Thursday, February 8, 2024

UWT NA KIPAUMBELE CHA MAZINGIRA WEZESHI KUINUA WANAWAKE KIUCHUMI

 


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt Doto Biteko akimkabidhi Nakala ya Makubaliano kati ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC)  Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda (MCC) jijini Dodoma Tarehe 07 February 2024.

.......................

DODOMA 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt Doto Biteko  amemkabidhi Nakala ya Makubaliano kati ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC)  kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda (MCC) katika Hafla ya Utiaji Saini wa Makubaliano hayo.

Aidha, Mwenyekiti Chatanda alishiriki hafla hii kwa lengo la kuhakikisha UWT inakuwa mstari wa mbele katika kuchangia uwepo wa mazingira wezeshi ya kuwainua Wanawake Kiuchumi kuanzia katika utoaji elimu na hamasa kwa jamii.

UWT IMARA JESHI LA MAMA SAMIA KAZI IENDELEE.


Tuesday, February 6, 2024

ALIYEMKATA KIGANJA KATIBU WA BAKWATA BUKOBA AUWAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA.

 

Na Alodia  Babara

Bukoba,

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Abdulmalick Yahya (42) mkazi wa wilaya ya Muleba ambaye alikuwa mtunza ghala katika mradi wa ujenzi wa BAKWATA Bukoba (BAKWATA COMPLEX) amefariki baada ya kushambiliwa na wananchi wenye hasira kufuatia tukio alilofanya la kumshambulia katibu wa BAKWATA wilaya ya Bukoba na kumkata kiganja cha mkono.

Katibu wa Bakwata wilaya ya Bukoba Hamza Zakaria (43) akiwa anaendelea na matibabu katika hospital ya rufaa ya mkoa, Bukoba amesimulia alivyoshambuliwa na aliyekuwa mtunza ghala la ujenzi wa BAKWATA Complex na kuanza kumkata kwa panga kisha kutenganisha kiganja na kiwiko cha mkono wa kushoto.

"Ilikuwa ni majira ya saa 10:00 asuhuhi siku ya Tarehe 2 februali 2024 wakati nikiwa kazini kwangu nilitoka kwenda duka la jirani kuangalia viatu kwa mtu mmoja anaitwa Khalid ndipo alitokea Abdulmalick Yahya akiwa ameshika panga na kuanza kunishambulia" amesema Hamza

Ameendelea kusimulia kuwa, alipomkata panga la kwanza alikinga mkono alipotaka kumkata tena walishikana mikono na badae akajitoa kwenye mikono yake na kutaka kukimbia kutokana na kwamba  alikuwa amevaa kanzu ambayo ilimtega miguu akashindwa  kukimbia na badala yake alianguka chini.

"Kwa kuwa alikuwa anaendelea kunifukuza alinikuta hapo hapo chini akaanza kunikata mapanga huku  nikiendelea kukinga mkono wa kushoto ndipo baadaye nilijifanya nimefariki dunia alipokata mara ya mwisho akaona sijitingishi akaondoka" ameongeza Hamza.

Amesema ndani ya dakika kama tano hivi alimuona mtu anayemfahamu akamuita wakampa msaada wa kumbeba na vijana wengine na kumpeleka hospital ya rufaa ya mkoa wa Kagera, Bukoba ambapo anaendelea kupatiwa matibabu na anaendelea vizuri.

Amesema huyo aliyemkata mapanga hakuwa na visa naye labda kama vilitokana na ujenzi uliokuwa unaendelea msikitini, siku zilizopita alikuwa ni mtunza ghala na alikuwa ni miongoni mwa watu waliokamatwa wanaiba nondo na saruji akawa amesimamishwa kuendelea kusimamia ghala hilo, sasa alihisi kuwa alichongewa na Hamza na alikuwa ni mtu wa muda mrefu pale msikitini.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera, Blasius Chatanda, amethibitisha kutokea kwa matukio hayo mawili na kusema kuwa, Abdulmalick Yahya (42) mkazi wa wilaya ya Muleba ambaye alikuwa mtunza ghala katika mradi wa ujenzi wa BAKWATA Bukoba (BAKWATA COMPLEX) kabla hajakumbwa na umauti Februari 02,2024 majira ya saa 11:30 asubuhi katika barabara ya Kawawa karibu na ofisi za Bakwata mkoa alifika na kuanza kumkata mapanga Hamza Zakaria (43) katibu wa BAKWATA wilaya ya Bukoba.

