Wednesday, March 25, 2020

SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA KUKABILIANA NA CORONA (COVID-19)

WAMJW – Dar es Salaam.


Serikali imepokea msaada wa vifaa kinga kutoka China kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na mlipuko wa maambukizi ya homa kali ya mapafu inayoambukizwa na virusi vya Corona (COVID-19) kutoka taasisi ya Jack Ma na Alibaba.


Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Serikali, Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Muhammed Bakari Kambi amesema msaada huo ambao umetolewa na Taasisi ya Jack Ma na Alibaba ni pamoja na mavazi (PPE) 1,000 ya kujikinga wakati wa kuhudumia watu waliobainika kuwa na ugonjwa huo ni pamoja na vitendanishi (Rapid Tests) 20,000 na Barakoa (Masks) 100,000.


Prof. Muhammed amesema msaada huo utawasaidia wataalamu wa afya nchini wakati wa kuwahudumia waliobainika na watakaobainika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.


“Tunashukuru kwa msaada huo kama serikali,tumekuja hapa kushuhudia sehemu ya shehena ya tani tatu ya vifaa-tiba vilivyotolewa na Taasisi ya Jack Ma na Alibaba ambavyo vimewasili usiku wa leo na ndege ya mizigo ya Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia Ethiopia,” amesema Prof. Muhammed.


Katika hatua nyingine, Prof. Muhammed amemshukuru Afisa Ubalozi wa Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia Ethiopia Ndg. Tewodros Girma ambaye amekabidhi msaada huo kwa niaba ya Balozi wa nchi hiyo, Mhe. Yonas Yosef.

Tuesday, March 24, 2020

MAGAZETI YA LEO MACHI 24, 2020.

CORONA YAITIKISA DUNIA

Image may contain: 1 person
 Na Albert Kawogo.


Huku China ikiwa tayari imelipunguza janga la tatizo la corona kwa zaidi ya asilimia 90; ugonjwa huo tayari umeshaua watu zaidi ya 6000 nchini Italia.


Kwa nchi ya Italia pekee yenye mnara mkubwa wa jedwali la vifo; Jumamosi iliyopita walifariki watu 627 Jumapili watu 793 na leo hii Jumatatu hadi sasa wamefariki 601 idadi ya waliopoteza uhai Italia tangu corona iingie nchini humo siku 64 zilizopita ni watu 6077 huku kukiwa na wagonjwa zaidi ya 40000 vitandani.
 

Wastani wa vifo 600 kwa siku ni idadi kubwa tunaona Waziri Mkuu wa taifa hilo Giuseppe Conte akitoa maoni ya kukata tamaa kupitia ukurasa wake wa twitter.
 

Dunia inapita katika wakati mgumu huku ikielezwa na kushuhudiwa kuwa huenda hili ni janga kubwa la kibinadamu ambalo rekodi yake haitaweza kumithilika siku zijazo.


Hoja kuu zinazoibuliwa na wanazuoni mbalimbali Duniani ni uwezo wa mataifa duniani hasa Ulaya Asia na Marekani kukabili ghafla na dharura huduma za tiba kwa watu wengi mahututi kwa pamoja.


Changamoto hiyo imeelezwa kuwa ndio sababu kuu inayofanya wagonjwa wengi wa corona kupoteza maisha kwenye nchi hizo tajiri Sana duniani.
 

Mataifa haya yenye uchumi mkubwa Ulaya ambao ni sehemu ya wanachama wa Jumuiya ya Ulaya EU ambayo ni Italia Ujerumani na Ufaransa zikiwa ni siku 70 sasa yameshindwa kabisa kuibuka na mpango wa dharura wa kupambana na corona huku Taasisi ya Afya ya Dunia WHO ikibainisha kuwa chanjo ya ugonjwa huo inaweza kuchukua mwaka mmoja na miezi 5 yaani miezi 17 au zaidi.
 

Hali hiyo inatuonyesha kwamba ni lazima uwepo mpango wa dharura wa kupambana kuenea kwa ugonjwa huu Ulaya Asia Afrika na Marekani.
 

Taarifa za Shirika la fedha la kidunia IMF zinaonya kuporomoka kwa uchumi duniani kutakakotokana kushuka kwa kiwango cha uzalishaji viwandani na upungufu mkubwa wa biashara ya kimataifa hasa ya mafuta gesi madini na mazao.
 

Hatua hiyo pia itaathiri sana sekta ya usafiri wa majini na anga hasa mashirika makubwa ya ndege hali itakayochangia kudhoofisha sekta ya utalii.
 

Pamoja na kuwa Afrika haijafikwa na wagonjwa wengi lakini watabiri wa mambo wanabainisha kuwa Afrika ndio itaathirika zaidi na ugonjwa wa corona kwakuwa sehemu kubwa masoko yake ya nje katika biashara yanategemea nchi zilizoathiriwa na ugonjwa huo huku baadhi ya nchi hizo bajeti zao zikiwa zinapata misaada ya fedha na ruzuku za maendeleo kutoka kwa nchi waathirika.


RAIS MAGUFULI ATEMBELEA MAENEO YENYE MAWE NDANI YA IKULU YA DODOMA

Image may contain: mountain, outdoor and nature
Rais Dk. John Magufuli akiwa kwenye miongoni mwa mawe yaliypo ndani ya Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, alipoamua kuzuru maeneo yenye mawe hayo 23 Machi 2020.
 Image may contain: one or more people, shoes, outdoor and nature

Rais Dk. John Magufuli akiwa kwenye mawe yaliypo ndani ya Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, akiwa anatafakari jambo, alipoamua kuzuru maeneo yenye mawe hayo 23 Machi 2020.
Image may contain: 1 person, standing, outdoor and nature

Rais Dk. John Magufuli akiwa kwenye mawe yaliypo ndani ya Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, alipoamua kuzuru maeneo yenye mawe hayo 23 Machi 2020, (Picha zote na Ikulu).