Posts

SWEETBERT NKUBA AAHIDI KULETA MABADILIKO TLS.

Image
  Na Mwandishi Wetu Mgombea wa urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Sweetbert Nkuba ameelezea namna ambavyo amejipanga kuleta mabadiliko ndani ya chama hicho endapo atachaguliwa kushika nafasi hiyo. Moja ya mipango yake amesema ni kuboresha miundombinu ya TLS, uimarishaji wa miundombinu ya kisheria na kiteknolojia ili kuwezesha huduma bora kwa wanachama na jamii hususani kuongeza uwekezaji katika mifumo ya kidijitali ya kurahisisha upatikanaji wa taarifa na huduma za kisheria na kuboresha ofisi za TLS katika mikoa mbalimbali kwa vifaa vya kisasa na miundombinu bora. Jambo la pili anasema atasisitiza mafunzo endelevu kwa wanachama wa TLS ili kuhakikisha kuwa wanasheria wanakuwa na ujuzi wa kisasa na uwezo wa kushindana kimataifa ikijumuisha kuanzisha programu za mafunzo ya mara kwa mara kuhusu sheria mpya na mabadiliko ya sheria pamoja na kushirikiana na taasisi za kimataifa kwa mafunzo na kubadilishana uzoefu. La tatu anasema atahakikisha TLS inakuwa na sauti yenye nguvu...

KATIBU MKUU CCM, DKT NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI MKAPA.

Image
  CCM YATOA MILIONI 10 KUBORESHA MAJENGO YA SHULE LUPASO Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi ametembelea kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya 3, hayati Benjamin William Mkapa katika Kijiji cha Lupaso mkoani Mtwara, leo Julai 28, 2024, kuhani familia na kuzungumza na wananchi wa Lupaso. Balozi Nchimbi amesema “naomba nikiri kuwa mimi ni mwanafunzi wa hayati na nimekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Taifa (UVCCM), katika kipindi chake, ndiye alinilipia ada ya kusoma chuo kikuu na alikuwa mfuatiliaji sana na alitulea vizuri, sio sisi tu, bali Watanzania wote aliwalea pia. Alikuwa mzalendo kwa nchi, alifanya mabadiliko makubwa kwa nchi yake na kwa Chama chake, lakini yote CCM chini ya Dkt Samia tutaendelea kuyaenzi yale yote aliyoyoacha hayati Benjamin Mkapa.  Pamoja hayo nimeambiwa kero za hapa na tumezichukua. CCM inatoa shilingi milioni 10 kuanza kukarabati shule ya hapa Lupaso.” Katika ziara hii Dk Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, ...

NANI KUUKWAA URAIS WA TLS UCHAGUZI WA IJUMAA?

Image
  Na Mwandishi Wetu KAMPENI za Uchaguzi Mkuu wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), ambao unatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa wiki hii zinaendelea kupamba  moto ambapo wagombea wanaendelea kunadi sera wakitaka kufanya mabadiliko kwenye taasisi hiyo. Mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo, Sweetbert Nkuba, alisema mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam kuwa anataka nafasi hiyo ili akapambane na mawakili ambao hawana sifa ya kufanyakazi hiyo. TLS ni taasisi muhimu inayochangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha mfumo wa sheria na haki nchini Tanzania na kwa mwaka huu wagombea wa nafasi ya urais kwenye uchaguzi huo watakuwa sita, ambao ni Boniface Mwabukusi,  Emmanuel Muga, Ibrahim Bendera,  Paul Kaunda, Revocatus Kuuli na Sweetbert Nkuba. Nkuba alisema anauzoefu wa muda mrefu wa uongozi katika ngazi mbalimbali na kuomba achaguliwe kwenye nafasi hiyo ili afanikishe vipaumbele vitano ikiwemo kuwaunganisha wanachama wa TLS na kuhakikisha maslahi ya kiuchumi ya wanachana wa...

SHAHIDI AELEZA MUME WAKE ALIVYOPIGWA NA NATHWANI MPAKA KUZIMIA.