Amesema wakati akitenda tukio hilo watu waliokuwepo walimzuia asiendelee kumshambulia bila mafanikio na walipoona anataka kuwashambulia na  wao walianza kumshambulia na alibahatika kuokolewa na jeshi la polisi na kumkimbiza hospital ya rufaa ya mkoa, Bukoba ambapo wakati akiendelea kupata matibabu alifariki dunia.

Kamanda Chatanda alieleza kwamba, chanzo cha tukio hilo ni kusimamishwa kazi ya kusimamia ghala la kutunza vifaa vya ujenzi wa BAKWATA complex  kwa Abdulmalick na kamati ya ujenzi Februari mosi ,2024 ambapo Abdulmalick alimtuhumu katibu wa BAKWATA, Bukoba kwamba ndiyo chanzo cha hayo yote na akaahidi kulipiza kisasi.

Amesema kuwa, alimkata mkono wa kushoto ambao kiganja chake alikitenganisha kabisa na kiwiko na alikatwa mapanga mengine mawili kichwani japo ni kwa bahati nzuri hayakuweza kupasua fuvu.

Ametoa rai kwa wananchi wa mkoa huo kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake kufuata sheria na taratibu za nchi.




HATUTAWAFUMBIA MACHO WANAOJIITA BOKO HARAMU NDANI YA MKOA WA PWANI - Mramba

 

Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Pwani ndg David Mramba amesema hawako tayari kuwafumbia macho wanaojiita boko haramu kwani kujiita hivyo ni kuhatarisha maisha ya Watanzania.

Mramba ameyasema hayo leo tarehe 06/02/2024 katika Ofisi za CCM Mkoa wa Pwani kuwa CCM ina macho mengi hata mtu akiwa kwenye shimo ataonekana na akibainika hataachwa salama kimaadili.

Amesema wako watu wanataka kuwatishia Wanaccm kwa kujiita wao ni boko haramu jambo ambalo si jema ndani ya CCM.

" Unapojiita boko haramu tafsiri yake wewe ni mtekaji na mbakaji hivyo lazima tuwashughulikie watu wa aina hiyo  amesema Mramba

Ameendelea kusema kuwa hakuna kikundi ndani ya CCM kitakachokuwa na uwezo wa kubadili mawazo ya Wanaccm kwa kuwatishia.

Amesema wako wanaowatishia Viongozi walioko madarakani wakidai kuanza kutengeneza safu zao huku wakijipachika majina ya aina hiyo.

Hatutawavumilia wanaokiuka taratibu za Chama na tuko tayari kuwaadhibu ili Chama na wanachama wabaki salama  amesema Mramba

Acheni vihelehele vya kuwasumbua Viongozi walioko madaraka waacheni watekeleze Ilani ya CCM kwa mioyo safi* - asema Mramba

Mramba amezungumzia usemi usemao kuwa acha haki iamue haki usitafute haki pasipo haki akimaanisha unaweza ukawa na haki ya kugombea nafasi yoyote lakini ukaipoteza haki hiyo kwa sababu ya rafu za mapema.

Amehitimisha kwa kuwataka Wanaccm kulinda heshima ya Chama na kujilinda wao ili wakati wa uchaguzi wasiwe kikwazo kwenye vikao vya mchujo.

Taarifa hii imeandaliwa na

Idara ya Siasa, Uenezi na Mafunzo CCM
Mkoa wa Pwani.


WAFANYABIASHARA WA MAFUTA ZINGATIENI MAISHA YA WANANCHI - DKT. BITEKO

 

Na Mwandishi wetu, Dodoma

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Chama cha Waagizaji na Wasambazaji wa Mafuta nchini (TAOMAC) ambapo amewataka wafanyabiashara hao pamoja na faida wanayoipata wazingatie maslahi wananchi wa hali ya chini.

