Thursday, August 29, 2019

WAKULIMA WA MUHOGO MKURANGA WAPATA KIWANDA KWA AJILI YA KUCHAKATA ZAO LA MUHOGO


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo kushoto akipeana mkono wa pongezi na Mkurugenzi mtendaji wa  kiwanda cha kuchakata zao la  muhogo mara baada ya halfa ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho amabcho kimejengwa katika kijiji cha Mgenge kata ya Beta Wilayani Mkuranga.
.............................
VICTOR  MASANGU, MKURANGA

KILIO cha muda mrefu ambacho kilkuwa kinawakabili wakulima wa zao la muhogo katika Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani hatimaye hivi karibuni  wanatarajia   kuondokana na changamoto sugu ya upatikanaji wa soko la uhakika   kufuatia kuanza  kwa  ujenzi wa mradi  wa kiwanda kikubwa cha kuchakata zao hilo  ambacho kitagharimu kiasi cha shilingi bilioni 9.5.


Hayo yamebainishwa na baadhi ya wakulima hao wakati wa Ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo wakati wa halfa ya uwekeaji wa jiwe la msingi katika kiwanda hicho ambacho kimejengwa na mwekezaji kutoka nchini China katika kijiji cha Mkenge  kata ya Beta Wilayani Mkuranga ambapo wamedai hapo awali walikuwa na tatizo la kuuza mihogo yao  kwa bei ya hasara.


“Sisi kama wakulima wa zao hili la muhogo katika Wilayah hii ya Mkuranga tumefarijika sana kwa ujio wa mradi wa kiwanda hiki ambacho kimejengwa na marafiki zetu wa kutoka nchini china, na tunashukuru kwa jitihada ambazo zinafanywa na Mkuu wetu wa Mkoa wa Pwani pamoja na Rais wetu Dk. John Pombe Magfuli kwa kuwaleta wawekezaji hawa ambao watatusaidia kuondokana na tatizo la kupata soko la uhakika,”walisema wakulima hao.


Kwa  upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amewataka maafisa kilimo wote kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ipasavyo kwa kuwasimamia vema wakulima wa zao hilo la muhogo  kutonyonywa na walanguzi na  kupata haki zao stahiki na kuahidi kuwaondoa kazini wale wote ambao watabainika kukwamisha juhudi za serikali  katika uwekezaji wa sekta ya  viwanda.


Aidha Ndikilo alisema kuwa lengo kubwa la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inawasaidia kwa hali na mali wananchi wake katika kuondokana na changamoto mbali mbali ambazo zinawakabili ikiwemo ukosefu wa masoko ya uhakika na ajaira, hivyo atahakikisha zao hilo la muhogo linapata soko kupitia viwanda ambavyo vinajengwa na wawekezaji katika maeneo mbali mbali na kuwahimiza wasikate tamaa na badala yake waendelee zaidi kulima mazao ya biashara ikiwemo ufuta, muhogo na korosho.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto  Sanga amesema kuwa  kipindi cha nyuma wakulima wengine walikuwa tayari  wameshakata tamaa  katika kilimo  cha zao la muhogo, hivyo kukamilika kwa kiwanda hicho kitaweza kuleta mabadiliko chanya kwa kuwapa fursa wananchi kuwa na soko la uhakika.


“Kwa kweli wananchi wangu hasa kwa wakulima wa zao hili la muhogo katika Wilaya ya Mkuranga baadhi yao walikuwa tayari wameanza kukata tamaa kabisa kutokana na mfumo ambao ulikuwepo wanauza mazao yao kwa bei ya hasara lakini kwa sasa kiwanda hiki kinachotarajiwa kukamilika mwaka huu wataondokana kabisa na changamoto ya soko,” alismema Sanga.


Awali akisoma Risala ya ujenzi wa mradi huo  mmoja wa vongozi  wa kiwanda hicho, Leonard Jambeli  kwa niaba ya Mkurugenzi amebainisha kwamba waanategemea kutoa fursa za ajira za moja kwa moja  kwa wazawa zaidi ya mia moja pindi uzalishaji utakapoanza kufanyika rasmi.


