Thursday, October 5, 2023
Wednesday, October 4, 2023
NG'OMBE WA BBT WAKO SALAMA - ULEGA
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema ng'ombe walio katika programu ya Jenga kesho iliyo bora (BBT) Mifugo, katika Kituo cha Shamba la Serikali Mabuki Mkoani Mwanza wako salama na vijana wanaendelea na shughuli zao za unenepeshaji wa ng'ombe hao.
Waziri Ulega amesema hayo alipotembelea katika kituo hicho kwa lengo la kuona maendeleo ya shughuli za unenepeshaji wa mifugo zinazoendelea kituoni hapo leo Oktoba 4, 2023.
Mhe. Ulega amesema pamoja na kutokea jaribio la wizi katika kituo cha Mabuki kilichopo Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza ambalo lilizua taharuki, ng'ombe wote wako salama, huku akitumia nafasi hiyo kuushukuru uongozi wa Mkoa wa Mwanza, Wananchi na Vijana kwa ushirikiano na kazi kubwa wanayoifanya kituoni hapo.
Amesema kuwa Serikali ya Rais, Dkt. Samia mwaka huu itaendelea kuongeza vituo vingine vya BBT ili vijana wengi zaidi wapate fursa ya kupata elimu hiyo na waweze kujikwamua kimaisha.
Ameongeza kuwa mwaka huu wanakwenda kuongeza vituo vingine kama hivyo katika mikoa ya Tabora, Morogoro, Pwani na Arusha.
Awali, Waziri Ulega ameielekeza Idara ya masoko iliyopo katika Wizara yake kuhakikisha inaendelea kutafuta masoko ya ng'ombe hao wa BBT ili vijana hao waweze kuendelea kufanya biashara na kutimiza lengo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutengeneza fursa nyingi za ajira kwa vijana nchini.
RAIS DKT. SAMIA ANA UTASHI WA KUKUZA MICHEZO -MAJALIWA
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana utashi mkubwa wa kisiasa katika kukuza sekta ya michezo kwa kufanya uwekezaji na mabadiliko kwenye sekta hiyo.
Amesema hayo leo (Jumatano, Oktoba 4, 2023) wakati wa hafla ya kukabidhi shilingi milioni 500 kwa timu ya Taifa ya mpira wa miguu (Taifa Stars) ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Dkt. Samia kwa timu hiyo baada ya kufuzu michuano ya AFCON 2024.
“Uamuzi wa Rais Dkt. Samia wa kuridhia asilimia tano ya kodi itokanayo na michezo ya kubashiri (sports betting) ipelekwe katika Mfuko wa Maendeleo ya Michezo ili kusaidia shughuli za maendeleo ya michezo hapa nchini umelenga kuikuza zaidi sekta hiyo.”
Ameongeza kuwa hatua ya Rais Samia kuiundia sekta ya michezo wizara yake ni uthibitisho tosha kwamba anataka kuhakikisha kwamba Tanzania inafikia hatua ambazo mataifa mengine yameshafikia kwenye sekta ya michezo.
“Hayo ni baadhi tu ya mambo ya kujivunia katika kipindi hiki cha utawala wa Jemedari na nguli wa michezo, kiongozi shupavu, mama yetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.”
Kabla ya kukabidhi hundi hiyo, Waziri Mkuu alikagua ukarabati unaoendelea kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa ikiwemo vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo, chumba cha matibabu, hali ya uwanja, chumba cha VAR na chumba cha kufuatilia kamera za ulinzi wa uwanjani. Alisema ameridhishwa na kazi ya ukarabati inayoendelea kwenye awamu hiyo ya kwanza.
Akimkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro alisema kutokana na ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, vijana wa timu ya Taifa walipambana hadi wakafuzu kwenda AFCON kwa mara ya tatu.
Alisema Tanzania, Kenya na Uganda ziliungana na kuomba kuwa wenyeji wa mashindano ya AFCON kwa mwaka 2027. “Nchi hizi tatu, kwa mara ya kwanza zitakutana huko Mombasa mwezi huu wa kumi ili kuratibu shughuli hii kwa pamoja,” alisema.
Mapema, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF), Wallace Karia alisema mbali na kujenga viwanja vipya huko Arusha na Dodoma, Benjamin Mkapa na Amri Abeid ni miongoni mwa viwanja vinavyofanyiwa ukarabati ili vitumike kufanya mazoezi wakati wa mashindano ya AFCON.
Aliiomba Serikali iwasaidie kupata usafiri wa moja kwa moja kwenda Morocco ili wawahi kurudi nyumbani kwa ajili ya mechi ya marudiano.
SEKTA YA MADINI KUFUNGAMANISHWA NA MIPANGO YA TAIFA UWEKEZAJI
PROF. MHANDO ANG’ATUKA ZIFF, SHIVJI AKABIDHIWA MIKOBA YAKE
Tuesday, October 3, 2023
NDEGE MPYA YA ABIRIA YAWASILI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE.
ATCL KUWA NA NDEGE ZAKE MPYA 16"-PROF. MBARAWA
MNKONDYA AFURAHISHWA NA KASI YA UKUAJI WA VANILLA UNUNIO DAR
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.
MKURUGENZI Mkuu wa Makampuni ya Kimataifa ya kilimo cha Vanilla Duniani, Simon Mnkondya amefurahishwa na kasi ya ukuaji wa Vanilla katika shamba lililopo Ununio beach, Dar Es Salaam ambalo limeanza kutoa maua na ustawi mzuri.
Mnkondya amefanya ziara katika shamba hilo akiwa ameambatana na Mke wake Mama Simon Mnkondya Bi. Upendo Ayo, imekuwa ziara yenye matumaini makubwa hasa baada ya kuona kasi ya ukuaji huo wa vanilla.
"Kwetu Vanilla ni zao lisilo na pingamizi kwenye ukuaji.
Soko na bila shaka linabakia kuwa zao la kwanza kwa bei Tanzania na kuwa Vanilla ni zao la pili kwa bei duniani" Amesema Mnkondya.
Aidha,ameongeza kuwa hatua hiyo inapelekea kupigia debe kubwa zao hilo la Vanilla ili ikiwezekana kiwe kilimo cha Taifa.
"Hichi kwetu ni kitu kinachotufanya tulipigie debe kubwa zao la vanilla na ikiwezekana kiwe ni kilimo cha Taifa kwa vile zaidi ya asilimia 80 ya nchi yetu Tanzania Vanilla inamea na kufanya vizuri ikiwa njia za kisasa za 'Greenhouses' na umwagiliaji wa matone zitatumika." Amesema Mnkondya.
Aidha, Mnkondya amesema kuwa, Shamba la Ununio ni shamba lililobezwa kwa sababu ya uwepo wa karibu na mchanga wa bahari mahali hapo lakini umakini wa kampuni ya Vanilla International Limited limekuwa shamba darasa kwa Dar Es salaam."Amesema Mnkondya
Hata hivyo, Mkurugenzi amewaasa wana Ununio na Dar Es salaam kuweza kutembelea kurasa za kampuni hiyo kwenye mitandai yao ilikuwezeshwa namna sahihi za ulimaji wa zao hilo.




















