Ameyasema hayo tarehe 06 Februari, 2024 jijini Dodoma katika kikao ambacho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo changamoto mbalimbali ambazo wanafanyabiashara hao wanazikabili.

Amesema Serikali siku zote iko tayari kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara na kuwekea mazingira wezeshi ya biashara zao ili waweze kuwajibika kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za usimamizi katika sekta husika.

“Tunapofanya biashara hii ya mafuta lazima tuangalie mtanzania maskini ambaye anategemea sekta hii kujikwamua kimaisha, isifike mahala kila mwisho wa mwezi watu wote wanashika vichwa wakihofia kupanda kwa bei ya mafuta… Serikali inafanya kila jitihada kupunguza makali ya bei ya mafuta hivyo nanyi mlizingatie suala hili.”amesema Dkt. Biteko

Dkt. Biteko ameishukuru TAOMAC kwa ushirikiano wao kwa Serikali katika kuhakikisha kuwa nchi inakuwa na mafuta ya kutosha na kueleza kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wao katika ukuaji wa Uchumi wa nchi.

Amesema uhusinao uliopo kati ya Serikali na TAOMAC unahitaji kuwa endelevu na pale zinapotokea changamoto zitafutwe njia za kukabiliana nazo kwa mstakabali wa Taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAOMAC, Kalpesh Mehta ameishukuru Serikali kwa mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara wa mafuta na utayari wa Serikali kushughulikia changamoto kadhaa zinazojitokeza katika sekta hiyo.

Akizungumzia mazingira hayo, Mkurugenzi Mtendaji, Raphael Mgaya amesema ushirikiano wa TAOMAC kwa serikali hauepukiki ili kuhakikisha nchi inapata mafuta ya kutosha hivyo wapo tayari kushirikiana na Serikali.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Watendaji kutoka  Taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Benki Kuu  ya Tanzania (BoT) Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba.







TAKUKURU KAGERA YABAINI MAPUNGUFU KATIKA MIRADI 16.

 

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kagera Pilly Mwakasege akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu  Octoba hadi Desemba 2023

..................................

Na Alodia Babara

Bukoba

TAASISI ya kuzuia na kupamba na Rushwa mkoa wa Kagera kwa kipindi cha Oktoba-Desemba 2023, imefuatilia miradi 19 yenye thamani  zaidi ya shilingi bilioni 6.1 ambapo kati ya hiyo miradi 16 yenye thamani zaidi ya shilingi bil.4.2 imebainika kuwa na mapungufu yaliyohitaji marekebisho.

Kamanda wa taasisi hiyo mkoani humo Pilly Mwakasege amesema kuwa kiasi hicho ni sawa na asilimia 68.50 ya fedha za miradi ambapo kumekuwa na ongezeko la asilimia 18.77 ya miradi hiyo, ukilinganisha na kipindi cha Julai-Septemba mwaka jana.

Mwakasege ameeleza hayo leo Februari 06,2024 wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao kwa kipindi cha robo tatu ya mwisho wa mwaka 2023 ambapo,miradi iliyohusika ni ya ujenzi wa miundombinu ya shule mpya za msingi na sekondari, maji, zahanati pamoja na ujenzi wa madarasa ya msingi na sekondari ili kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kuendana na thamani ya fedha iliyotumika.

Mwakasege amesema kuwa kwa kipindi hicho walipokea malalamiko 92 kati ya hayo 58 hayahusu rushwa ambapo 34 yanahusu rushwa na majalada yamefunguliwa ambapo 20 uchunguzi wake umekamilika na hatua stahiki zinatarajiwa kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria.

“Idara zilizolalamikiwa ni Halmashauri ambapo idara ya fedha kesi moja, Elimu 10, Afya saba, Utawala 12, Biashara moja, Kilimo nane, Ardhi saba, Mazingira tatu na mengine yalihusu sekta binafsi ambayo ni 12, ikiwemo  Maji tatu, Ujenzi tisa, Maliasili saba, Nishati moja, Uhamiaji mbili, Polisi nne, Mahakama tatu, Uchukuzi moja na mamlaka ya mapato Tanzania moja" ameeleza Mwakasege.