Kukamilika kwa mradi huo wa ujenzi wa kiwanda mwishoni mwa mwaka huu  kutaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa wakulima wa zao hilo katika halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani  ambao kwa miaka mingi walikuwa wanapata hasara kutokana na kunyonywa na walanguzi  kununua zao hilo  kwa bei ndogo.

Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kushoto Ramadhani Maneno akimshika mkono Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ikiwa ni moja ya ishara ya kumpongeza katika juhudi zake za kuunga mkono juhudi za serikali katika ujenzi wa viwanda.


 Mkuu wa Mkoa wa Pwani kushoto Mhandisi Evarist Ndikilo akipata maelekezo kutoka kwa mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha kuchakata muhogo wakati alipofanya ziaara yake ya kikazi kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho, (PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)

ASKARI WA USALAMA BARABARANI PWANI, WAPATA MAFUNZO KUTOKA ITDA.

Askari wa kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani wamepata Mafunzo kutoka kwa wataalam wa Chama cha Madereva Wasafirishaji wa Nchi za nje (ITDA).

Awali akifungua mafunzo hayo Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani, Mrakiibu wa Polisi (SP) Mosi B. Ndozero, alisema amefurahi kuona Mkoa wa Pwani umekuwa ni moja ya Mikoa ambayo imepatiwa Elimu hiyo ambayo itawasaidia Askari wa usalama Barabarani kuweza kumtambua Dereva anayeendesha gari husika na uelekeo wa gari hilo katika Nchi jirani.

Kwa upande wake afisa kutoka Chama cha Madereva Wasafirishaji wa Nchi za nje (ITDA), Solomon Kassa alisema mfumo huo utaongeza ufanisi katika kazi na uhakika katika kazi kwa ujumla kwa askari wa usalama barabarani ikiwemo kupunguza ajali za Barabarani zianazosababishwa na madereva (IN-TRANSIT VEHICLES) wasio na sifa Barabarani kwani kwa kutumia mfumo huu madereva wenye sifa ndio watakaoruhusiwa kuendesha magari ya IT.

Sambamba na hilo ameleeza kuwa Chama cha Madereva Wasafirishaji wa Nchi za nje (ITDA) kimedhamiria kuondoa vikwazo visivyo vya forodha ambavyo vipo Barabarani.

Aidha, askari wa usalama Barabarani Mkoa wa Pwani walishukuru maofisa kutoka Chama cha Madereva Wasafirishaji wa Nchi za nje (ITDA) kwa elimu waliyowapatia nakuahidi kwenda kuyafanyia kazi yale yote ambayo wameyapata toka kwa maofisa hao wa ITDA .

Jumla ya askari walioshiriki walikuwa 44, wawakilishi kutoka kila wilaya za Mkoa wa Pwani wakiwa ni watano, pamoja na ofisi ya RTO Pwani ambao wametakiwa kwenda kuwa mabalozi kwa wenzao kwa elimu waliyopata.

Mara baada ya askari hao kumaliza mafunzo hayo walienda Barabarani kufanya mazoezi kwa vitendo kwa kutumia mfumo wa kielectronic ambapo magari matano ya mfano yalibandikwa Bima ambayo namba ya gari kupitia taarifa ya Bima iliyobandikwa na Afisa wa ITDA inasomwa moja kwa moja kwenye system ya Google ( www.ITDA.co.tz//sticker_verification.php) kwa kumtambua dereva na maelezo yote ya gari anayoendesha na nchi anayokwenda.

Aidha, magari mengi ya IT yanayopita yaliweza kubainika yamebandikwa Bima feki toka Kariakoo kwa mawakala wa Clearing & Forwarding (C&F) kinyume cha utaratibu.

Elimu hiyo iliyotolewa kwa madereva itasaidia kubadilisha mfumo wa kimazoea wa magari ya IT kwenda mfumo wa teknolojia maridhawa kiasi ambacho dereva akifanya kosa/ajali nchini akielekea nchi yoyote ni rahisi kupatikana.