Image
  Na Mwandishi Wetu  SHAHIDI Kiran Lalit Ratilal (52), ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam jinsi mume wake alivyopigwa na mshtakiwa Bharat Nathwan (57) hadi kupoteza fahamu kutokana na ugomvi ambao ulikuwa unaendelea wa baina yao kuhusu ujenzi uliyokuwa unaendelea katika eneo la makazi yao.   Nathwan pamoja na mke wake Sangita Bharat (54) wanaoishi Mtaa wa Mrima - Kisutu, jengo la Lohana Dar es Salaam wanatuhumiwa kwa mashtaka manne likiwemo la kujeruhi waliyoyatenda Julai 21,2023 kinyume cha sheria.   Akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Grace Mwanga, Kiran alidai kuwa anakumbuka Julai 21, 2023 alikuwa nje ya akiendelea na majukumu yake nanpia shughuli za mapambo zilikuwa zinaendelea nyumbani kwake mafundi wakiweka vigae.   Alidai kuwa, mshtakiwa Sangita alitoka ndani akaanza kupaza sauti akitaka atoe malighafi (material) yote yaliyokuwepo kwenye kibaraza hicho, wakati yote yapo upande wa Kiran Lalit Ratilal na sio upande wake.  ...

MAAFISA UANDIKISHAJI DAFTARI LA MPIGA KURA KAGERA WALA KIAPO

Image
  Na Alodia Dominick,  Bukoba, Maafisa uandikishaji ngazi ya wilaya na maafisa ugavi mkoani Kagera wamekula kiapo ili kwenda kutekeleza shughuli mbalimbali za tume huru ya Taifa ya uchaguzi. Watu hao wa wameapishwa Julai 25,2024 na Hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Bukoba Frorah Kaijage uapisho uliofanyika katika ukumbi wa mkuu wa mkoa huo. Akifungua mafunzo hayo ya siku mbili mgeni rasmi Jaji mstaafu Mbarouk S Mbarouk amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kufanya kazi zao kwa ueledi, bidii na moyo wa kujituma ili kufanikisha zoezi hilo na kuwaelekeza wengine ambao hawakuwahi kushiriki zoezi kama hilo. “Wakati wa uboreshaji wa daftari mawakala wa vyama vya siasa wataruhusiwa kuwepo katika vituo vya kuandikisha wapiga kura, jambo hili ni muhimu na litasaidia kuleta uwazi wa zoezi zima pia mawakala watasaidia kuwepo uwazi ili kupunguza kuwepo kwa vurugu zisizo za lazima” Aidha alisema kuwa, tume imetoa vibali 157  vya asasi za kiraia kwa ajili ya kutoa elimu ya mpiga kura na...

TANZANIA KUWA MWENYEJI MKUTANO WA KIMATAIFA WA BARABARA.

Image
  Na Mwandishi Wetu TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano la tisa la Kimataifa la Usafiri Endelevu na Ubunifu Bora ambao umeandaliwa na Chama cha Wataalamu wa Barabara (TARA). Mkutano huo utakaofanyika jijini Arusha wiki ijayo utafunguliwa na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na utahudhuriwa na washiriki zaidi ya 300 wa ndani na  nje ya nchi. Mkurugenzi Mkuu wa TARA, Eliamlisi Joseph, alisema jana kuwa mada kuu ya kongamano hilo itakuwa  Usalama, Umakini na Uendelevu wa Mifumo ya Usafiri kwa Ukuaji wa Uchumi Duniani. Alisema madhumuni ya mkutano  huo wa Kimataifa wa usafiri endelevu na ubunifu bora ni kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya usafiri kuhusu usafiri salama, mahiri na endelevu na mifumo ya ukuaji wa uchumi ulimwenguni kupitia kubadilishana maarifa, uzoefu na mbinu bora. Alisema lengo ni kuwawezesha wadau katika sekta ya uchukuzi, kuchangia ipasavyo katika maendeleo, utekelezaji na usimamizi wa mifumo endelevu na bora ya usafiri na kutoa jukwaa la...