 Amesema katika progaramu ya Takukuru rafiki ambayo inatekelezwa kwa kushirikisha wadau katika ngazi ya kata ambapo wananchi hupata fursa ya kuibua kero zinazowakabili katika maeneo yao ambapo kwa kipindi cha Oktoba-Desemba walitembelea kata 11 na kupokea kero kuhusu sekta za Elimu, Afya, Maji, Fedha na Nishati ambapo ufuatiliaji wake unaendelea.

Aidha amevitaja vipaumbele vya Takukuru kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi mwaka huu ambavyo ni kuelimisha Umma kupitia njia mbalimbali ili kuongeza ushirikishwaji wa wananchi katika kuzuia vitendo vya rushwa, kutatua kero mbalimbali katika jamii kupitia programu ya Takukuru Rafiki na kuendelea kufuatilia rasilimali za Umma kupitia ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo ili kuzuia ufujaji wa fedha za Umma.

 Nyingine ni kufanya chambuzi za mifumo kwa lengo la kuzuia rushwa zinazosababishwa na mapungufu yaliyopo kwenye mifumo ya utendaji wa sekta ya Umma na sekta binafsi ambapo amewahimiza wasimamizi wa miradi ya maendeleo kuwa waadilifu na kuhakikisha fedha zote za miradi zinatumika vizuri.


Monday, February 5, 2024

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA MSD

 



Na. WAF, Dodoma

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI imeitaka Bohari ya Dawa (MSD) kuongeza ufanisi, ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha dawa zinanunuliwa, zinahifadhiwa sehemu sahihi, kusambaza dawa hizo kwa wakati katika sehemu zenye uhitaji na kukusanya madeni ili kuweza kuwa imara na taasisi endelevu.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI, Mhe. Stansilaus Nyongo baada ya kupokea taarifa ya hali ya utendaji na majukumu ya Bohari ya Dawa (MSD).

Mhe. Nyongo amesema kuwa wao kama wawakilishi wa wananchi wataendelea kuishinikiza serikali kuiwezesha MSD kupata mtaji ili kujiendesha kiufanisi katika kusambaza dawa kwa wakati.

“Bohari kuu ina majukumu ya kununua, kutengeneza, kuhifadhi dawa pamoja na kusambaza dawa katika vituo vya  vyote nchini”. Ameeleza  Mhe. Nyongo.

Mhe. Nyongo amesema kwa ujumla kamati imeridhishwa na hali ya utendaji wa Bohari ya Dawa na mipango yake ya utek


Sunday, February 4, 2024

PWANI YAHITIMISHA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 47 YA KUZALIWA KWA CCM

 


Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani leo tarehe 04/02/2024 kimehitimisha sherehe za  Maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa CCM katika Kata ya  FUKAYOSI Wilaya ya  Bagamoyo huku kikiwa na matumaini makubwa ya ushindi kuelekea uchaguzi Mkuu wa Serikali za Mitaa, Vijijini na Vitongoji 2024.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika kuhitimisha maadhimisho hayo ndg. Mwinshehe Mlao amesema ili CCM iweze kuendelea kudumu lazima Viongozi waondoe ubinafsi.

Mlao amesema unapofika wakati wa uchaguzi Kila mpiga kura ahakikishe anawachagua Viongozi wa Serikali wenye nia njema ya kuongoza na ikitokea  wakawachagua Viongozi kwa ajili ya maslahi yao binafsi basi watakuwa wamepoteza haki za wengine.

Ameendelea kusema kuwa ili kushinda chaguzi zijazo kunahitajika UMOJA huku akisisitiza kuwa kama Kuna mwanachama yeyote mwenye nia ya kugombea na anaonekana kuwa na dosari aambiwe sasa wasisubiri mpaka achukue fomu ndio waseme mabaya yake huko ni kuchafuana.

