Saturday, September 21, 2024

RAIS SAMIA AKUTANA NA MKUU WA JESHI LA POLISI IGP WAMBURA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura pamoja na Makamishna wa Jeshi hilo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 20 Septemba, 2024





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura pamoja na Makamishna wa Jeshi hilo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 20 Septemba, 2024


TAMASHA LA UTAMADUNI KITAIFA LAFUNGULIWA SONGEA.





Na Mwandishi Wetu, RUVUMA

WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro amewaasa watanzania kuzingatia miiko, mila na desturi za kitanzania na kuwarithisha watoto na vijana ili kujiepusha na tamaduni za kigeni zisizofaa kwa jamii.

Aidha, ameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuwachukulia hatua kali wale wanaoua mila na desturi za watanzania kwenye mitandao ya kijamii.

Akizindua Tamasha la tatu la Utamaduni Kitaifa kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea, alisema kusipokuwa na utamaduni hakutakuwa na utu na wasipouenzi hawatauendeleza.

“Ili Taifa liwe hai lazima tuenzi na kuendeleza utamaduni wetu, na lazima turithishe utamaduni wetu kwa vijana na watoto na lazima tuwafundishe watoto wetu mila na desturi za kitanzania, Kiswahili tuwafundishe miiko mbalimbali na historia yetu kwa kuwa hawa watoto ni taifa la kesho,”alisema.

Alisema katika maadhimisho ya tamasha hilo ilitolewa semina ya maadili na utamaduni iliyofundisha jinsi ya kuenzi utamaduni na namna ya kukabiliana na madhara ya sayansi na teknolojia katika kulinda, kuenzi na kuendeleza mila na desturi.

“Sasa hivi duniani kuna suala linaitwa haki za binadamu ni jambo linalopaswa kuliheshimu na kulizingatia lakini tusitumie haki za binadamu kuingiza tamaduni za kigeni zisizofaa katika jamii yetu,”alisema.

“Taasisi za elimu kuanzia chekechea hadi chuo kikuu ni muhimu kurithisha utamaduni wetu una mila zetu katika kupambana na mmonyoko wa maadili,”alisema.
 

Alikemea tabia ya familia kulaumu mmonyoko wa maadili badala ya kujikita kutoa elimu kwa watoto na vijana ili kuishi kwenye tamaduni za mtanzania.
 

Hata hivyo, alisema taasisi za dini zina nafasi ya kukabiliana na mmonyoko wa maadili na kurithisha utamaduni kwa watoto na vijana.


“Tuwafundishe maadili mema watoto wetu, viongozi wa dini mna kazi kubwa sana na maadili mengi ya dini yanatusaidia kulinda tamaduni zetu,”alisema.


Awali, Dk.Ndumbaro alibainisha kuwa Septemba 8, 2021 katika maadhimisho ya utamaduni Bujora mkoani Mwanza Rais Samia Hassan Suluhu alitoa maelekezo kwa Wizara hiyo kuandaa tamasha la kitaifa litakalofanyika kila mkoa.
 

“Maelekezo yale yametufanya tuwe Songea leo, uwepo wetu hapa ni maelekezo ya Rais Samia kudumisha tamaduni zetu, ”alisema.

 Alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na makabila zaidi ya 120 na lugha za kijamii zaidi ya 150 na ni utajiri wa kiutamaduni.

“Utamaduni wetu unategemea nguzo zifuatazo moja ni upendo, mshikamano, umoja, amani na utulivu, yote tunayoyafanya ili kuendeleza nguzo hizi,”alisema.

Tuesday, September 17, 2024

MADAKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA WAWEKA KAMBI MKOANI LINDI

 

Na Hadija Omary, LINDI.


