Saturday, August 12, 2023
Friday, August 11, 2023
SAFARI YA WACHIMBAJI NCHINI CHINA KULETA TIJA – DKT. KIRUSWA
Naibu Katibu Mkuu Ataka watumie ziara kujifunza
Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa ameutaka ujumbe wa wadau wa Sekta ya Madini wapatao 100 wakiwemo wachimbaji wadogo, wachimbaji wa Kati, Wafanyabiashara wa madini na watoa huduma migodini wanaotarajia kwenda nchini China kuhakikisha safari hiyo inaleta matunda kwa kuleta wawekezaji wengi na kupata vifaa vya kisasa ili kuongeza uzalishaji wa madini nchini.
Wadau wengine, wanaoshiriki katika ziara hiyo ni wataalam wa madini kutoka taasisi za Wizara ya Madini, taasisi za Fedha ikiwemo Benki ya CRDB na wadau wengine muhimu.
Dkt. Kiruswa ameyasema hayo katika hafla fupi ya kuiaga timu hiyo Agosti 11, 2023 jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kuwa, ubalozi wa China kwa kushirikiana na Kampuni ya Touchbroad ya nchi hiyo imeandaa ziara ya wachimbaji kutoka Tanzania ili kuwawezesha kukutana na wawekezaji wa Sekta ya Madini nchini China, kutembelea viwanda vya kutengeneza mitambo na vifaa vya uchimbaji na uchenjuaji wa madini na kuwawezesha kupata uzoefu na wafanyabishara wa madini waliopo China na kupata teknolojia za uchimbaji na uchenjuaji.
"Niwaombe kila mmoja wenu akiwa China ahakikishe anatimiza malengo yake kadri anavyoweza ili ujuzi mtakaoupata uje kuwasaidia kuboresha biashara zenu na kuongeza tija,” amesema Dkt. Kiruswa.
Vile vile, amezipongeza taasisi za fedha kwa kuendelea kuwasaidia wachimbaji na wafanyabiashara katika kuhakikisha wanapata mikopo ya fedha kwa kuwa karibu na wafanyabiashara wa madini na amewataka kuangalia uwezekano wa kupunguza riba ili kupata wateja wengi na kuruhusu wachimbaji wadogo kupata mikopo yenye riba ndogo.
Kwa upande mwingine, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo amewataka wachimbaji hao kutumia ziara hiyo kujifunza na kupata uzoefu watakapotembelea viwanda vya kutengeneza mitambo na vifaa vya uchimbaji.
Naye, Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji wa Madini nchini (FEMATA), John Bina amesema kuwa, ziara hiyo nchini China inakwenda kufungua milango ya nchi kuvutia wawekezaji wengi kuendelea kuja kwa kuwa nchi ina sera nzuri katika uwekezaji.
Viongozi wengine walioshiriki ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali, Mbunge wa Viti Maalum Iringa Dkt. Rita Kabadi, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Dkt. Venence Mwasse, Mjumbe wa Bodi ya STAMICO Lucas Seleli, mwakilishi wa benki ya CRDB pamoja na wataalam kutoka Wizara na taasisi zake katika safari inayolenga kukutana na wawekezaji wa Sekta ya Madini nchini China.
NAIBU WAZIRI WA MADINI KUWAAGA WACHIMBAJI WANAOTEMBELEA NCHINI CHINA
Thursday, August 10, 2023
Wednesday, August 9, 2023
WAHUDUMU WA AFYA MOI KUIMARISHA ZAIDI HUDUMA KWA WAGONJWA
Na Mwandishi wetu-MOI, 9 Agosti, 2023 Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof.Abel Makubi amefanya kikao cha kimkakati na watumishi wa kada za wahudumu wa afya na huduma kwa wateja na viongozi wao kwa lengo la kuboresha huduma kwa wateja wanaofika MOI kupata huduma.
Prof. Makubi amewapongeza wahudumu wa afya wa Taasisi ya MOI kwa kazi kubwa wanayoifanya kwani wao ni jicho la hospitali na ni sehemu kubwa katika uendeshaji wa Taasisi.
“Napenda kuwaomba idara zote tuongeze ufanisi katika kazi ili kuendelea kuboresha huduma na kuongeza mapato ambayo yataimarisha Taasisi kifedha ili kuboresha huduma zetu na uendeshaji wa hospitali" Alisema, Prof.Makubi.
Kwa upande mwingine Prof. Makubi amesema kwa sasa kipaumbele cha Wizara ya Afya chini ya Waziri Ummy Mwalimu (MB) ni ubora wa huduma hivyo lazima tutaboreshe huduma kutoka hapa tulipo kwenda mbele zaidi ikiwa ndio ajenda ya kwanza kuliko zote kwenye sekta ya Afya.
“Inabidi tuzingatie mambo muhimu kama salamu, kukaribisha mgonjwa, kumpa pole mgonjwa na ndugu wa mgonjwa wafikapo MOI, kumuelekeza anapotaka kufika pamoja ,kumuuliza kama anachangamoto au mahangaiko na kuondoa vitu kama chuki vilevile kuwa wepesi katika utoaji huduma ili mgonjwa asikae muda mrefu kusubiria matibabu" Alisema Prof Makubi.
Aidha ,Prof.Makubi amewaomba watumishi wote kubadilisha fikra, kuwa na mtazamo chanya kuwa na 'Sense of ownership' na kuzingatia maadili kama kutokupokea rushwa na kutoa taarifa potofu, kujituma vilevile utunzaji wa mali za Taasisi.
Kikao hichi ni muendelezo wa vikao baina ya Prof. Makubi na makundi mbalimbali ya watumishi kwa lengo la kuboresha huduma. Katika kikao hicho Prof Makubi amewakumbusha watumishi wote wa MOI kuhudhuria mkutano mkuu wa watumishi wote wa MOI siku ya Jumamosi tarehe 12/08/2023 katika ukumbi wa CPL Muhimbili.




















































