Tuesday, July 26, 2016

DC. KINONDONI AKUSUDIA KUONDOA TATIZO LA AJIRA KATIKA WILAYA YAKE.

Mkuu wa wilaya  ya  Kinondoni, Aliy Salum Hapi, akizungumza na wananchi wa manispaa yake leo.


Na Sara Zuberi.

MKUU  wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amesema amejidhatiti katika kuhakikisha anamaliza tatizo la ukosefu wa ajira katika wilaya hiyo baada ya kuanzisha   mpango wa kuondoa tatizo la ajira hususani kwa vijana.

Akizungumza  na watendaji wa kata,  wenyekiti wa serikali za mitaa pamoja  wajumbe wa maeneo, katika ukumbi  wa  King  Solomon uliopo  manispaa hiyo, Happy alisema amekusudia kumaliza changomoto ya ajira kwa vijana kwa lengo la kumaliza tatizo la uhalifu  analodai linachangiwa na ukosefu wa ajira.

Alisema kwa sasa ameandaa mpango ambao watendaji hao wa kata, vijiji wanatakiwa kwenda Nyumba hadi nyumba kuchukua orodha ya majina ya vijana ambao hawana ajira ili aweze kuwaunganisha na wajasiriamali,makampuni pamoja na wafanya biashara wakubwa ili waweze kuwasaidia na tatizo la ajira.

Aliwataka wananchi wote wa wilaya ya kinondoni kujitokeza kuandika majina siku tarehe 1 hadi tarehe 7 ya mwezi wa 8 mwaka huu.

Hapi alifafanua kuwa mara baada ya kumalika kuchukuliwa majina hayo  ambapo siku ya tarehe 15 ya mwenzi wa 8,wananchi hao watakaoandishwa majiana hayo watakutanishwa katika viwanja vya Posta Kijitonyama ambap siku hiyo wataunganishwa na wadau hao wa maendeleo.

Aidha, Hapi aliwasahii watendaji hao pamoja wajumbe wa kata kuweka ushirikiano katika mpango huo ili kuhakikisha wanaweza kumaliza tatizo la ajira. 

Wananchi wa manispaa ya Kinondoni  jijiniDar es Salaam wakimsikiliza mkuu wa wilaya  hiyo, Aliy Salum Hapi.

DC BAGAMOYO AKABIDHI MADAWATI KWA MKUU WA MKOA.

Mkuu wa Mkoa wa  Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo wa tatu kutoka kushoto, akijaribu  Madawati wilayani Bagamoyo,wa kwanza  kulia nimkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Hemed Mwanga, na wa kwanza kushoto ni Mbunge wa jimbo la  Bagamoyo, Mh. Shukuru  Jumanne Kawambwa, wa pili kushoto ni Mkurugenzi msaidizi wa Sayona Group, Aboubakari Mlawa.


Mkuu  wa wilaya ya Bagamoyo  Majid Hemed Mwanga, amekabidhi madawati kwa mkuu wa mkoa Pwani, na kufanikiwa kumaliza tatizo la  madawati  kwa wilaya  ya Bagamoyo.

Akisoma taarifa ya  utekelezaji wa agizo la Rais la kutengeneza madawati,  ambalo limesimamiwa na mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, alisema wilaya yake, imekamilisha mahitaji yote ya madawati  kwa shule za msingi na sekondari.

Aidha, mkuu huyo wa wilaya ya Bagamoyo alisema madawati yote hayo  yametengenezwa kwa msaada kutoka kwa wadau mbalimbali na hivyo kuokoa fedha za serikali zaidi ya milioni mia  tano ambazo  zingetumika  kutengeneza madawati  hayo.

Aliongeza kwa kusema jamii imejitolea kusaidia kwa namna mbalimbali kufanikisha zoezi hilo la utengenezaji  wa madawati ambapo alitumia  nafasi hiyo kuwashukuru wadau wote waliochangia upatikanaji wa madawati hayo akiwemo Shubashi Pateli ambae amechaniga madawti 1,200, na Mwenyekit wa makampuni ya IPP Reginald Mengi akiwa aliyechangia madawati 500.

Mkuu huyo wa wilaya  alisema wilaya imeandaa mikataba ya kuyatunza madawati hayo na kwamba mwalimu au mtumishi yeyote  atakaechangia uharibifu wa madawati hayo hatua zitachukuliwa dhidi yake.

Alisema wilaya imejiwekea mikakati ya kuhakikisha uhaba wa madawati hautokei tena  ili kuondoa tatizo la wanafunzi kukaa chini katika kipindi ambacho Rais ametangaza elimu bure kwa wote

Mkuu wa mkoa wa Pwani  akielezea jambo wakati akikagua Madawati, kulia  ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aliy Aliy  Issa.

Aikpokea taarifa hiyo ya madawati, mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist  Ndikilo, ameipongeza wilaya ya  Bagamoyo kwa kukamilisha utengenezaji wa madawati, na kuongeza kuwa mkoa wa Pwani umefanikiwa kutengeneza  madawati ya  sekondari kwa asilimia 100.4 huku yale ya  shule za msingi ni asilimia 93 ambapo asilimia saba iliyobaki yanaendelea kutengemnezwa.
 