Wananchi Mkoani Lindi wametakiwa kutumia siku sita za ujio wa madaktari bingwa na ubingwa bobezi wa Rais Samia kupata huduma za kibingwa kwa karibu katika hospitali za Wilaya  za Mkoa huo


 

Rai hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi Dkt Kheri Kagya Jana  septemba 16, 2024 wakati wa kuwapokea madaktari hao bingwa na bingwa bobezi wa Rais Samia katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa lindi kisha kuwakabidhi kwa waganga wakuu wa halmashauri sita za mkoa huo



Madaktari hao watakuwepo kwa muda wa siku 6 kuanzia Jana Septemba 16 hadi 21 wakitoa huduma za kibingwa kwenye hospitalli zote za halmashauri Mkoani Lindi lengo likiwa  kusogeza huduma za kibingwa na ubingwa bobezi karibu zaidi na wananchi pamoja na kuwajengea uwezo wataalam wa afya kwa ngazi ya halmashauri kutoa huduma hizo za kibingwa.



Dkt. Kagya ametaja madaktari waliopokelewa ni pamoja na madaktari bingwa wa huduma za magonjwa ya kike na uzazi, upasuaji, mfumo wa mkojo, magonjwa ya ndani, huduma za mifupa, watoto, ganzi na usingizi.



Amesema huduma hizo zitatumia bima na kwa wagonjwa wasio na bima watamuona daktari na Kuchangia Kiasi kidogo kwa utaratibu wa kawaida kama atahitajika kupata huduma nyingine ikiwemo vipimo, upasuaji na dawa.



Awali, akizungumza Mwakilishi kutoka Wizara ya afya ambaye pia na mratibu wa madaktari hao waliotoka hospitali mbalimbali hapa Nchini  Faraja Mgeni amewakumbusha Madaktari kwenda kufanya kazi kwa kujituma zaidi na kuzingatia maadili ili kutimiza lengo la Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Wizara ya Afya kwa wananchi huku akiomba waganga wakuu kwenye halmashauri kuwapa ushirikiano wa kutosha ili waweze kutimiza majukumu yao.





Thursday, September 12, 2024

MAGEUZI MAKUBWA WAKALA WA VIPIMO (WMA)

 

Na Albert Kawogo 


SERIKALI kupitia Wakala wa vipimo nchini (WMA)imefanya mageuzi makubwa yanayolenga kumlinda mlaji kwenye huduma na ubora wa vipimo vinavyotumika kwenye sekta za biashara, afya na mazingira.


 Mtendaji Mkuu wa WMA Alban Kiula amesema hayo jana wakati akiongea Jijini Dar es Salaam na Wahariri kutoka Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ukiwa ni mfululizo wa vikao vya Taasisi za Umma zilizoko chini ya msajili wa hazina. 


Kiula alisema WMA ina jukumu kubwa la kuilinda jamii kwenye athari zinazotokana na matokeo ya upimaji usio sahihi katika biashara na maeneo mengine mtambuka.


"Unaweza usiione hii hali lakini kuna madhara makubwa kijamii yatokanayo na upimaji usio sahihi hasa kiuchumi" Alisema Kiula


Mtendaji Mkuu alisema jukumu la WMA  haliishii tu kwenye kusimamia na kudhibiti vipimo bali pia taasisi hiyo inatoa ushauri wa kitaalam kuhusiana na vipimo Kwa serikali, mashirika ya umma na Taasisi binafsi.


Pia Kihula alisema moja ya mafanikio makubwa ya WMA ni kuongezeka kwa idadi ya vipimo vinavyohakikiwa na kuendelea na ununuzi wa vifaa vya kitaalam ambapo yote haya yameipa thamani taasisi hiyo


Akizungumza kwa niaba ya Wahariri Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania TEF Deodatus Balile alisema kazi kubwa ya kupongezwa imefanywa na WMA lakini bado changamoto ipo kwenye uchache wa watendaji kwakuwa jukumu lao kama WMA lina wigo mpana wa kiutendaji hasa kwenye yale maeneo yanayogusa walaji Kwa bidhaa za chakula na vifaa vya ujenzi.

