Friday, September 22, 2023
Thursday, September 21, 2023
USHIRIKI WA SEKTA BINAFSI NI MUHIMU KATIKA KUKABILIANA NA UPUNGUFU FEDHA ZA MAENDELEO.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ushiriki wa sekta binafsi ni muhimu katika kukabiliana na upungufu wa fedha za maendeleo ili kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) duniani.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akichangia katika mjadala wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu ufadhili wa maendeleo uliyokuwa na dhima ya kutafuta suluhisho la kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu (SDGs). Mkutano huo umefanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.
Makamu wa Rais amesema ili kushawishi sekta binafsi kushiriki katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu ni vema mataifa yakajielekeza katika kuweka sera rafiki kwa sekta binafsi. Ameongeza kwamba kupitia ripoti ya hivi karibuni ya Mtazamo wa Kiuchumi wa Afrika (AEO 2023) kuhusu ufadhili mbadala, inabainisha wazi kuwa sekta ya binafsi ni miongoni mwa wadau muhimu katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
Halikadhalika Makamu wa Rais amesema kwa kupitia ushirikiano wa kikanda na kimataifa, Tanzania imefanikiwa kuwa na njia mbalimbali za ufadhili ambazo ni rafiki kwa sekta binafsi ikiwemo kutengeneza ramani ya wawekezaji ya malengo ya maendeleo endelevu.
Ameongeza kwamba katika uboreshaji wa miundombinu, Tanzania imetumia mbinu ya Ufadhili wa Mikataba ya Ujenzi na Ununuzi wa Kihandisi (EPC+F) ili kuongeza ufadhili wa sekta binafsi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya usafiri.
Makamu wa Rais ametaja mifano mingine kuwa ni pamoja na utoaji wa hati fungani ya kwanza nchini yenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 300 iliotolewa na Benki ya CRDB kwa lengo la kufadhili miradi rafiki ya mazingira ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sekta za miundombinu, nishati mbadala , viwanda, ujenzi na usambazaji maji.
Vilevile Makamu wa Rais amesema kwamba ushirikiano baina ya sekta ya umma na binafsi nchini Tanzania katika kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuinua kipato cha watu, Benki Kuu ya Tanzania imeanzisha utaratibu wa kutoa mikopo kwa benki za biashara kwa ajili ya kukopesha wakulima kwa riba isiyozidi 9%. Amesema matokeo ya mpango huo wa ushirikiano yameleta tija ikiwemo kuongezeka kwa kasi ya ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi kwenye sekta ya kilimo kuongezeka kutoka asilimia 7.3 katika mwaka ulioshia Julai 2021 hadi asilimia 46.4% Julai mwaka 2023.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
21 Septemba 2023
New York - Marekani.
TUWALINDE WATOTO DUNIA IMEBADILIKA, WAZIRI MHAGAMA
Wednesday, September 20, 2023
MAJALIWA: TANZANIA KUWA WAZALISHAJI WAKUBWA WA NISHATI
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Septemba 20, 2023 amefungua Kongamano la Tano na Maonesho ya Nishati Tanzania na amesema kwamba Serikali imedhamiria kuwa mzalishaji mkubwa na nishati.
“Tunaendelea na utafutaji wa gesi, tunataka tuwe wazalishaji wakubwa wa nishati, tuwe na umeme wa kutosha utakaopatikana kwa urahisi na nafuu na ziada tutauza nje ya nchi.“
Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo baada ya kufungua kongamano hilo la siku mbili linalofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Amesema kuwa Tanzania haitegemei kuzalisha umeme kwa kutumia maji pekee bali inaendelea kuweka mkazo katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati nyingine kama gesi na jua.
Waziri Mkuu amesema katika kongamano hilo la kimataifa la nishati ambalo limehusisha viongozi na wadau kutoka katika mataifa mbalimbali Duniani litajadili namna bora ya kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa nishati.
Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa kuzisisitiza nchi zote wanachama kuhakikisha taasisi za mafunzo zinatoa programu maalum za mafunzo katika sekta za nishati ili kuongeza idadi ya watu walio na ujuzi na maarifa kwenye sekta hiyo.
Amesema kuwa nishati ni sekta muhimu katika kufikia lengo la uanzishwaji wa viwanda na katika kuimarisha na kuwezesha uzalishaji na shughuli nyingine za kiuchumi. “Lazima tufanye kazi kwa ushirikiano na wadau wote ili kufungua fursa kwa Watanzania wote.”
Amesema ili kuwaendeleza wafanyabiaahara wa ndani na Watanzania kushiriki katika sekta ya nishati, Serikali itaendelea kuhakikisha kanuni na taratibu zinazofaa zinawekwa ili kuwezesha ushirikishwaji katika mnyororo wa thamani wa maendeleo kwenye sekta ya nishati
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema wameendelea kutekeleza mipango mbalimbali waliojiwekea katika kuhakikisha umeme unapatikana wakati wote nchini.
Dkt. Biteko amesema zaidi ya kampuni 100 za nishati kutoka katika maeneo mbalimbali duniani zinashiriki katika kongamano hilo ambalo lilitanguliwa na mkutano wa viongozi wa nishati.
Tuesday, September 19, 2023
KAMATI YA SIASA BAGAMOYO YARIDHIISHWA NA UJENZI WA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO INAYOENDELEA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAGAMOYO.
Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Bagamoyo tarehe 18 September 2023 imetembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo ili kuona namna inavyoendelea.
Miradi iliyotembelewa ni pomoja na Mradi wa ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Dharura (EMD) katika Hospitali ya Wilaya Bagamoyo, mradi wa Ujenzi wa Shule ya Msingi mpya Kiharaka, Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Chasimba na Mradi wa ujenzi wa nyumba za walimu katika Shule ya Sekondari Makurunge.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Sharifu Zahoro ameridhishwa na kasi ya ujenzi ya miradi hiyo kwa hatua iliyofikiwa.
Mwenyekiti huyo amewaomba wataalamu wanaohusika katika kusimamia Miradi hiyo, kuhakikisha wanaendelea na kasi hiyo ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati kama ilivyopangwa.
"Niwapongeze sana wataaamu mnaosimamia mradi hii kwa kazi nzuri mnayoifanya miradi inaenda vizuri sana ninachowaambia muendelee na kasi hii mpaka kukamilika kwake huku mkizingatia thamani ya fedha inayotumika ilingane na ubora wa Miradi husika" amesema Mhe. Zahoro
Aidha Mwenyekiti huyo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zinazojenga miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamlyo, pia ametoa pongezi kwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo pamoja na MKurugenzi wa Halmashauri kwa kusimamia vizuri utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea Bagamoyo.
Nae Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bi..Halima Okashi amesema wataendelea kushirikiana bega kwa bega na watumishi wa Halmashauri kuhakikisha miradi hiyo na itakayokuja inafanyika kwa weledi na kukamilika ikiwa na ubora uliokusudiwa.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw. Shauri Selenda, Ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Hassan kwa kutoa fedha zinazosaidia kujenga miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye Halmashauri ya Bagamoyo,
"Tunamshukuru Mhe. Rais kwa kutupatia fedha nyingi zinazosaidia kujenga hii miradi ambayo leo tumetembelea na kuikagua, Serikali imetupatia takribani Bilioni 1.3 iliyowekezwa katika miradi hii.







































.jpeg)

.jpeg)