MUWEKEZAJI MTURUKI AMPIGA MFANYAKAZI WAKE KIBAHA.

Na Omary Mngindo, Kibaha.


Mkazi wa Kijiji cha Soga Kata ya Soga wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani Kashinde Maonaje, amejeruhiwa eneo la shingo kufuatia kupigwa Kareti na muwekezaji Mturuki akiwa kazini kampuni ya yapiMarkezi.
 


Mkazi huyo amepigwa na Mturuki huyo ambaye ni bosi wame, akiwa kazini saa 4 usiku, baada ya kumkabili kiongozi huyo akimwelezea moja ya changamoto iliyopo, inayohusiana na utendaji wa kazi anayoifanya kitengo cha umeme.


Alisema kuwa akiwa katika eneo lake la kazi, kulijitokeza tatizo la kiufundi kuhusu umeme, ambapo alimfuata bosi huyo akamwelezea hali hiyo, lakini cha kushangaza alijikuta anapigwa kareti eneo la shingo, hali iliyomsababishia madhara makubwa.


"Ilikuwa usiku kulijitokeza tatizo linaohusiana na umeme kwenye kebo, nikamkabili bosi wangu, ghafla nikamuona amekunja uso, nikajikuta nimepigwa kareti shingoni, kama mnavyoniona hata kugeuka ni shida," alisema Maonaje.


Baada ya kujionea tukio hilo baya na la kusikitisha, MNEC Haji alisema kuwa hawezi kukubaliana na unyanyasaji huo na kueleza kwamba matukio ya aina hiyo yanazidi kushamiri katika maeneo ya kazi, huku akitaka hatua za kisheria lazima zichukuliwe.


"Hatuwezi kuvumilia unyanyasaji aina hii ukiendelea, tunawakaribisha nchini kwetu, tunawapatia ardhi, mwisho wa siku wanatunyanyasa kiasi hiki, haya ni manyanyaso yasiyovumilika, kuna maeneo mengine wa-Tanzania wenzetu wanabakwa," alisema Haji.


Mbali ya tukio hilo, Haji aliyeungana na MNEC mwenzake Bundalla Richard kutokea Shinyanga, alipokea malalamiko kuhusiana na kampuni ya Mohamed Dewj, kupitia shamba lake lijulikanalo kwa jina la A lave, linalohusiana na kilimo cha mkonge.


Diwani wa Kata hiyo Ramadhani Chezeni na wakazi wake walimweleza Haji kwamba, pamoja na kuwepo kwa usitishaji wa undelezwaji wa eneo hilo, bado kampuni hiyo inashughulika na upandaji wa mkonge, hali inayowapa sintofahamu kubwa.


"Hili suala limefika katika ofisi ya Mkuu wa wilaya na Mkoa lakini mpaka sasa hatuoni kitu konachoendelea, tunakuomba MNEC lichukue ukamfikishie Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa Rais Dkt. John Magufuli," alisema Chezeni.


Baada ya taarifa hiyo alimpigia simu mbunge wa jimbo hilo Humoud Jumaa ambaye alimweleza kwamba suala hilo limefika kwa Waziri nwenye dhamana William Lukuvi, hivyo anaimani kuwa litakuwa katika hatua mbalimbali.


Kwa upande wake Haji alimuomba MNEC mwenzake amkumbushe watakapokuwa kwenye kikao chao mbele ya Mwenyekiti wao Dkt. Magufuli, ili amwelezee kilio hicho kinachodaiwa kudumu kwa zaidi ya miaka kumi sasa.


Haji aliyekuwa ziarani wilayani Kibaha, alianzia Kata za Gwata na Magindu, ambapo akiwa Gwata alikutana na mgogoro wa mifugo na mpaka wa vijiji vya Ndwati na Kigoda, ambapo aliwataka viongozi waumalize, kinyume chake ataufikisha wizarani ili vifutwe kiwe kimoja kama ilivyokuwa awali.