Tuesday, September 10, 2024

SHARIFA MKWANGO MWENYEKITI MPYA TWFA MKOA WA LINDI

 






NA HADIJA OMARY, LINDI.

Sharifa Mkwango ameshinda kuwa Mwenyekiti mpya wa chama cha mpira wa miguu Wanawake  (TWFA) Mkoa wa Lindi atakaehudumu nafasi hiyo kwa muda wa miaka mitano  baada ya kushinda kwa Kura za ndio

Uchaguzi huo umefanyika Jana huko Manispaaa ya Lindi ambao ulihusisha pia nafasi za wajumbe wawili wa kamati tendaji ambao ni Bi. Subira  Mwangata na Beatrice Victor pamoja na nafasi ya mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa (TWFA) Bi.Sifa Mwaya 

Akifungua mkutano huo  Afisa Michezo wa Manispaa  ya Lindi Jamal Lisuma  kwa niaba ya Katibu tawala wa Wilaya ya Lindi hudhaifa Rashid aliwataka  viongozi watakaochaguliwa kutatua changamoto zilizopo Katika Mkoa wa Lindi upande wa soka la Wanawake ikiwemo kuongeza vilabu vya timu za Wanawake na kuanzisha ligi ya Wanawake Ngazi za Wilaya na Mkoa 

Amesema lengo la hayo yote ni   kutafuta vipaji vya wachezaji  hao wanawake wanaoweza kuunda timu ya Mkoa inavyoweza kushiriki ligi kuu ya Wanawake Tanzania Bara.

Kwa upande wake Bi Sharifa Mkwango Mwenyekiti mpya wa (TWFA) ameahidi kufanya uhamasishaji kwa Jamii kuona Umuhimu wa kuwekeza Katika Michezo kwa watoto wa Kike.

Katibu wa kamati ya Uchaguzi Fidea Mnunduma amewapongeza wajumbe kwa kutimiza wajibu wao na kutenda haki  kwenye uchaguzi huo  na kwamba Kura zimepigwa vizuri hakuna zilizoharibika kila Mmoja ametumia  haki yake kwa kutimiza wajibu wake


"Kamati ya uchaguzi inawashukuru wajumbe wote  kwa ushirikiano uliouonysha lakini Leo mmeweza kupata viongozi wapya wa TWFA kamati ipo itadumu kwa miaka minne kama mutakuwa na tatizo lolote  kamati imefungua milango njooni mtuone"

Monday, September 9, 2024

DKT. BITEKO ASHIRIKI DUA YA MZEE MAJID NSEKELA

 




Na Alodia Dominick, Kyerwa.


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,  Dkt. Doto Biteko ameiasa jamii kuwa na utaratibu wa  kuwatunza na kuwajali  wazazi wao, amesisitiza upendo miongoni mwa jamii na kuendelea kuwaombea ambao hawapo hai.


Dkt. Biteko ameyasema hayo Septenba 7, 2024 akiwa Nyakatuntu, wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera wakati aliposhiriki katika dua ya kuwaombea baba mzazi na ndugu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Mussa Nsekela



“ Tuendelee kuwakumbuka na kuwaombea ndugu na wazazi waliotangulia mbele za haki ni jambo zuri na wajibu wetu tuliobaki, Sheikh wetu katika mawaidha yake ameliongelea kwa uzuri sana. Tulitilie maanani na sote tuendelelee kufanya hivi, na kama huwa hatuwafanyii hivi ndugu zetu, hatuna budi tuanze kwa moyo wote.” Amesema Dkt. Biteko.

 


“Ndugu zangu tusisahau mapito yetu, Katika mapito huwa kuna watu, Katika watu hawa, kuna wazazi wetu, Kama wazazi wako wapo hai, mmoja au wote au wale waliokulea, jua nawe una wajibu wa kuwalea na kuwatunza, siyo kifedha tu bali pia kwa mahusiano mema hasa ya kihisia kwa kuwa hivyo ndivyo impendezavyo Mungu.”ameongeza Dkt Biteko 


Ametolea mfano wa  Rais wa awamu ya pili, Marehemu Ally Hassan Mwinyi, Mzee Rukhsa kuwa aliiasa jamii kuwa maisha hapa duniani si kitu ila ni hadithi tu na kuwa wayafanye maisha yao yawe hadithi nzuri. 


