tanzania, Kampuni ya Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na TAQA Arabia.


Rais Samia aliipongeza Africa50 kwa kuendelea kuunga mkono ajenda ya miundombinu ya bara hilo na kuwataka pande zote kuhama haraka kutoka mikataba iliyosainiwa hadi miradi inayoleta maboresho yanayoonekana katika maisha ya watu.

SAMIA URGES FASTER INFRASTRUCTURE DELIVERY ACROSS AFRICA.

 

Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania,

has urged African governments to accelerate infrastructure delivery and transform the

continent’s economic potential into tangible benefits for its people.




Opening the Infra for Africa Forum and the Africa50 General Shareholders’ Meeting today in Dar es Salaam, President Samia said people measure progress through improved services and opportunities, rather than policies and development plans.




She cited reliable electricity, efficient ports, modern roads and railways, digital

connectivity, and decent jobs as the clearest indicators of meaningful development.

The President said stronger infrastructure would enhance Africa’s competitiveness, attract investment, expand intra-African trade, and strengthen economies against global shocks.




President Samia said Tanzania is implementing its National Development Vision 2050, which aims to build an inclusive, industrialised economy driven by innovation, skills development, and modern infrastructure.




She added that the Government is upgrading the Port of Dar es Salaam, the Standard Gauge Railway, roads, bridges, and strategic transport corridors to strengthen Tanzania’s position as a regional trade and logistics gateway.




The President noted that these investments also serve neighbouring land-linked countries, including Burundi, Rwanda, Uganda, Zambia, Malawi, and the Democratic Republic of the Congo.




President Samia said Tanzania’s membership in both the East African Community (EAC) and the Southern African Development Community (SADC) positions the country as a natural bridge for regional trade and investment.




She further urged African countries to process more of their natural resources locally, rather than exporting raw materials, in order to create jobs, build skills, and expand industrial capacity.




The President also highlighted natural gas as a strategic resource for strengthening energy

security, driving industrial growth, and supporting broader economic transformation in Tanzania and across Africa.




Speaking at the event, Kenyan Deputy President Prof. Kithure Kindiki said major infrastructure projects require sustained political leadership, predictable policies, and long-term planning.



He called for stronger domestic technical capacity, innovative financing, and greater

community participation to ensure development projects deliver broad and lasting benefits.




Africa50 Chairman and President of the African Development Bank Group, Dr. Sidi Ould Tah, said the institution would support governments in converting infrastructure

opportunities into bankable, investment-ready projects.




He said Africa50’s second decade should focus on faster project execution, deeper capital mobilisation, and stronger partnerships among governments, development finance institutions, and private investors.




Ministers from Tanzania, Mozambique, Nigeria, and Senegal also discussed energy and industrialisation, with particular emphasis on natural gas, value addition, and cross-border infrastructure.




The forum heard that more than 600 million Africans still lack access to electricity.

Meanwhile, Tanzania has increased access to clean cooking solutions from 6 per cent in

2021 to 28 per cent in 2026.




During the forum, Tanzania also signed agreements covering expanded renal care, public-private investment in electricity transmission, and increased industrial utilisation of natural gas.




The agreements involve Africa50, Tanzania’s Ministry of Health, the Tanzania Electric

Supply Company (TANESCO), the Tanzania Petroleum Development Corporation

(TPDC), and TAQA Arabia.




President Samia commended Africa50 for its continued support of the continent’s

infrastructure agenda and urged all parties to move swiftly from signed agreements to

projects that deliver tangible improvements in people’s lives.

RAIS SAMIA NA MUSEVEN WASHUHUDIA UTIAJI SAINI KITUO CHA NISHATI CHAKIKANDA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa kati ya Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bw. Mussa Makame, Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bi. Proscovia Nabbanja pamoja na Kampuni ya Biashara ya Mafuta na Nishati ya Vitol ya Bahrain, chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Tom Baker.