Monday, September 30, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA DPP KUHUSU WAHUJUMU UCHUMI.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akipokea toka kwa Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw. Biswalo Mganga taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw. Biswalo Mganga katika picha ya pamoja na ujumbe wake mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30,2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw.Biswalo Mganga baada ya kupiga naye picha ya pamoja na ujumbe wake mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea jambo na na Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw.Biswalo Mganga baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw.Biswalo Mganga baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30, 2019. Kushoto ni Katibu Mkuu Ikulu Mhe. Dkt. Moses Kusiluka.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea baada ya Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw. Biswalo Mganga kumkabidhi taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw.Biswalo Mganga akitoa muhtasari kabla ya kukabidhi taarifa ya
utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30,2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea toka kwa Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali (DPP) Bw. Biswalo Mganga taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu Septemba 30, 2019

PICHA NA IKULU

MGALU ASEMA, WANAWAKE NI JESHI KUBWA.

 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani, Subira Mgalu, (kulia) wakijadili jambo wakati wa maadhimisho ya Umoja wa Wanawake yaliyofanyika kiwilaya katika Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo.
 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani, Subira Mgalu, akizungumza katika maadhimisho hayo.
................................ 

Na Shushu Joel, Chalinze.

NAIBU Waziri wa Nishati Subra Mgalu ambaye pia ni mbunge wa viti maalum (UWT) kupitia mkoa wa Pwani, amewataka wanawake kujiamini zaidi kwa kuwa wao ni jeshi kubwa na lenye uwezo wa hali ya juu.

Akizungumza katika maadhimisho ya Umoja wa Wanawake kiwilaya yalivyofanyika katika Jimbo la Chalinze, wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, alisema kuwa wanawake wamekuwa ni tegemeo kwenye ufanikishaji wa mambo mbalimbali ya kijamii .

"Wanawake ni jeshi kubwa na lenye kutegemewa kwenye chama na serikali hivyo kinamama tuongeze uaminifu kwenye jamii zetu ili tuzidi kuendelea kuwa nguzo zaidi" Alisema Mgalu.

Aidha amewapongeza kinana wote waliojitokeza katika sherehe hizo na kuwataka kutembea kifua mbele kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za vijiji na mitaa kwani umoja wao ndio ushindi wao.

Mgalu amewataka kinamama kukumbuka wajibu wao wa kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi katika kuwachagua viongozi wa CCM ili kukIfanya chama hicho kuendelea kushika dola.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja huo wilaya ya Bagamoyo Rukia Masenga, amempongeza Naibu Waziri huyo kwa jinsi anavyofanya kazi za umoja wa Wanawake na hasa kuwaweka kitu kimoja wanawake wa mkoa wa Pwani.

Aidha aliongeza kuwa kinamama ni jeshi linalojitambua na hivyo amemuhakikishia naibu Waziri huyo kuwa ushindi ni lazima upatikane.

KIKWETE NI JEMBE LINALOLIMA KIANGAZI NA MASIKA: UWT.


Na Shushu Joel, chalinze.

Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, wamempongeza mbunge wa Jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete kwa Utendaji wake wa kazi katika jimbo hilo.

Kwa kawaida wakulima walio wengi hapa nchini hutumia muda mwingi katika shughuli ya kilimo kwenye kipindi cha masika lakini Mbunge wa Chalinze amekuwa akilima masika na kiangazi.

Maneno hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Bagamoyo, Bi. Rukia Masenga, alipokuwa akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya Umoja huo ambayo kiwilaya yalifanyika katika Kijiji Cha Msoga, halmashauri ya chalinze.

"Mbunge wa Chalinze Mh Ridhiwani Kikwete amekuwa ni kiongozi wa kuigwa katika taifa hili kutokanana na jinsi alivyosimamia maendeleo makubwa katika jimbo lake na sisi Umuiya ya Wanawake ndani ya wilaya hii tumeridhishwa na utekelezaji wa ilani katika Jimbo lake "Alisema Bi Rkia.

Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la chalinze Ridhiwani Kikwete amewashukuru kina mama hao kwa kuona kile kilichokuwa kinahitajika kwa wananchi kinatekelezeka kwa kiwango kikubwa.

Aliongeza kuwa chalinze imetekeleza ilani ya CCM kwa vitendo kutokana na kupunguza na kumaliza yale yaliyokuwa ni changamoto kubwa kwa Wananchi wa Halmashauri hiyo ikiwemo shida kubwa ya Maji na Afya ya kina Mama na Watoto.

Akizungumzia ujenzi wa Vituo cha afya katika Halmashauri ya Chalinze, Mh. MBunge alisema kazi kubwa imefanyika kujenga Zahanati kila kijiji na leo ni vijiji Vichache ambavyo Zahanati zao hazijakamilika.

Kwa Upande wa Vituo vya Afya hali ni nzuri sana kila Kata ispokuwa kata 3 tu, ambazo nazo ziko mbioni kwenye Ujenzi.

Kwa Upande wa Elimu wamejenga Vyumba zaidi ya madarasa 48, Umeme umesambazaa katika jimbo zima la Chalinze na Miundombinu ya Barabara inakwenda vizuri na Serikali imepanga kutumia Milioni 158.5 kwa ajili ya Barabara za Mji wa Chalinze ambazo zitajengwa kwa kiwango cha lami na madaraja madogo.

Wakati huo huo, Mh. Mbunge Kikwete ameipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Mh. Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kuipatia Chalinze Shilingi Bilioni 16 kwa ajili ya kutatua changamoto ya Maji iliyokuwa kero kubwa sana miaka ya nyuma.


Fedha ambazo amezieleza kuwa zinakwenda kumaliza shida ya maji sio tu kwa wana Chalinze lakini pia kwa Maeneo ya miji ya Jirani hasa Ngerengere, na Magindu kwa upande wa Kibaha Vijijini.

Mh. Mbunge pia amewapongeza wanawake kwa jinsi wananvyokuwa mstari wa mbele katika ufanisi wao wa kuchangamkia fursa ndogo ndogo za halmashauri.

Hadi sasa vikundi zaidi ya 80 vya wanawake vimeweza kufikiwa katima kata mbalimbali lakini kubwa pia ni jinsi wanavyorudisha mikopo hivyo.

Kwa hakika nyie ni wa kipekee, mh. Mbunge alimaliza.