"Kwa dua hii, kwa umati huu, kwa wanafamilia hawa wa Nsekela inadhihirisha bayana kabisa kuwa maisha ya Mzee wetu, Alhaji Tibihika Mussa Nsekela, na wengine tuliowaombea dua leo hapa yameacha hadithi nzuri kwa sisi tuliobaki hili ni jambo zuri la kujifunza.”

 

Aidha, Dkt. Biteko ameendelea kuiasa jamii kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao wanapotoka, kuendelea kuishi kwa upendo sambamba na kuishukuru familia hiyo kwa kumualika kushiriki katika dua hiyo.

 

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema kuwa Serikali  imeendelea na jitihada zake mbalimbali za kuwaletea maendeleo wananchi wa Nyakatuntu kwa kutekeleza miradi mbalimbali katika Wilaya ya Kyerwa  na tayari imetenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa mradi wa barabara.


Kwa upande wake, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuber amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Majid Nsekela kwa kuandaa dua hiyo kwa ajili ya baba yake na kusema kwa kufanya hivyo inaonesha anaipenda familia yake na dini yake ya kiislamu.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Majid Nsekela amesema kuwa tukio hilo kwao ni la kihistoria na wanamshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema hiyo.


“Kwa dua hii ya leo tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko pamoja na kuwa na kazi nyingi amejumuika nasi hapa na wote mliopo nasi leo kwa upendo wenu na familia yote imefurahi na inawashukuru,” amesema  Nsekela.


Aidha, Majid amewakumbusha na kuwatakia heri wananchi wa Nyakatuntu kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za 

Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu kwa kuchagua viongozi wanaofaa.

Monday, August 26, 2024

MTAALAMU BINGWA WA NYONGA NA MAGOTI ATUA DAR.

 



Ashirikiana na wataalamu wazawa upasuaji Mloganzila


Na Mwandishi Wetu


MTAALAMU bingwa wa ubadilishaji wa nyonga na magoti  kutoka hospitali kubwa nchini India ya Yashoda, Dk. Ram Mohan Reddy amewasili jijini Dar es Salaam kwaajili ya kambi ya matibabu hayo kwa watanzania.


Daktari huyo kwa kushirikiana na wataalamu wa ndani atafanya upasuaji huo kwenye kambi ya siku tano itakayofanyika katika hospitali ya Muhimbili Mloganzila  kuanzia leo Jumatatu hadi tarehe 30.


Aliwasili jana usiku katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo alipokelewa na wafanyakazi wa Global Medicare ambao wameratibu kambi hiyo kwa kushirikiana na Muhimbili Mloganzila.


 Akizungumza kwenye mapokezi hayo, Meneja Mkuu wa Global Medicare, Daniel Lazaro,  alisema wamefurahi kuona amefika salama nchini Tanzania na kwamba ujio wake utakuwa wa manufaa makubwa kwa watanzania wenye matatizo ya nyonga na magoti.


“Tunajua ni mara yako ya kwanza kuja kufanyakazi na madaktari wa hapa Tanzania  kwenye upasuaji wa aina hii lakini tunatarajia watanzania wengi watanufaika na ujio wako kwenye kambi hii ya siku tano itakayoanza katika hospitali ya Muhimbili Mloganzila,” alisema


Naye Dk. Reddy aliishukuru serikali ya Tanzania na taasisi ya Global Medicare kwa kuratibu vyema safari yake ya kuja nchini Tanzania na aliahidi kutoa huduma bora kwa wagonjwa watakaojitokeza kwenye kambi hiyo.


