Friday, November 29, 2024
VIONGOZI WATEULE WA VITONGOJI NA VIJIJI WAAPA BAGAMOYO.
CCM YASHINDA KWA ASILIMIA 98.82 LINDI
NA HADIJA OMARY, LINDI.
Msimamizi wa Uchaguzi Manispaa ya Lindi Mkoani Humo bwana Juma Mnwele Leo tarehe 29 November 2024 ametangaza matokeo ya Jumla ya uchaguzi wa Serikali za mitaa vijiji na vitongoji Katika Manispaa hiyo uliofanyika November 27 mwaka huu 2024
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake msimamizi huyo wa uchaguzi Manispaa ya Lindi amesema Kati ya nafasi za uongozi 1954 zilizoshindaniwa na Vyama vya siasa chama cha mapinduzi kimeshinda nafasi 1931 sawa na asilimia 98.82, chama cha ACT wazalendo wameshinda nafasi 21 sawa na asilimia 1.07
Alitaja chama chama kingine ni chadema ambacho kilishinda nafasi 2 sawa na asilimia 0.1 kikifuatiwa na chama cha wananchi cuf ambacho kimeshinda nafasi 1 sawa na asilimia 0.05 huku chama cha CHAUMA, NCCR MAGEUZI na TLP vikikosa ushindi kabisa
Monday, November 25, 2024
RAIS SAMIA KUSHIRIKIANA NA THE ISLAMIC FOUNDATION KUANZISHA CHUO CHA UALIMU NA MAADILI.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia kushirikiana na Taasisi ya The Islamic Foundation kuanzisha Chuo cha Ualimu na Maadili katika eneo la Kitungwa wilayani Morogoro.
Rais Dkt. Samia ameyasema hayo leo tarehe 25 Novemba 2024 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika Msikiti wa Al Ghaith uliopo maeneo ya Kilakala Flats/old Dar es Salaam Road mjini Morogoro unaomilikiwa na Taasisi ya The Islamic Foundation Chini ya Mwenyekiti wake Aref Nahdi
Aidha, Rais Dkt. Samia amesema katika kipindi hiki dunia imekumbwa na mmomonyoko wa maadili kuna haja kubwa ya kuongeza ujenzi wa Madrasa ili ziwe vituo vya kuwalea watoto kiimani na maadili.
Aliwahimiza wazazi kusimamia malezi bora ya watoto ili jamii iwe na kizazi chenye hofu ya Mungu, na maadili mema.
Akizungumzia mmomonyoko wa maadili, Mwenyekiti wa Taasisi ya The Islamic Foundation, Aref Nahdi, amesema jamii ya sasa imecha ushirikiano katika malezi jamno linalopelekea watoto kupoteza heshima katika jamii na kuharibikiwa kimaadili.
Alisema zamani ilikuwa mtoto akikosea anapewa onyo na mtu yeyote aliyemzidi umri na kwamba taarifa zikifika nyumba kwa mtoto huyo mzazi wa mtoto anaongeza kumpa adhabu ili iwe fundisho kwa mtoto huyo
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akifungua kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi Msikiti wa Al Ghaith uliopo maeneo ya Kilakala Flats/old Dar es Salaam Road mjini Morogoro unaomilikiwa na Taasisi ya The Islamic Foundation Chini ya Mwenyekiti wake Aref Nahdi (kushoto)
Saturday, November 16, 2024
HEART TO HEART YASAIDIA MRADI WA MAJI ZAHANATI YA NAMUPA
GHOROFA LAPOROMOKA KARIAKOO
Sunday, November 10, 2024
MUFTI NA SHEIK MKUU WA TANZANIA APONGEZA MRADI WA KUTAFSIRI QUR’AN TUKUFU NENO-KWA-NENO KWA LUGHA YA KISWAHILI
Tuesday, October 29, 2024
Thursday, October 24, 2024
DAKTARI KIZIMBANI KWA KUBAKA MTOTO WA MIAKA 12 BUKOBA.
Na Alodia Dominick, Bukoba
Daktari wa viungo Haruna Ayubu maarufu kama Rubai (63) mkazi wa kata ya Rwamishenyi manispaa ya Bukoba amepandishwa kizimbani kwa shitaka la ubakaji wa mtoto wa miaka 12.
Rubai amefikishwa katika mahakama ya wilaya Bukoba Oktoba 23 mwaka huu na kusomewa kesi ya jinai namba 30251/2024.
