Thursday, February 24, 2022

ULEGA AWATAKA VIONGOZI KUHAMASISHA WANANCHI KUHUSU UCHUMI WA BLUU.

 No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

........................................................................ 

Na Athumani Shomari, Bagamoyo.

 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewataka viongo mbalimbali wakiwemo wakuu wa Mikoa iliyopo ukanda wa Bahari ya hindi, kuwahamasisha wananchi ili watumie fursa za mazao ya bahari kujiongezea kipato.

 

Ulega ameyasema hayo mjini Bagamoyo leo February 24, 2022. Alipokuwa akifungua kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

 

Amesema miongoni mwa vipaumbele vya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ni pamoja na uchumi wa Bluu ambacho ni kipaumbele cha nane, na kwamba utekelezaji wake ni kusaidia kufikia kwa malengo ya Rais kukuza uchumi kwa wananchi.

 

Alifafanua kuwa uchumi wa bluu ni pamoja na kutumia mazao ya Baharini ikiwemo ufugaji wa Majongoo Bahari, ufugaji wa Kaa na Kilimo cha Mwani, ambvyo vyote hivyo soko lake ni kubwa kimataifa licha ya kuwa watu wengi wa ukanda wa Pwani hawafahamu.

 

Aliongeza kuwa, lengo la wizara ni kuona wananchi wanazifahamu fursa zinazotokana na Bahari ili wazitumie ipasavyo na kuwataka wataalamu waendelee kutoa elimu ya ufugaji wa viumbe hao wa maji ya bahari kwa wananchi.

 

Alisema mkakati uliopo wa serikali ni kutoa fedha kwa vikundi vitakavyojishughulisha na mazao hayo ili waweze kutekeleza miradi hiyo kwa ufanisi na kujiongezea kipato huku kukiwa na elimu ya namna ya utunzaji wa mazingira ya Bahari.

 

Aliendelea kusema kuwa, fursa za uchumi wa bluu katika kipengele cha Bahari ni nyingi sana lakini zinahitaji maandalizi ya namna ya kuzitumia fursa hizo ambapo amewaeleza viongozi hao kuwa, miongoni mwa maandalizi hayo ni pamoja kuwapa elimu wananchi juu ya fursa hizo huku akiwataka kuwa na vikundi vitakavyokuwa na mipango madhubuti ya maendeleo.

 

Aliongeza kwa kusema kuwa, fedha za miradi hiyo zitakapokuwa tayari hawatapewa watu ambao hawakujiandaa kitaaluma na badala yake watapewa wale ambao wamepata elimu, wameunda kikundi na kuanza utekelezaji wa mfano.

 

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu waziri, amewataka wataalamu walioajiriwa na serikali kutimiza wajibu wao kwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo huku wakitoa umuhimu kwenye vipaumbele vya Rais Samia Suluhu Hassan katika kufikia malengo ya serikali.

 

Alisema wataalamu wengi wamekuwa ni wakukaa ofisini wanashindwa kutekeleza majukumu yao kwa vitendo hali inayokatisha tama hata kwa wananchi wa kawaida huku akiwataka kubadilika ili waendane na kasi Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Aliwataka washiriki wa kikao hicho kutoka na mikakati ya utekelezaji wa majukumu ilia waweze kufikia malengo ya kuondoa umasikini kwa wananchi, kuongeza mapato ya serikali ambayo yatapelekea kufikisha huduma bora kwa wananchi.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo, akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo, wanaofuata kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga. 

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

No description available. 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi katika kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo. kushoto ni Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga.

No description available.No description available.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah akizungumza wakati wa kumkaribisha Mkuu wa Mkoa waPwani, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda.

No description available.

No description available.

Washiriki katika kikao kazi hicho ni viongozi kutoka Dar es salaam na Pwani wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo mkoani Pwani.

 No description available.

No description available.

Washiriki katika kikao kazi hicho ni viongozi kutoka Dar es salaam na Pwani wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo mkoani Pwani.

No description available. 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Madiwani wa Halmashauri ya Bagamoyo na watendaji kata, kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda.

No description available. 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwa katika picha ya pamoja na maafisa uvuvi, kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda.