“Natarajia tunashirikiana vizuri sana na wataalamu wenzangu wa hapa nchini kwenye kambi hii ya siku tano na kwa huduma hii natarajia tutaongeza chachu ya ushirikiano baina ya Tanzania na India na tutabadilishana uzoefu wa kufanya upasuaji wa aina hii kwa wataalamu na watu wa hapa nchini watakaokuja kusoma India,” alisema


Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Upasuaji wa hospitali ya Mloganzila, Goodlove   Mfuko, alisema hivi karibuni kuwa maandalizi yote yamekamilika na kwamba kwenye kambi hiyo watashirikiana na mtaalamu huyo Dk. Ram Mohan Reddy.


 


“Mtaalamu huyu atashirikiana na madaktari bingwa ambao ni wataalamu wa mifupa na ajali hapa Mloganzila, hii itakuwa mara ya pili kutoa huduma  kama hii kwani mara ya kwanza tuliwafanyia upasuaji wa kubadilisha nyonga na magoti wagonjwa 170 kwa mafanikio makubwa,” alisema


“Kwa hiyo kwenye kambi hii ambayo ni ya pili  tutashirikiana na daktari huyu mbobezi kutoka India kupata uzoefu ili tuweze kubadilishana naye uzoefu ili tuboreshe zaidi huduma zetu,” alisema


“Kwa hiyo watu wenye matatizo ya nyonga na magoti wafike Mloganzila mapema ili wafanyiwe uchunguzi wa mapema kwaajili ya kupewa hiyo huduma ya kubadilisha nyonga na magoti,” alisisitiza Dk. Mfuko.


 

WANAFUNZI WATAKAOFANYA VIZURI SHULE BRLILLIAN KUPELEKWA SERENGETI

 






Picha mbalimbali mahafali ya 14 ya kidato cha nne shule ya sekondari ya  Brilliant ya Kimara Mbezi kwa Msuguri jijini Dar es Salaam yaliyofanyika jana Jumamosi

...............................................

Na  Mwandishi Wetu

Mbunge wa Bukoba Vijijini (CCM), Dk. Jasson Rweikzia, ametangaza kwamba kwenye mtandao wa shule za St Anne Marie Academy unaominilikia pia shule ya Brilliant ya Kimara Mbezi kwa Msuguri jijini Dar es Salaam, hakuna mwanafunzi atakayefukuzwa shule baada ya wazazi wake kufariki na kushindwa kulipa ada ya kuendelea na masomo.


 


Alitangaza uamuzi huo mwishoni mwa wiki wakati wa mahafali ya  14 ya kidato cha nne ya shule ya Brilliant iliyoko Kimara Mbezi jijini Dar es Salaam.


 


Mtandao huo unamiliki shule za St Anne Marie Academy, Brilliant, Rweikiza Nursery and Primary na Sunshine ya Kibaha Mkoa wa Pwani.


 


Dk Rweikiza alisema shule hizo ziliwahi kupoteza wazazi 93 kwasababu mbalimbali na kusababisha baadhi ya wanafunzi kuacha masomo kwa kukosa ada hali ambayo alisema imeilazimu shule hiyo kuwapa msamaha wa ada wanaofiwa.


 


 " Tumekuwa tukipoteza wazazi wengi na mwezi huu pekee tumepoteza wazazi watatu na hali hii imekuwa ikiathiri sana wanafunzi kitaaluma na wengine kuacha shule kwa kushindwa kulipa ada lakini kuanzia sasa hakuna atakayefukuzwa shule kwa kukosa ada baada ya mzazi wake kufariki," alisema


 


 " Kama yuko darasa la kwanza na amefiwa na mzazi wake ataendelea kusoma mpaka darasa la saba na kama ni sekondari ataendelea mpaka kidato cha nne," alisema Dk. Rweikiza


 


Dk. Rweikiza alisema katika mpango wa kuinua taaluma shuleni hapo wameaandaa zawadi mbalimbali zikiwemo fedha taslimu kwa awatakaofanya vizuri kwenye masomo yao na ziara za kimasomo kwenye mbuga mbalimbali za wanyama.


