Tuesday, June 25, 2019

RAIS, DKT. MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA KUKAGUA UJENZI WA DARAJA LA TANZANITE.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mhandisi Mshauri wa kampuni ya Yoosin Engineering Mhandisi Suk-Joo Lee wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa daraja linalokatiza baharini na kuunganisha maeneo ya Aga Khan na Coco Beach Jijini Dar es Salaam. Daraja hilo limependekezwa kuitwa Tanzanite Bridge.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo ya ujenzi huo na Mhandisi Mshauri wa kampuni ya Yoosin Engineering Mhandisi Suk-Joo Lee.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipatiwa maelezo ya ujenzi huo na Mhandisi Mshauri wa kampuni ya Yoosin Engineering Mhandisi Suk-Joo Lee 


MAGAZETI YA LEO JUNI 25, 2019.

Monday, June 24, 2019

DC. BAGAMOYO AZINDUA SOKO LA WANAWAKE WAJASIRIAMALI.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa, (katikati) akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake wajasiriamali wilayani humo, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi, wilaya ya Bagamoyo, Teddy Davis.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi, wilaya ya Bagamoyo, Teddy Davis, (wa pili kulia) akipunga mkono mara baada ya Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Zainabu Kawawa (kushoto) kukata utepe kama ishara ya kuzinduliwa rasmi kwa soko la pamoja la wanawake wajasiriamali Bagamoyo.
.........................................

 Na Selestian James

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa  amezindua soko la Pamoja la wanawake wajasiriamali wilayani humo, ikiwa kama hatua ya kuwakwamua katika shughuli zao za kiuchumi.


Shuguli hiyo ya uzinduzi iliyofanyika hivi karibuni katika mgahawa wa smoke house uliopo kata ya Dunda wilayani Bagamoyo ilikutanisha wanawake wajasiriamali kutoka kata mbalimbali wilayani humo ikiwemo kata ya Dunda, Magomeni, Zinga, Kiromo na Nianjema.


Wanawake hao walifika wakiwa na bidhaa mbalimbali za ubunifu na mazao mbalimbali ya kilimo zikiwa kama shughuli kuu za kujiingizia kipato.


Aidha Mkuu huyo wa wilaya amewapongeza wanawake hao kwa hatua ya kuanzisha soko hilo kwa kutumia eneo lao binafsi badala ya kuisubiri serikali.


Alisema amefarijika na hatua hiyo na kwambaametoa ahadi ya kushirikiana nao bega kwa bega kuhakikisha wanapata  eneo kubwa zaidi kwa ajili ya ujenzi wa soko.


Alitumia nafasi hiyo kuwataka viongozi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi  wilayani humo kushirikiana nae na kumuonesha ni sehemu gani inayofaa kulingana na shughuli zao, ili nae kama kama kiongozi wa serikali afuate taratibu atimae wafanikishe.


"Hatuwezi kuwa na bidhaa nzuri kama hizi halafu tukakosa soko la kuuzia, bihaa nzuri kama hizi ndio alama ya Bagamoyo" Alisema Zainabu.


lakini pia kiongozi huyo amewakaribisha ofisini kwake kinamama hao ambapo kila siku za jumanne huwa anasikliza kero mbalimbali za wananchi na kuona ni namna gani anaweza kuzitatua akiwa na wataalam mbalimbali wakiwemo wanasheria.


Naye mweyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanaweke Kiuchumi wilaya ya Bagamoyo, Teddy Devis alimshukuru mkuu wa wilaya huyo kwa kuweza kufika eneo hilo  kuwatia moyo  na kuwaunga mkono.


Alisema kwa muda mrefu wamekosa sehemu ya kuwaunganisha  kama wanawake wajasiriamali, ambapo sasa kupitia soko  hilo litakalokua linafanyika kila siku ya jumamosi litawafungulia fursa kuweza kuuza na kutangaza bidhaa zao ndani na nje ya nchi.


kwa upande wa wanawake waliokuwepo katika eneo hilo wameonesha furaha zao kwa hatua hiyo iliyochukuliwa na kiongozi huyo.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa, akiwa anaangalia bidhaa za wajasiriamali katika uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake Bagamoyo.
 
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainabu Kawawa, pamoja na Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi, wilaya ya Bagamoyo, Teddy Davis, wakifurahia jambo wakati akitembelea bidhaa za wajasiriamali kwenye uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake Bagamoyo.
 
Viongozi mbalimbali wa chama na serikali waliofika kushuhudia uzinduzi wa soko la pamoja la wanawake Bagamoyo.

PICHA ZOTE NA SELESTIAN JAMES. 
    

ZAIDI YA TANI 5,000 ZA UFUTA ZAUZWA MKOANI LINDI.

Sehemu ya magunia ya zao la ufuta kama yanavyoonekana pichani wakati wa mnada uliofanyioka mkoani Lindi.
....................................................

