Thursday, November 8, 2018

ZAHANATI YA MSATA YAONGOZA MKOA WA PWANI KWA HUDUMA BORA ZA AFYA.

Zahanati ya kijiji cha Msata iliyopo kata ya Msata Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo, imeibuka kidedea kimkoa baada ya kufanya vizuri katika utoaji wa huduma za afya kwa wananchi kwa kuzingatia matokeo makubwa sasa(BRN) na kufanikiwa kupata nyota nne kati ya vituo vyote vya afya katika mkoa wa Pwani.

Ushindi huo umepatikana kutokana na ukaguzi uliofanywa na wizara ya Afya kwa ajili ya malipo kutokana na matokeo ya huduma kwa matokeo makubwa sasa ,Zahanati ya Msata ilionekana kukidhi vigezo vilivyowekwa na wizara ya Afya kwa kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuzingatia matokeo makubwa sasa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Chalinze Bi.Amina Kiwanuka, aliwapongeza watumishi wa zahanati ya Msata kwa kufanya kazi kwa kuzingatia vigezo vinavyotolewa na wizara ya Afya na kufanikiwa cheti chenye nyota tano.

Aidha, Mkurugenzi huyo, amevitaka vituo vingine vya afya na zahanati katika Halmashauri hiyo kuiga mazuri kutoka zahanati ya Msata ili kwa ukaguzi ujao vituo vyote vya afya katika halmashauri ya Chalinze viweze kuibuka kidedea na kupata nyota tano ili kufikia matokeo makubwa sasa katika sekta ya Afya.

 "Mganga Mkuu wa wilaya nakutaka sasa usimamie utoaji huduma za afya kwa wananchi na uhakikishe vigezo vyote vinavyotakiwa kwa mujibu wa matokeo makubwa sasa vinazingatiwa na kufanyiwa kazi." Kiwanuka alisema.

Naye Mganga Mkuu wa halmashauri ya Chalinze Dkt Rahim Hangai alipokea maelekezo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze na kuahidi kusimamia kwa ukaribu utoaji huduma na akaongezea na kusisitiza kwa watumishi wote wa afya kuzingatia miongozo ya wizara ili ukaguzi ujao vituo vyote vya afya vinafikia vigezo na kutunukiwa cheti cha ufanisi

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa (katikati) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze, Bi Amina Kiwanuka (kushoto) kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Saidi Zikatimu.
 

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akikabidhi vifaa vya Afya katika juhudi zake za kuwatumikia wananchi walimpigia kra ndani ya jimbo lake.


DKT. ABBASI: SERIKALI ITAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

SERIKALI imesema kamwe haitokatishwa tamaa na kauli ya baadhi ya Viongozi na wanasiasa kuhusu dhamira yake ya kutekeleza miradi mikubwa ya kimamkati yenye malengo ya kuleta maguezi ya kijamii na kiuchumi kwa Watanzania.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa ziara ya kutembelea Kituo cha Redio ya TBC Taifa na tathmini ya utendaji kazi katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Dkt. Abbasi alisema tangu kuingia madarakani kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Serikali ya Awamu imekuwa ikitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ambayo wadau mbalimbali wa maendeleo wameipongeza Serikai yake kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa lakini wapo baadhi ya baadhi ya Viongozi na wanasiasa wachache wamekuwa wakipinga mageuzi hayo pasipo na kutoa hoja za msingi.

“Mageuzi yanayoendelea kufanywa hayatakuwa na mwisho, Serikali ya Awamu ya Tano na Watendaji wote tunaomsaidia Rais John Pombe Magufuli tumedhamiria kuleta mapinduzi ya kweli kwa kuboresha huduma za msingi kwa wananchi na tutapokea maoni na ushauri lakini kamwe haturudishwi nyuma na Viongozi na watendaji wanaopinga mageuzi haya” alisema Dkt. Abbasi.

Akitolea mfano Dkt. Abbasi alisema mara baada ya Serikali kutangaza dhamira ya kuanzisha mradi wa kihistoria wa kufua umeme wa Stiegler’s Gorge uliopo Wilayani Rufiji mkoani Pwani wapo baadhi ya wanasiasa na Viongozi wamekuwa wakipinga mradi huo kwa kigezo cha uharibifu wa mazingira ya eneo hilo, jambo ambalo lililenga kupeleka taswira hasi kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Anasema mageuzi mengine yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ni pamoja na ujenzi wa ukuta katika machimbo ya madini ya Tanzanite, ambapo kutokana na hatua hizo katika kipindi cha mwezi Julai hadi Novemba Serikali imeweza kukusanya mapato ya kiasi cha Tsh Milioni 890.

Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema katika kuelekea katika mageuzi ya kijamii na kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na kuweka mfumo imara wa usimamizi wa fedha za umma ikiwemo makusanyo ya kodi, hatua inayoiwezesha Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli itaendelea kutekeleza sera na programu mbalimbali ikiwemo sera ya elimu bure katika ngazi za elimu ya awali, msingi na sekondari, ambapo Serikali imekuwa ikitoa Tsh Bilioni 23 kila mwezi kwa ajili ya gharama za uendeshaji wake.

Akifafanua zaidi alisema kutokana na kuongezeka kwa kiwango cha ukusanyaji wa kodi, Serikali imeweza kufanya mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali za kijamii ikihusisha afya, maji, barabara pamoja na ununuzi wa ndege mpya nne za Serikali na hivyo kufufua upya huduma za Shirika la ndege Nchini (ATCL) ambazo zilisimama kwa kipindi kirefu.

Akianisha mafanikio ya ATCL, Dkt. Abbasi anasema moja ya mageuzi makubwa yaliyofikiwa kwa sasa na shirika hilo ni pamoja na ongezeko la abiria kutoka abiria 3000-4000 kwa mwezi ambapo kwa sasa wateja wanaotumia Ndege za Shirika hilo wamefikia 30,000 kwa mwezi.

“Mpaka sasa tuna ndege nne za Serikali, na mwezi Desemba tutapokea ndege nyingine 2 aina ya Airbus na mwakani (2019) mwezi Oktoba tutapokea ndege nyingine 1 na kuzifanya ndege mpya za Serikali kufikia saba, na hivyo kufanya sekta ya uchukuzi kuwa katika mabadiliko makubwa ya utendaji na uendeshaji” alisema Dkt. Abbasi.

SERIKALI KUFUTA MASHAMBA PORI

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angellina Mabula akijibu swali wakati wa kikao cha pili cha Mkutano wa 13 wa Bunge jana Novemba 07, 2018 jijini Dodoma.
..................................................


Serikali imeendelea kuchukua hatua za kubatilisha milki za ardhi za mashamba yaliyotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Hayo yamesema Bungeni leo  na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula  wakati akijibu swali la Mhe. Dustan Kitandula Mbunge wa Mkinga kuhusu kufuta hati za mashamba yaliyotelekezwa.

“Katika kipindi cha Disemba, 2015 mpaka Octoba, 2018 mashamba yenye ukubwa wa ekari 84,240.803 yamebatilishwa katika Halmashauri za Ngorongoro, Arumeru, Moshi, Kinondoni,(Manispaa), Kigamboni(Manispaa), Mvomero, Kilombero, Kilosa, Mvomero, Iringa, Bukoba, Tarime, Kibaha, Serengeti, Busega, Muheza, Lushoto na Mkinga” amefafanua Naibu Waziri Mabula.

Mabula anasema kuwa, katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Shamba Na. 278 Mkomazi lenye ukubwa wa ekari 15,442 lililokuwa likimilikiwa na kampuni ya M/S Mkomazi Plantations Limited kwa Hati Namba 4268, 9780  na 9781 milki yake ilithibitishwa tarehe 20 Juni, 2018.

Aidha anafafanua kuwa, baada ya kubatilishwa kwa milki ya shamba hilo, Serikali ya Mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga zipange matumizi mapya ya shamba hilo kwa kuzingatia mahitaji ya ardhi katika eneo hilo kipaumbele kikiwa ni mahitaji ya wananchi na ardhi kwa ajili ya uwekezaji.

Mbali na hayo Mabula amezitaka Halmashauri zote nchini kubaini mashamba yaliyotelekezwa kutuma ilani kwa wamiliki wa mashamba hayo kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi (Sura 113) na kuwasilisha mapendekezo katika Wizara ya Ardhi kwa hatua za kubatilisha milki za mashamba hayo ziweze kufanyika.

RAIS DKT.MAGUFULI AFANYA UTEUZI