 


Alisema mwanafunzi atakayepata daraja la kwanza atapata sh 600,000 na atakayepata daraja la II atapata Sh 200,000 na kwamba lengo ni kuhakikisha hakuna daraja la nne wala daraja la tatu shuleni hapo.


 


Mkuu wa shule ya Brilliant, Edrick Phillemon alisema wahitimu hao wa kidato cha nne wameandaliwa vizuri kitaaluma na wanatarajiwa kufanya vizuri kwenye mitihani yao na kwamba ana uhakika wa kupata daraja la kwanza na la pili.


 


“Tuna uhakika wa kufanya vizuri kwani ukiangalia historia ya shule ya Brilliant huwa haipati daraja la nne wa daraja 0, mara nyingi tunafaulisha kwa daraja la kwanza na la pili,” alisema


 


 Alisema wanafunzi hao wamewezeshwa kufikia hapo na walimu wenye taaluma na uzoefu wa kutosha huku akimshukuru Mkurugenzi wa shule hizo, Dk. Rweikiza kwa kuendelea kufanya maboresho ya miundombinu ya shule hiyo.

Friday, August 23, 2024

JJAD KAGERA FARMERS YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA BEI NZURI YA KAHAWA

 

Na Mwandishi Wetu


KAMPUNI  inayojihusisha na kilmo cha kahawa  JJAD Kagera farmers imeishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan kwa kusaidia bei ya kahawa kupanda hadi kufikia shilingi 1,200 mwaka jana mpaka kufikia shilingi 5,300


Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendji wa wa Kampuni hiyo, Dk.  Albert Katagira, mara baada ya uzinduzi wa kongamano na maonyesho ya 21 ya kahawa bora Afrika.


Kongamano hilo lililoandaliwa na Chama cha Kahawa Bora Afrika (AFCA), linatarajiwa kufanyika mwezi wa pili mwakani na linatarajiwa kuwashirikisha zaidi ya washiriki 2,000 ambao ni wadau wa biashara ya kahawa Afrika na maeneo mengine duniani.


Kampuni ya JJAD Kagera Farmers Limited iliyoko wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera imekuwa ikiendesha kilimo cha kahawa aina ya Robusta kwenye mashamba yenye ekari 100.


“Zao la kahawa kwa mwananchi wa Kagera sasa limekuwa mkombozi mkubwa na nashukuru sana AFCA kuamua kuleta kongamano na maonyesho ya kahawa Tanzania mwakani, Kongamano ambalo  litatusaidia sana kuongeza mbinu mpya za kulima zao hili na tutapata masomo mengi,” alisema Dk. Katagira


Dk. Katagira alisema serikali ione umuhimu sasa wa kuwakopesha wakulima wa kahawa kwani kuandaa mashamba ya zao hilo kuna gharama kubwa sana.


“Kuendesha mashamba makubwa ya kahawa siyo kazi rahisi kwa hiyo tunaomba serikali ione umuhimu wa kuwa inawakopesha wakulima mikopo midogo midogo ya kulima kahawa ili wakulima wengi wahamasike kulima zao hili,” alisema


Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa (TCB), Primus Kimaryo alisema kongamano la 21 litafanyika mwakani na ni fursa ya kipekee kwa wakulima wa kahawa kwani uzalishaji wa kahawa hiyo umekuwa ukiongezeka.


Alisema bodi ya AFCA iliamua kuwa kongamano lao la  mwakani lifanyike  jijini Dar es Salaam na itakuwa fursa ya kipekee kwa wakulima wa kahawa Tanzania kuonyesha kahawa wanayozalisha kwaajili ya kutafuta masoko ya zao hilo.