Upande wa mashtaka unaongozwa na mawakili wawili ambao ni Matilda Assey pamoja na Alice Mutungi.
Akisoma maelezo ya awali wakili upande wa mashtaka amesema kuwa, kati ya Desemba 2023 na Oktoba 19, mwaka huu mshitakiwa amekuwa akimuingiza mhanga katika moja ya chumba katika ofisi yake iliyopo mtaa wa Pwani, kata ya Miembeni manispaa ya Bukoba.
Assey ameeleza kuwa, alipoingia katika chumba hicho alimvua mhanga nguo zake za ndani kisha na mshitakiwa kuvua nguo zake na kuchukua uume wake na kuuingiza kwenye uke wa mhanga baada ya mshitakiwa kumwingilia au kumbaka mhanga amekuwa akimpatia sh. 10,000 au 5,000 kwa ajili ya kuwapelekea wazazi wake.
Aidha amesema, Oktoba 19, mwaka huu mhanga alikwenda tena katika ofisi ya mshitakiwa kwa lengo la kuchukua fedha ambayo amekuwa akimpatia kama msaada na baada ya mhanga kufika mshitakiwa alimpeleka katika chumba kisha kumbaka na baada ya hapo alimpatia sh.1,000 akanunue soda.
Vilevile, mhanga alipotoka katika chumba hicho ndipo alitokea askari polisi na kumuhoji mhanga ndipo mshitakiwa aliweza kukamatwa na kisha kupelekwa kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiano.
Mhanga alipelekwa hospitali na daktari alithibitisha kuwa ni kweli aliingiliwa kutokana na michubuko sehemu ya uke wake akimaanisha kuwa mhanga alikuwa ameingiliwa.
Upelelezi wa shauri hilo umekamilika wapo tayari kuendelea na kesi na upande wa mashtaka wana mashahidi 10, vielelezo vya maandishi vitatu na ripoti ya daktari.
Wakili wa upande wa utetezi Frank John, ameeleza mahakama hiyo kuwa hawako tayari kuendelea na kesi jana na kudai kuwa ili mshtakiwa aweze kusikilizwa kikamilifu lazima awe amepewa maelezo ya mlalamikaji.
Wakili John, amesema pamoja na kusomewa shitaka bado mshitakiwa hajapewa hati ya mashtaka na hoja ya tatu apate muda wa kuongea na mteja wake ili aone ni jinsi gani ya kuweza kumtetea vizuri katika shtaka linalomkabili na ndiyo msingi muhimu wa haki ya kuwakilishwa na wakili.
Pia ameiomba mahakama kuahairisha shauri hilo kwa tarehe nyingine ambayo watakubaliana pande zote mbili upande wa utetezi na upande wa mashtaka kwa sababu siku moja kabla ya kesi hiyo alipata msiba wa kufiwa na kaka yake.
Akijibu hoja za wakili wa upande wa utetezi wakili wa Serikali Alice Mutungi,amesema mshitakiwa alifikishwa mahakamani tangu asubuhi hadi saa kumi jioni kama alitaka kuongea na mteja wake wangekuwa wameshaongea na kuiomba mahakama kuangalia maslahi ya mtoto ambaye ni mhanga katika shauri hilo ambaye pia amekuwepo mahakamani hapo tangu asubuhi kwa ajili ya kusikilizwa.
"Tukisema shauri hili liahirishwe mtoto aondoke na kurudi tena tunaona kwa mazingira haya sio salama kwa mtoto, tunaiomba mahakama yako tukufu kwa maslahi ya mtoto shauri hili lisikilizwe kwa haraka ili mtoto asiwe anakuja mahakamani na kurudi"amesema wakili Alice.
Amesema hati ya mashtaka amepewa wakili wa mshitakiwa na wakili hajakana amekiri kupokea hati hiyo kisheria, wakili ni muwakilishi wa mshitakiwa na yupo kwa ajili ya kumsemea.
Hakimu wa mahakama ya wilaya Endrew Kahabuka baada ya kusikiliza hoja za pande mbili, upande wa wakili wa utetezi na upande wa mawakili wa mashitaka amewataka upande wa utetezi kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni wadhamini wawili wakazi wa manispaa ya Bukoba wenye mali zisizohamishika zenye thamani ya sh.milioni nne kila mmoja na mtuhumiwa kutakiwa kutotoka ndani ya manispaa ya Bukoba labda kwa kibali maalum cha mahakama.