Tuesday, February 22, 2022

MILIONI 600 KUJENGA SEKONDARI MAKURUNGE BAGAMOYO.

 No description available. 

Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aloisi Damian Kaziyareli, (kushoto) na Mtendaji kata Makurunge, Chumi Joel (kulia) wakishiriki katika zoezi la kuchimba msingi kwaajili ya ujenzzi wa shule mpya ya Sekondari inayojengwa kitongoji cha Gezaulole kata ya Mkurunge, Halmashauri ya Bagamoyo, fedha hizo za ujenzi zimetolewa na Rais Samia Suluhu Hassan katika mpango wa kuhakikisha hakuna mtoto aneshindwa kwenda kidato cha kwanza kwa kukosa shule.

...................................

Na Athumani Shomari, Bagamoyo.

Wanachi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo wamejitokeza kuchimba msingi kwaajili ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa kwa fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aloisi Damian Kaziyareli, amesema ujenzi wa shule hiyo mpya utasaidia kuondoa adha kwa wanafunzi wanaoishi kata ya Makurunge ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitembea umbali wa kilomita zaidi ya kumi kufuata shule ya sekondari.

 

Ameongeza kuwa, kata hiyo ya Makurunge haikuwahi kuwa na shule ya Sekondari na kwamba ametumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kutenga milioni mia sita kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo ya sekondari.

 

Amesema tayari milioni 470 zimeshaingizwa kwaajili ya kazi hiyo ambapo zitatumika kujenga jengo la utawala, vyumba vya madarasa nane, Maabara za sayansi tatu, Maktaba, Vyoo pamoja na nyumba za walimu huku milioni 130 iliyobaki itatolewa baadae.

 

Afisa elimu huyo amesema kutokana na mpangilio wa majengo hayo, mara tu baada ya kukamilika ujenzi wa shule hiyo itakuwa imejitosheleza na kwamba itakuwa na ubora wa unaotakiwa kwaajili watoto kupata elimu.

 

Aidha, ametoa wito kwa wazazi kujipanga kusomesha watoto katika shule hiyo ambayo januari 2023 itapokea watoto wa kuanza kidato cha kwanza.

 

Nae Diwani wa kata ya Makurunge, Hamisi Mohamed, amesema wananchi wa kata hiyo wamefurahishwa sana na ujenzi wa shule ya sekondaari katika kata  hiyo na wapo tayari kutoa ushirikiaano wao pindi watakapohitajika kufanya hivyo.

 

Amesema ili kuthibisha kuwa wananchi hao wamefurahishwa na ujenzi huo, wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa ujenzi huo katika haatua ya awali ya kuchimba msingi wa madarasa.

 

Kwa upande wake Mtendaji kata Makurunge Chumi Joel amesema amefanikiwa kuunganisha nguvu za wananchi wa kata yote kupitia wenyeviti wa vitongoji ndani ya kata hiyo ambapo kila mwenyekiti wa kitongoji amfika na wananchi wake na kushiriki kazi kikamilifu.

 

 Aidha, amewataka wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kujitolea katika kazi za maendeleo ili kufanikisha malengo yao ndani ya kata.

 

 Nao wazazi wa kata ya Makurunge wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuwatengea fedha hizo za ujenzi wa shule ya sekondari ili watoto wao sasa wapate kusoma shule iliyo karibu nao.

No description available.No description available.

Wahandisi kutoka idara ya ujenzi Halmashauri ya Bagamoyo wakihakiki vipimo vilivyopo kwenye michoro katika zoezi la uchimbaji msingi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole Kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Wananchi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo, wakishiriki zoezi la uchimbaji msingi katika ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Wananchi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo, wakishiriki zoezi la uchimbaji msingi katika ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Mtendaji kata Makurunge, Chumi Joel akishirikiana na Wananchi wa kata hiyo iliyopo Halmashauri ya Bagamoyo, katika zoezi la uchimbaji msingi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Mtendaji kata Makurunge, Chumi Joel akishirikiana na Wananchi wa kata hiyo iliyopo Halmashauri ya Bagamoyo, katika zoezi la uchimbaji msingi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.

Wananchi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo, wakiwa na nyuso za furaha wakati wa wakishiriki zoezi la uchimbaji msingi katika ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.