“Hii ni fursa kubwa kwa wakulima kutafuta masoko ya kahawa na kuongeza ubora wa kahawa kwasababu bei ya kahawa duniani inazidi kuwa nzuri kwahiyo wanapaswa kuitumia hiyo fursa kuyafikia masoko ambayo ni makubwa,” alisema


Mwenyekiti wa Bodi ya AFCA, Amir Hamza alisema  Tanzania itakuwa mwenyeji wa kongamano na Maonyesho ya 21 ya Kahawa Bora za Afrika (Afrika Fine Coffee Conference & Exhibitions) kuanzia 26 – 28 Februari, 2025, jijini Dar es Salaam.


Alisema kongamano na maonyesho haya  ni jukwaa kubwa zaidi la biashara ya kahawa barani Afrika, na huvutia zaidi ya wadau wa kahawa 2,000 kutoka ndani na nje ya Afrika kila mwaka ikiwa ni pamoja na wazalishaji, wafanyabiashara wa kahawa, wakaangaji wa kahawa na pia wadau kutoka sekta ya umma na binafsi, na wawakilishi wa serikali.


Alisema kongamano na maonyesho haya yanafanyika hapa nchini kwa mara nyingine baada ya kufanyika kwa mara ya mwisho mwaka 2016.


“ Tanzania ni nchi yenye fursa kubwa katika sekta ya kahawa na kongamano na maonyesho haya yanadhihirisha ubora wa kipekee wa kahawa za Afrika na pia yanaimarisha dhamira ya nchi za Afica   kukuza ukuaji na ushirikiano katika sekta ya kahawa Africa,” alisema.


“Kauli mbiu ya Kongamano la 21 ni “Kuhuisha ongezeko la Thamani” ambapo kwenye Kongamano patakuwepo na orodha ya wazungumzaji maarufu kimataifa na kikanda. Aidha Maonyesho ya kahawa yatakayofanyika yataoonyesha ubunifu na maendeleo yaliyotokea hivi karibuni katika sekta ya kahawa,” alisema.


Alisema pia  kutakuwepo warsha ambazo zitakuwa na majadiliano yenya tija, kutoa fursa za kipekee za kuonja na kutathmini kahawa  na safari maalum zitakazoandaliwa ili kujifunza kuhusu kahawa.  



Alisema katika kongamano na maonyesho haya kutakuwepo na mashindano ya watayarisha kahawa Africa (Barista Championship) na Mashindano ya kahawa bora katika ukanda wa Afrika ili kuonyesha vipaji na bidhaa bora zaidi za kahawa kutoka kote barani.


Wednesday, August 21, 2024

ZAIDI YA WAVUVI ELFU 11 LINDI KUFIKIWA NA ELIMU YA UVUVI SALAMA

 





NA HADIJA OMARY, LINDI

Zaidi ya wavuvi elfu 11 Mkoani Lindi wanatarajiwa kufikiwa na kupatiwa elimu ya ufahamu juu ya masuala ya bahari ili kuongeza ufanisi na usalama katika shughuli zao za uvuvi.



Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya  uvuvi salama inayoendeshwa na chuo cha Bahari Dar es salaam Mkuu wa wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga, amesema  Elimu hiyo ni muhimu kwa wavuvi wa Lindi kwani itawasaidia kufanya shughuli zao kitaalam na kuachana na uvuvi wa mazoea 


Mkuu wa chuo cha Bahari Dar es salaam Dr. Tumaini Guruma Amesema lengo uzinduzi wa kampeni hiyo ni kuleta ufahamu wa  usalama baharini kwa wananchi huku akiweka bayana fursa mbalimbali zitokanazo na uvuvi ni pamoja na ajira kwa vijana


Mkuu wa idara ya kozi za umahiri Deism Mlay amesema kupitia kampeni hiyo kwa kipindi cha siku nne wataalam watapita katika shule, masoko ya samaki kukutana na wavuvi na kuwapatia elimu  ya kozi za usalama baharini, unahodha wa vyombo vya uvuvi pamoja na usalama katika shughuli za uvuvi.