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA

Image
  Na Alodia Dominick  Bukoba, Wadau mbalimbali  wa uchaguzi hapa nchini wameombwa kuhamasisha jamii kujitokeza wakati wa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.  Wito huo umetolewa Julai 24, 2024 na mwenyekiti wa tume huru ya taifa ya  uchaguzi Jaji Mbarouk S Mbarouk katika mkutano wa tume na wadau wa uchaguzi mkoani Kagera ambao ulilenga kutoa taarifa  mbalimbali za maandalizi ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura. Amesema kuwa, uzinduzi la daftari la kudumu ulifanyika mkoani Kigoma na Waziri  mkuu wa Tanzania Kasimu Majaliwa na kuwa uzinduzi awamu ya pili utafanyika kuanzia Agosti  05, mwaka huu hadi Agosti 11, mwaka huu katika mikoa ya Kagera na Geita. Amewaomba viongozi wa dini, makundi mbalimbali ya wenye ulemavu na wanawake kuhamasisha wananchi kujitokeza kupiga kura na akasema mama  wajawazito, wenye watoto wachanga, wazee na wenye ulemavu watapewa kipaumbele wakati wa kupiga kura.  Wakati huo huo, Kaimu mkurug...

MAONYESHO YA VYUO VIKUU 15 NJE YA NCHI KUFANYIKA ARUSHA

Image
  Na Mwandishi Wetu   VYUO 15 kutoka nje ya nchi vinatarajiwa kushiriki maonyesho yanayotarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi jijini Arusha. Maonyesho hayo ya siku moja yatafanyika siku ya Jumamosi tarehe 27 mwezi huu, kwenye hoteli ya Four point by Sheraton Hoteli, zamani ikijulikana kama New Arusha. Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel, alisema walianza kufanya maonyesho Zanzibar kuanzia tarehe 15 hadi 21 mwezi huu na mahitaji yamekuwa makubwa kwa wanafunzi. Alisema baada ya kumaliza maonyesho ya Zanzibar GEL ilifanya maonyesho mengine jijini Dar es Salaam lakini kutokana na mahitaji kuwa makubwa kwenye mikoa mingine wameandaa mengine jijini Arusha. “Maonyesho ya Zanzibar yalifana sana na wanafunzi wamekuwa wengi kwa hiyo tulipoona mahitaji yamekuwa makubwa tumeona tufanye na Arusha siku ya Jumamosi ili wanafunzi wengi  wapate fursa ya masomo,” alisema. Alisema mwanafunzi atakayeshiriki kwenye maonyesho hayo atapata taarifa zote kuhusu vyuo vikuu n...

CTI WADAU WA VIWANDA WATETA KUHUSU DIRA YA TAIFA 2050.

Image
  Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Wenye Viwanda (CTI), limependekeza maendeleo ya viwanda yapewe kipaumbele kwenye Dira ya Taifa ya 2050.   Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa CTI, Leodegar Tenga wakati wa mjadala wa wadau wa viwanda wakijadili Dira ya 2050 na kuzungumzia maendeleo ya viwanda kwa ujumla.   Mkutano huo ulioandaliwa na Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), pia ulizindua tuzo za Rais za Mzalishaji Bora Viwandani PMAYA ambazo hufanyika kila mwaka kwa wenye viwanda.   Tenga alisema hakuna  nchi duniani hata moja ambayo iliwahi kupiga hatua kubwa kiuchumi bila kuwekeza kwenye viwanda kwa hiyo lazima kuwe na mikakati madhubutu ya kukuza viwanda.   “Kuna msemo wa Kiswahili kwamba kupanga ni kuchagua kwa hiyo tuchague kuwekeza kwenye viwanda ili tusonge mbele na ili viwanda vifanye kazi vizuri lazima tuwe na watalamu wetu kwa hiyo tena lazima tuwekeze kwenye elimu bora,” alisema Tenga   Alisema ili viwanda viweze kufanya kazi ...

RAIS DKT. SAMIA AFANYA UTEUZI NA KUHAMISHA NA KUTENGUA BAADHI YA VIONGOZI.

Image