" Tusikubali kusababisha migogoro isiyo na tija tunapoelekea kwenye chaguzi zijazo na wala tusikubali watu watugawe kwa ajili ya maslahi yao" amesema Mlao

Maadhimisho hayo yameambatana na ukaguzi wa Kituo Cha afya cha Fukayosi kinachojengwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 1, Uzinduzi wa ujenzi wa Ofisi ya CCM kata ya Fukayosi, ugawaji wa vifaa vya Shule kwa wanafunzi wanaoishi katika Mazingira magumu, ugawaji wa vyeti vya PONGEZI kwa Kata zilizofanya vizuri katika uingizaji wanachama wapya na usajili kwa mfumo wa kielektroniki sambamba na zoezi la upandaji wa miti.

Taarifa hii imeandaliwa na:

David Mramba
Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo CCM
Mkoa wa Pwani.


Friday, February 2, 2024

LIONS CLUB YAKABIDHI MATENKI YA MAJI CHALINZE.

 

MUNTAZIR Bharwan mmoja wa Wanachama wa Taasisi ya Lions Club, akielekeza jambo mbele ya Diwani wa Kata hiyo Mussa Gama mwenye Balaghashia. Picha na Omary Mngindo.

Miriam Kihiyo (Watatu kutoka kwa aliyevaa Balaghashia) akimkanidhi moja ya zawadi mtoto anayetoka kwenye Kituo cha kulelea Watoto wenye Mazingira hatarishi. Picha na Omary Mngindo.


....................................

Na Omary Mngindo, Ruvu.

TAASISI ya Lions Club ya jijini Dar es Salaam imekabidhi matenki 8 ya kuhifadhia maji katika shule za msingi na Sekondari ndani ya Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani.

Matanki hayo yanalenga kuwaondolea adha wanafunzi kwenye shule hizo, yamekabidhiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Chalinze, Ramadhani Possi, aliyewakilishwa na Miriam Kihiyo Afisa Elimu Msingi.

Muntazir Bharwan alisoma taarifa ya taasisi kwa niaba ya Mwenyekiti wa Lions Host Kaniz Naghavi, iliyoeleza kuwa kukabidhiwa kwa matenki hayo kumetokana na diwani wa Kata hiyo Mussa Gama kuelezea uwepo wa changamoto kwenye shule hizo.

Hafla hiyo iliyotumika pia kumkaribisha Gavana wa Tanzania District 411C Happiness Nkya, matenki hayo yanakwenda katika shule za Msilale, Chamakweza, Sekibwa, Ruvu, Mnindi, Kitonga na Kwazoka.

"Baada ya kupokea maombi ya diwani Gama tukawasiliana na Kampuni ya Refuelling Solutions (T) Limited na wadau wengine wakiwemo wanachama wa Lions ambao tumefanikisha upatikanaji huu," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Gavana wa taasisi hiyo Nkya alisema kwamba kwa sasa wana wanachama 620 na Club 23, wakati Dar es Salaam zikiwa 14, na kwamba wamekuwa wakisaidia maeneo tofauti wakisaidiana na makampuni mengine.

Kwa upande wake diwani Gama ameishukuru Taasisi hiyo, huku akieleza kuwa imekuwa ikisaidia maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo vifaa katika Zahanati ya Ruvu Darajani, madaftari kwa wanafunzi ikiwemo matenki hayo.

"Club ya Lions imekuwa na msaada mkubwa sana kwetu wanaVigwaza, kwani wanasaidia kutatua matatizo kwenye kata yetu kwa kushirikiana na wadau wengine kutupatia misaada ya fedha na vitu katika sekta mbalimbali," alisema Gama.

Afisa Elimu awali na Msingi wa Halmashauri ya Chalinze, Mariam Kihiyo akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi hiyo,  aliishukuru taasisi hiyo, kwa misaada inayoendelea kuipeleka inayolenga kupunguza vikwazo kwa wanaVigwaza.

"Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze, Alhaj Ramadhani Possi, tunawashukuru sana ndugu zetu wa Lions Club kwa namna mnavyojitoa mkishirikiana na wadau wenu, wanaChalinze tunatambua na kuthamini mchango wenu mkubwa kwetu," alisema Kihiyo.

Samwel Mjema Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Ruvu Darajani alisema matenki hayo yatasaidia kutunza maji pindi yanapokatika, huku akiahidi utunzwaji yaweze kudumu kwa muda mrefu.