Haya ni baadhiya madawati yaliyotengenezwa wilayani Bagamoyo
Diwani  wa kata ya Dunda kushoto, Dikson  Makamba akipokea madawati kutoka kwa mkuu wa mkoa, kwaajili ya kata yake
Kutoka kushoto ni Mh.Togo Omari, Diwani viti maalum Yombo,  wa  pili  kutoka kushoto ni Mh. Subira Mgalu, Mbunge  viti maalum  Pwani, wa tatu ni Mh. Shumina Ismail Rashid, Diwani viti maalum Mwambao, wa nne ni Mh. Hafsa Juma Kilingo Diwani viti maalum Mwambao, na wa kwanza kulia ni Rehema Mwene, Diwani kata ya Lugoba. wakijaribu madawati katika ofisi ya mkuu wawilaya Bagamoyo
Diwani wa  kata  ya Mapinga,  Ibrahim Mbonde akipokea madawati kwaajili ya kata yake.
Diwani wa kata ya Nianjema, akipokea madawati kwaajili ya kata yake.

Monday, July 25, 2016

WATUMISHI HEWA MKOA WA PWANI NI 355, WILAYA YA BAGAMOYO PEKEE NI 91.

Mkuu  wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi, Everist  Ndikilo alipokuwa  akizungumza wilayani  Bagamoyo kwenye kikao  kilichowajumuisha mkuu wa wilaya, Madiwani na  baadhi ya watumishi wa wilaya  ya Bagamoyo.


Mkoa wa Pwani una jumla ya watumishi hewa 355 huku wilaya ya  Bagamoyo ikiwa na watumishi hewa 91.

Hayo yamebainishwa katiika kikao cha mkuu wa mkoa wa Pwani kilichofanyika katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, ambapo wilaya ya Bagamoyo imekabidhi taarifa ya watumishi hewa 91.

Akipokea Taarifa hiyo, ya wilaya ya Bagamoyo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi, Everisti Ndikilo amesema mpaka kufikia sasa mkoa wa Pwani una watumishi hewa 355 waliobainika.

Alisema kufuatia hali hiyo vyombo vya usalama mkoani Pwani vinaendelea na uchunguzi ili kubaini nani aliyesababisha kuwepo kwa watumishi hewa ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya muhusika.

Mhandisi Ndikilo, aliongeza kuwa baada ya kukamilika uchunguzi watakaobainika kuhusika na kuwepo kwa watumishi hewa watachukuliwa hatua kulingana na namna walivyoshiriki, ambapo wanaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu au za kisheria.

Awali akitoa Taarifa kwa mkuu wa mkoa wa Pwani, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Hemed  Mwanga, amesema wilaya ya Bagamoyo imebaini watumishi hewa 91 huku wengi kati yao ni walimu wa sekondari na Msingi.

Majid,  alisema wapo baadhi ya walimu wa sekondari na msingi  ambao wameenda masomoni bila ya ruhusa  na wanalipwa mishara kama kawaida, pia wanahesabika kuwa ni watumishi hewa.

Aidha, Mkuu wa wilaya alisema  kuwa ucheleweshaji  wa maombi yawalimu wanaotaka kwenda  kusoma  ni sababu iliyopelekea walimu kuondoka bila ya ruhusa na  hivyo kuisababishia  hasara  serikali kwa walipa watumishi mishahara bila yakuifanyia kazi.

Alisima wapo walimu kadhaa ambao walishaacha kazi  kwa ridhaa yao lakini  bado wanalipwa mishahara kama kawaida  akitolea mfano wa mwalimu mmoja  ambae ameacha kazi toka mwaka 2014 lakini bado alikuwa anaendelea kupata mshahara  mpaka lilipokuja agizo la kubaini watuymishi  hewa.

Aidha, aliongeza kuwa, katika idadi hiyo ya watumishi hewa 91,  watumishi 12  hawajulikani na wala hakuna kumbukumbu zao  zinazoonesha kwamba wao ni watumishi.
Madiwani wakimsikilizamkuu wa mkoawaPwani.
Mkuu wamkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo, kulia,akipokea ripoti ya watumishi hewa kutoka  kwa  mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Hemed  Mwanga.   
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo,Majid Hemed Mwanga, kulia akiwa na Katibu tawala wa wilaya, Erika liyegela wakisikiliza hutuba ya  mkuu wa mkoa.
Mkurugenzi waHalmashauriya  Bagamoyo, kulia, Azimina  Mbilinyi akiwa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya wakimsikilza mkuu wa mkoa wa  Pwani.
Watumishi namadiwani wakimsikiliza mkuu wa mkoawa  Pwani katika ukumbi wa mikutano ofisi ya mkuuwa wilaya ya Bagamoyo.
Madiwani wa Halmashauriya Bagamoyo wakimsikilizamkuu wamkoa.
Madiwani, wakimsikiliza mkuu wa mkoa.
Madiwani wa Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze, pamoja na watumishi wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Pwani.