 NA HADIJA HASSAN, LINDI.


Jumla ya Tani 5405 na kilo 791 za ufuta wa wakulima wa Chama kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao kinachojumuisha wakulima wa Wilaya za Lindi, Kilwa na Manispaa ya Lindi Mkoani humo zimeuzwa Katika Mnada wa Tatu wa zao hilo kwa Bei ya Juu ya Tsh. 2802 na Bei ya chini 2738.


Mnada huo wa Tatu umefanyika Katika ghara la chama cha Msingi Mnazi mmoja AMCOS kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo ambapo Jumla ya Makampuni 14 yaliomba kununua ufuta huo.


Akizungumza Mara baada ya kufanyika mnada huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Jomari Satura pamoja na mambo Mengine aliwaasa wananchi wa Lindi kwa ujumla kutumia fedha wanazozipata Katika mauzo ya ufuta kuwekeza Katika mambo ya kimaendele.


Alisema ili kilimo hicho kiweze kuonekana kimeleta tija Katika Mkoa huo ni vyama, wakulima baada ya kupata fedha zao wakafanya mambo yanayoweza kuwainua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba mzuri ambayo itaonyesha utofauti wa kabla ya Msimu na baada ya msimu


 Aliongeza kwa kusema kuwa, ni ajabu kuona mpaka Msimu wa mauzo unaisha Huku mabilioni ya fedha yakiwa yamewafikia wananchi lakini maendeleo ya Moja kwa Moja yasionekane.


Nae Mstahiki meya wa Manispaa Lindi Lidume Liumbo Akifunga mkutano huo wa Mnada wa ufuta Alitumia fulsa hiyo kuwaasa wananchi wa Manispaa hiyo kuongeza Tija ya uzalishaji wa zao hilo Ili kuweza kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja, Mkoa na nchi kwa ujumla.

Wananchi wakiwa katika mnada wa Ufuta mkoani Lindi.

DIWANI WA TENGELEA, MKURANGA ATATUA TATIZO LA MAJI.

DIWANI wa kata ya Tengelea wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Shabani Manda amefanikiwa kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa eneo hilo kwa muda mrefu.


Akizungumza na wananchi wa eneo kata hiyo, Manda alisema walikuwa wakisubiri huduma hiyo kwa muda mrefu na kwamba sasa imefanikiwa kwa wananchi hao kupata huduma ya maji.


"Maji ni uhai maji ni maisha ya kila siku kwa mahitaji ya viumbe hai hivyo kupatikana kwa mradi huu mkubwa wa kisima utasaidia wananchi wa kata yangu kuondokana na changamoto hiyo. Alisema Manda.


Alisema Awali wananchi hao walikuwa wakipata tabu kubwa sana kutokana na kutumia visima vya kienyeji.


Aliongeza kuwa kutokana na changamoto hiyo kudumu kwa muda mrefu aliweza kupambana kutafuta wadau na kufanikiwa kuwapata wafadhili waliojitolea kujengea kisima kirefu katika msikiti wa Sunguni.


Aidha alisema kuwa Al Fridaus Charitable Foundation ndio taasisi iliyojitolea kuwajengea wananchi wa kata yangu kisima Chenye uwezo mkubwa wa kuhudumia wananchi wasiopungua 500.


Aliongeza kuwa maji hayo ni ya wananchi wote bila ubaguzi wa dini wala kabila hivyo kila mmoja yuko huru kutumia maji hayo.


Kwa upande wake kiongozi wa msikiti huo Hamisi Mohamed amempongeza diwani huyo kwa jinsi anavyojituma katika kutafuta wafadhili mbalimbali kwa lengo la kuendeleza kata ya Tengelea.


Aidha ameipongeza taasisi ya Al Firdaus Charitable Foundation kwa msaada wa kisima walichokitoa kwa wakazi wa eneo hilo kwani walikuwa na changamoto kubwa ya maandalizi kwa ajili ya kupata huduma ya kutawadha wakati wa kuswali.


Naye mwakilishi wa taasisi hiyo hapa nchini Buddy Amour amesema kuwa Taasisi yao imejikita katika kutatua changamoto mbalimbali kwa lengo la kuisaidia serikali kwani peke yake ni vigumu kumaliza changamoto za wananchi wake.


"Tumejipanga kama taasisi ili kuhakikisha tunawasaidia wananchi wa maeneo tofauti tofauti ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa wananchi wake popote pale walipo " Alisema Amour.


Aidha amewapongeza wakazi wa eneo hilo kwa jinsi walivyokuwa wakijitolea kwa lengo la ufanikishaji wa mradi bila ya malipo ya aina yeyote.


Aliongeza kuwa kwa wilaya ya Mkuranga wamekabidhi visima 10 katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kutokomeza uhaba wa maji katika maeneo mbalimbali na hivyo takribani ya wananchi wote watakuwa na huduma ya maji.