Vilevile upande wa utetezi wametimiza masharti hayo na mshitakiwa amedhaminiwa kesi yake itatajwa Oktoba 29, mwaka huu.
Hata hivyo, baada ya kudhaminiwa mshitakiwa amekamatwa tena akiwa amefika nyumbani kwake.
Tuesday, October 22, 2024
TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO KUZINDULIWA TAREHE 23 OKTOBA 2024
Naibu waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Tamasha la sanaa Bagamoyo, leo tarehe 22 Oktoba 2024. katika ukumbi wa TaSUBa mjini Bagamoyo.
.................................
Na Athumani Shomari Mkwama.
Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo linatarajiwa kufunguliwa rasmi Tarehe 23 Oktoba 2024 katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa TaSUBa mjini Bagamoyo, Naibu waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amesema wizara kwa kushirikiana na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) wamejipanga kupokea wageni na kuwaburudisha kutokana na burudani za sanaa na utamaduni zitakazowasilishwa kwenye Tamasha hilo.
Amesema TaSUBa imekuwa ikifanya tamasha kama hilo kila mwaka na kwamba kila mwaka linakuwa bora zaidi kuliko mwaka uliopita na mwaka huu pia litakuwa bora zaidi ukilinganisha na miaka iliyopita.
Ameongeza kwa kusema kuwa, lengo la Tamasha hilo ni kutangaza kazi za wasanii kimataifa, kukuza vipaji na kutoa fursa kwa wasanii wa ndani kuweza kufanya kazi zao nje ya nchi kutokana na wageni kutoka nchi mbalimbali wanaohudhuria katika Tamasha hilo.
Alisema Serikali imejipanga kuinua kazi za wasanii na kuimarisha utamaduni wa Mtanzania ili asili ya furaha isiyoharibu maadili ya utamaduni wa mtanzania ibakie kama ilivyopokelewa kutoka kwa wazee waasisi wa Taifa hili lakini pia ndio malengo ya serikali katika awamu zote ikiwemo awamu hii ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Aliongeza kwa kusema kuwa wapo vijana wadogo wameanza kuonesha vipaji vyao vya sanaa na utamaduni hivyo ni wajibu wa serikali kwa kushirikiana na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kuwalea vijana hao ili kutimiza ndoto zao na kukuza vipaji vyao kwa kuzingatia maadili na utamadani wa kitanzania.
Naibu waziri huyo wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, ametumia nafasi hiyo kuwaalika watanzania wote kuhudhuria katika Tamasha hilo litakalodumu kwa muda wa siku nne ndani ya mji wa kihistoria Bagamoyo.
Akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu waziri, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga, amesema wamejipanga kuimarisha ulinzi wakati wote wa Tamasha na kuwahakikishia wageni wote watakaowasili Bagamoyo kuwa wapo katika eneo salama.
Amesema maandilizi yameenda vizuri ya kuhakikisha kila mgeni atakaewasili Bagamoyo kwaajili ya Tamasha la Sanaa na Utamaduni atapata sehemu ya kulala iliyokuwa bora na salama.
Awali akitoa Taarifa ya Tamasha hilo, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye, amesema Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, litahusisha shughuli mbalimbali za kisanii, kiuchumi na kijamii lengo likiwa ni kuvutia wadau na watazamaji kutoka ndani na nje ya nchi.
Amesema Tamasha hilo litahusisha jumla ya vikundi 74 ambapo vikundi 61 ni kutoka Tanzania Bara na Zanzibar 2, na vikundi 11 vya kimataifa kutoka nchi za Afrika ya kusini, Zambia, India, Ujerumani, Brazil, Uhispania, Botswana na visiwa vya Mayote.
Ameeleza kuwa, vikundi hivyo vitafanya maonesho ya Sanaa za jukwaani ikiwemo ngoma, za asili na za kisasa muziki wa asili na wakisasa maigizo, sarakasi, ushairi, vichekesho na mazingaumbwe.
Alifafanua kuwa, Tamasha la 43 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo litafunguliwa rasmi tarehe 23 Oktoba 2024 na mgeni rasmi anatarjiwa kuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Dkt. Damas Ndumbaro na kilele chake kitakuwa tarehe 26 Oktoba 2024 ambapo mgeni rasmi wa kufunga Tamasha hilo anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Tulia Ackson.
































