Wednesday, August 21, 2024

ZAIDI YA WAVUVI ELFU 11 LINDI KUFIKIWA NA ELIMU YA UVUVI SALAMA

 





NA HADIJA OMARY, LINDI

Zaidi ya wavuvi elfu 11 Mkoani Lindi wanatarajiwa kufikiwa na kupatiwa elimu ya ufahamu juu ya masuala ya bahari ili kuongeza ufanisi na usalama katika shughuli zao za uvuvi.



Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya  uvuvi salama inayoendeshwa na chuo cha Bahari Dar es salaam Mkuu wa wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga, amesema  Elimu hiyo ni muhimu kwa wavuvi wa Lindi kwani itawasaidia kufanya shughuli zao kitaalam na kuachana na uvuvi wa mazoea 


Mkuu wa chuo cha Bahari Dar es salaam Dr. Tumaini Guruma Amesema lengo uzinduzi wa kampeni hiyo ni kuleta ufahamu wa  usalama baharini kwa wananchi huku akiweka bayana fursa mbalimbali zitokanazo na uvuvi ni pamoja na ajira kwa vijana


Mkuu wa idara ya kozi za umahiri Deism Mlay amesema kupitia kampeni hiyo kwa kipindi cha siku nne wataalam watapita katika shule, masoko ya samaki kukutana na wavuvi na kuwapatia elimu  ya kozi za usalama baharini, unahodha wa vyombo vya uvuvi pamoja na usalama katika shughuli za uvuvi.

No comments:

Post a Comment