Thursday, February 1, 2024

DED BAGAMOYO AZINDUA HUDUMA KITUO CHA AFYA FUKAYOSI.

 

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw. Shauri Selenda Leo tarehe 1 Februari, 2024 amezindua rasmi utoaji wa huduma katika kituo Cha Afya Fukayosi.

Akizungumza na watumishi wa Afya pamoja na Kamati ya Maendeleo ya Kata Fukayosi (WARDC) Selenda, alisisitiza kufanya kazi Kwa weledi pamoja na  kunyenyekea wagonjwa kama sehemu ya miiko ya tasnia ya utoaji wa huduma za afya.

" Mgonjwa mpaka anafika hospitali maana yake anahitaji huduma hivyo haina budi kumpokea kwa unyenyekevu na kumsikiliza shida yake na kumpatia matibabu". Alisema Bwana Selenda.           

Kituo Cha Afya Fukayosi kimejengwa kwa kutumia fedha toka Serikali Kuu na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kwa lengo la kuimarisha huduma za afya ikiwemo Huduma ya Mama na Mtoto, Afya ya dharura na upasuaji wa wajawazito, Maabara, Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD), Mionzi, na Jengo la kufulia.

Mkurugenzi Mtendaji alipanda miti kama ishara ya Uzinduzi wa huduma katika kituo hicho Cha Afya Fukayosi. Kituo Cha Afya Fukayosi kilianza Ujenzi Mwaka wa fedha 2021/2022 na kinategemea kuhudumia zaidi ya wakazi 17,000






DC. OKASH ATATUA KERO ZA BODABODA BAGAMOYO.

 

Na Daria Abdul, Hamisi Hamisi, Bagamoyo.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Halima Okash, akishirikiana na  viongozi mbalimbali wa Halmashauri  ya Wilaya hiyo, amefanya kikao na madereva wa pikipiki zinazobeba abiria (BODABODA)  Januari 31,2024 katika ukumbi wa flexible hall Chuo cha Sanaa Bagamoyo (TASUBA), kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili katika utendaji kazi wao wa kila siku.

 Mhe.Okash, amewasisitiza bodaboda kutii sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali, pia wajiepushe na matukio ya uhalifu wa kupora mali za wateja wao.

”Ndugu zangu lazima tutii sheria za usalama barabarani kwani tunawategemea ninyi vijana kuwa ndio Taifa la kesho hizo rizki tunazozipata kuna watu wanatutegemea tusipotii sheria za usalama barabarani, kutakuwa na ajali za mara kwa mara zitakazopelekea kupoteza maisha na kuleta ulemavu.” Amesema Okash

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Usalama barabarani,  Wilaya ya Bagamoyo (DTO)  Azizi Zubeir, amewataka bodaboda kuhakikisha wanasajili vyombo vyao vya usafiri, leseni pamoja na bima ili wasikamatwe na vyombo vya usalama na kueleza Zaidi kuwa bima itasidia kupunguza gharama ya matengenezo ya vyombo hivyo na matibabu kwa dereva anapopata ajali.

"Ni waambie tu  bodaboda ili ufanye kazi kihalali lazima usajili vyombo vyetu, tuwe na leseni ya udereva pamoja na bima ya chombo husika ili itusaidie kupunguza gharama za matengenezo na matibabu inapotokea ajali.” Amesema Zubeir

Akitoa kero yake katika hafla hiyo Mwenyekit wa Bodaboda kata ya Dunda Ndug, James Mapunda, amesema kuwa wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya usalama barabarani na vyuo mbalimbali vikishirikiana na Jeshi la polisi Wilayani hapo na kuahidiwa kupatiwa leseni za udereva baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo, badala yake hawapewi leseni zao licha ya kulipia fedha kwa ajili ya leseni hizo.

Kwa upande wake Waziri Mohammed (BODABODA), ameeleza kuwa wamekuwa wakinyanyaswa na kukamatwa na Mgambo  kwa mabavu katika vituo vyao vya kazi (vijiwe) bila ya uwepo wa askari wa Jeshi la polisi kinyume na sheria hali inayopelekea kushindwa kufanya shughuli zao usafirishaji kwa amani.